< Hesabu 25 >

1 Israeli akakaa Shitimu, na wanaume wakaanza kufanya ukahaba na wanawake wa Moabu,
Israel [God prevails] stayed in Shittim; and the people began to play the prostitute with the daughters of Moab [From father];
2 kwa kuwa Wamoabu waliwakaribishsa kutoa sadaka kwa miungu yao. Kwa hiyo watu wakala na kuisujudia miungu ya Moabu.
for they called the people to the sacrifices of their deities. The people ate and bowed down to their deities.
3 Watu wa Israeli wakaungana kumwabudu Baali wa Peori, na hasira ya BWANA ikawaka dhidi ya Israeli.
Israel [God prevails] joined himself to Baal Peor. Adonai’s anger burned against Israel [God prevails].
4 BWANA akamwambia Musa, “Waue viongozi wote wa watu na uwanyonge mbele yangu ili waonekane wakati wa mchana, ili kwamba hasira yangu kali iondoke kwa Israeli.”
Adonai said to Moses [Drawn out], “Take all the chiefs of the people, and hang them up to Adonai before the sun, that the fierce anger of Adonai may turn away from Israel [God prevails].”
5 Kwa hiyo Musa akawaambia viongozi wa Israeli, “Kila mmoja wenu lazima awanyonge watu wake ambao wameshiriki kumwabudu Baali wa Peori.”
Moses [Drawn out] said to the judges of Israel [God prevails], “Everyone kill his men who have joined themselves to Baal Peor.”
6 Kisha mtu mmoja wa Israeli akaleta mwanamke mmoja aliyekuwa miongoni mwa familia yake. Hili lilitokea mbele ya macho ya Musa na watu wa Israeli, wakati walipokuwa wakilia mbele ya lango la hema ya kukutania.
Behold, one of the children of Israel [God prevails] came and brought to his brothers a Midianite [Descendant of Strife] woman in the sight of Moses [Drawn out], and in the sight of all the congregation of the children of Israel [God prevails], while they were weeping at the door of the Tent of Meeting.
7 Finehasi mwana wa Eliazari, mwana wa Haruni kuhani, alipoona hivyo, akainuka kutoka jamii ya watu akachukua mkuki mkononi mwake.
When Pinchas [Bronze skin], the son of Eleazar [Help of God], the son of Aaron [Light-bringer] the priest, saw it, he rose up from the middle of the congregation, and took a spear in his hand.
8 Akamfuata yule mwanaume Muisraeli hemani na kuwachoma kwa mkuki wote wawili kwenye miili yao, wote yule Muisraeli na yule mwanamke. Kwa hiyo ile tauni ambayo Mungu alikuwa ameituma kwa watu wa Israeli ikakoma.
He went after the man of Israel [God prevails] into the pavilion, and thrust both of them through, the man of Israel [God prevails], and the woman through her body. So the plague was stayed from the children of Israel [God prevails].
9 Idadi ya wale waliokufa kwa tauni walikuwa elfu ishirini na nne.
Those who died by the plague were twenty-four thousand.
10 BWANA akanena na Musa, akasema,
Adonai spoke to Moses [Drawn out], saying,
11 “Finehasi mwana wa Eliazari mwana wa Haruni, kuhani amaigeuza hasira yangu isiwe kwa wana wa Israeli kwa sababu alikuwa na wivu kati yao juu ya wivu wangu. Kwa hiyo sijawaangamiza watu wa Israeli kwa hasira yangu.
“Pinchas [Bronze skin], the son of Eleazar [Help of God], the son of Aaron [Light-bringer] the priest, has turned my wrath away from the children of Israel [God prevails], in that he was jealous with my jealousy among them, so that I didn’t consume the children of Israel [God prevails] in my jealousy.
12 Kwa hiyo waambie, 'BWANA anasema, “Tazama, Ninampa Finehasi agano la amani.
Therefore say, ‘Behold, I give to him my covenant ·binding contract between two or more parties· of peace.
13 Kwake na kwa wana wake baada yake, litakuwa agano la kudumu la ukuhani kwa sababu alikuwa na wivu juu yangu, Mungu wake. Amewapatanisha wana wa Israeli.
It shall be to him, and to his offspring after him, the covenant of an everlasting priesthood, because he was jealous for his God, and made atonement for the children of Israel [God prevails].’”
14 Sasa yule Muisraeli aliyeuwawa pamoja na Yule mwanamke Mmidiani alikuwa Zimri mwana wa Salu, kiongozi wa familia ya uzao wa Simeoni.
Now the name of the man of Israel [God prevails] that was slain, who was slain with the Midianite [Descendant of Strife] woman, was Zimri, the son of Salu, a prince of a fathers’ house among the Simeonites.
15 Jina la yule Mmidiani aliyeuwawa lilikuwa Cozibi binti wa Zuri, ambaye alikuwa mkuu wa familia wa kabila huko Midiani.
The name of the Midianite [Descendant of Strife] woman who was slain was Cozbi, the daughter of Zur. He was head of the people of a fathers’ house in Midian [Strife].
16 Kwa hiyo BWANA akanena na Musa na kusema,
Adonai spoke to Moses [Drawn out], saying,
17 “Watendee Wamidiani kama maadui na uwaangamize, kwa kuwa waliwatendea kama maadui
“Harass the Midianites [Descendants of Strife], and strike them,
18 kwa kuwadanganya. Waliwaongoza katika uovu kwa swala la Peori na kwa swala la dada yao Cozibi, binti wa kiongozi wa Wamidiani, ambaye aliuawa siku ile ya tauni kwa swala la Peori.”
for they harassed you with their wiles, with which they have deceived you in the matter of Peor, and in the matter of Cozbi, the daughter of the prince of Midian [Strife], their sister, who was slain on the day of the plague in the matter of Peor.”

< Hesabu 25 >