< Hesabu 3 >

1 Sasa hii ndiyo historia ya uzao wa Haruni na Musa wakati BWANA aliposema na Musa kwenye mlima Sinai.
Und dies die Geburten Aharons und Moses am Tage, da Jehovah mit Mose redete am Berge Sinai.
2 Majina ya watoto wa Haruni walikuwa Nadabu ambaye ndiyo mtoto wa kwanza, na Abihu, na Eliezeri, na Ithamari.
Und dies sind die Namen der Söhne Aharons: Der Erstgeborene Nadab, und Abihu, Eleasar und Ithamar.
3 Haya ndiyo majina ya wana wa Haruni, makuhani waliokuwa wamepakwa mafuta na kuwekwa wakfu kutumika kama makuhani.
Das sind die Namen der Söhne Aharons, der gesalbten Priester, deren Hand er gefüllt hatte zum Priesterdienst.
4 Lakini Nadabu na Abihu walikufa mbele ya BWANA walipomtolea moto usiokubalika walipokuwa katika nyika ya Sinai. Nadabu na Abihu hawakuwa na watoto, kwa hiyo Eliazari na Ithamari walitumika kama makuhani pamoja na baba yao.
Und Nadab und Abihu starben vor Jehovah, da sie in der Wüste Sinai fremdes Feuer vor Jehovah darbrachten, und hatten keine Söhne. Und Eleasar und Ithamar taten Priesterdienst vor ihrem Vater Aharon.
5 BWANA alinena na Musa, akamwambia,
Und Jehovah redete zu Mose und sprach:
6 “Walete kabila ya Lawi na uwaweke kwa Haruni kuhani ili wamsaidie
Laß den Stamm Levi sich nahen und laß ihn vor Aharon, den Priester stehen, daß sie ihm Dienste tun,
7 Nao lazima wafanye majukumu badala ya Haruni na jumuiya yote mbele ya hema ya kukutania. Lazima watumike hemani.
Und halten seine Hut und die Hut der ganzen Gemeinde vor dem Versammlungszelt, daß sie den Dienst der Wohnung dienen.
8 Watayatunza mapambo ya hema ya kukutania, na watawatumikia makabila ya Israel kwa huduma ya hemani.
Und hüten all die Geräte des Versammlungszeltes und der Hut der Söhne Israels, um zu dienen den Dienst der Wohnung.
9 Uwaweke Walawi kwa Haruni na watoto wake. Nimewatoa kikamilifu ili wamsaidie kuwatumikia watu wa Israel.
Und sollst die Leviten dem Aharon und seinen Söhnen geben. Gegeben, gegeben seien sie ihm von den Söhnen Israels.
10 Umchague Haruni na watoto wake kuwa makuhani, lakini mgeni yeyote atakayekaribia lazima auawe.”
Und Aharon und seine Söhne sollst du mustern, daß sie ihren Priesterdienst halten. Und der Fremde, der sich naht, soll sterben.
11 BWANA alinena na Musa. akamwambia,
Und Jehovah redete zu Mose und sprach:
12 “Tazama, nimewachagua Walawi katika watu wa Israel. Nimefanya hivyo badala ya kuchukua mzaliwa wa kwanza wa kiume wa wana wa Israel. Hawa Walawi ni wangu.
Und Ich, siehe, Ich habe die Leviten aus der Mitte der Söhne Israels genommen, statt aller Erstgeburt, die den Mutterschoß bricht, von den Söhnen Israels, und Mein sollen die Leviten sein;
13 Na hata wazaliwa wa kwanza ni mali yangu. Katika siku ambyo niliwavamia wazaliwa wote wa kwanza wa nchi ya Misri, Niliwatenga wazaliwa wa kwanza wa Israeli kwa ajili yangu, watu na wanyama pia. Ni mali yangu. Mimi ndimi BWANA.”
