< Hesabu 13 >

1 Kisha BWANA akanena na Musa, akamwambia, “tuma watu waende kuipeleleza nchi ya Kanani, ambayo nimewapa wana wa Israeli.
And he spoke Yahweh to Moses saying.
2 Tuma mwanamume mmoja kutoka kila jamaa ya kabila. Kila mwanamume awe kiongozi katika kabila lake.”
Send for yourself men so they may spy out [the] land of Canaan which I [am] about to give to [the] people of Israel a man one a man one for [the] tribe of ancestors his you will send every [one] a leader among them.
3 Musa akawatuma kutoka jangwa la Parani, ili watii amri ya BWANA. Watu wote hao walikuwa viongozi wa watu wa Israeli.
And he sent them Moses from [the] wilderness of Paran on [the] mouth of Yahweh all of them [were] men [who were] [the] heads of [the] people of Israel they.
4 Majina yao yalikuwa haya yafuatayo: kutoka kabila la Reubeni, Shamua mwana wa Zakuri;
And these [are] names their for [the] tribe of Reuben Shammua [the] son of Zaccur.
5 Kutoka kabila la Simeoni, Shafati mwana wa Hori;
For [the] tribe of Simeon Shaphat [the] son of Hori.
6 Kutoka kabila la Yuda, Kalebu mwana wa Yefune;
For [the] tribe of Judah Caleb [the] son of Jephunneh.
7 Kutoka kabila la Isakari, Igali mwana wa Yusufu,
For [the] tribe of Issachar Igal [the] son of Joseph.
8 Kutoka kabila la Efraimu, Hoshea mwana wa Nuni;
For [the] tribe of Ephraim Hoshea [the] son of Nun.
9 Kutoka kabila la Benjamini, Paliti mwana wa Rafu;
For [the] tribe of Benjamin Palti [the] son of Raphu.
10 kutoka kabila ya Zabuloni, Gadieli mwana wa Sodi;
For [the] tribe of Zebulun Gaddiel [the] son of Sodi.
11 kutoka kabila la Yusufu (hiyo inamaanisha kutoka kabila la Manase), Gadi mwana wa Susi;
For [the] tribe of Joseph for [the] tribe of Manasseh Gaddi [the] son of Susi.
12 kutoka kabila la Dani, Amieli mwana wa Gemalili;
For [the] tribe of Dan Ammiel [the] son of Gemalli.
13 kutoka kabila Asheri, Setu mwana wa Mikaili;
For [the] tribe of Asher Sethur [the] son of Michael.
14 kutoka kabila la Naftali, Nabi mwana wa Vofisi;
For [the] tribe of Naphtali Nahbi [the] son of Vopshi.
15 kutoka kabila la Gadi, Geuli mwana wa Machi.
For [the] tribe of Gad Geuel [the] son of Maki.
16 Haya ndiyo majina ya wanaume ambao Musa aliwatuma kwenda kuipelelza ile nchi. Musa akamwita Hoshea mwana wa Nuni kwa jina la Joshua.
These [are] [the] names of the men whom he sent Moses to spy out the land and he called Moses Hoshea [the] son of Nun Joshua.
17 Musa akawatuma kwenda kuipeleleza ile nchi ya Kanani. Naye akawaambia, “Mkaanzie Negebu hadi mahali pa milima.
And he sent them Moses to spy out [the] land of Canaan and he said to them go up this in the Negev and you will go up the hill country.
18 Kaipelelezeni nchi kujua ni nchi ya namna gani. Wachunguzeni watu wake, kama ni watu wenye nguvu au dhaifu, kama ni wachache au ni wengi.
And you will see the land what? [is] it and the people which dwells on it ¿ strong [is] it ¿ feeble ¿ few [is] it or? many.
19 Chunguzeni nchi hiyo wanayoishi ni nchi ya namna gani. Ni nzuri au mbaya? Miji yao ikoje? Je iko kama kambi au ni miji yenye ngome?
And what? [is] the land which it [is] dwelling in it ¿ good [is] it or? bad and what? [are] the cities which it [is] dwelling in them ¿ in camps or? in fortresses.
20 Chunguzeni ni nchi ya namna gani, kama ni njema kwa mazao au la kama kuna miti au hapana. Mwe hodari mkalete sampuli za mazao ya nchi,” Sasa ni muda wa msimu wa malimbuko ya mizabibu.
And what? [is] the land ¿ fat [is] it or? lean ¿ [is] there in it wood or? not and you will show yourselves strong and you will take some of [the] fruit of the land and the days [were the] days of [the] first-fruits of grapes.
