< Nehemia 12 >

1 Hawa ndio makuhani na Walawi waliokuja pamoja na Zerubabeli mwana wa Shealueli, pamoja na Yoshua Seraya, Yeremia, Ezra,
And these are the priests and the Levites that went up with Zerubbabel the son of Shealtiel, and Jeshua: Seraiah, Jeremiah, Ezra,
2 Amaria, Maluki, Hatushi,
Amariah, Malluch, Hattush,
3 Shekania, Harimu na Meremothi.
Shechaniah, Rehum, Meremoth,
4 Kulikuwa na Iddo, Ginethoni, Abiya,
Iddo, Ginnethoi, Abijah,
5 Miyamini, Maazia, Bilgai,
Mijamin, Maadiah, Bilgah,
6 Shemaya, Yoyaribu, Yedaya,
Shemaiah, and Joiarib, Jedaiah,
7 Salu, Amoki, Hilkia, na Yedaya. Hawa walikuwa wakuu wa makuhani na washirika wao katika siku za Yoshua.
Sallu, Amok, Hilkijah, Jedaiah. These were the chief of the priests and of their brethren in the days of Jeshua.
8 Walawi walikuwa Yeshua, Binui, Kadmieli, Sherebia, Yuda, na Matania, aliyekuwa akiongoza nyimbo za shukrani, pamoja na washirika wake.
And the Levites: Jeshua, Binnui, Kadmiel, Sherebiah, Judah, Mattaniah, [who was] over the thanksgiving, he and his brethren;
9 Bakbukia na Uno, washirika wao, walisimama pembeni yao wakati wa huduma.
and Bakbukiah and Unni, their brethren, were over against them as watches.
10 Yoshua alikuwa babaye Yoyakimu, Yoyakimu alikuwa baba wa Eliashibu, Eliashibu alikuwa babaye Yoyada,
And Jeshua begot Joiakim, and Joiakim begot Eliashib, and Eliashib begot Joiada,
11 Yoyada alimzaa Yonathani, Yonathani akamzaa Yadua.
and Joiada begot Jonathan, and Jonathan begot Jaddua.
12 Katika siku za Yoyakimu hawa walikuwa makuhani, wakuu wa jamaa; Meraya alikuwa mkuu wa Seraya, Hanania alikuwa kiongozi wa Yeremia,
And in the days of Joiakim were priests, chief fathers: of Seraiah, Meraiah; of Jeremiah, Hananiah;
13 Meshulam alikuwa kiongozi wa Ezra, Yehohanani alikuwa kiongozi wa Amaria,
of Ezra, Meshullam; of Amariah, Jehohanan;
14 Yonathani alikuwa kiongozi wa Maluki, na Yusufu alikuwa kiongozi wa Shekania.
of Melicu, Jonathan; of Shebaniah, Joseph;
15 Ili kuendelea, Adna alikuwa kiongozi wa Harimu, Helkai kiongozi wa Meremothi,
of Harim, Adna; of Meraioth, Helkai;
16 Zekaria alikuwa kiongozi wa Ido, Meshulamu alikuwa kiongozi wa Ginethoni, na
of Iddo, Zechariah; of Ginnethon, Meshullam;
17 Zikri alikuwa kiongozi wa Abia wa Miyaamini. Piltai alikuwa kiongozi wa Maazia.
of Abijah, Zichri; of Miniamin [and] Moadiah, Piltai;
18 Shamua alikuwa kiongozi wa Bilgai, Yehonathani alikuwa kiongozi wa Shemaya,
of Bilgah, Shammua; of Shemaiah, Jehonathan;
19 Matenai alikuwa kiongozi wa Yoyaribu, Uzi alikuwa kiongozi wa Yedaya,
and of Joiarib, Mattenai; of Jedaiah, Uzzi;
20 Kalai alikuwa kiongozi wa Salu, Eberi alikuwa kiongozi wa Amok,
of Sallai, Kallai; of Amok, Eber;
21 Hashabia alikuwa kiongozi wa Hilkia, na Nethanel alikuwa kiongozi wa Yedaya.
of Hilkijah, Hashabiah; of Jedaiah, Nethaneel.
22 Katika siku za Eliashibu, Walawi Eliashibu, Yoyada, Yohana, na Yadua waliandikwa kama vichwa vya familia, na makuhani waliandikwa wakati wa utawala wa Dariyo wa Persia.
of the Levites, the chief fathers were recorded in the days of Eliashib, Joiada, and Johanan, and Jaddua, and the priests, until the reign of Darius the Persian.
