< Hesabu 1 >

1 Mungu alimwambia Musa katika hema ya kukutania walipokuwa katika jangwa la Sinai. Hii ilitokea katika siku ya kwanza ya mwezi wa pili miaka miwili baadaya Waisraeli kutoka nchi ya Misri. Mungu alisema,
PAN przemówił do Mojżesza na pustyni Synaj, w Namiocie Zgromadzenia, pierwszego [dnia] drugiego miesiąca, w drugim roku po ich wyjściu z ziemi Egiptu, tymi słowy:
2 'fanya sensa ya wanaume wote wa Israel kutoka kila ukoo, katika familia za baba zao. Wahesabu kwa majina, wahesabu kila mume, kila mwanamume
Policzcie całe zgromadzenie synów Izraela według ich rodzin i według domów ich ojców, licząc imiona wszystkich mężczyzn, głowa po głowie;
3 kuanzia umri a miaka ishirini na zaidi. Uwahesabu wote wanaoweza kupigana kama askari wa Israel. Wewe na Haruni mtaandika idadi ya wanaume katika makundi ya majeshi yao.
Od dwudziestu lat wzwyż, wszystkich w Izraelu zdolnych do walki. Ty i Aaron policzycie ich według ich oddziałów.
4 Kila mwanamume kwa kila kabila, kichwa cha ukoo, lazima atumike na wewe kama kiongozi wa kabila.
I będzie z wami jeden mężczyzna z każdego pokolenia, głowa domu swoich ojców.
5 Haya ndiyo majina ya viongozi ambao watapigana pamoja na wewe: Kutoka kabila la Reubeni, Elizuri mwana wa Shedeuri;
A oto imiona mężczyzn, którzy będą z wami: z [pokolenia] Rubena – Elizur, syn Szedeura;
6 kutoka kabila la Simeoni, Shelumiel mwana wa Zurishadai
Z Symeona – Szelumiel, syn Suriszaddaja;
7 Kutoka kabila la Yuda, Nashoni mwana wa Aminadabu;
Z Judy – Nachszon, syn Amminadaba;
8 Ktoka kabila la Isakari, Nethaneli mwana wa Zuari;
Z Issachara – Netaneel, syn Suara;
9 kutoka kabila Zebuluni, Eliabu mwana wa Heloni
Z Zebulona – Eliab, syn Chelona;
10 kutoka kabila la Efraimu mwana wa Yusufu, Elishama mwana wa Ammihudi; kutoka kabila la Manase, Gamaliel mwan wa Pedazuri;
Z synów Józefa: z Efraima – Eliszama, syn Ammihuda, z Manassesa – Gamliel, syn Pedahsura;
11 kutoka kabila la Benjamini mwana wa Ysufu, Abidani mwan wa Gidion;
Z Beniamina – Abidan, syn Gideoniego;
12 Kutoka kabila la Dan, Ahizeri mwana wa Amishadai;
Z Dana – Achiezer, syn Ammiszaddaja;
13 kutoka kabila Asheri, Pagieli mwana wa Okirani;
Z Aszera – Pagiel, syn Okrana;
14 kutoka kabila la Gadi, Eliasafu mwana wa Deuli;
Z Gada – Eliasaf, syn Deuela;
15 na kutoka kabila la Naftali, Ahira mwana wa Enani.”
Z Neftalego – Achira, syn Enana.
16 Hawa ndio wanaume waliochaguliwa kutoka kwa watu. Waliongoza kabila za mababu zao. Walikuwa viongozi wa koo katika Israel.
Ci powołani, [sławni] spośród zgromadzenia, byli naczelnikami pokoleń swych ojców, wodzami tysięcy w Izraelu.
17 Musa na Haruni wakawachukua wale wanaume, waliokuwa wameandikwa kwa majina,
Mojżesz i Aaron przyjęli więc tych mężczyzn, którzy zostali imiennie wyznaczeni.
