< Hesabu 2 >

1 BWANA akasema na Musa na Haruni tena. Akamwambia,
The LORD spoke to Moses and to Aaron, saying,
2 Kila mtu atapanga kulingana na mahali pake, pamoja na mabango ya baba zao. Watapanga kuzunguka hema ya kukutania kila upande.
"The children of Israel shall camp every man by his own standard, with the banners of their fathers' houses: at a distance from the Tent of Meeting shall they camp around it."
3 Wale watakaopanga mashariki mwa hema ya kukutania, mahali ambapo juu huonekana wakati wa jua kuchomoza, ni makambi ya Yuda nao watakuwa katika kundi lao. Nashoni mwana wa Aminadabu ni kiongozi wa watu wa Yuda.
Those who camp on the east side toward the sunrise shall be of the standard of the camp of Judah, according to their divisions: and the prince of the people of Judah shall be Nahshon the son of Amminadab.
4 Idadi ya watu wa Yuda ni 74, 600.
His division, and those who were numbered of them, were seventy-four thousand six hundred.
5 Kabila la Isakari litapanga mbele ya Yuda. Nethaneli mwana wa Zuari ataliongoza jeshi la Isakari.
Those who camp next to him shall be the tribe of Issachar: and the prince of the people of Issachar shall be Nethanel the son of Zuar.
6 Idadi ya kikosi chake ni wanaume 54, 000.
His division, and those who were numbered of it, were fifty-four thousand four hundred.
7 Kabila la Zabuloni litapanga mbele ya Isakari. Eliabu mwana wa Heloni ndiye atakayeliongoza jeshi la Zabuloni.
The tribe of Zebulun: and the prince of the people of Zebulun shall be Eliab the son of Helon.
8 Idadi ya kikosi chake ni 57, 400.
His division, and those who were numbered of it, were fifty-seven thousand four hundred.
9 Idadi yote ya kambi y a Yuda ni 186, 400. Watakuwa wa kwanza kuondoka.
All who were numbered of the camp of Judah were one hundred eighty-six thousand four hundred, according to their divisions. They shall set out first.
10 Upande wa kusini kutakuwa na kambi ya Reubeni katika kundi lao. Kiongozi wa kundi la Reubeni ni Elizuri mwana wa Shedeuri.
"On the south side shall be the standard of the camp of Reuben according to their divisions. The prince of the people of Reuben shall be Elizur the son of Shedeur.
11 Idadi ya kikosi chake ni 46, 500.
His division, and those who were numbered of it, were forty-six thousand five hundred.
12 Simeoni atapanga mbele ya Reubeni. Kiongozi wa watu wa Simeoni ni Shelumieli mwana wa Zurishadai.
"Those who camp next to him shall be the tribe of Simeon. The prince of the people of Simeon shall be Shelumiel the son of Zurishaddai.
13 Waliohesabiwa kwenye kikosi chake ni 59, 300.
His division, and those who were numbered of them, were fifty-nine thousand three hundred.
14 Kabila la Gadi litafuatia. Kiongozi wa watu wa Gadi ni Eliasafu mwana wa Deuli.
"The tribe of Gad: and the prince of the people of Gad shall be Eliasaph the son of Reuel.
15 Idadi ya kikosi chake ni 45, 650.
His division, and those who were numbered of them, were forty-five thousand six hundred fifty.
16 Wote waliohesabiwa kwenye kambi ya Reubeni, kulingana na kikosi chake, ni 151, 450. Watakuwa wa pili kuondoka.
"All who were numbered of the camp of Reuben were one hundred fifty-one thousand four hundred fifty, according to their armies. They shall set out second.
17 Kifuatacho, ni hema la kukutania kuondoka kambini pamoja na Walawi likiwa katikati ya kambi zote. Lazima waondoke hapo kambini kwa mpangilio huo kama walivyoingia kwenye kambi. Kila mwanamume lazima awe mahali pake kwa kufuata bango lake.
"Then the Tent of Meeting shall set out, with the camp of the Levites in the midst of the camps. As they camp, so shall they set out, every man in his place, by their standards.
