< Hesabu 34 >

1 BWANA akanena na Musa akasema,
Und Jehovah redete zu Mose und sprach:
2 “Waamuru watu wa Israeli na uwaambie, 'Mtakapoingia katika nchi ya Kanaani, nchi ambayo itakuwa mali yenu, nchi ya Kanaani na mipaka yake, mpaka wenu wa kusini utaendelea kutoka nyika ya Sini hadi mpaka wa Edomu.
Gebiete den Söhnen Israels und sprich zu ihnen: So ihr in das Land Kanaan kommet, so sei das das Land, das euch zum Erbe fällt, das Land Kanaan nach seinen Grenzen.
3 Mwisho wa mpaka wa kusini utakuwa mwisho wa bahari ya chumvi kuelekea mashariki.
Und die Ecke im Mittag soll euch sein von der Wüste Zin an bei der Seite Edom, eure Mittagsgrenze soll sein vom Ende des Salzmeeres nach Osten zu.
4 Mpaka wenu utageukia kusini kutoka mlima kuelekea Akrabimu na kupitia nyika ya Sini. na kutokea huko utaelelkea kusini mwa Kadeshi Barinea na kuelekea Hazari Adari mpaka Azimoni.
Und es wendet sich euch die Grenze herum mittäglich von Maaleh Akkrabin und zieht sich nach Zin hinüber; und ihre Ausgänge seien mittäglich von Kadesch Barnea und gehen aus nach Chazar Addar und ziehen sich hinüber nach Azmon;
5 Kutoka huko, mpaka utageuka kutoka Azimoni kuelekea kijito cha Misri na kukifuata mpaka baharini.
Und von Azmon wende sich die Grenze herum nach dem Bache Ägyptens, und ihre Ausgänge seien nach dem Meere hin.
6 Mpaka wa Magharibi utakuwa pwani ya bahari kuu. Huu ndio utakuwa mpaka wenuwa Magharibi.
Und die Grenze nach dem Meere zu soll euch sein das große Meer und seine Grenze. Dies soll euch die Grenze nach dem Meere zu sein.
7 Mpaka wenu wa kaskazini utaanzia kwenye bahari kuu hadi Mlima Hori,
Und die Grenze nach Mitternacht soll euch diese sein: Von dem großen Meere sollt ihr euch abmessen bis zum Berge Hor;
8 kisha kutoka Mlima Hori hadi Lebo Hamathi, kisha Zedadi.
Vom Berge Hor sollt ihr abmessen bis man gen Hamath kommt, und sollen sein die Ausgänge der Grenze bis nach Zedad hin.
9 Mpaka utaendelea hadi Zifroni na kuishia Hazari Enani. Huu ndio utakuwa mpaka wenu wa kaskazini.
Und die Grenze gehe dann aus gen Siphron und ihre Ausgänge seien Chazar Enan. Dies soll euch die Grenze nach Mitternacht sein.
10 Kisha mtaweka alama za mpaka wenu wa mashariki ambao utaanzia Hazari Enani kuelekea kusini Shefamu.
Und messet ab für euch als Grenze gegen Osten von Chazar Enan bis Schepham.
11 Kisha mpaka wa kusini utaendelea kutoka Shefamu hadi Ribla, upande wa masharikia mwa Aini. Mpaka utaedelea upande huo wa mashariki hadi upande wa mashariki wa bahari ya Kinerethi.
Und die Grenze gehe hinab von Schepham nach Riblah östlich von Ain und die Grenze gehe hinab und stoße auf das Ufer des Meeres Kinnereth gegen den Osten.
12 Kisha mpaka utaendelea kuelekea kusini hadi mto Yorodani na hadi bahari ya chumvi. Hii ndiyo itakuwa nchi yenu, kwa kuifuata mipaka yake yote inayozunguka.'”
Und die Grenze gehe hinab nach dem Jordan und ihre Ausgänge seien das Salzmeer. Das sei euch das Land nach seinen Grenzen ringsumher.
13 Kisha Musa akawaamuru watu wa Israeli akasema, “Hii ndiyo nchi ambayo mtaipokes kwa kura, ambayo BWANA ameamuru kuwapa wale makabila tisa na nusu.
