< Obadia 1 >

1 Maono ya Obadia. Bwana MUNGU asema hivi juu ya Edomu Tumesikia habari kutoka kwa Bwana, na mjumbe ametumwa kati ya mataifa, akisema, Inukeni! Tuinuke dhidi yake kwa vita!”
The vision of Obadiah. Thus saith the Lord GOD concerning Edom: We have heard tidings from the LORD, and an ambassador is sent among the nations, [saying], Arise ye, and let us rise up against her in battle.
2 Tazama, nitawafanya wadogo kati ya mataifa, mutadharauliwa sana.
Behold, I have made thee small among the nations: thou art greatly despised.
3 Kiburi cha moyo wako kimekudanganya wewe, wewe ambaye unishi katika makaburi ya miamba, katika nyumba yako ya juu; asemaye moyoni mwako, 'Ni nani atakayenishusha mimi chini?'
The pride of thine heart hath deceived thee, O thou that dwellest in the clefts of the rock, whose habitation is high; that saith in his heart, Who shall bring me down to the ground?
4 Ingawa unasimama juu kama tai na ingawa kiota chako huwekwa kati ya nyota, nitakushusha chini kutoka huko, asema Yahweh.
Though thou mount on high as the eagle, and though thy nest be set among the stars, I will bring thee down from thence, saith the LORD.
5 Kama wezi walikuja kwako, ikiwa wanyang'anyi wangekujilia usiku (jinsi ungekatilwa mbali!), Wasingeweza kuiba vya kuwatosha? Ikiwa wakusanya zabibu wangekujilia, wasingeacha mavuno?
If thieves came to thee, if robbers by night, (how art thou cut off!) would they not steal till they had enough? if grapegatherers came to thee, would they not leave some gleaning grapes?
6 Jinsi Esau amekwisha kupigwa, na hazina zake zilizofichwa zimewekwa nje!
How are [the things of] Esau searched out! how are his hidden treasures sought up!
7 Watu wote wa ushirikiano wako watakupeleka katika njiani ya hadi mpakani. Watu waliokuwa na amani pamoja nawe wamekudanganya, na kukushinda. Wale wanaokula mkate wako wameweka mtego chini yako. Hakuna uelewa ndani yake.
All the men of thy confederacy have brought thee on thy way, even to the border: the men that were at peace with thee have deceived thee, and prevailed against thee; [they that eat] thy bread lay a snare under thee: there is none understanding in him.
8 Je! Sikuweza siku hiyo, asema Bwana, kuwaangamiza watu wenye hekima kutoka Edomu na kuelewa kutoka mlima wa Esau?
Shall I not in that day, saith the LORD, destroy the wise men out of Edom, and understanding out of the mount of Esau?
9 Mashujaa wako watafadhaika, Temani, ili kila mtu akatiliwe mbali kutoka mlima wa Esau kwa kuuawa.
And thy mighty men, O Teman, shall be dismayed, to the end that every one may be cut off from the mount of Esau by slaughter.
10 Kwa sababu ya ukatili uliofanywa kwa ndugu yako Yakobo, utafunikwa na aibu, nawe utakatiliwa mbali milele.
For the violence done to thy brother Jacob shame shall cover thee, and thou shalt be cut off for ever.
11 Siku ile ulikuwa umesimama, siku wageni walichukua mali zake, na waliokuwa wageni katika malango yake, na kupiga kura kwa Yerusalemu, wewe ulikuwa kama mmoja wao.
In the day that thou stoodest on the other side, in the day that strangers carried away his substance, and foreigners entered into his gates, and cast lots upon Jerusalem, even thou wast as one of them.
12 Lakini usifurahi siku ya ndugu yako, siku ya msiba wake, wala usifurahi juu ya watu wa Yuda siku ya uharibifu wao; msijisifu siku ya dhiki yao.
But look not thou on the day of thy brother in the day of his disaster, and rejoice not over the children of Judah in the day of their destruction; neither speak proudly in the day of distress.
13 Usiingie mlango wa watu wangu siku ya msiba wao; usifurahi juu ya taabu yao siku ya msiba wao, wala msipotee utajiri wao siku ya uharibifu wao.
Enter not into the gate of my people in the day of their calamity; yea, look not thou on their affliction in the day of their calamity, neither lay ye [hands] on their substance in the day of their calamity.
14 Usisimama kwenye njia panda, ili kuwakatilia mbali wakimbizi wake na usiwatoe waathirika wake katika siku ya dhiki.
And stand thou not in the crossway, to cut off those of his that escape; and deliver not up those of his that remain in the day of distress.
15 Kwa maana siku ya Bwana iko karibu na mataifa yote. Kama ulivyofanya, itafanyika kwako; matendo yako yatarudi juu ya kichwa chako mwenyewe.
For the day of the LORD is near upon all the nations: as thou hast done, it shall be done unto thee; thy dealing shall return upon thine own head.
16 Kwa vile mlivyokunywa katika mlima wangu mtakatifu, ndivyo mataifa yote yatakavyo kunywa daima. Watakunywa na kumeza na itakuwa kana kwamba hawakuwepo kabisa.
For as ye have drunk upon my holy mountain, so shall all the nations drink continually, yea, they shall drink, and swallow down, and shall be as though they had not been.
17 Lakini katika Mlima Sayuni kutakuwa na wale waliookoka na watakuwa watakatifu; na nyumba ya Yakobo watamiliki miliki zao.
But in mount Zion there shall be those that escape, and it shall be holy; and the house of Jacob shall possess their possessions.
18 Nyumba ya Yakobo itakuwa moto, na nyumba ya Yusufu ni mwali wa moto, na nyumba ya Esau itakuwa mabua makavu, nao watawaunguza, na kuwateketeza. Hakutakuwa na waathirika kwa nyumba ya Esau, kwa kuwa Bwana amesema.
And the house of Jacob shall be a fire, and the house of Joseph a flame, and the house of Esau for stubble, and they shall burn among them, and devour them: and there shall not be any remaining to the house of Esau; for the LORD hath spoken it.
19 Wote kutoka Negebu watamiliki mlima wa Esau na wale wa Shepela watamiliki nchi ya Wafilisti. Wao wataimiliki nchi ya Efraimu na nchi ya Samaria; na Benyamini atamiliki Gileadi.
And they of the South shall possess the mount of Esau; and they of the lowland the Philistines and they shall possess the field of Ephraim, and the field of Samaria: and Benjamin [shall possess] Gilead.
20 Wahamiaji wa jeshi hili la watu wa Israeli watamiliki ardhi ya Kanaani mpaka Sarepta. Wahamiaji wa Yerusalemu, waliopo Sefaradi, wataimiliki miji ya Negebu.
And the captivity of this host of the children of Israel, which are [among] the Canaanites, [shall possess] even unto Zarephath; and the captivity of Jerusalem, which is in Sepharad, shall possess the cities of the South.
21 Waokoaji watakwenda hadi juu ya Mlima Sayuni kutawala nchi ya vilima ya Esau, na ufalme utakuwa wa Bwana.
And saviours shall come up on mount Zion to judge the mount of Esau; and the kingdom shall be the LORD’S.

< Obadia 1 >