< Hesabu 15 >

1 Kisha BWANA akanena na Musa, akasema,
Adonai spoke to Moses [Drawn out], saying,
2 “Sema na wana wa Israeli uwaambie, 'Mtakapoingia katka nchi ambayo mtaishi, ambayo BWANA atawapa,
“Speak to the children of Israel [God prevails], and tell them, ‘When you have come into the land of your habitations, which I give to you,
3 mtatakiwa kuandaa sadaka kwa moto kwa BWANA, sadaka ya kuteketezwa au sadaka ya kukamilisha kiapo au sadaka ya hiari, au sadaka katika sikukuu zenu, ili kutoa harufu nzuri kwa BWANA ya ng'ombe au ya kondoo.
and will make an offering by fire to Adonai, a burnt offering, or a sacrifice, to accomplish a vow, or as a free will offering, or in your set feasts, to make a pleasant aroma to Adonai, of the herd, or of the flock;
4 Utamtolea BWANA sadaka ya kuteketezwa pamoja na sehemu ya kumi ya efa ya sadaka ya unga mwembamba uliochanganywa na robo ya hini ya mafuta.
then he who offers his offering shall offer to Adonai a meal offering of one tenth of an ephah [an omer; 2.3 q; 2.2 L] of fine flour mixed with the fourth part of a hin [2.6 qt; 1.2 L] of oil.
5 Na tena mtatoa pamoja na sadaka ya kuteketezwa, au kwa sadaka ya divai robo ya hini ya sadaka ya vinywaji kwa kila mwanakondoo.
You shall prepare wine for the drink offering, the fourth part of a hin [2.6 qt; 1.2 L], with the burnt offering, or for the sacrifice, for each lamb.
6 Kama unatoa sadaka ya kondoo dume, utaandaa sadaka ya unga ya sehemu za kumi mbili za efa ya unga mwembamba uliochanganywa na sehemu ya tatu ya hini ya divai.
“‘Or for a ram, you shall prepare for a meal offering one tenth of an ephah [two omers; 4.6 q; 4.4 L] of fine flour mixed with the third part of a hin [2.6 qt; 1.24 L] of oil;
7 Kwa sadaka ya kinywaji, mtatoa sehemu ya tatu ya hini ya divai ambayo itatoa harufu nzuri kwa BWANA.
and for the drink offering you shall offer the third part of a hin [2.6 qt; 1.24 L] of wine, of a pleasant aroma to Adonai.
8 Utakapoandaa fahari kwa ajiliy a sadaka ya kuteketezwa au sadaka ya kutimiza kiapo, au sadaka ya amani kwa BWANA,
When you prepare a bull for a burnt offering, or for a sacrifice, to accomplish a vow, or for peace offerings to Adonai;
9 Ndipo utakapotoa sadaka ya fahari pamoja na sadaka ya unga ya sehemu za kumi tatu za unga mwembamba uliochanganywa na nusu ya hini ya mafuta.
then shall he offer with the bull a meal offering of three tenths of an ephah [three omers; 6.9 q; 6.6 L] of fine flour mixed with half a hin [5.2 qt; 2.4 L] of oil:
10 Mtatoa sadaka ya kinywaji nusu ya hini ya divai, sadaka iloyotengenezwa kwa moto ili kufanya harufu nzuri kwa BWANA.
and you shall offer for the drink offering half a hin [5.2 qt; 2.4 L] of wine, for an offering made by fire, of a pleasant aroma to Adonai.
11 Itafanyika hivi kwa kila fahari, kwa kila kondoo dume, na kila mwanakondoo dume au mbuzi mchanga.
Thus shall it be done for each bull, or for each ram, or for each of the male lambs, or of the young goats.
12 Kila sdaka utakayoindaa na kuitoa itafanyika kama ilivyoanishwa hapa.
According to the number that you shall prepare, so you shall do to everyone according to their number.
13 Wazawa wote wa Israeli watafanya mambo haya kwa utaratibu huu, yeyote atakayeleta sadaka iliyotengenezwa kwa moto, ili kufanya harufu nzuri kwa BWANA.
“‘All who are native-born shall do these things in this way, in offering an offering made by fire, of a pleasant aroma to Adonai.
14 Na kama kuna mgeni anayeishi kati yenu, au yeyote atakayeishi na watu wa vizazi vyenu vyote, lazima atengeneze sadaka iliytoengenezwa kwa moto, ili kutoa harufu nzuri kwa BWANA. Atafanya kama mnavyofanya.
