< Hesabu 2 >

1 BWANA akasema na Musa na Haruni tena. Akamwambia,
And the LORD spoke unto Moses and unto Aaron, saying:
2 Kila mtu atapanga kulingana na mahali pake, pamoja na mabango ya baba zao. Watapanga kuzunguka hema ya kukutania kila upande.
'The children of Israel shall pitch by their fathers' houses; every man with his own standard, according to the ensigns; a good way off shall they pitch round about the tent of meeting.
3 Wale watakaopanga mashariki mwa hema ya kukutania, mahali ambapo juu huonekana wakati wa jua kuchomoza, ni makambi ya Yuda nao watakuwa katika kundi lao. Nashoni mwana wa Aminadabu ni kiongozi wa watu wa Yuda.
Now those that pitch on the east side toward the sunrising shall be they of the standard of the camp of Judah, according to their hosts; the prince of the children of Judah being Nahshon the son of Amminadab,
4 Idadi ya watu wa Yuda ni 74, 600.
and his host, and those that were numbered of them, threescore and fourteen thousand and six hundred;
5 Kabila la Isakari litapanga mbele ya Yuda. Nethaneli mwana wa Zuari ataliongoza jeshi la Isakari.
and those that pitch next unto him shall be the tribe of Issachar; the prince of the children of Issachar being Nethanel the son of Zuar,
6 Idadi ya kikosi chake ni wanaume 54, 000.
and his host, even those that were numbered thereof, fifty and four thousand and four hundred;
7 Kabila la Zabuloni litapanga mbele ya Isakari. Eliabu mwana wa Heloni ndiye atakayeliongoza jeshi la Zabuloni.
and the tribe of Zebulun; the prince of the children of Zebulun being Eliab the son of Helon,
8 Idadi ya kikosi chake ni 57, 400.
and his host, and those that were numbered thereof, fifty and seven thousand and four hundred;
9 Idadi yote ya kambi y a Yuda ni 186, 400. Watakuwa wa kwanza kuondoka.
all that were numbered of the camp of Judah being a hundred thousand and fourscore thousand and six thousand and four hundred, according to their hosts; they shall set forth first.
10 Upande wa kusini kutakuwa na kambi ya Reubeni katika kundi lao. Kiongozi wa kundi la Reubeni ni Elizuri mwana wa Shedeuri.
On the south side shall be the standard of the camp of Reuben according to their hosts; the prince of the children of Reuben being Elizur the son of Shedeur,
11 Idadi ya kikosi chake ni 46, 500.
and his host, and those that were numbered thereof, forty and six thousand and five hundred;
12 Simeoni atapanga mbele ya Reubeni. Kiongozi wa watu wa Simeoni ni Shelumieli mwana wa Zurishadai.
and those that pitch next unto him shall be the tribe of Simeon; the prince of the children of Simeon being Shelumiel the son of Zurishaddai,
13 Waliohesabiwa kwenye kikosi chake ni 59, 300.
and his host, and those that were numbered of them, fifty and nine thousand and three hundred;
14 Kabila la Gadi litafuatia. Kiongozi wa watu wa Gadi ni Eliasafu mwana wa Deuli.
and the tribe of Gad; the prince of the children of Gad being Eliasaph the son of Reuel,
15 Idadi ya kikosi chake ni 45, 650.
and his host, even those that were numbered of them, forty and five thousand and six hundred and fifty;
16 Wote waliohesabiwa kwenye kambi ya Reubeni, kulingana na kikosi chake, ni 151, 450. Watakuwa wa pili kuondoka.
all that were numbered of the camp of Reuben being a hundred thousand and fifty and one thousand and four hundred and fifty, according to their hosts; and they shall set forth second.
17 Kifuatacho, ni hema la kukutania kuondoka kambini pamoja na Walawi likiwa katikati ya kambi zote. Lazima waondoke hapo kambini kwa mpangilio huo kama walivyoingia kwenye kambi. Kila mwanamume lazima awe mahali pake kwa kufuata bango lake.
Then the tent of meeting, with the camp of the Levites, shall set forward in the midst of the camps; as they encamp, so shall they set forward, every man in his place, by their standards.