Denn Mein ist alle Erstgeburt: Am Tage, da Ich alle Erstgeburt im Lande Ägypten schlug, heiligte Ich Mir alle Erstgeburt in Israel vom Menschen bis zum Vieh. Mein sind sie. Ich bin Jehovah.
14 BWANA alinena na Musa katika nyika ya Sinai. Akasema,
Und Jehovah redete zu Mose in der Wüste Sinai und sprach:
15 “Wahesabu uzao wa Lawi katika kila familia, katika nyumba za koo zao. Hesabu kila mume kuanzia mwezi mmoja au zaidi.”
Mustere die Söhne Levis nach dem Hause ihrer Väter, nach ihren Familien, alles Männliche von einem Monat und darüber sollst du sie mustern.
16 Musa aliwahesabu, kufuata maelekezo ya BWANA, kama alivyoamriwa kufanya.
Und Mose musterte sie nach dem Munde Jehovahs, wie Er geboten hatte.
17 Majina ya watoto waLawi yalikuwa Gerishoni, Kohathi, na Merari.
Und das waren die Söhne Levis in ihren Namen: Gerschon und Kohath und Merari.
18 Ukoo uliotokana na watoto wa Gerishoni walikuwa ni Libni na Shimei.
Und das sind die Namen der Söhne Gerschons nach ihren Familien: Libni und Schimei.
19 Ukoo uliotokana na watoto Kohathi walikuwa ni Amramu na, Izihari, Hebroni, na Uzieli.
Und die Söhne Kohaths nach ihren Familien: Amram und Jizhar, Chebron und Ussiel.
20 Ukoo uliotokana na watoto wa Merari walikuwa ni Mahili na Mushi. Hizi ndizo koo za Walawi, zilizoorodheshwa ukoo kwa ukoo.
Und die Söhne Meraris nach ihren Familien: Machli und Muschi. Das sind sie, die Familien Levis nach dem Haus ihrer Väter.
21 Koo za Walibini na Washimei zilitokana na Wagerishoni. Hizi ndizo koo za Wagerishoni.
Für Gerschon ist die Familie des Libniten und die Familie des Schimiten. Das sind sie, die Familien der Gerschoniten.
22 Wanaume wote wenye umri wa mwezi mmoja au zaidi walihesabiwa na kufikia idadi ya 7, 500.
Ihre Gemusterten in ihrer Zahl, alles Männliche von einem Monat und darüber. Ihre Gemusterten waren siebentausendfünfhundert.
23 Koo za Wagerishoni watapanga upande wa magharibi wa hema.
Die Familien der Gerschoniten sollen lagern hinter der Wohnung gegen das Meer hin.
24 Eliasafu mwana wa Laeli ataongoza koo za uzao wa Wagerishoni.
Und Fürst des Vaterhauses der Gerschoniten war Eljasaph, Laels Sohn.
25 Familia ya Gerishoni watalilinda hema la kukutania pamoja na hiyo masikani. Watalilinda hema, kifuniko chake, na lile pazia la lango la hema ya kukutania.
Und die Hut der Söhne Gerschons war im Versammlungszelt die Wohnung und das Zelt, ihre Decke und der Behang an dem Eingang des Versammlungszeltes.
26 Wataulinda ua, lile pazia la kwenye lango—ua unaozunguka mahali patakatifu na madhabahu. Watazilinda kamba za hema ya kukutania na vyote vilivyomo.
Und die Umhänge des Vorhofs und der Behang des Eingangs des Vorhofs, der rings um die Wohnung und den Altar ist, und seine Seile für all den Dienst.
27 Koo zifuatazo zinatokana na Kohathi: ukoo wa Waamrami, ukoo wa Waizihari ukoo wa Wahebroni, na ukoo wa Wauzieli. Koo hizi zinatokana na Wakohathi.
Und für Kohath die Familie des Amramiten, und die Familie des Jizhariten, und die Familie des Chebroniten, und die Familie des Ussieliten. Das sind die Familien des Kohathiten.