18 na pamoja na wanaume hao waliwakusanya wanume wote katika siku ya kwanza ya mwezi wa pili. Kisha kila mwanume wa miaka ishirini na zaidi alitambua babu zake. Alitakiwa kutaja koo na famila kutoka katika ukoo.
I zebrali całe zgromadzenie w pierwszym dniu drugiego miesiąca, a każdy podawał swoje pochodzenie według swych rodzin, według domów swych ojców i według liczby imion, od dwudziestu lat wzwyż, głowa po głowie.
19 Kisha Musa akaandika hesabu yao huko katika nyika ya Sinai, Kama Mungu alivyokuwa amemwamuru kufanya.
Jak PAN rozkazał Mojżeszowi, tak policzył ich na pustyni Synaj.
20 Kutoka uzao wa Reubeni, mtoto wa kwanza wa Israel, yalihesabiwa majina yote ya kila mwanamume mwenye umri wa miaka ishirini na zaidi wenye uwezo wa kwenda vitani, kutoka hesabu ya ukoo na familia.
Synów Rubena, pierworodnego Izraela, ich potomków według ich rodzin, według domów ich ojców, według liczby imion, głowa po głowie, wszystkich mężczyzn od dwudziestu lat wzwyż, wszystkich zdolnych do walki;
21 Waliwahesabu wanaume 46, 000 kutoka ukoo wa Reubeni.
Naliczono z pokolenia Rubena czterdzieści sześć tysięcy pięciuset.
22 Kutoka uzao wa Simeoni yalihesabiwa majina yote ya kila mwanamume mwenye umri wa miaka ishirini na zaidi au wenye uwezo wa kwenda vitani, kutokana na hesabu ya ukoo na familia.
Synów Symeona, ich potomków według ich rodzin, według domów ich ojców, naliczonych według liczby imion, głowa po głowie, wszystkich mężczyzn od dwudziestu lat wzwyż, wszystkich zdolnych do walki;
23 Walihesabu wanaume 59, 300 kutoka kabila la Simeoni.
Naliczono z pokolenia Symeona pięćdziesiąt dziewięć tysięcy trzystu.
24 Kutoka uzao wa Gadi yalihesabiwa majina yote ya kila mwanamume mwenye umri wa miaka ishirini au zaidi na wenye uwezo wa kwenda vitani, kutoka kwenye hesabu ya ukoo na familia.
Synów Gada, ich potomków według ich rodzin, według domów ich ojców, według liczby imion, od dwudziestu lat wzwyż, wszystkich zdolnych do walki;
25 Walihesabu wanaume 45, 650 kutoka kabila la Gadi.
Naliczono z pokolenia Gada czterdzieści pięć tysięcy sześciuset pięćdziesięciu.
26 Kutoka uzao wa Yuda yalihesabiwa majina yote ya wanaume wenye umri wa miaka ishirini au zaidi na wenye uwezo wa kwenda vitani, kutoka kwenye hesabu ya ukoo na familia.
Synów Judy, ich potomków według ich rodzin, według domów ich ojców, według liczby imion, od dwudziestu lat wzwyż, wszystkich zdolnych do walki;
27 walihesabiwa wanume 74, 000 kutoka kabila la Yuda.
Naliczono z pokolenia Judy siedemdziesiąt cztery tysiące sześciuset.
28 Kutoka uzao wa Isakari yalihesabiwa majina yote ya kila mwanamume mwenye umri wa miaka ishirini au zaidi na wenye uwezo wa kwenda vitani, kutoka kwenye hesabu ya ukoo na familia.
Synów Issachara, ich potomków według ich rodzin, według domów ich ojców, według liczby imion, od dwudziestu lat wzwyż, wszystkich zdolnych do walki;
29 Walihesabiwa wanaume 54, 000 kutoka kabila la Isakari.
Naliczono z pokolenia Issachara pięćdziesiąt cztery tysiące czterystu.
