< Hesabu 33 >

1 Hizi ndizo safari za wana wa Israeli hapo walipotoka katika nchi ya Misri pamoja na makundi yao ya kijeshi chini ya uongozi wa Musa na Haruni.
And these are the stages of the children of Israel, as they went out from the land of Egypt with their host by the hand of Moses and Aaron.
2 Musa aliandika maeneo yote tangu walipoondoka mpaka walipofika, kama alivyoamuriwa na BWANA. Hizi ndizo safari zao kama kutoka kwao kulivyokuwa kwa kila walipotoka.
And Moses wrote their removals and their stages, by the word of the Lord: and these are the stages of their journeying.
3 Mwezi wa kwanza walisafiri kutoka Ramesi, waliondoka siku ya kumi na tano. Asubuhi siku iliyofuata baada ya Pasaka, Wana wa Israeli waliondoka wazi wazi, mbele ya machoya Wamisri wote.
They departed from Ramesses in the first month, on the fifteenth day of the first month; on the day after the passover the children of Israel went forth with a high hand before all the Egyptians.
4 Hii ilitokea wakati Wamisiri walipokuwa wakizika wazaliwa wao wa kwanza, ambao BWANA alikuwa amewaua miongoni mwao, kwa kuwa pia alikuwa ameiadhibu miungu yao.
And the Egyptians buried those that died of them, even all that the Lord struck, every firstborn in the land of Egypt; also the Lord executed vengeance on their gods.
5 Wana wa Israeli walisafiri kutoka Ramesi na kuweka kambi
And the children of Israel departed from Ramesses, and encamped in Socchoth:
6 Sukothi. Walisafiri toka Sukothi na kuweka kambi Ethamu, mwisho wa nyika.
and they departed from Socchoth and encamped in Buthan, which is a part of the wilderness.
7 Wakasafiri kutoka Ethamu wakarudi mpaka Pi-Hahirothi, ambayo inaikabili Baali Zephoni, ambapo waliweka kambi kuikabili Migidoli
And they departed from Buthan and encamped at the mouth of Iroth, which is opposite Beel-sepphon, and encamped opposite Magdol.
8 Kisha wakasafiri toka mkabala wa Pi-Hairothi na kupita katikati ya bahari kuelekea nyikani. Wakasafiri safari ya siku tatu katika nyika ya Ethamu na kuweka kambi Mara.
And they departed from before Iroth, and crossed the middle of the sea into the wilderness; and they went a journey of three days through the wilderness, and encamped in Picriae.
9 Wakasafiri kutoka Mara kufika Elimu. Pale Elimu kulikuwa na chemichemi kumi na mbili za maji na miti sabini ya mitende. hapo ndipo walipoweka kambi.
And they departed from Picriae, and came to Aelim; and in Aelim [were] twelve fountains of water, and seventy palm-trees, and they encamped there by the water.
10 Walisafiri kutoka Elimu na kuweka kambi karibu na Bahari ya Shamu.
And they departed from Aelim, and encamped by the Red Sea.
11 Walisafiri kutoka Bahari ya Shamu na kuweka kambi katika nyika ya Sini.
And they departed from the Red Sea, and encamped in the wilderness of Sin.
12 Walisafiri kutoka nyika ya Sini na kuweka kambi Dofka.
And they departed from the wilderness of Sin, and encamped in Raphaca.
13 Wakasafiri kutoka Dofka na kuweka kambi Alushi.
And they departed from Raphaca, and encamped in Aelus.
14 Wakasafiri kutoka Alushi na kuweka kambi Refidimu, ambapo watu walikosa maji ya kunywa.
And they departed from Aelus, and encamped in Raphidin; and there was no water there for the people to drink.
15 Walisafiri kutoka Refidimu na kuweka kambi kwenye nyika ya Sinai.
And they departed from Raphidin, and encamped in the wilderness of Sina.
16 Walisafiri kutoka nyika ya Sinai na kuweka kambi Kibrothi Hataava.
And they departed from the wilderness of Sina, and encamped at the Graves of Lust.
17 Walisafiri kutoka Kibrothi Hataava na kuweka kambi Hazerothi.
And they departed from the Graves of Lust, and encamped in Aseroth.
