< Mika 3 >

1 Nimesema'”Sasa sikilizeni, ninyi viongozi wa Yakobo na kutawala nyumba ya Israeli: Je siyo sahihi kwenu kuielewa haki?
And he shall say, Hear now these words, you heads of the house of Jacob, and you remnant of the house of Israel; is it not for you to know judgement?
2 Ninyi manaochukia mazuri na kupenda uovu, ninyi mnaoambua ngozi yao, miili yao kutoka kwenye mifupa yao-
[who] hate good, and seek evil; [who] tear their skins off them, and their flesh off their bones:
3 ninyi mnaokula pia miili ya watu wangu, na kuambua ngozi yao, kuvunja mifupa yao, na kuwakatakata katika vipande vipande, kama nyama kwenye chungu, kama nyama kwenye sufuria kubwa.
even as they devoured the flesh of my people, and stripped their skins off them, and broke their bones, and divided [them] as flesh for the cauldron, and as meat for the pot,
4 Kisha ninyi watawala mtalia kwa Yahwe, lakini hatawajibu. Atauficha uso wake kutoka kwenu kipindi hicho, kwasababu mmefanya matendo maovu.”
thus they shall cry to the Lord, but he shall not listen to them; and he shall turn away his face from them at that time, because they have done wickedly in their practices against themselves.
5 Yahwe asema hivi kuhusu manabii ambao wawafanyao watu wangu kushindwa, “Kwa wale wawalishao wanatangaza, 'Kutakuwa na ustawi.' Lakini kwa wale wasioweka kitu kwenye vinywa vyao, wanaanzisha vita dhidi yake.
Thus says the Lord concerning the prophets that lead my people astray, that bit with their teeth, and proclaim peace to them; and [when] nothing was put into their mouth, they raised up war against them:
6 Kwa hiyo, itakuwa usiku kwenu usiokuwa na maono juu yenu; itakuwa giza ili kwamba msiweze kubashiri. Jua litakwenda chini juu ya manabii, na siku itakuwa giza juu yao.
therefore there shall be night to you instead of a vision, and there shall be to you darkness instead of prophecy; and the sun shall go down upon the prophets, and the day shall be dark upon them.
7 Waonaji watawekwa kwenye aibu, waaguzi wa watachanganyikiwa. Wote watafunga midomo yao, kwa kuwa hakuna jibu kutoka kwangu.”
And the seers of night-visions shall be ashamed, and the prophets shall be laughed to scorn: and all the people shall speak against them, because there shall be none to listen to them.
8 Lakini kwangu, nimejazwa nguvu kutoka kwa Roho wa Yahwe, na nimejaa haki na uweza, kumwambia Yakobo kosa lake, na Israeli dhambi yake.
Surely I will strengthen myself with the Spirit of the Lord, and of judgement, and of power, to declare to Jacob his transgressions, and to Israel his sins.
9 Sasa sikieni hii, ninyi viongozi wa nyumba ya Yakobo, na watawala wa nyumba ya Israeli, ninyi ambao mnaochukia haki, na kupotosha kila haki.
Hear now these words, you chiefs of the house of Jacob, and the remnant of the house of Israel, who hate judgement, and pervert all righteousness;
10 Mnaijenga Sayuni kwa damu na Yerusalemu kwa uovu.
who build up Sion with blood, and Jerusalem with iniquity.
11 Viongozi wenu huhukumu kwa rushwa, makuhani wenu hufundisha kwa hijara, na manabii wenu hufanya utabiri kwa ajili ya pesa. Hata hivyo bado mtamtegemea Yahwe na kusema, “Je hayupo Yahwe pamoja nasi? Hakuna uovu utakaokuja juu yetu.”
The heads thereof have judged for gifts, and the priests thereof have answered for hire, and her prophets have divined for silver: and [yet] they have rested on the Lord, saying, Is not the Lord amongst us? no evil shall come upon us.
12 Kwa hiyo, kwasababu yenu, Sayuni italimwa kama shamba, Yerusalemu itakuwa rundo la kifusi, na mwinuko wa hekalu utakuwa kama mwinuko wa msituni.
Therefore on your account Sion shall be ploughed as a field, and Jerusalem shall be as a storehouse of fruits, and the mountain of the house as a grove of the forest.

< Mika 3 >