If a stranger lives as a foreigner with you, or whoever may be among you throughout all your generations, and will offer an offering made by fire, of a pleasant aroma to Adonai; as you do, so he shall do.
15 Kutakuwa na sheria hiyo hiyo kwa watu wote na kwa mgeni anayeishi kati yenu, sheria ya kudumu kwa watu wote wa uzao wako. Ninyi mlivyo, ndivyo atakavyokuwa mgeni aliyeishi kati yenu. Atafanya kama mnavyofanya mbele ya BWANA.
For the assembly, there shall be one statute for you and for the stranger who lives as a foreigner, a statute forever throughout all your generations. As you are, so shall the foreigner be before Adonai.
16 Sheria na amri hiyohiyo ndiyo itakayotumika kwa mgeni anayeishi kati yenu.”
One Torah ·Teaching· and one judgement shall be for you, and for the stranger who lives as a foreigner with you.’”
17 Tena BWANA akanena na Musa, akasema,
Adonai spoke to Moses [Drawn out], saying,
18 “Nena wana wa Israeli uwaambie, 'mtakapofika katika nchi ninayowapeleka,
“Speak to the children of Israel [God prevails], and tell them, ‘When you come into the land where I bring you,
19 mtakapokula chakula kinachozalishwa katika nchi hiyo, mtatoa sadaka ya kunipendeza mimi.
then it shall be that when you eat of the bread of the land, you shall offer up a wave offering to Adonai.
20 Kutoka kwenye mikate yenu ya kwanza mtatoa mkate wa kuinuliwa kama sadaka iliyoinuliwa kutoka mahali pa kupuria nafaka. Mtaiinua kwa jinsi hii.
Of the first of your dough you shall offer up a cake for a wave offering. As the wave offering of the threshing floor, so you shall heave it.
21 Watu wa uzao wako wote wtanitolea sadaka ya kuinuliwa kutoka kwenye unga wenu wa kwanza.
Of the first of your dough, you shall give to Adonai a wave offering throughout all your generations.
22 Wakati mwingine mtafanya dhambi pasipo kukusudia, Kama hamtatii amri zote hizi ambazo nimemwambia Musa
“‘If by mistake you fail to observe all these mitzvot ·instructions·, which Adonai has spoken to Moses [Drawn out],
23 -kila kitu ambacho nimewaamuru kupitia Musa kuanzia siku ambayo nilianza kuwaamuru na kuendelea kwa watu wote wa uzao wako.
even all that Adonai has enjoined you by Moses [Drawn out], from the day that Adonai gave commandment, and onward throughout all your generations;
24 Kwa swala la dhambi isiyokusudiwa ambayo watu wote hawaijui, basi watu wote watatoa fahari mchanga sadaka ya kuteketezwa ili kufanya harufu nzuri kwa BWANA. Pamoja na haya yote, lazima itengenezwe sadaka ya unga na sadaka ya kinywaji, kama ilivyoagaizwa katika amri, na beberu mmoja kuwa sadaka ya dhambi.
then it shall be, if it was done unwittingly, without the knowledge of the congregation, that all the congregation shall offer one young bull for a burnt offering, for a pleasant aroma to Adonai, with its meal offering, and its drink offering, according to the judgement, and one male goat for a sin offering.
25 Kuhani atafanya sadaka upatanisho kwa watu wote wa Israeli. Watasemehewa kwa sababu dhambi haikukusudiwa. Wametoa sadaka yao, sadaka iliyotengenezwa kwa moto kwa ajili yangu. Wameleta sadaka yao kwangu iliyotengenezwa kwa moto. Wameleta sadaka yao ya uovu mbele yangu kwa ajili ya kosa lao.
The priest shall make atonement for all the congregation of the children of Israel [God prevails], and they shall be forgiven; for it was an error, and they have brought their offering, an offering made by fire to Adonai, and their sin offering before Adonai, for their error.
26 Ndipo watu wote wa Israeli watasamehewa, pia wageni wote wanaoishi kati yao, kwa sababu watu wote walitenda dhambi pasipo kukusudia.
All the congregation of the children of Israel [God prevails] shall be forgiven, as well as the stranger who lives as a foreigner among them; for with regard to all the people, it was done unwittingly.
