< Hesabu 12 >

1 Kisha Miriamu na Haruni wakasema kinyume na Musa kwa sababu ya mwanamke Mkushi ambaye alikuwa amemwoa.
Miriam and Aaron [Light-bringer] spoke against Moses [Drawn out] because of the Cushite woman whom he had married; for he had married a Cushite woman.
2 Walisema. “Hivi BWANA amesema na Musa tu? Ni kweli hajawahi kusema nasi pia? Sasa BWANA akasikia kile walichokuwa wanaongea. Sasa
They said, “Has Adonai indeed spoken only with Moses [Drawn out]? Has not he spoken also with us?” And Adonai sh'ma ·heard obeyed· it.
3 Musa alikuwa mtu mpole sana, mpole kuliko mtu yeyote duniani.
Now the man Moses [Drawn out] was very humble, more than all the men who were on the surface of the earth.
4 Wakati huo, BWANA akanena na Musa, Haruni na Miriamu: “tokeni nje ninyi watatu kwenye hema ya kukutania.” kwa hiyo wale watatu wakatokanje.
Adonai spoke suddenly to Moses [Drawn out], to Aaron [Light-bringer], and to Miriam, “You three come out to the Tent of Meeting!” The three of them came out.
5 Kisha BWANA akashuka katika nguzo ya wingu. Akasimama kwenye lango la hema na akamwita Haruni na Miriamu. wote wakaja mbele.
Adonai came down in a pillar of cloud, and stood at the door of the Tent, and called Aaron [Light-bringer] and Miriam; and they both came forward.
6 BWANA akasema, “Sasa sikilizeni maneo yangu, Nabii wangu anapokuwa nanyi, Mimi nitajifunua kwake kwa maono na kusema naye katika ndoto.
He said, “Now sh'ma ·hear obey· my words. If there is a prophet among you, I, Adonai, will make myself known to him in a vision. I will speak with him in a dream.
7 Lakini si hivyo kwa mtumishi wangu Musa. Yeye ni mwaminifu katika nyumba yangu yote.
My servant Moses [Drawn out] is not so. He is faithful in all my house.
8 Mimi huongea na Musa moja kwa moja, si kwa maono wala mafumbo. Yeye huniona umbo langu. Kwa hiyo, kwa nini hamuogoopi kumnenea kinyume, mtumishi wangu Musa?”
With him, I will speak mouth to mouth, even plainly, and not in riddles; and he shall see Adonai’s form. Why then were you not afraid to speak against my servant, against Moses [Drawn out]?”
9 Hasira ya BWANA ikawawakia, kisha akawaacha.
Adonai’s anger burned against them; and he departed.
10 Lile wingu likainuka juu ya hema, Miriamu akapata ukoma ghafla - akawa mweupe kama theluji. Naye Haruni alipogeuka kumwona Miriamu, akamwona amepata ukoma.
The cloud departed from over the Tent; and behold, Miriam was leprous, as white as snow. Aaron [Light-bringer] looked at Miriam, and behold, she was leprous.
11 Haruni akamwambia Musa, “Bwana wangu, usituadhibu kwa uovu wetu huu. Tumenena katka upumbuvu, na tumetenda dhambi.
Aaron [Light-bringer] said to Moses [Drawn out], “Oh, my lord, please don’t count this sin against us, in which we have done foolishly, and in which we have sinned.
12 Tafadhali nakuomba usimwache akawa kama mtoto mchanga aliyekufa ambaye nusu ya nyama yake imeoza tangu kuzaliwa”
Let her not, I pray, be as one dead, of whom the flesh is half consumed when he comes out of his mother’s womb.”
13 Kwa hiyo Musa akamwomba BWANA, akasema, “Mungu ninakusihi umponye tafadhali.”
Moses [Drawn out] cried to Adonai, saying, “Heal her, God, I beg you!”
14 BWANA akamwambia Musa, “kama baba yake angemtemea usoni angepata aibu kwa muda wa siku saba. Umfungie nje ya kambi kwa muda wa siku saba. Kisha umrejeshe ndani tena.”
Adonai said to Moses [Drawn out], “If her father had but spit in her face, should not she be ashamed seven days? Let her be shut up outside of the camp seven days, and after that she shall be brought in again.”
15 Kwa hiyo Miriamu akafungiwa nje ya kambi kwa siku saba. Watu hawakusafiri mpaka aliporudi kambini.
Miriam was shut up outside of the camp seven days, and the people didn’t travel until Miriam was brought in again.
16 Kisha watu wakasafiri kutoka Hazeroti na kuweka kambi kwenye jangwa la Parani.
Afterward the people traveled from Hazeroth, and encamped in the wilderness of Paran.

< Hesabu 12 >