< Hesabu 33 >

1 Hizi ndizo safari za wana wa Israeli hapo walipotoka katika nchi ya Misri pamoja na makundi yao ya kijeshi chini ya uongozi wa Musa na Haruni.
Estas fueron las estaciones de los hijos de Israel, cuando salieron de Egipto divididos en escuadrones bajo el mando de Moisés y Aarón.
2 Musa aliandika maeneo yote tangu walipoondoka mpaka walipofika, kama alivyoamuriwa na BWANA. Hizi ndizo safari zao kama kutoka kwao kulivyokuwa kwa kila walipotoka.
Moisés apuntó, por orden de Yahvé, los lugares de donde partieron, conforme a sus estaciones. He aquí sus estaciones según sus partidas.
3 Mwezi wa kwanza walisafiri kutoka Ramesi, waliondoka siku ya kumi na tano. Asubuhi siku iliyofuata baada ya Pasaka, Wana wa Israeli waliondoka wazi wazi, mbele ya machoya Wamisri wote.
Partieron de Ramesés, el primer mes el día quince del mes primero. Al día siguiente a la Pascua salieron los hijos de Israel con mano alzada, a la vista de todos los egipcios,
4 Hii ilitokea wakati Wamisiri walipokuwa wakizika wazaliwa wao wa kwanza, ambao BWANA alikuwa amewaua miongoni mwao, kwa kuwa pia alikuwa ameiadhibu miungu yao.
mientras los egipcios sepultaban a los que Yahvé había muerto de entre ellos, todos los primogénitos, y Yahvé hacía justicia también contra los dioses de ellos.
5 Wana wa Israeli walisafiri kutoka Ramesi na kuweka kambi
Partieron, pues, los hijos de Israel de Ramesés, y acamparon en Sucot.
6 Sukothi. Walisafiri toka Sukothi na kuweka kambi Ethamu, mwisho wa nyika.
Partieron de Sucot, y acamparon en Etam, que está en la frontera del desierto.
7 Wakasafiri kutoka Ethamu wakarudi mpaka Pi-Hahirothi, ambayo inaikabili Baali Zephoni, ambapo waliweka kambi kuikabili Migidoli
Partieron de Etam, y dieron una vuelta hacia Fihahirot, que está frente a Baalsefón, y acamparon delante de Migdol.
8 Kisha wakasafiri toka mkabala wa Pi-Hairothi na kupita katikati ya bahari kuelekea nyikani. Wakasafiri safari ya siku tatu katika nyika ya Ethamu na kuweka kambi Mara.
Partieron de Fihahirot, y pasaron por medio del mar hacia el desierto, y después de tres días de camino por el desierto de Etam, acamparon en Mará.
9 Wakasafiri kutoka Mara kufika Elimu. Pale Elimu kulikuwa na chemichemi kumi na mbili za maji na miti sabini ya mitende. hapo ndipo walipoweka kambi.
Partieron de Mará, y vinieron a Elim. En Elim había doce fuentes de agua y setenta palmas; allí acamparon.
10 Walisafiri kutoka Elimu na kuweka kambi karibu na Bahari ya Shamu.
Partieron de Elim y acamparon junto al Mar Rojo.
11 Walisafiri kutoka Bahari ya Shamu na kuweka kambi katika nyika ya Sini.
Partieron del Mar Rojo y acamparon en el desierto de Sin.
12 Walisafiri kutoka nyika ya Sini na kuweka kambi Dofka.
Partieron del desierto de Sin y acamparon en Dafcá.
13 Wakasafiri kutoka Dofka na kuweka kambi Alushi.
Partieron de Dafcá y acamparon en Alus.
14 Wakasafiri kutoka Alushi na kuweka kambi Refidimu, ambapo watu walikosa maji ya kunywa.
Partieron de Alus y acamparon en Rafidim, donde faltó al pueblo agua para beber.
15 Walisafiri kutoka Refidimu na kuweka kambi kwenye nyika ya Sinai.
Partieron de Rafidim y acamparon en el desierto del Sinaí.
16 Walisafiri kutoka nyika ya Sinai na kuweka kambi Kibrothi Hataava.
Partieron del desierto del Sinaí y acamparon en Kibrot-Hataavá.
