< Hesabu 14 >

1 Usiku huo watu wote walilia kwa sauti.
All the congregation lifted up their voice, and cried; and the people wept that night.
2 Watu wote wa Israeli wakamlalamikia Musa na Haruni. Watu wote wakawaambia, “Ni bora kama tungelifia katika nchi ya Misri, au katika hili!
All the children of Israel murmured against Moses and against Aaron: and the whole congregation said to them, "Would that we had died in the land of Egypt, or would that we had died in this wilderness.
3 Kwa nini BWANA alituleta katika nchi hii ili tufe kwa upanga? Wake zetu na watoto wetu watakuwa watumwa wao. Je, si bora kwetu kurudi Misri?”
Why does Jehovah bring us to this land, to fall by the sword? Our wives and our little ones will be a prey: wouldn't it be better for us to return into Egypt?"
4 Wakasemezana wao kwa wao, “Na tuchague kiongozi mwingine, turudi Misri.”
And they said to one another, "Let us make a captain, and let us return into Egypt."
5 Ndipo Musa na Haruni wakalala kifudifudi mbele ya kundi lote la wana wa Israeli.
Then Moses and Aaron fell on their faces before all the assembly of the congregation of the children of Israel.
6 Joshua mwana wa Nuni na Kalebu mwana wa Yefune, ambao walikuwa miongoni mwa wale waliokuwa waemtumwa kwenda kuipeleleza nchi wakachana mavazi yao.
Joshua the son of Nun and Caleb the son of Jephunneh, who were of those who spied out the land, tore their clothes:
7 Wakawaambia watu wote wa Israeli. Walisema, “Ile nchi tuliyopita katikati yake ni nchi nzuri sana.
and they spoke to all the congregation of the children of Israel, saying, "The land, which we passed through to spy it out, is an exceeding good land.
8 Kama BWANA amependezwa nasi, basi atatuingiza katika nchi hii na kutupatia. Ile nchi inatiririka maziwa na asali.
If Jehovah delights in us, then he will bring us into this land, and give it to us; a land which flows with milk and honey.
9 Lakini msimwasi BWANA, na msiwahofie hao wakazi wa nchi hiyo. Tutawateketeza kwa urahisi kama kula chakula. Ulinzi wao utaondolewa kutoka kwao, kwa sababu BWANA yuko pamoja nasi. Msiwahofie.”
Only do not rebel against Jehovah, neither fear the people of the land; for they are bread for us: their defense is removed from over them, and Jehovah is with us. Do not fear them."
10 Lakini watu wote walitishia kuwapiga kwa mawe mpaka wafe. Kisha utukufuwa BWANA ukaonekana kwenye hema ya kukutania kwa watu wote wa Israeli.
But all the congregation threatened to stone them with stones. Then the glory of Jehovah appeared at the Tent of Meeting to all the children of Israel.
11 BWANA akamwambi Musa, “watu hawa watanidharau hadi lini? Wataendelea kutoniamini mpaka lini? Nijapokuwa nimefanya ishara kwa nguvu zangu kati yao?
Jehovah said to Moses, "How long will this people despise me? And how long will they not believe in me, for all the signs which I have worked among them?
12 Nitawapiga kwa mapigo, na kuwaondolea urithi, na kufanya taifa kubwa kutoka kwenye ukoo wako ambalo litakuwa kubwa na lenye nguvu kuliko wao.
I will strike them with the pestilence, and disinherit them, and I will make of you and your father's house a nation greater and mightier than they."
13 Musa akamwambia BWANA, “Kama utafanya hivi, Na Wamisiri wakisikia habari hizi, na kwa sababu uliwaokoa kutoka kwao kwa nguvu zako.
Moses said to Jehovah, "Then the Egyptians will hear it; for you brought up this people in your might from among them;
14 Basi watawaambia wakazi wa nchi hii. Wamesikia ya kuwa wewe BWANA u kati ya watu hawa, kwa sababu uso wako waonekana. Wingu lako husimama juu ya watu wetu. Wewe huwatangulia katika nguzo ya wingu wakati wa mchana na katika nguzo ya moto wakati wa usiku.
and they will tell it to the inhabitants of this land. They have heard that you Jehovah are in the midst of this people; for you Jehovah are seen face to face, and your cloud stands over them, and you go before them, in a pillar of cloud by day, and in a pillar of fire by night.