28 Wanaume 8, 600 wenye umri wa mwezi mmoja au zaidi walihesabiwa ili kulinda vitu vya BWANA.
In der Zahl alles Männlichen von einem Monat und darüber waren es achttausendsechshundert, welche die Hut des Heiligtums hüteten.
29 Familia ya uzao wa Kohathi watapanga upande wa kusini wa Hema.
Die Familien der Söhne des Kohaths lagerten zur Seite der Wohnung rechts.
30 Elizafani mwana wa Uzieli ndiye atakayeongoza ukoo wa Wakohathi.
Und Fürst des Vaterhauses nach den Familien des Kohathiten war Elizaphan, der Sohn Ussiels.
31 Watalilinda sanduku, meza, vikalishio vya taa, madhabahu, vitu vitakatifu ambvyo hutumika katika huduma yao, pazia, na kazi zote zinazoambatana na hema.
Und ihre Hut war die Lade, und der Tisch und der Leuchter und die Altäre und Geräte des Heiligtums, damit sie Dienst taten, und der Behang und all sein Dienst.
32 Eliazari mwana wa Haruni kuhani atawaongoza wanaume wanaowaongoza Walawi. Atawasimamia wanaume wanaongoza eneo takatifu.
Und Fürst über die Fürsten der Leviten war Eleasar, Sohn Aharons des Priesters, der bestellt war über die Hüter der Hut des Heiligtums.
33 Koo mbili zimetoka kwa Merari: Ukoo wa Mahili na ukoo wa Mushi. Koo hizi zimetokana na Merari,
Für Merari, die Familie der Machliten und die Familie der Muschiten. Das sind sie, Meraris Familien.
34 Wanaume 6, 200 wenye umri wa mwezi mmoja na zaidi walihesabiwa.
Und ihre Gemusterten waren in der Zahl alles Männlichen von einem Monat und darüber sechstausendzweihundert.
35 Zurieli mwana wa Abihaili ataongoza ukoo wa Merari. Hawa watapanga upande wa kaskazini mwa hema.
Und Fürst des Vaterhauses für die Familien des Merariten war Zuriel, Abichails Sohn. Sie lagerten auf der Seite der Wohnung gegen Mitternacht.
36 Uzao wa Merari utatunza mbao za hema, mataruma, nguzo, makalishio, viifaa vya ujenzi na vitu vyote vinavyohusika,
Und das Anvertraute der Hut der Söhne Meraris waren die Bretter der Wohnung und ihre Riegel und ihre Säulen und ihre Unter- sätze, und alle ihre Gerätschaften und ihr Dienst.
37 na nguzo za ua zinazozunguka hema, makalishio, vigingi na kamba zake.
Und die Säulen des Vorhofs ringsum und ihre Untersätze und ihre Pflöcke und ihre Seile.
38 Musa na Haruni na watoto wake watapanga upande wa mashariki wa masikani, mbele ya hema ya kukutania kuelekea mawio ya jua. Wao wataajibika na majukumu ya mahali patakatifu na majukumu ya wana wa Israeli. Mgeni atakayekaribia mahali patakatifu auawe.
Und die, so vor der Wohnung vorn vor dem Versammlungszelt gegen Aufgang lagerten, waren Mose, und Aharon und seine Söhne, welche die Hut des Heiligtums, die Hut der Söhne Israels hüteten; und der Fremde, der naht, soll sterben.
39 Musa na Haruni wakawahesabu wanaume wote wa ukoo wa Walawi walikuwa na umri wa mwezi mmoja na zaidi, kama vile BWANA alivyokuwa ameagiza. Walihesabu wanaume ishirini na mbili elfu.
Alle Gemusterten der Leviten, die Mose und Aharon musterten, nach Jehovahs Munde, nach ihren Familien, alles Männliche von einem Monat und aufwärts, waren es zweiundzwanzigtausend.
