< Nahumu 1 >

1 Maono kuhusu Ninawi. Kitabu cha maono ya Nahumu, Mwelkoshi.
Burden of Nineveh. The Book of the Vision of Nahum the Elkoshite.
2 Yehova ni Mungu mwenye wivu na analipa kisasi; Yehova hulipa kisasi na amejaa ghadhabu; Yohova analipiza kisasi kwa adui zake, na huiendeleza hasira yake kwa adui zake.
A God zealous and avenging [is] Jehovah, An avenger [is] Jehovah, and possessing fury. An avenger [is] Jehovah on His adversaries, And He is watching for His enemies.
3 Yehova ni mwenye nguvu nyingi na mpole wa hasira; hatakuwa na namna ya kuacha kuwahesabia hatia adui zake. Yehova hufanya njia yake kwenye upepo wa kisulisuli na dhoruba, na mawingu ni mavumbi ya miguu yake.
Jehovah [is] slow to anger, and great in power, And Jehovah doth not entirely acquit, In a hurricane and in a tempest [is] His way, And a cloud [is] the dust of His feet.
4 Huikemea bahari na kuifanya ikauke; hukausha mito yote. Bashani ni dhaifu, na Karmeli pia; maua ya Lebanoni ni dhaifu.
He is pushing against a sea, and drieth it up, Yea, all the floods He hath made dry, Languishing [are] Bashan and Carmel, Yea, the flower of Lebanon [is] languishing.
5 Milima hutetema kwenye uwepo wake, na vilima huyeyuka; dunia huanguka mbele zake, kabisa, dunia na watu wote wanaoishi ndani yake.
Mountains have shaken because of Him, And the hills have been melted; And lifted up [is] the earth at His presence, And the world and all dwelling in it.
6 Ni nani anaweza kusimama mbele ya ghadhabu yake? Nani anaweza kuzuia ukali wa hasira yake? Ghadhabu yake imemwagwa kama moto, na miamba ameibomoa mbalimbali.
Before His indignation who doth stand? And who riseth up in the heat of His anger? His fury hath been poured out like fire, And the rocks have been broken by Him.
7 Yehova ni mwema, boma katika siku ya taabu; na yeye ni mwaminifu kwa wale wanaomkimbilia.
Good [is] Jehovah for a strong place in a day of distress. And He knoweth those trusting in Him.
8 Lakini atafanya mwisho wa adui zake kwa mafuriko ya kutisha; atawawinda kwenye giza.
And with a flood passing over, An end He maketh of its place, And His enemies doth darkness pursue.
9 Watu wanapanga nini dhidi ya Yehova? Yeye atakomesha; taabu haitainuka mara ya pili.
What do we devise against Jehovah? An end He is making, arise not twice doth distress.
10 Maana watakuwa wamevurugika kama michongoma; wataloweshwa katika kinywaji chao mwenyewe; wataharibiwa kabisa kwa moto kama mashina ya mabua.
For while princes [are] perplexed, And with their drink are drunken, They have been consumed as stubble fully dried.
11 Mtu mmoja aliinuka miongoni mwenu, Ninawi, aliyepanga ubaya dhidi ya Yehova, mtu ambaye aliimarisha uovu.
From thee hath come forth a deviser of evil Against Jehovah — a worthless counsellor.
12 Hivi ndivyo anavyosema Yehova, “Hata kama wananguvu zao timilifu na idadi timilifu, hata hivyo watanyolewa, watu wao hawatakuwepo tena. Bali wewe, Yuda: Ingawa nimekutesa, sitakutesa tena.
Thus said Jehovah: Though complete, and thus many, Yet thus they have been cut off, And he hath passed away. And I afflicted thee, I afflict thee no more.
13 Sasa nitaivunja ile nira ya watu kutoka kwako; nitaikata minyororo yako.
And now I break his rod from off thee, And thy bands I do draw away.
14 Yehova ametoa amri juu yako, Ninawi: “Hakutakuwa na kizazi tena chenye kubeba jina lako. Nitazizuia sanamu zilizochongwa na kuziondoa sanamu za chuma kutoka kwenye nyumba za miungu yenu. Nitachimba makaburi yenu, kwa kudharauliwa kwenu.”
And commanded concerning thee hath Jehovah, 'No more of thy name doth spread abroad, From the house of thy gods I cut off graven and molten image, I appoint thy grave, for thou hast been vile.
15 Tazama, juu ya milima kuna miguu ya mtu aletaye habari njema, anayetangaza amani! Sherehekeeni sikukuu zenu, Yuda, na tunzeni nadhiri zenu, kwa maana mwovu hatawavamia tena; ameondolewa kabisa.
Lo, on the mountains the feet of one proclaiming tidings, sounding peace! Celebrate, O Judah, thy festivals, complete thy vows, For add no more to pass over into thee doth the worthless, He hath been completely cut off!

< Nahumu 1 >