23 Wana wa Lawi na viongozi wao wa familia waliandikwa katika Kitabu cha tarehe hadi siku za Yohana mwana wa Eliashibu.
The children of Levi, the chief fathers, were recorded in the book of the chronicles, even until the days of Johanan the son of Eliashib.
24 Wakuu wa Walawi walikuwa Hashabia, Sherebia, na Yeshua mwana wa Kadmieli, pamoja na washirika wao, waliokuwa wamesimama mbele yao kumtukuza na kumshukuru, akijibu sehemu kwa sehemu, kwa kutii amri ya Daudi, mtu wa Mungu.
And the chief Levites: Hashabiah, Sherebiah, and Jeshua the son of Kadmiel, with their brethren over against them, to praise [and] to give thanks, according to the commandment of David the man of God, ward over against ward.
25 Matania, Bakbukia, Obadiya, Meshulamu, Talmoni na Akubu walikuwa walinzi wa malango waliokuwa wakiwa wamesimama katika vyumba vya hazina penye malango.
Mattaniah and Bakbukiah, Obadiah, Meshullam, Talmon, Akkub, were doorkeepers keeping the ward at the storehouses of the gates.
26 Walitumika katika siku za Yoyakimu, mwana wa Yoshua, mwana wa Yosadaki, na katika siku za Nehemiya, gavana na Ezra kuhani na mwandishi.
These were in the days of Joiakim the son of Jeshua the son of Jozadak, and in the days of Nehemiah the governor, and of Ezra the priest, the scribe.
27 Katika kujitolea kwa ukuta wa Yerusalemu, watu walitafuta Walawi popote walipokuwa wakiishi, wakawaleta Yerusalemu ili kusherehekea kujitolea kwa furaha, pamoja na shukrani na kuimba kwa ngoma, vinanda na vinubi.
And at the dedication of the wall of Jerusalem they sought the Levites out of all their places, to bring them to Jerusalem, to hold the dedication with gladness, both with thanksgivings, and with singing, [with] cymbals, lutes and harps.
28 Ushirika wa waimbaji walikusanyika pamoja kutoka wilaya iliyozunguka Yerusalemu na kutoka vijiji vya Wanetofathi.
And the children of the singers were assembled, both from the plain [of Jordan] round about Jerusalem, and from the villages of the Netophathites,
29 Walikuja kutoka Beth-gilgali na kutoka katika mashamba ya Geba na Azmawethi, kwa kuwa waimbaji walikuwa wamejijengea vijiji karibu na Yerusalemu.
also from Beth-Gilgal, and out of the fields of Geba and Azmaveth; for the singers had built themselves hamlets round about Jerusalem.
30 Makuhani na Walawi wakajitakasa, kisha wakawatakasa watu, milango na ukuta.
And the priests and the Levites purified themselves; and they purified the people, and the gates and the wall.
31 Kisha nilikuwa na viongozi wa Yuda kwenda juu ya ukuta, na mimi kuteua mikutano miwili mikubwa ya hao walioshukuru. Mmoja alienda upande wa kulia juu ya ukuta kuelekea lango la jaa.
And I brought up the princes of Judah upon the wall, and appointed two great choirs and processions, on the right hand upon the wall towards the dung-gate.
32 Hoshaya na nusu ya viongozi wa Yuda walimfuata,
And after them went Hoshaiah, and half of the princes of Judah,
33 na baada yake akaenda Azaria, Ezra na Meshulamu,
and Azariah, Ezra, and Meshullam,
34 Yuda, Benyamini, Shemaya, Yeremia
Judah and Benjamin, and Shemaiah, and Jeremiah,
35 na wana wa makuhani waliokuwa na tarumbeta, na Zekaria mwana wa Yonathani, mwana wa Shemaya, mwana wa Mataniya, mwana wa Mikaya, mwana wa Zakuri, mwana wa Asafu.
and [certain] of the priests' sons with trumpets: Zechariah the son of Jonathan, the son of Shemaiah, the son of Mattaniah, the son of Micaiah, the son of Zaccur, the son of Asaph;
36 Na pia jamaa za Zekaria, Shemaya, Azareli, Milalai, Gilalai, Maai, Nethaneli, Yuda, Hanani, pamoja na vyombo vya muziki vya Daudi mtu wa Mungu. Ezra mwandishi alikuwa mbele yao.
and his brethren, Shemaiah, and Azareel, Milalai, Gilalai, Maai, Nethaneel, and Judah, Hanani, with the musical instruments of David the man of God; and Ezra the scribe before them.
