< Hesabu 25 >

1 Israeli akakaa Shitimu, na wanaume wakaanza kufanya ukahaba na wanawake wa Moabu,
And Israel dwelleth in Shittim, and the people begin to go a-whoring unto daughters of Moab,
2 kwa kuwa Wamoabu waliwakaribishsa kutoa sadaka kwa miungu yao. Kwa hiyo watu wakala na kuisujudia miungu ya Moabu.
and they call for the people to the sacrifices of their gods, and the people eat, and bow themselves to their gods,
3 Watu wa Israeli wakaungana kumwabudu Baali wa Peori, na hasira ya BWANA ikawaka dhidi ya Israeli.
and Israel is joined to Baal-Peor, and the anger of Jehovah burneth against Israel.
4 BWANA akamwambia Musa, “Waue viongozi wote wa watu na uwanyonge mbele yangu ili waonekane wakati wa mchana, ili kwamba hasira yangu kali iondoke kwa Israeli.”
And Jehovah saith unto Moses, 'Take all the chiefs of the people, and hang them before Jehovah — over-against the sun; and the fierceness of the anger of Jehovah doth turn back from Israel.'
5 Kwa hiyo Musa akawaambia viongozi wa Israeli, “Kila mmoja wenu lazima awanyonge watu wake ambao wameshiriki kumwabudu Baali wa Peori.”
And Moses saith unto the judges of Israel, 'Slay ye each his men who are joined to Baal-Peor.'
6 Kisha mtu mmoja wa Israeli akaleta mwanamke mmoja aliyekuwa miongoni mwa familia yake. Hili lilitokea mbele ya macho ya Musa na watu wa Israeli, wakati walipokuwa wakilia mbele ya lango la hema ya kukutania.
And lo, a man of the sons of Israel hath come, and bringeth in unto his brethren the Midianitess, before the eyes of Moses, and before the eyes of all the company of the sons of Israel, who are weeping at the opening of the tent of meeting;
7 Finehasi mwana wa Eliazari, mwana wa Haruni kuhani, alipoona hivyo, akainuka kutoka jamii ya watu akachukua mkuki mkononi mwake.
and Phinehas, son of Eleazar, son of Aaron, the priest, seeth, and riseth from the midst of the company, and taketh a javelin in his hand,
8 Akamfuata yule mwanaume Muisraeli hemani na kuwachoma kwa mkuki wote wawili kwenye miili yao, wote yule Muisraeli na yule mwanamke. Kwa hiyo ile tauni ambayo Mungu alikuwa ameituma kwa watu wa Israeli ikakoma.
and goeth in after the man of Israel unto the hollow place, and pierceth them both, the man of Israel and the woman — unto her belly, and the plague is restrained from the sons of Israel;
9 Idadi ya wale waliokufa kwa tauni walikuwa elfu ishirini na nne.
and the dead by the plague are four and twenty thousand.
10 BWANA akanena na Musa, akasema,
And Jehovah speaketh unto Moses, saying,
11 “Finehasi mwana wa Eliazari mwana wa Haruni, kuhani amaigeuza hasira yangu isiwe kwa wana wa Israeli kwa sababu alikuwa na wivu kati yao juu ya wivu wangu. Kwa hiyo sijawaangamiza watu wa Israeli kwa hasira yangu.
'Phinehas, son of Eleazar, son of Aaron the priest, hath turned back My fury from the sons of Israel, by his being zealous with My zeal in their midst, and I have not consumed the sons of Israel in My zeal.
12 Kwa hiyo waambie, 'BWANA anasema, “Tazama, Ninampa Finehasi agano la amani.
'Therefore say, Lo, I am giving to him My covenant of peace,
13 Kwake na kwa wana wake baada yake, litakuwa agano la kudumu la ukuhani kwa sababu alikuwa na wivu juu yangu, Mungu wake. Amewapatanisha wana wa Israeli.
and it hath been to him and to his seed after him a covenant of a priesthood age-during, because that he hath been zealous for his God, and doth make atonement for the sons of Israel.'
14 Sasa yule Muisraeli aliyeuwawa pamoja na Yule mwanamke Mmidiani alikuwa Zimri mwana wa Salu, kiongozi wa familia ya uzao wa Simeoni.
And the name of the man of Israel who is smitten, who hath been smitten with the Midianitess, [is] Zimri son of Salu, prince of the house of a father of the Simeonite;
15 Jina la yule Mmidiani aliyeuwawa lilikuwa Cozibi binti wa Zuri, ambaye alikuwa mkuu wa familia wa kabila huko Midiani.
and the name of the woman who is smitten, the Midianitess, [is] Cozbi daughter of Zur, head of a people — of the house of a father in Midian [is] he.
16 Kwa hiyo BWANA akanena na Musa na kusema,
And Jehovah speaketh unto Moses, saying,
17 “Watendee Wamidiani kama maadui na uwaangamize, kwa kuwa waliwatendea kama maadui
'Distress the Midianites, and ye have smitten them,
18 kwa kuwadanganya. Waliwaongoza katika uovu kwa swala la Peori na kwa swala la dada yao Cozibi, binti wa kiongozi wa Wamidiani, ambaye aliuawa siku ile ya tauni kwa swala la Peori.”
for they are adversaries to you with their frauds, [with] which they have acted fraudulently to you, concerning the matter of Peor, and concerning the matter of Cozbi, daughter of a prince of Midian, their sister, who is smitten in the day of the plague for the matter of Peor.'

< Hesabu 25 >