18 Migawanyiko ya kambi y Efraimu kufuata mahali pake. Kiongozi wa watu wa Efraimu ni Elishama mwana wa Amihudi.
"On the west side shall be the standard of the camp of Ephraim according to their divisions: and the prince of the people of Ephraim shall be Elishama the son of Ammihud.
19 Hesabu ya kikosi hiki ni 40, 500.
His division, and those who were numbered of them, were forty thousand five hundred.
20 Baada ya hao lilifuata kabila la Manase. Kiongozi wa Manase ni Gamaliel mwana wa Pedazuri.
"Next to him shall be the tribe of Manasseh: and the prince of the people of Manasseh shall be Gamaliel the son of Pedahzur.
21 Hesabu ya kikosi hiki ni 32, 200.
His division, and those who were numbered of them, were thirty-two thousand two hundred.
22 Kabila litakalofuata ni la Benjamini. Kiongozi wa Benjamini n Abidani mwana wa Gidioni.
"The tribe of Benjamin: and the prince of the people of Benjamin shall be Abidan the son of Gideoni.
23 Hesabu ya kikosi hiki ni 35, 000
His army, and those who were numbered of them, were thirty-five thousand four hundred.
24 Wote waliohesabiwa katika kambi ya Efraimu ni 108, 100. Watakuwa wa tatu kuondoka.
"All who were numbered of the camp of Ephraim were one hundred eight thousand one hundred, according to their divisions. They shall set out third.
25 Upande wa kaskazini kutakuwa na kambi ya kikosi cha Dani. Kiongozi wa watu wa Dani ni Ahiezeri mwana wa Amishadai.
"On the north side shall be the standard of the camp of Dan according to their divisions: and the prince of the people of Dan shall be Ahiezer the son of Ammishaddai.
26 Hesabu ya kikosi hiki ni 62, 700.
His division, and those who were numbered of them, were sixty-two thousand seven hundred.
27 Watu wa kabila ya Asheri watapanga mbele ya Dani. Kiongozi wa Asheri ni Pagieli mwana wa Okirani.
"Those who camp next to him shall be the tribe of Asher: and the prince of the people of Asher shall be Pagiel the son of Ochran.
28 Hesabu ya Kikosi hiki ni 41, 500.
His division, and those who were numbered of them, were forty-one thousand and five hundred.
29 Kabila la Naftali ndilo litakalofuatia. Kiongozi wa Naftali ni Ahira mwana wa Enani.
"The tribe of Naphtali: and the prince of the people of Naphtali shall be Ahira the son of Enan.
30 Hesabu ya kikosi hiki ni 53, 400.
His division, and those who were numbered of them, were fifty-three thousand four hundred.
31 Wote waliohesabiwa kwenye kambi ya Dani ni 157, 600. Hawa watakuwa wa mwisho kuondoka kambini, wakifuata bango lao.
"All who were numbered of the camp of Dan were one hundred fifty-seven thousand six hundred. They shall set out last by their standards."
32 Hawa ndio Waisraeli, waliohesabiwa kufuata familia zao. Wote waliohesabiwa kwenye kambi zao, kwa kufuata vikosi vyao ni 603, 550.
These are those who were numbered of the children of Israel by their fathers' houses. All who were numbered of the camps according to their armies were six hundred three thousand five hundred fifty.
33 Lakini Musa na Haruni hawakujumuisha Walawi kwenye Hesabu ya Waisrael. Ilikuwa kama BWANA alivyokuwa amemwagiza Musa.
But the Levites were not numbered among the children of Israel; as the LORD commanded Moses.
34 Watu wa Israel walifanya yote ambayo BWANA alimwagiza Musa. Walipanga kwa kufuata mabango yao. Walisafiri kutoka kambini kwa kufuata jamaa zao, kwa mpangilio wa familia za koo zao.
Thus the children of Israel did. According to all that the LORD commanded Moses, so they camped by their standards, and so they set out, everyone by their families, according to their fathers' houses.

< Hesabu 2 >