< Hesabu 18 >

1 BWANA akamwambia Haruni, “Wewe, wana wako, na uzao wa baba yako watawajibika kwa dhambi zote zilizotendwa mahali patakatifu. Lakini wewe na wana wako pekee mtawajibika kwa uovu uliofanywa na yeyote mahali patakatifu.
Jehovah said to Aaron, "You and your sons and your fathers' house with you shall bear the iniquity of the sanctuary; and you and your sons with you shall bear the iniquity of your priesthood.
2 Na ndugu zako nao wa kabila ya Lawi, kabila la ukoo wako, utawaleta pamoja na wewe ili kwamba waweze kuungana na wewe ili wakusaidie wakati wewe na wanao mnapokuwa mnatumikia mbele ya hema ya amri ya agano.
Your brothers also, the tribe of Levi, the tribe of your father, bring near with you, that they may be joined to you, and minister to you: but you and your sons with you shall be before the tent of the testimony.
3 Watakutumikia wewe na hema yote. Hata hivyo, wasisogee karibu na chochote ndani ya mahali patakatifu au kitu chochote kilichounganishwa na madhabahu, vinginevyo wewe na wao mtakufa.
They shall keep your commands, and the duty of all the Tent: only they shall not come near to the vessels of the sanctuary and to the altar, that they not die, neither they, nor you.
4 Wataungana na wewe na kuitunza hema ya kukutania, kwa kazi zote zinazohusiana na hema. Mtu mgeni asikusogelee.
They shall be joined to you, and keep the responsibility of the Tent of Meeting, for all the service of the Tent: and a stranger shall not come near to you.
5 Wewe utaajibika kwa ajili ya mahali patakatifu na kwa ajili ya madhabahu ili kwamba hasira yangu isiwajilie watu wa Israeli tena.
"You shall perform the duty of the sanctuary, and the duty of the altar; that there be no more wrath on the children of Israel.
6 Tazama, Mmi mwenyewe nimewachagua ndugu zako wa kabila ya Walawi kutoka mioingoni mwa uzao wa Israeli. Wao ni zawadi kwako. walitolewa kwangu ili waifanye kazi inayohusiana na hema ya kukutania.
And as for me, look, I have taken your brothers the Levites from among the children of Israel; they are a gift to you, given to Jehovah, to do the service of the Tent of Meeting.
7 Lakini ni wewe pekee yako na wanao ndio mnaoruhusiwa kufanya kazi ya ukuhani kuhusiana na kila kitu kilichounganishwa na madhabahu na kitu chochote ndani ya lile pazia. Wewe mwenyewe lazima ukamilishe majukumu hayo. Mimi ninakupa ukuhani kama zawadi. Mgeni yeyote anayekaribia atauawa.”
You and your sons with you shall keep your priesthood for everything concerning the altar, and for that inside the veil; and you shall serve: I give you the priesthood as a service of gift: and the stranger who comes near shall be put to death."
8 Kisha BWANA akamwambia Haruni, “Tazama, Nimekupa majukumu ya kusimamia sadaka za kuinuliwa kwangu, na sadaka zengine takatifu ambazo wana wa Israeli wanatoa kwangu. Nimekupa sadaka hizi wewe na wana wako kuwa haki yako milele.
Jehovah spoke to Aaron, "I, look, I have given you the command of my wave offerings, even all the holy things of the children of Israel; to you have I given them by reason of the anointing, and to your sons, as a portion forever.
9 Hivi ni vitu vitakatifu sana, amabavyo visiteketezwe kwa moto: kutoka kwenye sadaka zao-kila sadaka ya unga, kila sadaka ya dhambi, na kila sadaka ya hatia- ni vitu vitakatifu sana kwa ajili yako na wana wako.
This shall be yours of the most holy things from the fire: every offering of theirs, even every meal offering of theirs, and every sin offering of theirs, and every trespass offering of theirs, which they shall render to me, shall be most holy for you and for your sons.
10 Sadaka hizi ni takatifu sana; kila mume lazima aile, kwa kuwa ni vitakatifu kwako.
You shall eat of it like the most holy things. Every male shall eat of it. It shall be holy to you.