18 Walisafiri kutoka Hazerothi na kuweka kambi Rithima.
And they departed from Aseroth, and encamped in Rathama.
19 Walisafiri kutoka Rithima na kuweka kambi Rimoni Perezi.
And they departed from Rathama, and encamped in Remmon Phares.
20 Walisafiri kutoka Rimoni Perezi na kuweka kambi Libna.
And they departed from Remmon Phares, and encamped in Lebona.
21 Walisafiri kutoka Libna na kuweka kambi Risa.
And they departed from Lebona, and encamped in Ressan.
22 Walisafiri kutoka Risa na kuweka kambi Kehelatha.
And they departed from Ressan, and encamped in Makellath.
23 Walisafiri kutoka Kehelatha na kuweka kambi kwenye Mlima Sheferi.
And they departed from Makellath, and encamped in Saphar.
24 Walisafiri kutoka Mlima Sheferi na kuweka kambi Harada.
And they departed from Saphar, and encamped in Charadath.
25 Walisafiri kutoka Harada na kuweka kambi Makelothi.
And they departed from Charadath, and encamped in Makeloth.
26 Walisafiri kutoka Makelothi na kuweka kambi Tahathi.
And they departed from Makeloth, and encamped in Kataath.
27 Walisafiri kutoka Ttahalathi na kuweka kambi Tera.
And they departed from Kataath, and encamped in Tarath.
28 Walisafiri kutokaTera na kuweka kambi Mithika.
And they departed from Tarath, and encamped in Mathecca.
29 Walisafiri kutoka Mithika na kuweka kambi Hashimona.
And they departed from Mathecca, and encamped in Selmona.
30 Walisafiri kutoka Hashimona na kuweka kambi Moserothi.
And they departed from Selmona, and encamped in Masuruth.
31 Walisafiri kutoka Moserothi na kuweka kambi Bene Jaakani.
And they departed from Masuruth, and encamped in Banaea.
32 Walisafiri kutoka Bene Jaakani na kuweka kambi Hori Hagidigadi.
And they departed from Banaea, and encamped in the mountain Gadgad.
33 Walisafiri kutoka Hori Hagidigadi na kuweka kambi Jotibatha.
And they departed from the mountain Gadgad, and encamped in Etebatha.
34 Walisafiri kutoka Jotibatha na kuweka kambi Abrona.
And they departed from Etebatha, and encamped in Ebrona.
35 Walisafiri kutoka Abrona na kuweka kambi Ezioni Geberi.
And they departed from Ebrona, and encamped in Gesion Gaber.
36 Walisafiri toka Ezioini Geberi na kuweka kambi katika nyika ya Sini kule Kadeshi.
And they departed from Gesion Gaber, and encamped in the wilderness of Sin; and they departed from the wilderness of Sin, and encamped in the wilderness of Pharan; this is Cades.
37 Walisafiri kutoka Kadeshi na kuweka kambi Mlima Hori, Pembezoni mwa nchi ya Edomu.
And they departed from Cades, and encamped in mount Or near the land of Edom.
38 Hapo ndipo Haruni kuhani alipoenda kwenye Mlima Hori kwa amri ya BWANA na kufa kule mwaka wa arobaini bada ya Wisraeli kutoka katika nchi ya Misri, katika siku ya kwanza ya mwezi wa tano.
And Aaron the priest went up by the command of the Lord, and died there in the forties year of the departure of the children of Israel from the land of Egypt, in the fifth month, on the first [day] of the month.
39 Haruni alikuwa na umri wa mika 123 alipokufa pale juu ya Mlima Hori.
And Aaron was a hundred and twenty-three years old, when he died in mount Or.
40 Wakanaani, mfalme wa Aradi, ambao waliishi kusini mwa nyika katika nchi ya Kanaani, walisikia juu ya ujio wa wana wa Israeli.
And Arad the Chananitish king (he too lived in the land of Chanaan) having heard when the children of Israel were entering [the land]—
41 Walisafiri kutika Mlima Hori n a kuweka kambi Zalimona.
then they departed from mount Or, and encamped in Selmona.