27 Kama mtu atatenda dhambi bila kukusudia, atatoa mbuzi jike wa umri wa mwaka mmoja kuwa sadaka ya dhambi.
“‘If one person sins unwittingly, then he shall offer a female goat a year old for a sin offering.
28 Naye kuhani atafanya upatanisho kwa BWANA kwa ajili ya mtu yule aliyefanya dhambi pasipo kukusudia. Yule mtu atasamehewa baada ya upatanisho kufanyika.
The priest shall make atonement for the soul who errors, when he sins unwittingly before Adonai, to make atonement for him; and he shall be forgiven.
29 Mtakuwa na sheria hiyohiyo kwa mtu yeyote anayefanya dhambi hiyo pasipo kukusudia, sheria hiyohiyo hata kwa mzawa wa Isreli na kwa wageni wanaoishi kati yao.
You shall have one Torah ·Teaching· for him who does anything unwittingly, for him who is native-born among the children of Israel [God prevails], and for the stranger who lives as a foreigner among them.
30 Lakini mtu afanyaye chochote kwa KUkusudia, awe mzawa au mgeni, ananikufuru mimi. Huyo mtu ataondolewa kati ya watu wake.
“‘But the soul who does anything with a high hand, whether he is native-born or a foreigner, the same blasphemes Adonai. That soul shall be cut off from among his people.
31 Kwa sababu atakuwa amedharau neno langu na amevunja neno amri yangu, mtu huyo ataondolewa kabisa. Dhambi yake itakuwa juu yake.'”
Because he has despised Adonai’s word, and has broken his order, that soul shall utterly be cut off. His iniquity shall be on him.’”
32 Wakati wana wa Israeli walipokuwa katika jangwa, wakamuona mwanamume akikusanya kuni sikiu ya Sabato.
While the children of Israel [God prevails] were in the wilderness, they found a man gathering sticks on the Sabbath ·To cease· day.
33 Wale waliomwona wakamleta kwa Musa, Haruni na kwa watu wote.
Those who found him gathering sticks brought him to Moses [Drawn out] and Aaron [Light-bringer], and to all the congregation.
34 Wakamweka kifungoni kwa sababu ilikuwa haijaamuliwa atakachotendewa.
They put him in custody, because it had not been declared what should be done to him.
35 Kisha BWANA akanena na Musa, “Yule mwanamume lazima auawe. Watu wote lazima wampige kwa mawe nje ya kambi.”
Adonai said to Moses [Drawn out], “The man shall surely be put to death. All the congregation shall stone him with stones outside of the camp.”
36 Kwa hiyo watu wote wakamtoa nje ya kambi nao wakampiga kwa mawe mpaka akafa kama vile BWANA alivyokuwa amemwamuru Musa.
All the congregation brought him outside of the camp, and stoned him to death with stones, as Adonai enjoined Moses [Drawn out].
37 BWANA akanena na Musa tena, akasema,
Adonai spoke to Moses [Drawn out], saying,
38 “Waambie wana wa Israeli na uwaamuru wajifanyie vishada wavining'inize katika mapindo ya mavazi yao, wavining'ineze katika ncha zote kwa nyuzi za rangi ya samawi. Watu wote watafanya hivi kwa watu wote wa kizazi chote.
“Speak to the children of Israel [God prevails], and tell them that they should make themselves fringes in the borders of their garments throughout their generations, and that they put on the fringe of each border a cord of blue:
39 Huu utakuwa ukumbusho maalumu kwenu, kila mtakapovitazama, mtakumbuka amri zangu, na kuzishika ili kwamba msije mkatangatanga katika mioyo na macho yenu na kuwa waasherati wa hayo.
and it shall be to you for a fringe, that you may look on it, and remember all Adonai’s mitzvot ·instructions·, and do them; and that you not follow after your own heart and your own eyes, after which you use to play the prostitute;
40 Fanyeni hivi ili kwamba mweze kukumbuka na kutii amri zangu zote, na ili kwamba mpate kuwa watakatifu, waliotunzwa kwa ajili yangu, Mungu wenu.
that you may remember and do all my mitzvot ·instructions·, and be holy to your God.
41 Mimi ndimi BWANA Mungu wenu niliyekutoa toka nchi ya Misri, ili niwe Mungu wenu. Mimi ndimi BWANA Mungu wenu.”
I am Adonai your God, who brought you out of the land of Egypt [Abode of slavery], to be your God: I am Adonai your God.”

< Hesabu 15 >