15 Sasa kama utawaua hawa watu kama mtu mmoja, basi mataifa ambao wamesikia sifa zako watasema,
Now if you killed this people as one man, then the nations which have heard the fame of you will speak, saying,
16 “Kwa Sababu BWANA hana uwezo wa kuwapeleka watu hawa katika nchi ambayo aliwaapia kuwapa, ndiyo maana amewaua katika jangwa hili.'
'Because Jehovah was not able to bring this people into the land which he swore to them, therefore he has slain them in the wilderness.'
17 Sasa, nakusihi, utumie uweza wako. Kwa kuwa umesema kuwa,
Now please let the power of the Lord be great, according as you have spoken, saying,
18 'BWANA si mwepesi wa hasira na ni mwingi wa uaminifu katika agano. Yeye husamehe uovu na uasi. Kwa vyovyote vile atafutilia hatia atakapoleta hukumu ya dhambi za mababu juu ya wazao wao, kwa kizazi cha tatu na cha nne.'
'Jehovah is slow to anger, and abundant in loving kindness, forgiving iniquity and disobedience; and that will by no means clear [the guilty], visiting the iniquity of the fathers upon the children, and upon the children's children, upon the third and upon the fourth [generation].'
19 Ninakusihi uwasameha watu hawa dhambi zao kwa sababu ya ukuu wa uaminifu wa agano lako, kama vile ambavyo umekuwa ukiwasamehe watu hawa tokea wakati wakiwa Misri mpaka sasa.”
Please pardon the iniquity of this people according to the greatness of your loving kindness, and according as you have forgiven this people, from Egypt even until now."
20 BWANA akasema, Nimewasamehe kwa kama ulivyoomba,
Jehovah said, "I have pardoned according to your word.
21 bali kama Niishivyo, na kama vile dunia yote itakavyojazwa na utukufu wangu,
But truly, as I live, and as all the earth shall be filled with the glory of Jehovah;
22 watu wote walioona utukufu wangu na ishara za nguvu zangu nilizotenda kule Misri na kule jangwani - Lakini bado wamenijaribu mara kumi sasa na hawakuisikiliza sauti yangu.
because all those men who have seen my glory, and my signs, which I worked in Egypt and in the wilderness, yet have tempted me these ten times, and have not listened to my voice;
23 Kwa hiyo nasema kwamba hakika hawataiona nchi ile ambayo niliwaahdi kuwapa mababu zao. Hakuna hata mmoja wao ambao wamenidharau watakaoiona,
surely they shall not see the land which I swore to their fathers, neither shall any of those who despised me see it:
24 isipokuwa mtumishi wangu Kalebu, kwa sababu alikuwa na roho nyingine. Yeye amenifuata kwa ukamilifu; Yeye nitampeleka katika nchi hiyo ambayo alienda kuipeleleza. Wazao wake wataimilki.
but my servant Caleb, because he had another spirit with him, and has followed me fully, him will I bring into the land into which he went; and his descendants shall possess it.
25 (Sasa Waamaleki na Wakanani waliishi katika bonde.) Kesho mtageuka na kwenda katika jangwa kwa njia ya bahari ya Shamu.”
Now the Amalekite and the Canaanite dwell in the valley: tomorrow turn, and go into the wilderness by the way to the Red Sea."
26 BWANA akanena na Musa na Haruni, akasema,
Jehovah spoke to Moses and to Aaron, saying,
27 “Nitaivumilia jamii ya watu hawa waovu ambao wananinung'unikia mpaka lini? Nimeyasikia malalamiko ya wana wa Israeli dhidi yangu.
"How long shall I bear with this evil congregation, that murmur against me? I have heard the murmurings of the children of Israel, which they murmur against me.
28 Waambie, 'Kama niishivyo,' asema BWANA, 'kama vile mlivyosema katika masikio yake, nitawafanyia jambo hili:
Tell them, 'As I live, says Jehovah, surely as you have spoken in my ears, so will I do to you:
29 Maiti zenu zitaanguka katika jangwa hili, Ninyi nyote mliolalamika dhidi yangu, ninyi mliohesabiwa kwenye ile sensa, idadi yote ya watu kuanzia umri wa mika ishirini na kuendelea.
your dead bodies shall fall in this wilderness; and all who were numbered of you, according to your whole number, from twenty years old and upward, who have murmured against me,
30 Kwa hakika hamtaingia kwenye ile nchi ambayo niliahidi kuwapa kuwa makazi yenu, isipokuwa Kalebu mwana wa Yefune na Joshua mwana wa Nuni.
surely you shall not come into the land, concerning which I swore that I would make you dwell in it, except Caleb the son of Jephunneh, and Joshua the son of Nun.
