< Hesabu 17 >

1 BWANA akanena na Musa, akasema,
And the LORD spoke unto Moses, saying:
2 “Waambie wana wa Israeli wakuletee fimbo za kutembelea moja kwa kila jamaa, fimbo kumi na mbili. Uandika jina la kila mmoja kwenye hizo fimbo.
'Speak unto the children of Israel, and take of them rods, one for each fathers' house, of all their princes according to their fathers' houses, twelve rods; thou shalt write every man's name upon his rod.
3 Utaandika jina la Haruni kwenye jina la Lawi. Kutakuwa na fimbo moja kwa kila kiongozi kutoka kwenye kabila la mababu zake.
And thou shalt write Aaron's name upon the rod of Levi, for there shall be one rod for the head of their fathers' houses.
4 Utaziweka hizo fimbo kwenye hema ya kukutania mbele ya amri za agano, ambapo Mimi hukutana na wewe. Itakuwa hivi,
And thou shalt lay them up in the tent of meeting before the testimony, where I meet with you.
5 fimbo ya mtu yule ninayemchagua itachipua. Nitazuia watu wa Israeli walalamikao, ambao wanaongea kinyume na wewe.”
And it shall come to pass, that the man whom I shall choose, his rod shall bud; and I will make to cease from Me the murmurings of the children of Israel, which they murmur against you.'
6 Kwa hiyo Musa akawaambia wana wa Israeli. Viongozi wote wa kabila wakampatia fimbo, fimbo moja kutoka kwa kila kiongozi, aliyechaguliwa kutoka kwenye kila kabila ya babu zao, jumla yake fimbo kumi na mbili. Fimbo ya Haruni ilikuwa miongoni mwa fimbo hizo.
And Moses spoke unto the children of Israel; and all their princes gave him rods, for each prince one, according to their fathers' houses, even twelve rods; and the rod of Aaron was among their rods.
7 Ndipo Musa alipoziweka zile fimbo mbele ya BWANA katika hema ya amri ya agano.
And Moses laid up the rods before the LORD in the tent of the testimony.
8 Siku iliyofuata Musa aliingia kwenye hema ya amri ya agano, na tazama, fimbo ya Haruni kwa ajili ya Kabila la Lawi ilikuwa imetoa machipukizi. Machipukizi yalikuwa hadi kuchanua maua na kuzaa malozi mabivu!
And it came to pass on the morrow, that Moses went into the tent of the testimony; and, behold, the rod of Aaron for the house of Levi was budded, and put forth buds, and bloomed blossoms, and bore ripe almonds.
9 Musa akazitoa fimbo zote kutoka kwa BWANA kwa watu wote wa Israeli, na kila mtu akachukua fimbo yake.
And Moses brought out all the rods from before the LORD unto all the children of Israel; and they looked, and took every man his rod.
10 BWANA akamwambua Musa, “Iweke fimbo ya Haruni mbele ya amri za agano. Iweke iwe ishara ya hatia mbele ya watu waliopinga ili ukomeshe malalamiko dhidi yangu, vinginevyo watakufa.”
And the LORD said unto Moses: 'Put back the rod of Aaron before the testimony, to be kept there, for a token against the rebellious children; that there may be made an end of their murmurings against Me, that they die not.'
11 Musa akafanya kama BWANA alivyoagiza.
Thus did Moses; as the LORD commanded him, so did he.
12 Wana wa Israeli wakanena na Musa wakisema, “tutakufa hapa! Wote tutaangamia!
And the children of Israel spoke unto Moses, saying: 'Behold, we perish, we are undone, we are all undone.
13 Kila mmoja anayekuja hapa, anayekaribia masikani ya BWANA, atakufa. Je, ni lazima wote tuangamie?”
Every one that cometh near, that cometh near unto the tabernacle of the LORD, is to die; shall we wholly perish?'

< Hesabu 17 >