< Nahumu 1 >

1 Maono kuhusu Ninawi. Kitabu cha maono ya Nahumu, Mwelkoshi.
[the] oracle of Nineveh [the] document of [the] vision of Nahum the Elkoshite.
2 Yehova ni Mungu mwenye wivu na analipa kisasi; Yehova hulipa kisasi na amejaa ghadhabu; Yohova analipiza kisasi kwa adui zake, na huiendeleza hasira yake kwa adui zake.
[is] a God Jealous and avenging Yahweh [is] avenging Yahweh and a lord of rage [is] avenging Yahweh to opponents his and [is] maintaining he to enemies his.
3 Yehova ni mwenye nguvu nyingi na mpole wa hasira; hatakuwa na namna ya kuacha kuwahesabia hatia adui zake. Yehova hufanya njia yake kwenye upepo wa kisulisuli na dhoruba, na mawingu ni mavumbi ya miguu yake.
Yahweh [is] long of anger (and great of *Qk) power and certainly not he will leave unpunished Yahweh [is] in storm-wind and in storm way his and [is] cloud [the] dust of feet his.
4 Huikemea bahari na kuifanya ikauke; hukausha mito yote. Bashani ni dhaifu, na Karmeli pia; maua ya Lebanoni ni dhaifu.
[he is] rebuking the Sea and he made dry it and all the rivers he dries up it withers Bashan and Carmel and [the] blossom of Lebanon it withers.
5 Milima hutetema kwenye uwepo wake, na vilima huyeyuka; dunia huanguka mbele zake, kabisa, dunia na watu wote wanaoishi ndani yake.
Mountains they quake from him and the hills they melt and it lifted up the earth from before him and [the] world and all [those who] dwell in it.
6 Ni nani anaweza kusimama mbele ya ghadhabu yake? Nani anaweza kuzuia ukali wa hasira yake? Ghadhabu yake imemwagwa kama moto, na miamba ameibomoa mbalimbali.
Before indignation his who? will he stand and who? will he endure at [the] burning of anger his rage his it is poured out like fire and the rocks they are pulled down from him.
7 Yehova ni mwema, boma katika siku ya taabu; na yeye ni mwaminifu kwa wale wanaomkimbilia.
[is] good Yahweh a refuge in a day of trouble and [he is] knowing [those who] take refuge in him.
8 Lakini atafanya mwisho wa adui zake kwa mafuriko ya kutisha; atawawinda kwenye giza.
And with a flood [which] passes over complete destruction he will make place its and enemies his he will pursue darkness.
9 Watu wanapanga nini dhidi ya Yehova? Yeye atakomesha; taabu haitainuka mara ya pili.
Whatever you will plot! against Yahweh complete destruction he [will be] making not it will arise two times trouble.
10 Maana watakuwa wamevurugika kama michongoma; wataloweshwa katika kinywaji chao mwenyewe; wataharibiwa kabisa kwa moto kama mashina ya mabua.
For to thorns interwoven and like drink their drunkards they will be consumed like stubble dry full.
11 Mtu mmoja aliinuka miongoni mwenu, Ninawi, aliyepanga ubaya dhidi ya Yehova, mtu ambaye aliimarisha uovu.
From you he has come out [one who] plots on Yahweh evil a counselor of worthlessness.
12 Hivi ndivyo anavyosema Yehova, “Hata kama wananguvu zao timilifu na idadi timilifu, hata hivyo watanyolewa, watu wao hawatakuwepo tena. Bali wewe, Yuda: Ingawa nimekutesa, sitakutesa tena.
Thus - he says Yahweh though complete and thus numerous and thus they will be cut down and he will pass away and I have afflicted you not I will afflict you again.
13 Sasa nitaivunja ile nira ya watu kutoka kwako; nitaikata minyororo yako.
And now I will break yoke-bar his from on you and fetters your I will tear apart.
14 Yehova ametoa amri juu yako, Ninawi: “Hakutakuwa na kizazi tena chenye kubeba jina lako. Nitazizuia sanamu zilizochongwa na kuziondoa sanamu za chuma kutoka kwenye nyumba za miungu yenu. Nitachimba makaburi yenu, kwa kudharauliwa kwenu.”
And he has commanded on you Yahweh not it will be sown from name your again from [the] house of gods your I will cut off idol and molten image I will make grave your for you are insignificant.
15 Tazama, juu ya milima kuna miguu ya mtu aletaye habari njema, anayetangaza amani! Sherehekeeni sikukuu zenu, Yuda, na tunzeni nadhiri zenu, kwa maana mwovu hatawavamia tena; ameondolewa kabisa.
There! on the mountains [the] feet of [one who] bears news [one who] proclaims peace celebrate a festival O Judah festivals your pay vows your for not he will repeat again (to pass *Qk) in you a worthless person all of him it will be cut off.

< Nahumu 1 >