18 Migawanyiko ya kambi y Efraimu kufuata mahali pake. Kiongozi wa watu wa Efraimu ni Elishama mwana wa Amihudi.
On the west side shall be the standard of the camp of Ephraim according to their hosts; the prince of the children of Ephraim being Elishama the son of Ammihud,
19 Hesabu ya kikosi hiki ni 40, 500.
and his host, and those that were numbered of them, forty thousand and five hundred;
20 Baada ya hao lilifuata kabila la Manase. Kiongozi wa Manase ni Gamaliel mwana wa Pedazuri.
and next unto him shall be the tribe of Manasseh; the prince of the children of Manasseh being Gamaliel the son of Pedahzur,
21 Hesabu ya kikosi hiki ni 32, 200.
and his host, and those that were numbered of them, thirty and two thousand and two hundred;
22 Kabila litakalofuata ni la Benjamini. Kiongozi wa Benjamini n Abidani mwana wa Gidioni.
and the tribe of Benjamin; the prince of the children of Benjamin being Abidan the son of Gideoni,
23 Hesabu ya kikosi hiki ni 35, 000
and his host, and those that were numbered of them, thirty and five thousand and four hundred;
24 Wote waliohesabiwa katika kambi ya Efraimu ni 108, 100. Watakuwa wa tatu kuondoka.
all that were numbered of the camp of Ephraim being a hundred thousand and eight thousand and a hundred, according to their hosts; and they shall set forth third.
25 Upande wa kaskazini kutakuwa na kambi ya kikosi cha Dani. Kiongozi wa watu wa Dani ni Ahiezeri mwana wa Amishadai.
On the north side shall be the standard of the camp of Dan according to their hosts; the prince of the children of Dan being Ahiezer the son of Ammishaddai,
26 Hesabu ya kikosi hiki ni 62, 700.
and his host, and those that were numbered of them, threescore and two thousand and seven hundred;
27 Watu wa kabila ya Asheri watapanga mbele ya Dani. Kiongozi wa Asheri ni Pagieli mwana wa Okirani.
and those that pitch next unto him shall be the tribe of Asher; the prince of the children of Asher being Pagiel the son of Ochran,
28 Hesabu ya Kikosi hiki ni 41, 500.
and his host, and those that were numbered of them, forty and one thousand and five hundred;
29 Kabila la Naftali ndilo litakalofuatia. Kiongozi wa Naftali ni Ahira mwana wa Enani.
and the tribe of Naphtali; the prince of the children of Naphtali being Ahira the son of Enan,
30 Hesabu ya kikosi hiki ni 53, 400.
and his host, and those that were numbered of them, fifty and three thousand and four hundred;
31 Wote waliohesabiwa kwenye kambi ya Dani ni 157, 600. Hawa watakuwa wa mwisho kuondoka kambini, wakifuata bango lao.
all that were numbered of the camp of Dan being a hundred thousand and fifty and seven thousand and six hundred; they shall set forth hindmost by their standards.'
32 Hawa ndio Waisraeli, waliohesabiwa kufuata familia zao. Wote waliohesabiwa kwenye kambi zao, kwa kufuata vikosi vyao ni 603, 550.
These are they that were numbered of the children of Israel by their fathers' houses; all that were numbered of the camps according to their hosts were six hundred thousand and three thousand and five hundred and fifty.
33 Lakini Musa na Haruni hawakujumuisha Walawi kwenye Hesabu ya Waisrael. Ilikuwa kama BWANA alivyokuwa amemwagiza Musa.
But the Levites were not numbered among the children of Israel; as the LORD commanded Moses.
34 Watu wa Israel walifanya yote ambayo BWANA alimwagiza Musa. Walipanga kwa kufuata mabango yao. Walisafiri kutoka kambini kwa kufuata jamaa zao, kwa mpangilio wa familia za koo zao.
Thus did the children of Israel: according to all that the LORD commanded Moses, so they pitched by their standards, and so they set forward, each one according to its families, and according to its fathers' houses.

< Hesabu 2 >