21 Kwa hiyo wale wanaume wakaenda kuipeleleza ile nchi kutoka jangwa la Sini mpaka Rehobi, karibu na Lebo Hamati.
And they went up and they spied out the land from [the] wilderness of Zin to Rehob Lebo Hamath.
22 Walienda kutoka Negebu nao wakafika Hebroni. Ahimani, Sheshai, na Talmai, Uzao wa Anaki nao walikuweko, Sasa Hebroni ilikuwa imejengwa miaka saba iliyokuwa imepita kabla ya Zoani wa Misri.
And they went up in the Negev and he came to Hebron and [were] there Ahiman Sheshai and Talmai those born of Anak and Hebron seven years it was built before Zoan Egypt.
23 Nao walipofika katika bonde la Eshikoli, walikata matawi ya mizabibu lenye kishada cha zabibu. Na makundi mawili ya wapelelezi wakakibeba kwenye mti. Pia wakaleta makomamanga na mtini.
And they came to [the] wadi of Eshcol and they cut down from there a branch and a cluster of grapes one and they carried it on the pole two and some of the pomegranates and some of the figs.
24 Mahali pale paliitwa Eshikoli, kwa sababu ya kishada cha mizabibu ambacho wana wa Israeli walikata kule.
the Place that someone called [the] wadi of Eshcol on [the] causes of the cluster which they cut down from there [the] people of Israel.
25 Baada ya siku arobaini, wakarudi kutoka kuipeleleza nchi.
And they returned from spying out the land from [the] end of forty day[s].
26 Wakaja kwa Musa, Haruni na kwa watu wote wa Israeli katka jangwa la Parani, kule Kadeshi. Wakaleta taarifa kwao na kwa Waisraeli wote, na kuwaonyesha matunda ya nchi ile.
And they went and they came to Moses and to Aaron and to all [the] congregation of [the] people of Israel to [the] wilderness of Paran Kadesh towards and they brought back them word and all the congregation and they showed them [the] fruit of the land.
27 Wakamwambia Musa, “Tulifika katika ile nchi uliyotutuma. Kwa hakika ni nchi ya kutiririka maziwa na asali. Na baadhi ya matunda yake ni haya hapa.
And they recounted to him and they said we went into the land which you sent us and also [is] flowing of milk and honey it and this [is] fruit its.
28 Hata hivyo, watu wanaoishi huko ni wenye nguvu. Miji yao ni mikubwa tena ina maboma. Pia tuliwaona wana wa Anaki huko.
Nevertheless for [is] strong the people which dwells in the land and the cities [are] fortified large very and also those born of Anak we saw there.
29 Waamaleki wanaishi Negebu. Wahiti, Wayebusi, na Waamori nao wanaishi katika milima ya hiyo nchi. Wakanaani wanaishi kando ya bahari na mto Yorodani.”
Amalek [is] dwelling in [the] land of the Negev and the Hittite[s] and the Jebusite[s] and the Amorite[s] [is] dwelling in the hill country and the Canaanite[s] [is] dwelling at the sea and on [the] side of the Jordan.
30 Kisha Kalebu akawatuliza watu waliokuwa mbele ya Musa, akasema, “Twendeni tukaiteke nyara hiyo nchi, kwa kuwa tuna uhakika wa kuikamata.”
And he silenced Caleb the people to Moses and he said certainly we will go up and we will take possession of it for certainly we will prevail to it.
31 Lakini wale watu waliokuwa wameenda naye walisema, “Hatutaweza kuwashinda hao watu kwa kuwa wao ni hodari kuliko sisi.”
And the men who they had gone up with him they said not we are able to go up against the people for [is] strong it more than us.
32 Kwa hiyo wakasambaza taarifa za kukatisha tamaa kwa Wana wa Israeli juu ya nchi ile waliyoipeleleza. Walisema, “Ile nchi tuliyoiona ni nchi inayowala watu wake. Watu wote tuliowaona ni watu warefu.
And they brought out bad report of the land which they had spied out it to [the] people of Israel saying the land which we passed in it to spy out it [is] a land [which] devours inhabitants its it and all the people which we saw in [the] midst of it [were] men of stature.
33 Kule tuliiona majitu, wana wa uzao wa Anaki, ambao nii uzao wa majitu. Sisi tulionekana kama panzi machoni mwao tulipojilingsnisha nao, hivyo ndivyo tulivyoonekana machoni mwao pia.”
And there we saw the Nephilim [the] descendants of Anak [were] from the Nephilim and we were in own eyes our like grasshoppers and thus we were in eyes their.

< Hesabu 13 >