< Hesabu 28 >

1 BWANA akanena na Musa akamwambia,
And the Lord spoke to Moses, saying,
2 “Waamuru wana wa Isrseli uwaambie, 'Mtanitolea sadaka kwa wakati uliopangwa, chakula cha sadaka yangu kilichotengenezwa kwa moto ili kutoa harufu nzuri kwa ajili yangu.
Charge the children of Israel, and you shall speak to them, saying, You shall observe to offer to me in my feasts my gifts, my presents, my burnt offerings for a sweet smelling savour.
3 Pia uwaambie, 'Hii ni sadaka iliyotengenezwa kwa moto ambayo mtaitoa kwa BWANA- mwanakondoo dume wa mwaka mmoja asiyekuwa na waa, wawili kila siku kuwa sadaka ya kuteketezwa ya kila siku.
And you shall say to them, These are the burnt offerings, all that you shall bring to the Lord; two lambs of a year old without blemish daily, for a whole burnt offering perpetually.
4 Mwanakodoo mmoja atatolewa sadaka asubuhi, na mwingine atatolewa sadaka jioni.
You shall offer one lamb in the morning, and you shall offer the second lamb towards evening.
5 Mtatoa sadaka ya sehemu ya kumi ya efa ya unga mwembamba kuwa sadaka ya unga, uliochanganywa na robo ya hini ya mafuta yaliyokamuliwa.
And you shall offer the tenth part of an ephah of fine flour for a meat-offering, mingled with oil, with the fourth part of a hin.
6 Hii ni sadaka ya ya kuteketezwa ya kila siku iliyoamriwa mlima Sinai ili kutoa harufu nzuri, sadaka iliyotengenezwa kwa moto kwa ajili ya BWANA.
[It is] a perpetual whole burnt offering, a sacrifice offered in the mount of Sina for a sweet smelling savour to the Lord.
7 Pamoja na robo ya hini ya sadaka ya kinywaji kwa mmoja wa hao wanakondoo. Utaimimina mahali patakatifu hiyo sadaka ya kinywaji kwa BWANA.
And its drink-offering, the fourth part of a hin to each lamb; in the holy place shall you pour strong drink as a drink-offering to the Lord.
8 Yule mwanakondoo mwingine utamtoa sadaka jioni pamoja na sadaka ya unga kama kama yule wa asubuhi alivyotolewa. Pia utatoa tena sadaka ya kinywaji pamoja naye, sadaka iliyotengenezwa kwa moto ili kutoa harufu nzuri kwa BWANA.
And the second lamb you shall offer towards evening; you shall offer it according to its meat-offering and according to its drink-offering for a smell of sweet savour to the Lord.
9 Katika siku ya Sabato utatoa wanakondoo dume wawili, wa umri wa mwaka mmoja kila mmoja wasiokuwa na dosari, na sehemu ya kumi mbili ya efa ya unga mwembamba kwa sadaka ya unga, uliochanganywa na mafuta, pamoja na sadaka ya kinywaji.
And on the sabbath-day you shall offer two lambs of a year old without blemish, and two tenth deals of fine flour mingled with oil for a meat-offering, and a drink-offering.
10 Hii itakuwa sadaka ya kuteketezwa kwa kila siku ya Sabato, kama nyongeza ya ile sadaka ya kila siku pamoja na ile sadaka ya kinywaji.
[It is] a whole burnt offering of the sabbaths on the sabbath days, besides the continued whole burnt offering, and its drink offering.
11 Kila mwanzo wa mwezi, mtatoa sadaka za kuteketezwa kwa BWANA. Utatoa sadaka ya fahari wawili wachanga, kondoo dume mmoja, na wanakondoo dume saba wa umri wa mwaka mmoja wasiokuwa na dosari.
And at the new moons you shall bring a whole burnt offering to the Lord, two calves of the herd, and one ram, seven lambs of a year old without blemish.
12 Pia mtatoa sehemu ya kumi tatu ya efa unga mwembamba kuwa sadaka ya unga uliochanganywa na mafuta kwa kila fahari, na sehemu za kumi mbili za unga mwembamba kuwa sadaka ya unga uliochanganywa na mafuta kwa yule kondoo mume mmoja.
Three tenth deals of fine flour mingled with oil for one calf, and two tenth deals of fine flour mingled with oil for one ram.
13 Pia mtatoa sehemu ya kumi ya efa ya unga mwembamba uliochanganywa na mafuta kuwa sadaka ya unga kwa kila mwanakondoo. Hii itakuwa sadaka ya kuteketezwa, ya kutoa harufu nzuri, sadaka iliyotengenezwa kwa moto kwa ajilI ya BWANA.
A tenth deal of fine flour mingled with oil for each lamb, as a meat-offering, a sweet smelling savour, a burnt offering to the Lord.
14 Sadaka ya kinywaji ya watu itakuwa nusu ya hini ya divai ya yule fahari, sehemu ya tatu ya hini ya kondoo dume, na robo ya hini ya mwanakondoo. Hii ndiyo itakuwa sadaka ya kuteketezwa ya kila mwezi kwa miezi yote ya mwaka.
Their drink-offering shall be the half of a hin for one calf; and the third of a hin for one ram; and the fourth part of a hin of wine for one lamb: this [is] the whole burnt offering monthly throughout the months of the year.
