< Hesabu 28 >

1 BWANA akanena na Musa akamwambia,
Yavé habló a Moisés:
2 “Waamuru wana wa Isrseli uwaambie, 'Mtanitolea sadaka kwa wakati uliopangwa, chakula cha sadaka yangu kilichotengenezwa kwa moto ili kutoa harufu nzuri kwa ajili yangu.
Manda a los hijos de Israel: Tendrán cuidado de presentar mi ofrenda, mi alimento por medio de mis sacrificios quemados de olor que me apacigua, en su tiempo señalado.
3 Pia uwaambie, 'Hii ni sadaka iliyotengenezwa kwa moto ambayo mtaitoa kwa BWANA- mwanakondoo dume wa mwaka mmoja asiyekuwa na waa, wawili kila siku kuwa sadaka ya kuteketezwa ya kila siku.
Y les dirás: El sacrificio quemado que presentarán a Yavé cada día será dos corderos añales sin defecto para el holocausto continuo.
4 Mwanakodoo mmoja atatolewa sadaka asubuhi, na mwingine atatolewa sadaka jioni.
Ofrecerán el primer cordero en la mañana, y el segundo, al llegar la noche.
5 Mtatoa sadaka ya sehemu ya kumi ya efa ya unga mwembamba kuwa sadaka ya unga, uliochanganywa na robo ya hini ya mafuta yaliyokamuliwa.
La ofrenda vegetal será 2,2 litros de flor de harina, amasada con 0,9 litros de aceite de olivas machacadas.
6 Hii ni sadaka ya ya kuteketezwa ya kila siku iliyoamriwa mlima Sinai ili kutoa harufu nzuri, sadaka iliyotengenezwa kwa moto kwa ajili ya BWANA.
Es un holocausto continuo, un sacrificio quemado a Yavé que fue ordenado en la Montaña Sinaí como olor que apacigua, una ofrenda ofrecida por fuego a Yavé.
7 Pamoja na robo ya hini ya sadaka ya kinywaji kwa mmoja wa hao wanakondoo. Utaimimina mahali patakatifu hiyo sadaka ya kinywaji kwa BWANA.
Su libación de vino será 0,9 litros con cada cordero. En el Santuario derramarás la libación de licor fuerte a Yavé.
8 Yule mwanakondoo mwingine utamtoa sadaka jioni pamoja na sadaka ya unga kama kama yule wa asubuhi alivyotolewa. Pia utatoa tena sadaka ya kinywaji pamoja naye, sadaka iliyotengenezwa kwa moto ili kutoa harufu nzuri kwa BWANA.
El segundo cordero lo ofrecerán al llegar la noche. Lo harán como el sacrificio de la mañana con su libación. Es un sacrificio quemado de olor que apacigua a Yavé.
9 Katika siku ya Sabato utatoa wanakondoo dume wawili, wa umri wa mwaka mmoja kila mmoja wasiokuwa na dosari, na sehemu ya kumi mbili ya efa ya unga mwembamba kwa sadaka ya unga, uliochanganywa na mafuta, pamoja na sadaka ya kinywaji.
Pero el día sábado ofrecerán dos corderos añales sin defecto, y 4,4 litros de flor de harina amasada con aceite, como ofrenda vegetal con su libación.
10 Hii itakuwa sadaka ya kuteketezwa kwa kila siku ya Sabato, kama nyongeza ya ile sadaka ya kila siku pamoja na ile sadaka ya kinywaji.
Este es el holocausto de cada sábado, además del holocausto continuo y su libación.
11 Kila mwanzo wa mwezi, mtatoa sadaka za kuteketezwa kwa BWANA. Utatoa sadaka ya fahari wawili wachanga, kondoo dume mmoja, na wanakondoo dume saba wa umri wa mwaka mmoja wasiokuwa na dosari.
Al principio de cada mes ofrecerán en holocausto a Yavé dos becerros de la manada vacuna, un carnero y siete corderos añales sin defecto,
12 Pia mtatoa sehemu ya kumi tatu ya efa unga mwembamba kuwa sadaka ya unga uliochanganywa na mafuta kwa kila fahari, na sehemu za kumi mbili za unga mwembamba kuwa sadaka ya unga uliochanganywa na mafuta kwa yule kondoo mume mmoja.
6,6 litros de flor de harina amasada con aceite, como ofrenda vegetal con cada becerro, y 4,4 litros de flor de harina amasada con aceite, como ofrenda vegetal con el carnero,
13 Pia mtatoa sehemu ya kumi ya efa ya unga mwembamba uliochanganywa na mafuta kuwa sadaka ya unga kwa kila mwanakondoo. Hii itakuwa sadaka ya kuteketezwa, ya kutoa harufu nzuri, sadaka iliyotengenezwa kwa moto kwa ajilI ya BWANA.
y 2,2 litros de flor de harina amasada con aceite, como ofrenda vegetal con cada cordero. Es holocausto de olor que apacigua, sacrificio quemado a Yavé.
14 Sadaka ya kinywaji ya watu itakuwa nusu ya hini ya divai ya yule fahari, sehemu ya tatu ya hini ya kondoo dume, na robo ya hini ya mwanakondoo. Hii ndiyo itakuwa sadaka ya kuteketezwa ya kila mwezi kwa miezi yote ya mwaka.
