< Nehemia 13 >

1 Siku hiyo walisoma Kitabu cha Musa katika masikio ya watu. Ilionekana imeandikwa ndani yake kwamba hakuna Mwamoni au Mmoabu anapaswa kuja katika kusanyiko la Mungu, milele.
On that day there was read in the book of Moses, in the ears of the people, and it hath been found written in it that an Ammonite and Moabite doth not come into the assembly of God — unto the age,
2 Hii ilikuwa kwa sababu hawakuja kwa watu wa Israeli na mkate na maji, bali walikuwa wamemwajiri Balaamu kulaani Israeli. Hata hivyo, Mungu wetu aligeuza laana kuwa baraka.
because they have not come before the sons of Israel with bread and with water, and hire against them Balaam to revile them, and our God turneth the reviling into a blessing.
3 Mara tu waliposikia sheria, waliwatenga Israeli toka kwa kila mgeni.
And it cometh to pass, at their hearing the law, that they separate all the mixed people from Israel.
4 Sasa kabla ya hapo Eliashibu kuhani akawekwa juu ya vyumba vya nyumba ya Mungu wetu. Alikuwa na uhusiano na Tobia.
And before this Eliashib the priest, appointed over chambers of the house of our God, [is] a relation of Tobiah,
5 Eliashibu alimuandalia Tobia chumba kikubwa, ambako hapo awali waliweka sadaka ya nafaka, uvumba, makala, na sehemu ya kumi ya nafaka, divai, na mafuta, ambazo ziliwekwa kwa ajili ya Walawi, waimbaji, walinzi wa mlango, na michango kwa makuhani.
and he maketh for him a great chamber, and there they were formerly putting the present, the frankincense, and the vessels, and the tithe of the corn, the new wine, and the oil — the commanded thing of the Levites, and the singers, and the gatekeepers — and the heave-offering of the priests.
6 Lakini wakati huu wote sikuwepo Yerusalemu. Kwa mwaka wa thelathini na mbili wa Artashasta mfalme wa Babeli, nilikwenda kwa mfalme. Baada ya muda nikamwomba mfalme ruhusa ya kuondoka,
And during all this I was not in Jerusalem, for in the thirty and second year of Artaxerxes king of Babylon did I come unto the king, and at the end of days I have asked of the king,
7 na nikarudi Yerusalemu. Nikafahamu mabaya ambayo Eliashibu alikuwa amefanya kwa kumpa Tobia chumba cha kuhifadhi katika mahakama ya nyumba ya Mungu.
and I come in to Jerusalem, and understand concerning the evil that Eliashib hath done for Tobiah, to make to him a chamber in the courts of the house of God,
8 Nilikuwa na hasira sana na nikatupa vitabu vya nyumba ya Tobia nje ya chumba cha kuhifadhi.
and it is very displeasing to me, and I cast all the vessels of the house of Tobiah without, out of the chamber,
9 Niliamuru kwamba watakase vituo vya kuhifadhi, nami nikarudisha ndani yao makala ya nyumba ya Mungu, sadaka ya nafaka, na uvumba.
and I speak, and they cleanse the chambers, and I bring back thither the vessels of the house of God with the present and the frankincense.
10 Niligundua kwamba sehemu zilizotolewa kwa ajili ya kuwapa Walawi hazikutolewa kwao, ili waweze kuondoka haraka hekaluni, kila mmoja kwenda shambani kwake, kama waimbaji waliofanya walivyoondoka.
And I know that the portions of the Levites have not been given, and they flee each to his field — the Levites and the singers, doing the work.
11 Kwa hiyo nikawasiliana na maafisa na kusema, 'Kwa nini nyumba ya Mungu imeachwa?' Niliwakusanya pamoja na kuwaweka kwenye nafasi zao.
And I strive with the prefects, and say, 'Wherefore hath the house of God been forsaken?' and I gather them, and set them on their station;
12 Kisha Yuda wote wakaleta zaka ya nafaka, divai mpya, na mafuta kwenye vituo vya kuhifadhi.
and all Judah have brought in the tithe of the corn, and of the new wine, and of the oil, to the treasuries.
13 Nikawaweka kama watunza hazina juu ya hazina, Shelemia kuhani, na Sadoki mwandishi, na Walawi, Pedaya. Hanani, mwana wa Zakuri, mwana wa Matania, alikuwa na wafuasi wao, kwa sababu walihesabiwa kuwa waaminifu. Kazi yao ilikuwa kusambaza vifaa kwa washirika wao.
And I appoint treasurers over the treasuries, Shelemiah the priest, and Zadok the scribe, and Pedaiah of the Levites; and by their hand [is] Hanan son of Zaccur, son of Mattaniah, for stedfast they have been reckoned, and on them [it is] to give a portion to their brethren.
14 Nikumbuke, Ee Mungu wangu, juu ya hili, wala usiondoe matendo mema niliyoyatenda kwa ajili ya nyumba ya Mungu wangu na huduma zake.
Be mindful of me, O my God, for this, and do not blot out my kind acts that I have done, for the house of my God, and for its charges.
15 Siku hizo nikaona watu wa Yuda waliokanyaga mvinyo siku ya Sabato, na kuleta makundi ya nafaka, na kuwapakia punda, na divai, na zabibu, na tini, na kila aina ya mizigo nzito, waliyoleta Yerusalemu siku ya Sabato. Nikashuhudia kuwa walikuwa wakiuza chakula siku hiyo.
In those days I have seen in Judah those treading wine-vats on sabbath, and bringing in the sheaves, and lading on the asses, and also, wine, grapes, and figs, and every burden, yea, they are bringing in to Jerusalem on the sabbath-day, and I testify in the day of their selling provision.