11 Hizi ni sadaka ambazo zitakuwa zako: Sadaka zao, sadaka zote za kuinuliwa za wana wa Israeli. Nimekupa wewe, wana wako na binti zako kuwa gawio lako la milele. Kila mmoja ambaye ni msafi katika familia yako anaweza kula sadaka zozote katika hizi.
"This is yours, too: the wave offering of their gift, even all the wave offerings of the children of Israel. I have given them to you, and to your sons and to your daughters with you, as a portion forever. Everyone who is clean in your house shall eat of it.
12 Mafuta yote mazuri, ile divai nzuri yote mpya na unga, malimbuko ambyo watu hutoa kwangu- vitu hivi vyote nimekupa wewe.
"All the best of the oil, and all the best of the vintage, and of the grain, the first fruits of them which they give to Jehovah, to you have I given them.
13 Mavuno ya kwanza yaliyoiva yaliyo katika ardhi yao ambayo wanaleta kwangu, yatakuwa yako. Kila mtu aliye msafi kwenye famila yako anaweza kula vitu hivi.
The first-ripe fruits of all that is in their land, which they bring to Jehovah, shall be yours; everyone who is clean in your house shall eat of it.
14 Kila kitu kilichotolewa wakfu katika Israeli kitakuwa chako.
"Everything devoted in Israel shall be yours.
15 Kila kitu kinachofungua tumbo, kila limbuko ambalo watu hutoa kwa BWANA, vyote vya watu na wanyama, vitakuwa vyako. Hata hivyo, watu lazima wawakomboe wazaliwa wa kwanza wa kiume, na watawakomboa wazaliwa wa kwanza wa wanyama wasio safi.
Everything that opens the womb, of all flesh which they offer to Jehovah, both of man and animal shall be yours: nevertheless you shall surely redeem the firstborn of man, and you shall redeem the firstborn of unclean animals.
16 Wale ambao wanahitaji kukombolewa na watu watakombolewa wakiwa na umri wa mwezi mmoja. Ndipo watu watawakomboa kwa bei ya shekeli tano, kwa kiwango cha shekeli za mahali patakatifu, ambacho ni sawa na gera ishirini.
You shall redeem those who are to be redeemed of them from a month old, according to your estimation, for five shekels of money, after the shekel of the sanctuary, which is twenty gerahs.
17 Lakini mzaliwa wa kwanza wa ng'ombe, au mzaliwa wa kwana wa kondoo, au mzaliwa wa kwanza wa mbuzi-msiwakomboe hawa wanyama, wametengwa kwa ajili yangu. Utanyunyizia damu yake madhabahuni na kuteketeza mafuta yao kama sadaka ya moto, ambayo ni harufu nzuri ya kumpendeza BWANA.
"But you shall not redeem the firstborn of a cow, or the firstborn of a sheep, or the firstborn of a goat. They are holy. You shall sprinkle their blood on the altar, and shall burn their fat for an offering made by fire, for a pleasant aroma to Jehovah.
18 Nyama yao itakuwa yako. Kama kidali cha kuinuliwa na paja la kulia, nyama yao itakuwa yako.
Their flesh shall be yours, as the wave offering breast and as the right thigh, it shall be yours.
19 Sadaka yote takatifu ambayo watu wa Israeli wanaitoa kwa BWANA, nimekupa wewe, na wana wako na binti zako walio pamoja nawe. Kama gawio la kudumu. Hili ni agano la milele la chumvi, agano linalofunga milele, mbele za BWANA kwako wewe na uzao wako walio pamoja na wewe.”
All the wave offerings of the holy things, which the children of Israel offer to Jehovah, have I given you, and your sons and your daughters with you, as a portion forever: it is a covenant of salt forever before Jehovah to you and to your descendants with you."
20 BWANA akasema na Haruni. “hautakuwa na urithi katika ardhi ya watu, wala hautakuwa na gawio miongoni mwa watu. Mimi ndimi gawiio lenu na urithi wenu miongoni mwa watu wa Israeli.
Jehovah said to Aaron, "You shall have no inheritance in their land, neither shall you have any portion among them. I am your portion and your inheritance among the children of Israel.
