< Filemoni 1 >

1 Paulo, mfungwa wa Kristo Yesu, na ndugu Timotheo kwa Filemoni, mpendwa rafiki yetu na mtenda kazi pamoja nasi,
Paul, prisonnier de Jésus Christ, et le frère Timothée, à Philémon, le bien-aimé et notre compagnon d’œuvre,
2 na kwa Afia dada yetu, na kwa Arkipas askari mwenzetu, na kwa kanisa lile linalokutana nyumbani kwako.
et à la sœur Apphie, et à Archippe notre compagnon d’armes, et à l’assemblée qui [se réunit] dans ta maison:
3 Neema iwe kwenu na amani itokayo kwa Mungu Baba yetu na kwa Bwana Yesu Kristo.
Grâce et paix à vous, de la part de Dieu notre Père et du seigneur Jésus Christ!
4 Wakati wote namshukuru Mungu. Ninakutaja katika maombi yangu.
Je rends grâces à mon Dieu, faisant toujours mention de toi dans mes prières,
5 Nimesikia upendo na imani uliyonayo katika Bwana Yesu na kwa ajili ya waumini wote.
apprenant l’amour et la foi que tu as envers le seigneur Jésus et pour tous les saints;
6 Ninaomba kwamba ushirika wa imani yenu iwe na ufanisi katika ujuzi wa kila jambo jema lililoko kati yetu katika Kristo.
en sorte que ta communion dans la foi opère en reconnaissant tout le bien qui est en nous à l’égard du christ Jésus.
7 Kwa kuwa nimekuwa na furaha na faraja kwa sababu ya upendo wako, kwa sababu mioyo ya waumini imekuwa ikitulizwa nawe, ndugu.
Car nous avons une grande joie et une grande consolation dans ton amour, parce que les entrailles des saints sont rafraîchies par toi, frère.
8 Kwa hiyo, ingawa nina ujasiri wote katika Kristo kukuamuru wewe kufanya kile unachoweza kufanya,
C’est pourquoi, tout en ayant une grande liberté en Christ de te commander ce qui convient,
9 lakini kwa sababu ya upendo, badala yake nakusihi - mimi, Paulo niliye mzee, na sasa ni mfungwa kwa ajili ya Kristo Yesu.
– à cause de l’amour, je te prie plutôt, étant tel que je suis, Paul, un vieillard, et maintenant aussi prisonnier de Jésus Christ,
10 Ninakusihi kuhusu mwanangu Onesmo, niliyemzaa katika vifungo vyangu.
je te prie pour mon enfant que j’ai engendré dans les liens, Onésime,
11 Kwa kuwa mwanzoni hakukufaa, lakini sasa anakufaa wewe na mimi.
qui t’a été autrefois inutile, mais qui maintenant est utile à toi et à moi,
12 Nimemtuma- yeye ambaye ni wa moyo wangu hasa - kurudi kwako.
lequel je t’ai renvoyé, – lui, mes propres entrailles.
13 Nataraji angeendelea kubaki pamoja nami, ili anitumikie badala yako, wakati niwako kifungoni kwa ajili ya injili.
Moi, j’aurais voulu le retenir auprès de moi, afin qu’il me serve pour toi dans les liens de l’évangile;
14 Lakini sikutaka kufanya jambo lolote bila ruhusa yako. Nilifanya hivi ili kwamba jambo lolote zuri lisifanyike kwa sababu nilikulazimisha, bali kwa sababu ulipenda mwenyewe kulitenda.
mais je n’ai rien voulu faire sans ton avis, afin que le bien que tu fais ne soit pas l’effet de la contrainte, mais qu’il soit volontaire.
15 Labda ni sababu alitengwa nawe kwa muda, ilikuwa hivyo ili uwe pamoja naye milele. (aiōnios g166)
Car c’est peut-être pour cette raison qu’il a été séparé [de toi] pour un temps, afin que tu le possèdes pour toujours, (aiōnios g166)
16 Ili kwamba asiwe tena mtumwa, bali bora zaidi ya mtumwa, kama ndugu mpendwa, hasa kwangu, na zaidi sana kwako, katika mwili na katika Bwana.
non plus comme un esclave, mais au-dessus d’un esclave, comme un frère bien-aimé, spécialement de moi, et combien plus de toi, soit dans la chair, soit dans le Seigneur.
17 Na hivyo kama wanichukulia mimi mshirika, mpokee kama ambavyo ungenipokea mimi.
Si donc tu me tiens pour associé [à toi], reçois-le comme moi-même;
18 Lakini kama amekukosea jambo lolote, au unamdai kitu chochote, kidai hicho kutoka kwangu.
mais, s’il t’a fait quelque tort ou s’il te doit quelque chose, mets-le-moi en compte.
19 Mimi Paulo, ninaandika kwa mkono wangu mwenyewe: mimi nitakulipa. Sisemi kwako kwamba nakudai maisha yako hasa.
Moi, Paul, je l’ai écrit de ma propre main; moi, je paierai, pour ne pas te dire que tu te dois toi-même aussi à moi.
20 Naam ndugu, acha nipate furaha ya Bwana toka kwako: uburudishe moyo wangu katika Kristo.
Oui, frère, que moi, je tire ce profit de toi dans le Seigneur: rafraîchis mes entrailles en Christ.
21 Nikiwa na imani kuhusu utii wako, nakuandikia nikijua kwamba utafanya hata zaidi ya vile ninavyokuomba.
Ayant de la confiance dans ton obéissance, je t’ai écrit, sachant que tu feras même plus que je ne dis.
22 Wakati huo huo andaa chumba cha wageni kwa ajili yangu, kwa kuwa ninatumaini kupitia maombi yako nitakutembelea hivi karibuni.
Mais en même temps, prépare-moi aussi un logement, car j’espère que, par vos prières, je vous serai donné.
23 Epafra, mfungwa mwenzangu katika Kristo Yesu anakusalimu,
Épaphras, mon compagnon de captivité dans le christ Jésus,
24 na kama afanyavyo Marko, Aristarko, Dema, Luka, watendakazi pamoja nami.
Marc, Aristarque, Démas, Luc, mes compagnons d’œuvre, te saluent.
25 Neema ya Bwana Yesu Kristo iwe pamoja na roho yako. Amina.
Que la grâce de notre seigneur Jésus Christ soit avec votre esprit!

< Filemoni 1 >