17 Walisafiri kutoka Kibrothi Hataava na kuweka kambi Hazerothi.
Partieron de Kibrot-Hataavá y acamparon en Haserot.
18 Walisafiri kutoka Hazerothi na kuweka kambi Rithima.
Partieron de Haserot y acamparon en Ritma.
19 Walisafiri kutoka Rithima na kuweka kambi Rimoni Perezi.
Partieron de Ritma y acamparon en Rimonfares.
20 Walisafiri kutoka Rimoni Perezi na kuweka kambi Libna.
Partieron de Rimonfares y acamparon en Libná.
21 Walisafiri kutoka Libna na kuweka kambi Risa.
Partieron de Libná y acamparon en Risa.
22 Walisafiri kutoka Risa na kuweka kambi Kehelatha.
Partieron de Risa y acamparon en Quehelata.
23 Walisafiri kutoka Kehelatha na kuweka kambi kwenye Mlima Sheferi.
Partieron de Quehelata y acamparon en el monte Séfer.
24 Walisafiri kutoka Mlima Sheferi na kuweka kambi Harada.
Partieron del monte Séfer y acamparon en Haradá.
25 Walisafiri kutoka Harada na kuweka kambi Makelothi.
Partieron de Haradá y acamparon en Maquelot.
26 Walisafiri kutoka Makelothi na kuweka kambi Tahathi.
Partieron de Maquelot y acamparon en Táhat.
27 Walisafiri kutoka Ttahalathi na kuweka kambi Tera.
Partieron de Táhat y acamparon en Tare.
28 Walisafiri kutokaTera na kuweka kambi Mithika.
Partieron de Tare y acamparon en Mitcá.
29 Walisafiri kutoka Mithika na kuweka kambi Hashimona.
Partieron de Mitcá y acamparon en Hasmoná.
30 Walisafiri kutoka Hashimona na kuweka kambi Moserothi.
Partieron de Hasmoná y acamparon en Moserot.
31 Walisafiri kutoka Moserothi na kuweka kambi Bene Jaakani.
Partieron de Moserot y acamparon en, Bené-Yaacán.
32 Walisafiri kutoka Bene Jaakani na kuweka kambi Hori Hagidigadi.
Partieron de Bené-Yaacán y acamparon en Hor-Hagadgad.
33 Walisafiri kutoka Hori Hagidigadi na kuweka kambi Jotibatha.
Partieron de Hor-Hagadgad y acamparon en Jotbata.
34 Walisafiri kutoka Jotibatha na kuweka kambi Abrona.
Partieron de Jotbata y acamparon en Abroná.
35 Walisafiri kutoka Abrona na kuweka kambi Ezioni Geberi.
Partieron de Abroná y acamparon en Esionguéber.
36 Walisafiri toka Ezioini Geberi na kuweka kambi katika nyika ya Sini kule Kadeshi.
Partieron de Esionguéber y acamparon en el desierto de Sin, que es Cades.
37 Walisafiri kutoka Kadeshi na kuweka kambi Mlima Hori, Pembezoni mwa nchi ya Edomu.
Partieron de Cades y acamparon en el monte Hor, en la frontera del país de Edom.
38 Hapo ndipo Haruni kuhani alipoenda kwenye Mlima Hori kwa amri ya BWANA na kufa kule mwaka wa arobaini bada ya Wisraeli kutoka katika nchi ya Misri, katika siku ya kwanza ya mwezi wa tano.
Y por orden de Yahvé subió el sacerdote Aarón al monte Hor, y allí murió, a los cuarenta años de la salida de los hijos de Israel de la tierra de Egipto, el primer día del quinto mes.
39 Haruni alikuwa na umri wa mika 123 alipokufa pale juu ya Mlima Hori.
Tenía Aarón ciento veinte y tres años cuando murió en el monte Hor.
40 Wakanaani, mfalme wa Aradi, ambao waliishi kusini mwa nyika katika nchi ya Kanaani, walisikia juu ya ujio wa wana wa Israeli.
Entonces el cananeo, el rey de Arad, que habitaba en el Négueb, en el país de Canaán, supo que venían los hijos de Israel.
41 Walisafiri kutika Mlima Hori n a kuweka kambi Zalimona.
Partieron del monte Hor y acamparon en Salmoná.