16 Watu kutoka Tiro waliokaa Yerusalemu walileta samaki na kila aina ya bidhaa, na wakawauza siku ya Sabato kwa watu wa Yuda na katika mji!
And the Tyrians have dwelt in it, bringing in fish, and every ware, and selling on sabbath to the sons of Judah and in Jerusalem.
17 Kisha nikawaambia viongozi wa Yuda, “Je! ni ubaya gani huu mnafanya, kuinajisi siku ya Sabato?
And I strive with the freemen of Judah, and say to them, 'What [is] this evil thing that ye are doing, and polluting the sabbath-day?
18 Je! Baba zenu hawakufanya hivyo? Je, Mungu wetu hakuleta mabaya haya juu yetu na juu ya mji huu? Sasa unaleta ghadhabu zaidi juu ya Israeli kwa kudharau Sabato.”
Thus did not your fathers do? and our God bringeth in on us all this evil, and on this city, and ye are adding fierceness on Israel, to pollute the sabbath.'
19 Mara ilipokuwa giza kwenye milango ya Yerusalemu kabla ya Sabato, niliamuru milango ifungwe na kwamba haifai kufunguliwa hadi baada ya Sabato. Niliwaweka baadhi ya watumishi wangu kwenye malango ili mzigo wowote usiweze kuletwa siku ya Sabato.
And it cometh to pass, when the gates of Jerusalem have been dark before the sabbath, that I speak, and the doors are shut, and I say, that they do not open them till after the sabbath; and of my servants I have stationed at the gates; there doth not come in a burden on the sabbath-day.
20 Wafanyabiashara na wauzaji wa kila aina ya bidhaa walikimbia nje ya Yerusalemu mara moja au mbili.
And they lodge — the merchants and sellers of all ware — at the outside of Jerusalem, once or twice,
21 Lakini niliwaonya, “Mbona mnakaa nje ya ukuta? Ikiwa mtafanya hivyo tena, nitakuweka mikononi!” Kutoka wakati huo hawakuja siku ya sabato.
and I testify against them, and say unto them, 'Wherefore are ye lodging over-against the wall? if ye repeat [it], a hand I put forth upon you;' from that time they have not come in on the sabbath.
22 Nikawaamuru Walawi kujitakasa, na kuja kulinda milango, ili kutakasa siku ya Sabato. Nikumbuke kwa hili pia, Mungu wangu, na kunipatia huruma kwa sababu ya uaminifu wa agano ulilonalo kwangu.
And I say to the Levites, that they be cleansed, and, coming in, keeping the gates, to sanctify the sabbath-day. Also, this, remember for me, O my God, and have pity on me, according to the abundance of Thy kindness.
23 Katika siku hizo niliona Wayahudi waliokuwa wameoa wanawake wa Ashdodi, Amoni na Moabu.
Also, in those days, I have seen the Jews [who] have settled women of Ashdod, of Ammon, of Moab.
24 Nusu ya watoto wao walizungumza lugha ya Ashdodi, lakini hawakuweza kuzungumza lugha ya Yuda, lakini lugha ya mmoja wa watu wengine.
And of their sons, half are speaking Ashdoditish — and are not knowing to speak Jewish — and according to the language of people and people.
25 Nami nikawasiliana nao, na mimi niliwaadhibu, na nikawapiga baadhi yao na kuvuta nywele zao. Naliwaapisha kwa Mungu, nikisema, Msiwape wana wao binti zenu, wala msiwachukue binti zao kwa ajili ya wana wenu, wala ninyi wenyewe.
And I strive with them, and declare them vile, and smite certain of them, and pluck off their hair, and cause them to swear by God, 'Ye do not give your daughters to their sons, nor do ye take of their daughters to your sons, and to yourselves.
26 Je, Sulemani mfalme wa Israeli hakufanya dhambi kwa sababu ya wanawake hawa? Miongoni mwa mataifa mengi hapakuwa na mfalme kama yeye, na alipendwa na Mungu wake. Mungu akamfanya awe mfalme juu ya Israeli wote. Hata hivyo, wake zake wa kigeni walimfanya atende dhambi.
'By these did not Solomon king of Israel sin? and among the many nations there was no king like him, and beloved by his God he was, and God maketh him king over all Israel — even him did the strange women cause to sin.
27 Je, tunapaswa kukusikiliza na kufanya uovu huu hata kumhalifu Mungu wetu na kuwaoa wanawake wageni?
And to you do we hearken to do all this great evil, to trespass against our God, to settle strange women?'
28 Mmoja wa wana wa Yoyada, mwana wa Eliashibu, kuhani mkuu, alikuwa mkwewe na Sanbalati Mhoroni. Kwa hiyo nilimondoa kutoka mbele yangu.
And [one] of the sons of Joiada son of Eliashib the high priest, [is] son-in-law to Sanballat the Horonite, and I cause him to flee from off me.
29 Wakukumbushe, Mungu wangu, kwa sababu wameunajisi ukuhani, na agano la ukuhani na Walawi.
Be mindful of them, O my God, for the redeemed of the priesthood, and the covenant of the priesthood, and of the Levites.
30 Kwa hiyo nimewatakasa kutoka kila kitu kigeni, na kuimarisha kazi za makuhani na Walawi, kila mmoja kwa kazi yake mwenyewe.
And I have cleansed them from every stranger, and appoint charges to priests and to Levites, each in his work,
31 Nilitoa sadaka za kuni wakati uliowekwa na matunda ya kwanza. Nikumbuke, Mungu wangu, kwa mema.
and for the wood-offering at appointed times, and for first-fruits. Be mindful of me, O my God, for good.

< Nehemia 13 >