42 Walisafiri kutoka Zalimona na kuweka kambi Punoni.
And they departed from Selmona, and encamped in Phino.
43 Walisafiri kutoka Punoni na kuweka kambi Obothi.
And they departed from Phino, and encamped in Oboth.
44 Walisafiri kutoka Obothi na kuweka kambi Abarimu, katika mpaka wa Moabu.
And they departed from Oboth, and encamped in Gai, on the other side [Jordan] on the borders of Moab.
45 Walisafiri kutoka Abarimu na kuweka kambi Diboni Gadi.
And they departed from Gai, and encamped in Daebon Gad.
46 Walisafiri kutoka Diboni Gadi na kuweka kambi Alimoni Diblathaimu.
And they departed from Daebon Gad, and encamped in Gelmon Deblathaim.
47 Walisafiri kutoka Alimoni Diblathaimu na kuweka kambi kwenye milima ya Abarimu mkabala na Nebo.
And they departed from Gelmon Deblathaim, and encamped on the mountains of Abarim, over against Nabau.
48 Walisafiri kutoka mlima wa Abarimuna kuweka kambi kwenye nyanda za Moabu karibu na Yorodani huko Yeriko.
And they departed from the mountains of Abarim, and encamped on the west of Moab, at Jordan by Jericho.
49 Waliweka kambi karibu na Yorodani, kutoka Bethi Jeshimothi mpaka Abeli Shitimu katika nyanda za Moabu.
And they encamped by Jordan between Aesimoth, as far as Belsa to the west of Moab.
50 Hapo BWANA alinenana Musa katika nyanda za Moabu karibu na Yorodani kule Yeriko akasema,
And the Lord spoke to Moses at the west of Moab by Jordan at Jericho, saying,
51 “Nena na wana wa Israeli uwaambie. 'Mtakapovuka mto Yorodani kuingia Kanaani,
Speak to the children of Israel, and you shall say to them, You are to pass over Jordan into the land of Chanaan.
52 ndipo mtakapowafukuza wenyeji wote mbele yenu. Mtaziharibu sanamu zote za kuchongwa. Mtaziharibu sanamu zao za kusubu na kuharibu mahali pao pote palipoinuka.
And you shall destroy all that dwell in the land before your face, and you shall abolish their high places, and all their molten images you shall destroy, and you shall demolish all their pillars.
53 Mtachukua hiyo ardhi iwe mali yenu na muishi ndani yake, kwa sababu nimewapeni hiyo nchi iwe mali yenu.
And you shall destroy all the inhabitants of the land, and you shall dwell in it, for I have given their land to you for an inheritance.
54 Mtairithi hiyo nchi kwa kupiga kura, kwa kufuata kila ukoo. Kwa zile koo kubwa kubwa mtawapa sehemu kubwa ya ardhi, na kwa zile koo ndogo ndogo mtawapa sehemu ndogo ya ardhi. Kura itakapoanguka kwenye kila ukoo, hiyo ardhi itakuwa mali yake. Mtairithi ardhi kufuata ukoo wa kabilla la jamaa zenu.
And you shall inherit their land according to your tribes; to the greater number you shall give the larger possession, and to the smaller you shall give the less possession; to whatever [part] a man's name shall go forth [by lot], there shall be his [property]: you shall inherit according to the tribes of your families.
55 Lakini kama hamtawafukuza wenyeji wa nchi hiyo watoke mbele yenu, ndipo wale watu mtakaowaruhusu wakae nanyi watakapokuwa kama sindano machoni mwenu na miiba katika mbavu zenu. Watayafanya maisha yenu yawe magumu katika nchi mnayoishi.
But if you will not destroy the dwellers in the land from before you, then it shall come to pass that whoever of them you shall leave shall be thorns in your eyes, and darts in your sides, and they shall be enemies to you on the land on which you shall dwell;
56 Ndipo itakapotokea kuwa kile ambacho Mimi ninakusudia kufanya kwa wale watu, Nitawafanyia pia ninyi'”
and it shall come to pass that as I had determined to do to them, so I will do to you.

< Hesabu 33 >