30 Kutoka uzao wa Zabuloni yalihesabiwa majina yote ya kila mwanamume mwenye umri wa miaka ishirini au zaidi na wenye uwezo wa kwenda vitani, kutoka kwenye hesabu ya ukoo na familia.
Synów Zebulona, ich potomków według ich rodzin, według domów ich ojców, według liczby imion, od dwudziestu lat wzwyż, wszystkich zdolnych do walki;
31 Walihesabiwa wanume 57, 400 kutoka kabila la Zabuloni.
Naliczono z pokolenia Zebulona pięćdziesiąt siedem tysięcy czterystu.
32 Kutoka uzao wa Efraimu mwana wa Yusufu yalihesabiwa majina yote ya kila mwanaume mwenye umri wa miaka ishirini au zaidi na wenye uwezo wa kwenda vitani, kutoka kwenye hesabu ya ukoo na familia.
Synów Józefa, z synów Efraima, ich potomków według ich rodzin, według domów ich ojców, według liczby imion, od dwudziestu lat wzwyż, wszystkich zdolnych do walki;
33 Walihesabiwa wanaume 40, 500 kutoka kabila la Efraimu.
Naliczono z pokolenia Efraima czterdzieści tysięcy pięciuset.
34 Kutoka uzao wa Manase mwana wa Yusufu yaliheabiwa majina yote ya kila mwanaume mwenye umri wa miaka ishirini au zaidi na wenye uwezo wa kwenda vitani, kutoka kwenye hesabu y a ukoo na familia.
Synów Manassesa, ich potomków według ich rodzin, według domów ich ojców, według liczby imion, od dwudziestu lat wzwyż, wszystkich zdolnych do walki;
35 Walihesabiwa wanaume 32, 000 kutoka kabila la Manase.
Naliczono z pokolenia Manassesa trzydzieści dwa tysiące dwustu.
36 Kutoka uzao wa Benjamini yalihesabiwa majina yote ya kila mwanaume mwenye umri wa miaka ishirini au zaidi na wenye uwezo wa kwenda vitani, kutoka kwenye hesabu ya ukoo na familia.
Synów Beniamina, ich potomków według ich rodzin, według domów ich ojców, według liczby imion, od dwudziestu lat wzwyż, wszystkich zdolnych do walki;
37 Walihesabiwa wanaume 35, 000 kutoka kabila la Benjamini.
Naliczono z pokolenia Beniamina trzydzieści pięć tysięcy czterystu.
38 Kutoka uzao wa Dani yalihesabiwa majina yote ya kila mwanaume mwenye umri wa miaka ishirini au zaidi na mwenye uwezo wa kwenda vitani, Kutoka kwenye hesabu ya ukoo na familia.
Synów Dana, ich potomków według ich rodzin, według domów ich ojców, według liczby imion, od dwudziestu lat wzwyż, wszystkich zdolnych do walki;
39 Walihesabiwa wanaume 62, 000 kutoka kabila la Dani.
Naliczono z pokolenia Dana sześćdziesiąt dwa tysiące siedmiuset.
40 Kutoka uzao wa Asheri yalihesabiwa majina yote ya kila mwanume mwenye umri wa miaka ishirini au zadi na mwenye uwezo wa kwenda vitani, kutoka kwenye hesabu y a ukoo na familia.
Synów Aszera, ich potomków według ich rodzin, według domów ich ojców, według liczby imion, od dwudziestu lat wzwyż, wszystkich zdolnych do walki;
41 Walihesabiwa wanaume 41, 500 kutoka ukoo wa Asheri.
Naliczono z pokolenia Aszera czterdzieści jeden tysięcy pięciuset.
42 Kutoka ukoo wa Naftali yalihesabiwa majina yote ya kila mwanaume mwenye umri wa miaka ishirini au zaidi na mwenye uwezo wa kwenda vitani, kutoka kwenye hesabu ya ukoo na familia.
