< Nahumu 1 >

1 Maono kuhusu Ninawi. Kitabu cha maono ya Nahumu, Mwelkoshi.
Carga sobre Nínive. Libro de la visión de Nahúm de Elkosch.
2 Yehova ni Mungu mwenye wivu na analipa kisasi; Yehova hulipa kisasi na amejaa ghadhabu; Yohova analipiza kisasi kwa adui zake, na huiendeleza hasira yake kwa adui zake.
Yahvé es un Dios celoso y vengador; vengador es Yahvé y lleno de ira. Yahvé ejerce la venganza contra sus adversarios, y guarda rencor a sus enemigos.
3 Yehova ni mwenye nguvu nyingi na mpole wa hasira; hatakuwa na namna ya kuacha kuwahesabia hatia adui zake. Yehova hufanya njia yake kwenye upepo wa kisulisuli na dhoruba, na mawingu ni mavumbi ya miguu yake.
Yahvé es longánimo y grande en poder, y no deja impune (al impío). Marcha Yahvé en el torbellino y en la tempestad, y las nubes son el polvo de sus pies.
4 Huikemea bahari na kuifanya ikauke; hukausha mito yote. Bashani ni dhaifu, na Karmeli pia; maua ya Lebanoni ni dhaifu.
Increpa al mar y lo deja seco, y agota todos los ríos. Faltos de lozanía están Basán y el Carmelo, y el verdor del Líbano se marchita.
5 Milima hutetema kwenye uwepo wake, na vilima huyeyuka; dunia huanguka mbele zake, kabisa, dunia na watu wote wanaoishi ndani yake.
Delante de Él se estremecen los montes, y se derriten los collados. Ante su faz se conmueve la tierra, el orbe y cuantos en él habitan.
6 Ni nani anaweza kusimama mbele ya ghadhabu yake? Nani anaweza kuzuia ukali wa hasira yake? Ghadhabu yake imemwagwa kama moto, na miamba ameibomoa mbalimbali.
¿Quién podrá subsistir ante su ira? ¿Quién resistir el ardor de su cólera? Se derrama como fuego su indignación, y ante Él se hienden las rocas.
7 Yehova ni mwema, boma katika siku ya taabu; na yeye ni mwaminifu kwa wale wanaomkimbilia.
Yahvé es bueno, es fortaleza en el día de la tribulación, Él conoce a los que en Él confían,
8 Lakini atafanya mwisho wa adui zake kwa mafuriko ya kutisha; atawawinda kwenye giza.
Con inundación arrolladora destruirá por completo aquel lugar, y las tinieblas perseguirán a sus enemigos.
9 Watu wanapanga nini dhidi ya Yehova? Yeye atakomesha; taabu haitainuka mara ya pili.
¿Qué maquináis contra Yahvé? El hace devastación completa, no surge dos veces la tribulación.
10 Maana watakuwa wamevurugika kama michongoma; wataloweshwa katika kinywaji chao mwenyewe; wataharibiwa kabisa kwa moto kama mashina ya mabua.
Pues bien atados entre sí, como espinos, esos embriagados de su vino serán consumidos cual paja enteramente seca.
11 Mtu mmoja aliinuka miongoni mwenu, Ninawi, aliyepanga ubaya dhidi ya Yehova, mtu ambaye aliimarisha uovu.
De ti salió el que piensa mal contra Yahvé, el que traza designios de iniquidad.
12 Hivi ndivyo anavyosema Yehova, “Hata kama wananguvu zao timilifu na idadi timilifu, hata hivyo watanyolewa, watu wao hawatakuwepo tena. Bali wewe, Yuda: Ingawa nimekutesa, sitakutesa tena.
Así dice Yahvé: “Aunque sean sanos y salvos y muy numerosos, con todo serán cortados y desaparecerán.” Te he humillado, pero no te humillaré más.
13 Sasa nitaivunja ile nira ya watu kutoka kwako; nitaikata minyororo yako.
Ahora romperé su yugo (que pesa) sobre ti, y haré pedazos tus coyundas.
14 Yehova ametoa amri juu yako, Ninawi: “Hakutakuwa na kizazi tena chenye kubeba jina lako. Nitazizuia sanamu zilizochongwa na kuziondoa sanamu za chuma kutoka kwenye nyumba za miungu yenu. Nitachimba makaburi yenu, kwa kudharauliwa kwenu.”
Yahvé ha decretado respecto de ti: “Ya no habrá más posteridad que lleve tu nombre. Exterminaré de la casa de tus dioses las estatuas e ídolos de fundición; y Yo te haré el sepulcro, porque serás consumida muy pronto.”
15 Tazama, juu ya milima kuna miguu ya mtu aletaye habari njema, anayetangaza amani! Sherehekeeni sikukuu zenu, Yuda, na tunzeni nadhiri zenu, kwa maana mwovu hatawavamia tena; ameondolewa kabisa.
He aquí sobre los montes los pies de aquel que trae buenas nuevas, de aquel que anuncia la paz. Celebra, Judá, tus fiestas, cumple tus votos; que ya no volverá a pasar por ti aquel Belial. Ha sido completamente extirpado.

< Nahumu 1 >