21 Tazama, Nimewapatia uzao wa Lawi, zaka zote za Israeli kuwa urithi wao kwa sababu ya huduma wanayotoa katika hema ya kukutania.
"To the descendants of Levi, look, I have given all the tithe in Israel for an inheritance, in return for their service which they serve, even the service of the Tent of Meeting.
22 Kuanzi a sasa, watu wa Israeli wasisogee karibu na hema ya kukutania, vinginevyo wataajibika kwa dhambi hii na kufa.
Hereafter the children of Israel shall not come near the Tent of Meeting, lest they bear sin, and die.
23 Walawi wafanya kazi inayohusiana na hema ya kukutania. Wataajibika kwa dhambi inyohusiana na hema. Hii itakuwa sheri ya kudumu kwa watu wote wa uzao wako. Na miongoni mwa watu wa Israeli hawa hawatakuwa na urithi.
But the Levites shall do the service of the Tent of Meeting, and they shall bear their iniquity: it shall be a statute forever throughout your generations; and among the children of Israel they shall have no inheritance.
24 Kwa kuwa zaka za wana wa Israeli, wanazotoa kama mchango kwangu -ndivyo hivyo ambavyo nimewapa Walawi kuwa urithi wao. Hiyo ndiyo sababu ya kuwaambia, Kuwa hawatakuwa na urithi kati ya watu wa Israeli.
For the tithe of the children of Israel, which they offer as a wave offering to Jehovah, I have given to the Levites for an inheritance: therefore I have said to them, 'Among the children of Israel they shall have no inheritance.'"
25 BWANA akanena na Musa, akamwambia,
Jehovah spoke to Moses, saying,
26 “Inakupasa ukaseme na Walawi uwaambie, 'Mnapopokea zaka toka kwa watu ambayo BWANA amewapa kutoka kwao kuwa urithi, ndipo na nyie mtakapotoa sehemu ya kumi ya zaka hizo.
"Moreover you shall speak to the Levites, and tell them, 'When you take of the children of Israel the tithe which I have given you from them for your inheritance, then you shall offer up a wave offering of it for Jehovah, a tithe of the tithe.
27 Zaka yenu itahesabika kama moja ya mapato ya sakafu ya kupuria nafaka ya mazao yenu au mazao ya vinu vya kukamulia zabibu.
Your wave offering shall be reckoned to you, as though it were the grain of the threshing floor, and as the fullness of the winepress.
28 Kwa hiyo na ninyi lazima mtoe mchango wenu kwa BWANA kutokana na zaka mnazopata kutoka kwa watu wa Israeli. Kutokana na hizo mtatoa matoleo yenu kwa Haruni yule kuhani.
Thus you also shall offer a wave offering to Jehovah of all your tithes, which you receive of the children of Israel; and of it you shall give Jehovah's wave offering to Aaron the priest.
29 Kwa kila sadaka mnayopata, mtatoa matoleo yenu kwa BWANA. Mtafanya hivi kutokana na vitu vizuri na vitakatifu sana ambavyo mmepewa.
Out of all your gifts you shall offer every wave offering of Jehovah, of all its best, even the holy part of it out of it.'
30 Kwa hiyo utawaambia, 'Mnapotoa hayo matoleo mazuri, ndipo itahesabika kwa Walawi kuwa ni mazao yao kutoka kwenye sakafu za kupuria na vinu vyao vya kukamulia.
"Therefore you shall tell them, 'When you heave its best from it, then it shall be reckoned to the Levites as the increase of the threshing floor, and as the increase of the winepress.
31 Ndipo matakapokula nafaka zote zinazobaki mahali popote, ninyi na famailia zenu kwa sababu ndiyo malipo yenu ya kazi y a kwenye hema ya kukutania.
You shall eat it in every place, you and your households: for it is your reward in return for your service in the Tent of Meeting.
32 Hamtakuwa na hatia yeyote kwa kuvila na kuvinywa, kama mtatoa kwa BWANA matoleo yenu mazuri mliyopokea. Lakini msizinajisi sadaka takatifu za wana wa Israeli, vinginevyo mtakufa.,”
You shall bear no sin by reason of it, when you have heaved from it its best: and you shall not profane the holy things of the children of Israel, that you not die.'"

< Hesabu 18 >