15 Mtatoa beberu mmoja kuwa sadaka ya dhambi kwa BWANA. Hii itakuwa nyongeza kwa ile sadaka ya kila siku pamoja na ile sadaka ya viinywaji.
And [he shall offer] one kid of the goats for a sin-offering to the Lord; it shall be offered beside the continual whole burnt offering and its drink-offering.
16 Katika siku kumi na nne, ya mwezi wa kwanza itakuwa Pasaka ya BWANA.
And in the first month, on the fourteenth day of the month, [is] the passover to the Lord.
17 Katika sku ya kumi na tano ya mwezi huu kutakuwa na sikukuu. Mtakuka mikate isiyo na chachu kwa siku saba.
And on the fifteenth day of this month [is] a feast; seven days you shall eat unleavened bread.
18 Katika siku ya kwanza kutakuwa na kusanyiko takatifu la kumheshimu BWANA. Katika siku hiyo msifanye kazi zenu za kila siku
And the first day shall be to you a holy convocation; you shall do no servile work.
19 Hata hivyo, mtatoa sadaka iliyotengenezwa kwa moto, sadaka ya kuteketezwa kwa BWANA. Mtatoa sadaka ya fahari wawili, kondoo dume mmoja, na kondoo dume saba wa umri wa mwaka mmoja wakamilifu.
And you shall bring whole burnt offerings, a sacrifice to the Lord, two calves of the herd, one ram, seven lambs of a year old; they shall be to you without blemish.
20 Pamoja na yule fahari, mtatoa sadaka sehemu za tatu efa za unga mwembamba uliochanganywa na mafuta, pamoja na yule kondoo mume sehemu za pili za kumi.
And their meat-offering shall be fine flour mingled with oil; three tenth deals for one calf, and two tenth deals for one ram.
21 Kwa kila wale wanakondoo saba, mtatoa sehemu ya kumi ya efa ya unga mwembamba uliochanganywa na mafuta,
You shall offer a tenth for each lamb, for the seven lambs.
22 na beberu mmoja kuwa sdaka ya dhambi ili kufanya upatanisho kwa ajili yenu.
And [you shall offer] one kid of the goats for a sin-offering, to make atonement for you.
23 Mtotoa hivi vitu kama sadaka ya nyongeza katika ile sadaka ya kila siku inayotakiwa kila asubuhi.
Beside the perpetual whole burnt offering in the morning, which is a whole burnt sacrifice for a continuance,
24 Kama ilivyofafanuliwa hapa, mtatoa sadaka hizi kila siku, kwa zile siku saba za Pasaka, kile chakula cha sadaka kilichotengenezwa kwa moto kuwa harufu nzuri kwa BWANA. Hiki kitatolewa kuwa sadaka ya nyongeza ya ile sadaka ya kuteketezwa na pamoja na ile sadaka ya vinywaji.
these shall you thus offer daily for seven days, a gift, a sacrifice for a sweet smelling savour to the Lord; beside the continual whole burnt offering, you shall offer its drink-offering.
25 Siku ya saba mtakuwa na kusanyiko takatifu ili kumheshimu BWANA, na katika siku hiyo msifanye zile kazi zenu zakila siku.
And the seventh day shall be to you a holy convocation; you shall do no servile work in it.
26 Pia katika siku ya malimbuko, mtakapokuwa mnatoa sadaka ya unga mpya katika sikukuu zenu za Majuma, mtakuwa na kusanyiko takatifu la kumheshimu BWANA, na katika siku hiyo msifanye kazi zenu za kila siku.
And on the day of the new corn, when you shall offer a new sacrifice [at the festival] of weeks to the Lord, there shall be to you a holy convocation; you shall do no servile work,
27 Mtatoa sadaka ya kuteketezwa ili kutoa harufu nzuri kwa BWANA. Mtatoa fahari wawili wachanga, kondoo mume mmoja, na wanakondoo saba waume wa mwaka mmoja.
and you shall bring whole burnt offerings for a sweet smelling savour to the Lord, two calves of the herd, one ram, seven lambs without blemish.
28 Pamoja na hiyo mtatoa sadaka ya unga: unga mwembamba uliochanganywa na mafuta, sehemu tatu za kumi za efa za unga mwembamba uliochanganywa na mafuta kwa kila fahari na sehemu kumi mbili za yule kondoo mume.
Their meat-offering [shall be] fine flour mingled with oil; there shall be three tenth deals for one calf, and two tenth deals for one ram.
29 Toeni sehemu ya kumi ya efa ya unga mwembamba uliochanganywa na mafuta kwa kila wale wanakondoo saba,
A tenth for each lamb separately, for the seven lambs; and a kid of the goats,
30 na beberu mmoja ili kufanya upatanisho kwa ajili yenu.
for a sin-offering, to make atonement for you; beside the perpetual whole burnt offering: and
31 Mtakapotoa hao wanyama wasio na dosari, pamoja na sadaka zake za vinywaji, hii itakuwa sadaka ya nyongeza katika zile sadaka za kila siku na pamoja na zile sadaka za unga.'”
you shall offer to me their meat-offering. They shall be to you unblemished, and you shall offer their drink-offerings.

< Hesabu 28 >