Und Mose gebot den Söhnen Israels und sprach: Dies ist das Land, das ihr unter euch durch das Los zum Erbe verteilen sollt, das Jehovah gebot zu geben den neun Stämmen und dem halben Stamm.
14 Kabila ya uzao wa Reubeni, kwa kufuata jinsi walivyopewa urithi kwa jamaa ya kabila yao, na uzao wa kabila la Gadi, kwa kufuata jinsi walivyopewa urithi kwa jamaa ya kabila yao, na nusu ya Manase wamepata ardhi yao.
Denn es haben genommen der Stamm der Söhne des Rubeniten nach dem Hause ihrer Väter und der Stamm der Söhne des Gaditen nach dem Hause ihrer Väter und der halbe Stamm Menaschehs - sie haben ihr Erbe genommen.
15 Wale makabila mawili na nusu wameshapata mgawo wao ng'ambo ya mto Yorodani upande wa mashariki, kuelekea kule linakotokea jua.”
Die zwei Stämme und der halbe Stamm haben ihr Erbe genommen diesseits des Jordans bei Jericho auf der Ostseite gegen den Aufgang.
16 BWANA akanena na Musa akasema,
Und Jehovah redete zu Mose und sprach:
17 “Haya ndiyo majinaya watu watakaoigawa ardhi kwa ajili ya urithi wao: Eliazari kuhani na Joshua mwana wa Nuni.
Das sind die Namen der Männer, welche euch das Land zum Erbe verteilen sollen: Eleasar, der Priester, und Jehoschua, der Sohn Nuns.
18 Mtachagua kiongozi mmoja toka kila kabila ili kuigawa ardhi kwa koo zao.
Und je einen Fürsten von dem Stamme sollt ihr nehmen, das Land als Erbe zu verteilen.
19 Haya ndiyo majina ya wanaume: Kutoka kabila la Yuda, Kalebu mwana wa Yefune.
Und das sind die Namen der Männer: Vom Stamme Judah Kaleb, der Sohn Jephunnehs.
20 Kutoka kwenye kabila la uzao wa Simeoni, Shemueli mwana wa Amihudi.
Und vom Stamme der Söhne Schimeons Schemuel, Sohn Ammihuds.
21 Kutoka kabila la Benjamini, Elidadi mwana wa Kisloni.
Vom Stamme Benjamins Elidad, der Sohn Chislons.
22 Kiongozi kutoka kabila la uzao wa Dani, Buki mwana wa Jogili.
Und vom Stamme der Söhne Dans ein Fürst, Bukki, Joglis Sohn.
23 Kiongozi kutoka uzao wa Yusufu, kwenye kabila la Manase, Hannieli mwana wa Efodi.
Für die Söhne Josephs vom Stamme der Söhne Menaschehs ein Fürst, Hanniel, Ephods Sohn.
24 Kiongozi kutoka kwenye kabila la uzao wa Efraimu, Kemueli mwana wa Shiftani.
Und vom Stamme der Söhne Ephraims ein Fürst, Kemuel, ein Sohn Schiphtans.
25 Kiongozi kutoka kabila la uzao wa Zabuloni, Elizafani mwana wa Parinaki.
Und vom Stamme der Söhne Sebuluns ein Fürst, Elizaphan, Parnachs Sohn.
26 Kiongozi kutoka kwenye kabila la uzao wa Isakari, Palitieli mwana wa Azzani.
Und vom Stamme der Söhne Issaschars ein Fürst, Paltiel, Assans Sohn.
27 Kiongozi kutoka kabila la uzao wa Asheri, Ahihudi mwana wa Shelomi.
Und vom Stamme der Söhne Aschers, ein Fürst, Achihud, Schelomis Sohn.
28 Kiongozi kutoka kabila la uzao wa Naftali, Pedaheli mwana wa Amihudi.”
Und vom Stamme der Söhne Naphthalis ein Fürst, Pedahel, der Sohn Ammihuds.
29 BWANA aliwaamuru wanaume hawa kuigawa nchi ya Kanaani na kuwapa kila kabla sehemu yao.
Diese sind es, denen Jehovah gebot, den Söhnen Israels das Erbe zu verteilen im Lande Kanaan.

< Hesabu 34 >