37 Na kwa Lango la Chemchemi walikwenda moja kwa moja na madaraja ya mji wa Daudi juu ya kupanda kwa ukuta, juu ya nyumba ya Daudi, kwenye lango la Maji upande wa mashariki.
And at the fountain-gate, and over against them, they went up by the stairs of the city of David, at the ascent of the wall, above the house of David, even to the water-gate eastward.
38 Na waimbaji wengine ambao walishukuru wakaenda upande mwingine. Niliwafuata juu ya ukuta pamoja na nusu ya watu, juu ya mnara wa vinyago, hadi kuta kubwa,
And the second choir went in the opposite direction upon the wall, and I after them, and the half of the people, from beyond the tower of the furnaces even to the broad wall;
39 na juu ya lango la Efraimu, na mlango wa kale, na kwa lango la samaki na mnara wa Hananeli na mnara wa Hamea, kwa lango la Kondoo, na wakasimama kwenye mlango wa walinzi.
and from above the gate of Ephraim, and above the gate of the old [wall], and above the fish-gate, and the tower of Hananeel, and the tower of Meah, even to the sheep-gate; and they stood still in the prison-gate.
40 Kwa hiyo, mikutano miwili ya wale waliomshukuru walipata nafasi yao katika nyumba ya Mungu, na mimi pia nikachukua nafasi yangu na nusu ya viongozi pamoja nami.
And both choirs stood in the house of God, and I, and the half of the rulers with me;
41 Na makuhani wakachukua nafasi zao Eliakimu, Maaseya, Miyamini, Mikaya, Elioenai, Zekaria, na Hanania wenye tarumbeta,
and the priests, Eliakim, Maaseiah, Miniamin, Micaiah, Elioenai, Zechariah, Hananiah, with trumpets;
42 Maaseya, na Shemaya, Eleazari, Uzi, Yehohanani, Malkiya, Elamu, Ezeri. Waimbaji waliimba na Yezrahia kama wasimamizi.
and Maaseiah, and Shemaiah, and Eleazar, and Uzzi, and Jehohanan, and Malchijah, and Elam, and Ezer. And the singers sang loud; and Jizrahiah was their overseer.
43 Walitoa dhabihu kubwa siku ile, wakafurahi, kwa sababu Mungu alikuwa amewafurahisha kwa furaha kubwa. Pia wanawake na watoto walifurahi. Hivyo furaha ya Yerusalemu ikasikiwa toka mbali.
And that day they offered great sacrifices, and rejoiced: for God had made them rejoice with great joy; and also the women and the children rejoiced. And the joy of Jerusalem was heard even afar off.
44 Siku hiyo watu waliteuliwa juu ya nyumba ya hazina kwa ajili ya michango, matunda ya kwanza, na zaka, ili kuzikusanya ndani yao sehemu zinazohitajika katika sheria za makuhani na Walawi. Kila mmoja aliteuliwa kufanya kazi mashambani karibu na miji. Kwa maana Yuda alifurahi juu ya makuhani na Walawi waliokuwa wamesimama mbele yao.
And at that time men were appointed over the chambers of the treasures for the heave-offerings, for the first-fruits, and for the tithes, to gather into them, out of the fields of the cities, the portions assigned by the law for the priests and the Levites; for Judah rejoiced over the priests, and over the Levites that waited.
45 Walifanya utumishi wa Mungu wao, na huduma ya utakaso, kwa mujibu wa amri ya Daudi na ya mwanawe Sulemani, na hivyo
And, with the singers and the doorkeepers, they kept the ward of their God, and the ward of the purification, according to the commandment of David [and] of Solomon his son.
46 Zamani za kale, katika siku za Daudi na Asafu, kulikuwa na wasimamizi wa waimbaji, na kulikuwa na nyimbo za sifa na shukrani kwa Mungu.
For of old, in the days of David and Asaph, there were the chiefs of the singers, and songs of praise and thanksgivings to God.
47 Katika siku za Zerubabeli na katika siku za Nehemia, Israeli wote walitoa sehemu za kila siku kwa waimbaji na walinzi wa mlango. Wakaweka pembeni sehemu ya Walawi, na Walawi waliweka sehemu ya wana wa Haruni.
And all Israel, in the days of Zerubbabel and in the days of Nehemiah, gave the portions of the singers and the doorkeepers, every day what was needed, and they consecrated things for the Levites; and the Levites consecrated for the children of Aaron.

< Nehemia 12 >