Sus libaciones de vino son: 1,8 litros por cada becerro, 1,2 litros por el carnero y 0,9 litros por cada cordero. Este es el holocausto de cada mes para todos los meses del año.
15 Mtatoa beberu mmoja kuwa sadaka ya dhambi kwa BWANA. Hii itakuwa nyongeza kwa ile sadaka ya kila siku pamoja na ile sadaka ya viinywaji.
También se ofrecerá a Yavé un macho cabrío como sacrificio por el pecado, además del holocausto continuo con su libación.
16 Katika siku kumi na nne, ya mwezi wa kwanza itakuwa Pasaka ya BWANA.
En el mes primero, el día 14 del mes, es Pascua de Yavé.
17 Katika sku ya kumi na tano ya mwezi huu kutakuwa na sikukuu. Mtakuka mikate isiyo na chachu kwa siku saba.
El día 15 de ese mes será la fiesta solemne. Durante siete días se comerán panes sin levadura.
18 Katika siku ya kwanza kutakuwa na kusanyiko takatifu la kumheshimu BWANA. Katika siku hiyo msifanye kazi zenu za kila siku
El primer día habrá una santa convocación. No harán obra servil.
19 Hata hivyo, mtatoa sadaka iliyotengenezwa kwa moto, sadaka ya kuteketezwa kwa BWANA. Mtatoa sadaka ya fahari wawili, kondoo dume mmoja, na kondoo dume saba wa umri wa mwaka mmoja wakamilifu.
Ofrecerán un sacrificio quemado en holocausto a Yavé de dos becerros de la manada vacuna, un carnero y siete corderos añales, y serán perfectos.
20 Pamoja na yule fahari, mtatoa sadaka sehemu za tatu efa za unga mwembamba uliochanganywa na mafuta, pamoja na yule kondoo mume sehemu za pili za kumi.
Su ofrenda vegetal será de harina amasada con aceite, 6,6 litros por cada becerro y 4,4 litros por el carnero.
21 Kwa kila wale wanakondoo saba, mtatoa sehemu ya kumi ya efa ya unga mwembamba uliochanganywa na mafuta,
Ofrecerás 2,2 litros por cada uno de los siete corderos
22 na beberu mmoja kuwa sdaka ya dhambi ili kufanya upatanisho kwa ajili yenu.
y un macho cabrío como sacrificio por el pecado para hacer sacrificio que apacigua a favor de ustedes.
23 Mtotoa hivi vitu kama sadaka ya nyongeza katika ile sadaka ya kila siku inayotakiwa kila asubuhi.
Ofrecerán éstos, además del holocausto de la mañana, que es el holocausto continuo.
24 Kama ilivyofafanuliwa hapa, mtatoa sadaka hizi kila siku, kwa zile siku saba za Pasaka, kile chakula cha sadaka kilichotengenezwa kwa moto kuwa harufu nzuri kwa BWANA. Hiki kitatolewa kuwa sadaka ya nyongeza ya ile sadaka ya kuteketezwa na pamoja na ile sadaka ya vinywaji.
Harán estas cosas cada uno de los siete días. Es alimento y sacrificio quemado de olor que apacigua a Yavé. Se ofrecerán además del holocausto continuo con su libación.
25 Siku ya saba mtakuwa na kusanyiko takatifu ili kumheshimu BWANA, na katika siku hiyo msifanye zile kazi zenu zakila siku.
El séptimo día tendrán una santa convocación. No harán obra servil.
26 Pia katika siku ya malimbuko, mtakapokuwa mnatoa sadaka ya unga mpya katika sikukuu zenu za Majuma, mtakuwa na kusanyiko takatifu la kumheshimu BWANA, na katika siku hiyo msifanye kazi zenu za kila siku.
En el día de las primicias, cuando ofrezcan una ofrenda vegetal nueva a Yavé en su fiesta solemne de las semanas, tendrán una santa convocación. No harán obra servil.
27 Mtatoa sadaka ya kuteketezwa ili kutoa harufu nzuri kwa BWANA. Mtatoa fahari wawili wachanga, kondoo mume mmoja, na wanakondoo saba waume wa mwaka mmoja.
Ofrecerán en holocausto, en olor que apacigua a Yavé, dos becerros de la manada vacuna, un carnero, siete corderos añales,
28 Pamoja na hiyo mtatoa sadaka ya unga: unga mwembamba uliochanganywa na mafuta, sehemu tatu za kumi za efa za unga mwembamba uliochanganywa na mafuta kwa kila fahari na sehemu kumi mbili za yule kondoo mume.
y la ofrenda vegetal de ellos, flor de harina amasada con aceite, 6,6 litros por cada becerro, 4,4 litros por el carnero
29 Toeni sehemu ya kumi ya efa ya unga mwembamba uliochanganywa na mafuta kwa kila wale wanakondoo saba,
y 2,2 litros por cada uno de los siete corderos,
30 na beberu mmoja ili kufanya upatanisho kwa ajili yenu.
además de un macho cabrío para hacer sacrificio de olor que apacigua por ustedes.
31 Mtakapotoa hao wanyama wasio na dosari, pamoja na sadaka zake za vinywaji, hii itakuwa sadaka ya nyongeza katika zile sadaka za kila siku na pamoja na zile sadaka za unga.'”
Esto ofrecerán, además del holocausto continuo y de su ofrenda vegetal. Los ofrecerán sin defecto con su libación.

< Hesabu 28 >