Synów Neftalego, ich potomków według ich rodzin, według domów ich ojców, według liczby imion, od dwudziestu lat wzwyż, wszystkich zdolnych do walki;
43 Walihesabiwa wanaume 53, 400 kutoka kabila la Naftari
Naliczono z pokolenia Neftalego pięćdziesiąt trzy tysiące czterystu.
44 Musa na Haruni waliwahesabu wanaume wote hawa, pamoja na wale wanaume kumi na wawili waliokuwa wakiongoza yale makabila kumi na mawili ya Israeli.
To są ci, których policzyli Mojżesz, Aaron i książęta Izraela, dwunastu mężczyzn, po jednym z każdego domu swych ojców.
45 Kwa hiyo wanaume wote wa Israeli wenye umri wa miak ishirini au zaidi, wote wenye uwezo wa kwenda vitani, walihesabiwa kutoka kwenye familia zao.
I było wszystkich policzonych synów Izraela, według domów ich ojców, od dwudziestu lat wzwyż, wszystkich zdolnych do walki w Izraelu;
46 Walihesabu wanaume 603, 550.
Wszystkich policzonych było sześćset trzy tysiące pięciuset pięćdziesięciu.
47 Lakini wanaume toka uzao wa Lawi hawakuhesabiwa,
Lecz Lewici nie zostali policzeni z nimi według pokolenia swych ojców.
48 Kwa sababu BWANA alimwambia Musa,
PAN rozkazał bowiem Mojżeszowi:
49 “usiwahesabu wale wa kabila la Lawi wala kuwajumuisha kwenye jumla ya watu wa Israeli.
Tylko pokolenia Lewiego nie spisuj i nie licz go razem z synami Izraela;
50 Badala yake, waagize Walawi kuliangalia hema la amri za agano, na kuangalia mapambo ya hema na vyote vilivyomo. Walawi watalazimika kulibeba hema na lazima wayabebe mapambo ya hema. Lazima waliangalie hema na kuyatengeneza mazingira yake. Wataiangalia masikani na kuzitengeneza kambi zinazolizunguka.
Lecz ustanowisz Lewitów nad Przybytkiem Świadectwa i nad wszystkimi jego naczyniami, i nad wszystkim, co do niego należy. Oni będą nosić przybytek i wszystkie jego sprzęty; oni też będą go obsługiwać i rozbijać obóz dokoła przybytku.
51 Kila hema litakapotakiwa kuhamishiwa eneo jingine, Walawi ndio watakaolipeleka pale. Na kila hema litakapotakiwa kusimamishwa, Walawi ndio watakao lisimamisha. Na mgeni yeyote atakayelisogelea hema lazima auawe.
A gdy przybytek będzie miał wyruszyć, Lewici go rozbiorą; także gdy przybytek ma być wznoszony, Lewici ustawią go; a obcy, który się do niego zbliży, poniesie śmierć.
52 Wakati watu wa Israeli watakaposimamisha hema zao, kila mwanaume lazima awe karibu na bango la jeshi lake.
I synowie Izraela będą rozbijać namioty, każdy w swoim obozie i każdy pod swoim sztandarem, według swych zastępów.
53 Hata hivyo Walawi lazima waweke hema zao kuizunguka hiyo masikani ya amri za agano ili kwamba hasira yangu isije ikawaka juu ya wana wa Israeli. Walawi lazima wailinde hiyo masikani ya amri za agano.”
Lecz Lewici rozbiją obóz wokół Przybytku Świadectwa, aby gniew nie spadł na zgromadzenie synów Izraela. Lewici będą pełnić straż przy Przybytku Świadectwa.
54 Wana wa Israeli walifanya yote haya. Walifanya yote ambayo BWANA aliagiza kupitia Musa.
I synowie Izraela uczynili zgodnie ze wszystkim, co PAN rozkazał Mojżeszowi, tak właśnie uczynili.

< Hesabu 1 >