40 BWANA alisema na Musa, “Wahesabu wanaume wote ambo ni wazaliwa wa kwanza wa Israeli ambao wana umri wa mwezi mmoja na zaidi. Orodhesha majina yao.
Und Jehovah sprach zu Mose: Mustere alle männliche Erstegeburt für die Söhne Israels von einem Monat und darüber, und nimm die Zahl ihrer Namen auf.
41 Unitwalie walawi kwa ajili yangu badala ya wazaliwa wa kwanza wa Israeli, Mimi ndimi BWANA. Na utwae wanyama wa Walawi badala ya wazaliwa wa kwanza wa wanyama wa uzao wa Israeli,”
Und nimm für Mich die Leviten, Ich bin Jehovah, statt aller Erstgeburt unter den Söhnen Israels, und das Vieh der Leviten, statt aller Erstgeburt unter dem Vieh der Söhne Israels.
42 Musa akawahesabu wazaliwa wa kwanza wote wa Israeli kama BWANA alivyomwagiza kufanya.
Und Mose musterte, wie ihm Jehovah geboten hatte, alle Erstgeburt unter den Söhnen Israels.
43 Aliwahesabu wazaliwa wote wa kwanza kwa mjina, wenye umri wa mwezi mmoja na zaidi. Alihesabu wanaume 22, 273.
Und alle männliche Erstgeburt in der Zahl der Namen von einem Monat und aufwärts nach ihren Gemusterten war zweiundzwanzigtausend und dreiundsiebzig und zweihundert.
44 Tena BWANA alinena na Musa. Akasema,
Und Jehovah redete zu Mose und sprach:
45 “Watwae Walawi badala ya wazaliwa wote wa kwanza wa wana wa Israeli. Na utwae wanyama wa Walawi badala ya wanyama wa Waisreli wengine. Walawi ni mali yangu. Mimi ndimi BWANA.
Nimm die Leviten statt aller Erstgeburt unter den Söhnen Israels und das Vieh der Leviten, statt ihres Viehs, und die Leviten sollen Mein sein. Ich bin Jehovah.
46 Unikusanyie shekeli tano za wokovu kwa kila hao 273 za hao wazaliwa wa kwanza wa Israeli za hao wanaozidi idadi ya Walawi.
Und für die Einlösung der dreiundsiebzig und zweihundert Erstgeburten der Söhne Israels, die überzählig sind über die Leviten,
47 Utazitumia hizo shekeli tano kwa kipimo cha mahali patakatifu. Shekeli moja ni sawa na gera ishirini.
Sollst du je fünf Schekel nehmen für den Kopf. Nach dem Schekel des Heiligtums sollst du es nehmen, zwanzig Gera der Schekel.
48 Utawalipa hizo shekeli za wokovu kwa Haruni na wanawe.”
Und das Silber gib Aharon und seinen Söhnen als Einlösung für die Überzähligen unter ihnen.
49 Kwa hiyo Musa akakusanya shakeli za wokovu kutoka kwa wale waliozidi idadi ya wale waliookolewa na Walawi.
Und Mose nahm das Silber der Einlösung von den Überzähligen über die Einlösung der Leviten,
50 Musa akakusanya zile fedha kutoka kwa hao wazaliwa wa kwanza wa wana wa Israeli. Alikusanya jumla ya shekeli 1, 365, zenye kipimo sawa na mahali patakatifu. Musa akamlipa Haruni na wanawe hizo shekeli za wokovu.
Von dem Erstgeborenen der Söhne Israels nahm er das Silber, fünfundsechzig und dreihundert und tausend nach dem Schekel des Heiligtums;
51 Musa akafanya kila kitu alichoagizwa na neno la BWANA kama BWANA alivyomwagiza.
Und Mose gab das Silber der Eingelösten dem Aharon und seinen Söhnen, nach Jehovahs Munde, wie Jehovah dem Mose geboten hatte.

< Hesabu 3 >