31 Bali watoto wenu ambao mlisema kuwa watakuwa watumwa, wao ndio nitakaowapeleka katika nchi hiyo. Wao wataifurahia nchi ambayo nInyi mmeikataa!
But your little ones, that you said should be a prey, them will I bring in, and they shall know the land which you have rejected.
32 Lakini ninyi, maiti zenu zitaanguka katika jangwa hili.
But as for you, your dead bodies shall fall in this wilderness.
33 Watoto wenu watakuwa wachungaji katika jangwa hili kwa muda wa miaka arobaini. Lazima watabeba madhara ya matendo yenu ya kutokuamini mpaka mwisho wa maiti ya mwisho jangwani.
Your children shall be wanderers in the wilderness forty years, and shall bear your prostitution, until your dead bodies be consumed in the wilderness.
34 Kama vile ilivyo hesabu ya siku ambayo mliipeleleza nchi—siku arobaini, vivyo hivyo mtabeba madhara ya dhambi zenu kwa muda wa miaka arobaini—mwaka mmoja kwa kila siku moja, na mtajua kuwa ni sawa na kuwa adui yangu.
After the number of the days in which you spied out the land, even forty days, for every day a year, you will bear your iniquities, even forty years, and you will know my alienation.'
35 Mimi BWANA nimesema. Hakika nitafanya hivi kwa kizazi hiki chote kiovu ambacho kimekusanyika kinyume na Mimi. Wao watakatwa kabisa, na watafia hapa.'”
I, Jehovah, have spoken, surely this will I do to all this evil congregation, who are gathered together against me: in this wilderness they shall be consumed, and there they shall die."
36 Kwa hiyo wale wanaume ambao Musa aliwatuma kwenda kuingalia ile nchi wote walikufa kwa tauni mbele ya BWANA.
The men, whom Moses sent to spy out the land, who returned, and made all the congregation to murmur against him, by bringing up an evil report against the land,
37 Hawa ni wale ambao waliorudi na kutoa taarifa mbaya juu ya nchi. Hii iliwafanya watu wote wamlalamikie Musa.
even those men who brought up an evil report of the land, died by the plague before Jehovah.
38 Kati ya watu wale waliokuwa wameenda kuiangalia nchi ile, ni Joshua mwana wa Nuni na Kalebu mwana wa Yefune tu ndio waliobaki hai.
But Joshua the son of Nun, and Caleb the son of Jephunneh, remained alive of those men who went to spy out the land.
39 Musa alipowataarifu mambo haya watu wote wa Israeli waliomboleza sana.
Moses told these words to all the children of Israel: and the people mourned greatly.
40 Waliamka asubuhi na mapema wakaenda juu ya mlima na kisha wakasema, “Tazama, tuko hapa, na tutaenda mahali pale ambapo BWANA ametuahidi, kwa kuwa tumetenda dhambi.”
They rose up early in the morning, and went up to the top of the mountain, saying, "Look, we are here, and will go up to the place which Jehovah has promised: for we have sinned."
41 Lakini Musa akasema, “Kwa nini sasa mnapinga amri ya BWANA? hamtafanikiwa.
Moses said, "Why now do you disobey the commandment of Jehovah, since it shall not prosper?
42 Msiende, kwa sababu BWANA hayuko pamoja nanyi kuwalinda dhidi ya maadui zenu.
Do not go up, for Jehovah isn't among you; that you not be struck down before your enemies.
43 Waamaleki na Wakanaani wako kule, na mtakufa kwa upanga kwa sababu mliumtegea mgongo BWANA na hamkumfuata. Kwa hiyo hatakuwa pamoja nanyi.
For there the Amalekite and the Canaanite are before you, and you shall fall by the sword: because you are turned back from following Jehovah, therefore Jehovah will not be with you."
44 Lakini walithubutu kukwea mlimani; lakini si Musa wala Sanduku la agano la BWANA walioondoka kambini.
But they presumed to go up to the top of the mountain: nevertheless the ark of the covenant of Jehovah, and Moses, did not depart out of the camp.
45 Kisha Waamaleki walikuja chini, pia wale Wakanaani walioshi kwenye hiyo milima. Wakawavamia Waisreli wakawapiga na kuwaangusha mpaka Horima.
Then the Amalekite came down, and the Canaanite who lived in that mountain, and struck them and beat them down, even to Hormah.

< Hesabu 14 >