< Hesabu 20 >

1 Kwa hiyo wana wa Israeli, na jamii yote ya watu, wakaenda katika jangwa la Sini katika mwezi wa kwanza; wakaa Kadeshi. Hapo ndipo Miriamu alipofia na kuzikwa.
And the children of Israel, even the whole congregation, came into the wilderness of Zin in the first month; and the people abode in Kadesh; and Miriam died there, and was buried there.
2 Huko hapakuwa na maji kwa ajili ya watu, kwa hiyo wakakusanyika kinyume na Musa na Haruni huko.
And there was no water for the congregation; and they assembled themselves together against Moses and against Aaron.
3 Watu wakamlalamikia Musa. Wakasema, “Ilikuwa ni bora kama tungelikufa wakati Waisraeli wenzetu walipokufa mbele za BWANA.
And the people strove with Moses, and spoke, saying: 'Would that we had perished when our brethren perished before the LORD!
4 Kwa nini umewaleta watu wa BWANA kufia katika jangwa hili, sisi na wanyama wetu?
And why have ye brought the assembly of the LORD into this wilderness, to die there, we and our cattle?
5 Kwa nini ulitutoa Misri na kutuleta katika eneo hili baya? Hapa hakuna nafaka, wala mitini, wala mizabibu, wala makomamanga. Na hakuna maji ya kunywa.”
And wherefore have ye made us to come up out of Egypt, to bring us in unto this evil place? it is no place of seed, or of figs, or of vines, or of pomegranates; neither is there any water to drink.'
6 Basi Musa na Haruni wakatoweka mbele ya mkutano huo. Wakaenda kwenye hema ya kukutania wakalala kifudifudi. Ndipo pale utukufu wa Busara wa BWANA ukaonekana kwao.
And Moses and Aaron went from the presence of the assembly unto the door of the tent of meeting, and fell upon their faces; and the glory of the LORD appeared unto them.
7 BWANA akanena na Musa, akamwambia,
And the LORD spoke unto Moses, saying:
8 “Chukua fimbo yako na uwakusanye watu, wewe na Haruni ndugu yako. Uumbie huu mwamba mbele ya macho yao, na uumuru utoe maji. Nawe utawapa maji kutoka kwenye huu mwamba, nawe utawapa maji ya kunywa hao watu na wanyama wao.”
'Take the rod, and assemble the congregation, thou, and Aaron thy brother, and speak ye unto the rock before their eyes, that it give forth its water; and thou shalt bring forth to them water out of the rock; so thou shalt give the congregation and their cattle drink.'
9 Musa akachukua hiyo fimbo mbele ya BWANA, kama vile BWANA alivyokuwa amemwamuru kufanya.
And Moses took the rod from before the LORD, as He commanded him.
10 Kisha Musa na Haruni wakawakusanya watu pamoja mbele ya ule mwamba. Ndipo Musa akawaambia, “Sasa sikilizeni, enyi wapinzani. Lazima tuwape maji kutoka kwenye huu mwamba?”
And Moses and Aaron gathered the assembly together before the rock, and he said unto them: 'Hear now, ye rebels; are we to bring you forth water out of this rock?'
11 Ndipo Musa akanyosha mkono wake na kuupiga ule mwamba mara mbili kwa fimbo yake, na maji mengi yakatoka. Wale watu wakanywa pamoja na wanyama wao.
And Moses lifted up his hand, and smote the rock with his rod twice; and water came forth abundantly, and the congregation drank, and their cattle.
12 Kisha BWANA akamwambia Musa na Haruni, “Kwa kuwa hamkuniheshimu mimi na kuniamini mbele ya watu wa Israeli, hamtawaingiza hawa watu katika nchi niliyowaahidi.
And the LORD said unto Moses and Aaron: 'Because ye believed not in Me, to sanctify Me in the eyes of the children of Israel, therefore ye shall not bring this assembly into the land which I have given them.'
13 Mahali hapa paliitwa maji ya Meriba kwa sababu wana wa Israeli walitofautiana na BWANA pale, na akajionyesha kwao kuwa mtakatifu.
These are the waters of Meribah, where the children of Israel strove with the LORD, and He was sanctified in them.
14 Musa akatuma wajumbe kutoka Kadeshi kwa mfalme wa Edom: Ndugu yako Israeli anasema hivi: “Wewe unajua magumu yote ambayo yametupata.
