< Mithali 10 >

1 Mithali za Sulemani. Mwana mwenye hekima humfurahisha baba yake lakini mwana mpumbavu huleta majonzi kwa mama yake.
The proverbs of Solomon. A wise son makes a glad father; but a foolish son brings grief to his mother.
2 Hazina zilizolimbikizwa kwa uovu hakosa thamani, bali kwa kutenda haki hujilinda mbali na kifo.
Treasures of wickedness profit nothing, but righteousness delivers from death.
3 Yehova hawaachi wale watendao haki wapate njaa, bali hamu ya waovu huizuia.
Jehovah will not allow the soul of the righteous to go hungry, but he thrusts away the desire of the wicked.
4 Mkono mlegevu humfanya mtu awe masikini, bali mkono wa mtu mwenye bidii hupata utajiri.
He becomes poor who works with a lazy hand, but the hand of the diligent brings wealth.
5 Mwana mwenye busara hukusanya mazao wakati wa kiangazi, bali ni aibu kwake alalaye wakati wa mavuno.
He who gathers in summer is a wise son, but he who sleeps during the harvest is a son who causes shame.
6 Zawadi kutoka kwa Mungu zipo juu ya kichwa cha wale watendao haki; bali kinywa cha uovu hufunikwa kwa jeuri.
Blessings are on the head of the righteous, but violence covers the mouth of the wicked.
7 Mtu atendaye haki anatufurahisha tunapomkumbuka, bali jina la mwovu litaoza.
The memory of the righteous is blessed, but the name of the wicked will rot.
8 Wale wenye akili hukubali maagiza, bali mpumbavu mwenye maneno mengi ataangamia.
The wise in heart accept commandments, but a chattering fool will fall.
9 Yeye anayetembea katika uadilifu hutembea katika usalama, bali yule anayepotosha njia zake, ataonekana.
He who walks blamelessly walks surely, but he who perverts his ways will be found out.
10 Yeye ambaye hukonyeza kwa jicho lake huleta majonzi, bali mpumbavu mwenye maneno mengi atatupwa chini.
The one who winks with the eye causes trouble, but the one who boldly rebukes makes peace.
11 Kinywa cha mwenye kutenda haki ni kama chemchemi ya maji ya uzima, bali kinywa cha uovu hufunikwa kwa jeuri.
The mouth of the righteous is a spring of life, but violence covers the mouth of the wicked.
12 Chuki huchochea mafarakano, bali upendo hufunika juu ya makwazo yote.
Hatred stirs up strife, but love covers all wrongs.
13 Hekima inapatikana kwenye kinywa cha mtu mwenye ufahamu, bali fimbo ni kwa ajili ya mgongo wa yule asiye na akili.
Wisdom is found on the lips of him who has discernment, but a rod is for the back of him who is void of understanding.
14 Watu wenye hekima hutunza maarifa, bali kinywa cha mpumbavu huleta uharibifu karibu.
Wise men lay up knowledge, but the mouth of the foolish is near ruin.
15 Mali ya mtu tajiri ni mji wake mwenye ngome; ufukara wa masikini ni uharibifu wao.
The rich man's wealth is his strong city. The destruction of the poor is their poverty.
16 Mshahara wa watenda haki huelekea kwenye uzima; manufaa ya waovu huelekea dhambini.
The labor of the righteous leads to life. The increase of the wicked leads to sin.
17 Kuna njia kwenda kwenye uzima kwa yule anayefuata maongozo, bali anayekataa maonyo hupotea.
He is in the way of life who heeds correction, but he who forsakes reproof leads others astray.
18 Yeye afichaye chuki anamidomo ya uongo, na yeye anayesambaza kashfa ni mpumbavu.
He who hides hatred has lying lips. He who utters a slander is a fool.
19 Katika maneno mengi, hapakosi uhalifu, bali aliyemwangalifu katika usemi wake ni mwenye busara.
In the multitude of words there is no lack of disobedience, but he who restrains his lips does wisely.
20 Ulimi wa yule atendaye haki ni fedha safi; kuna thamani ndogo katika moyo wa mbaya.
The tongue of the righteous is like choice silver. The heart of the wicked is of little worth.
21 Midomo ya yule atendaye haki huwastawisha wengi, bali wapumbavu hufa kwa sababu ya kukosa akili.
The lips of the righteous feed many, but the foolish die for lack of understanding.
22 Zawadi njema za Yehova huleta utajiri na haweki maumivu ndani yake.
Jehovah's blessing brings wealth, and he adds no trouble to it.
23 Uovu ni mchezo achezao mpumbavu, bali hekima ni furaha kwa mtu mwenye ufahamu.
It is a fool's pleasure to do wickedness, but wisdom is a man of understanding's pleasure.
24 Hofu ya mwenye uovu humkumba ghafla, bali shauku ya mwenye haki itatimizwa.
What the wicked fear, will overtake them, but the desire of the righteous will be granted.
25 Waovu ni kama dhoruba inayopita, na hawapo tena, bali mwenye haki ni msingi unaodumu milele.
When the whirlwind passes, the wicked is no more; but the righteous stand firm forever.
26 Kama siki kwenye meno na moshi kwenye macho, ndivyo alivyo mvivu kwa wale waliomtuma.
As vinegar to the teeth, and as smoke to the eyes, so is the sluggard to those who send him.
27 Hofu ya Yehova huongeza maisha, bali miaka ya waovu itakuwa mifupi.
The fear of Jehovah prolongs days, but the years of the wicked shall be shortened.
28 Matumaini ya wale watendao haki ndiyo furaha yao, bali miaka ya waovu itakuwa mifupi.
The prospect of the righteous is joy, but the hope of the wicked will perish.
29 Njia ya Yehova huwalinda wale wenye uadilifu, bali kwa waovu ni uhalibifu.
The way of Jehovah is a stronghold to the upright, but it is a destruction to evildoers.
30 Wale watendao haki hawataondolewa, bali waovu hawatabaki katika nchi.
The righteous will never be removed, but the wicked will not dwell in the land.
31 Katika kinywa cha wale watendao haki hutoka tunda la hekima, bali ulimi wa kupotosha utakatwa.
The mouth of the righteous brings forth wisdom, but the perverse tongue will be cut off.
32 Midomo ya wale watendao mema huyajua yanayokubalika, bali kinywa cha waovu, huyajua yanayopotosha.
The lips of the righteous know what is acceptable, but the mouth of the wicked is perverse.

< Mithali 10 >