42 Walisafiri kutoka Zalimona na kuweka kambi Punoni.
Partieron de Salmoná y acamparon en Punón.
43 Walisafiri kutoka Punoni na kuweka kambi Obothi.
Partieron de Punón y acamparon en Obot.
44 Walisafiri kutoka Obothi na kuweka kambi Abarimu, katika mpaka wa Moabu.
Partieron de Obot y acamparon en Iyé-Abarim, en los confines de Moab.
45 Walisafiri kutoka Abarimu na kuweka kambi Diboni Gadi.
Partieron de Iyim y acamparon en Dibón-Gad.
46 Walisafiri kutoka Diboni Gadi na kuweka kambi Alimoni Diblathaimu.
Partieron de Dibón-Gad y acamparon en Almón-Diblataim.
47 Walisafiri kutoka Alimoni Diblathaimu na kuweka kambi kwenye milima ya Abarimu mkabala na Nebo.
Partieron de Almón-Diblataim y acamparon en las montañas de Abarim, frente al Nebo.
48 Walisafiri kutoka mlima wa Abarimuna kuweka kambi kwenye nyanda za Moabu karibu na Yorodani huko Yeriko.
Partieron de las montañas de Abarim, y acamparon en las campiñas de Moab, junto al Jordán, frente a Jericó.
49 Waliweka kambi karibu na Yorodani, kutoka Bethi Jeshimothi mpaka Abeli Shitimu katika nyanda za Moabu.
Acamparon a lo largo del Jordán, desde Bet- Jesimot hasta Abel-Sitim, en los llanos de Moab.
50 Hapo BWANA alinenana Musa katika nyanda za Moabu karibu na Yorodani kule Yeriko akasema,
Yahvé habló a Moisés en las campiñas de Moab, junto al Jordán, frente a Jericó, diciendo:
51 “Nena na wana wa Israeli uwaambie. 'Mtakapovuka mto Yorodani kuingia Kanaani,
“Habla a los hijos de Israel y diles: Cuando después de pasar el Jordán entrareis en el país de Canaán,
52 ndipo mtakapowafukuza wenyeji wote mbele yenu. Mtaziharibu sanamu zote za kuchongwa. Mtaziharibu sanamu zao za kusubu na kuharibu mahali pao pote palipoinuka.
arrojaréis de delante de vosotros a todos los habitantes del país, y destruiréis todos sus simulacros; destruiréis también todas sus imágenes fundidas y devastaréis todos sus lugares altos.
53 Mtachukua hiyo ardhi iwe mali yenu na muishi ndani yake, kwa sababu nimewapeni hiyo nchi iwe mali yenu.
Y tomaréis posesión del país, y en él habitaréis, pues a vosotros os he dado esta tierra para que la poseáis.
54 Mtairithi hiyo nchi kwa kupiga kura, kwa kufuata kila ukoo. Kwa zile koo kubwa kubwa mtawapa sehemu kubwa ya ardhi, na kwa zile koo ndogo ndogo mtawapa sehemu ndogo ya ardhi. Kura itakapoanguka kwenye kila ukoo, hiyo ardhi itakuwa mali yake. Mtairithi ardhi kufuata ukoo wa kabilla la jamaa zenu.
Os repartiréis la tierra por suertes con arreglo a vuestras familias; a una grande daréis mayor herencia, y a una pequeña daréis una herencia más pequeña. Cada una tendrá la herencia que le tocare en suerte. Haréis la repartición con arreglo a las tribus de vuestros padres.
55 Lakini kama hamtawafukuza wenyeji wa nchi hiyo watoke mbele yenu, ndipo wale watu mtakaowaruhusu wakae nanyi watakapokuwa kama sindano machoni mwenu na miiba katika mbavu zenu. Watayafanya maisha yenu yawe magumu katika nchi mnayoishi.
Pero si no arrojareis de delante vosotros a los habitantes del país sucederá que los que de ellos dejareis os serán como espinas en vuestros ojos, y como aguijones en vuestros flancos, y os tratarán como enemigos en la tierra que vais a habitar.
56 Ndipo itakapotokea kuwa kile ambacho Mimi ninakusudia kufanya kwa wale watu, Nitawafanyia pia ninyi'”
Y Yo haré con vosotros eso mismo que tenía resuelto hacer con ellos.”

< Hesabu 33 >