And Moses sent messengers from Kadesh unto the king of Edom: 'Thus saith thy brother Israel: Thou knowest all the travail that hath befallen us;
15 Na unajua kuwa babu zetu walienda Misri na waliishi Misri kwa muda mrefu. Wamisri walitutendea vibaya pamoja na babu zetu.
how our fathers went down into Egypt, and we dwelt in Egypt a long time; and the Egyptians dealt ill with us, and our fathers;
16 Tulipomlilia BWANA, akatusikia na kututumia malaika ambaye alitutoa toka Misri. Tazama, sasa tuko Kadeshi, mji unaopakana na nchi yako.
and when we cried unto the LORD, He heard our voice, and sent an angel, and brought us forth out of Egypt; and, behold, we are in Kadesh, a city in the uttermost of thy border.
17 Tunakuomba uturuhusu kupita katika nchi yako. Hatutapita mashambani wala kwenye mashamba ya mizabibu, wala hatutakunywa maji ya visima vyako. Tutapita kwenye njia kuu ya mfalme. Hatutageuka upande wa kulia wala upande wa kushoto mpaka tutakapopita mpaka wako.”
Let us pass, I pray thee, through thy land; we will not pass through field or through vineyard, neither will we drink of the water of the wells; we will go along the king's highway, we will not turn aside to the right hand nor to the left, until we have passed thy border.'
18 Lakini mfalme wa Edomu akamjibu, “Msipite hapa. Kama mtafanya hivyo, Nitakuja na upanga kukuvamia.”
And Edom said unto him: 'Thou shalt not pass through me, lest I come out with the sword against thee.'
19 Ndipo wana wa Israeli wakamwambia,”tutapitia njia kuu. Kama sisi au wanyama wetu watakunywa maji yako, basi tutalipa. Tunaomba uturuhusu tupite tukitembea kwa miguu yetu, bila kufanya jambo lolote lile.”
And the children of Israel said unto him: 'We will go up by the highway; and if we drink of thy water, I and my cattle, then will I give the price thereof; let me only pass through on my feet; there is no hurt.'
20 Lakini mfalme wa Edomu akajibu, “Usipite hapa.” Kwa hiyo nfalme wa Edomu akawa kinyume cha Israeli kwa mkono wenye nguvu pamoja na jeshi kubwa sana.
And he said: 'Thou shalt not pass through.' And Edom came out against him with much people, and with a strong hand.
21 Mfame wa Edomu akawazuia wana wa Israeli kupita kwenye mipaka yake. Kwa sababu ya hili, Israeli akageuka kuiacha nchi ya Edomu.
Thus Edom refused to give Israel passage through his border; wherefore Israel turned away from him.
22 Kwa hiyo watu wakasafiri kutoka Kadeshi. Wana wa Israeli, watu wote, wakafika Mlima Hori.
And they journeyed from Kadesh; and the children of Israel, even the whole congregation, came unto mount Hor.
23 BWANA akanena na Musa na Haruni hapo kwenye Mlima Hori, kwenye mpaka wa Edomu. Akasema,
And the LORD spoke unto Moses and Aaron in mount Hor, by the border of the land of Edom, saying:
24 “Sasa ni wakati wa Haruni kukusanyika na watu wake, hataingia katika nchi ile niliyowaahidi wana wa Israeli. Hii ni kwa sababu ninyi wawili hamkuitii sauti yangu pale kwenye maji ya Meriba.
'Aaron shall be gathered unto his people; for he shall not enter into the land which I have given unto the children of Israel, because ye rebelled against My word at the waters of Meribah.
25 Mchukue Haruni na Eliazari mwanaye, na uwalete juu ya Mlima Hori.
Take Aaron and Eleazar his son, and bring them up unto mount Hor.
26 Umvulishi HarunI yale mavazi ya kikuhani na umvalishe Eliazari mwanaye. Haruni atakufa na kulazwa pamoja na watu wake.”
And strip Aaron of his garments, and put them upon Eleazar his son; and Aaron shall be gathered unto his people, and shall die there.'
27 Musa akafanya kama BWANA alivyomwamuru. Wakaenda juu y a Mlima Hori na watu wote wakiona.
And Moses did as the LORD commanded; and they went up into mount Hor in the sight of all the congregation.
28 Musa akamvulisha Haruni yale mavazi ya kikuhani na kumvalisha Mwanaye Eliazari. Haruni akafa pale juu ya Mlima Hori. Kisha Musa na Eliazari wakashuka.
And Moses stripped Aaron of his garments, and put them upon Eleazar his son; and Aaron died there in the top of the mount; and Moses and Eleazar came down from the mount.
29 Watu walipoona kuwa Haruni amekufa, taifa lote wakamlilia Haruni kwa siku arobaini.
And when all the congregation saw that Aaron was dead, they wept for Aaron thirty days, even all the house of Israel.

< Hesabu 20 >