< Mathayo 9 >

1 Yesu akaingia kwenye boti, akavuka na akafika kwenye mji alipokuwa anaishi.
Тогава Той влезе в една ладия, премина и дойде в Своя Си град.
2 Tazama, wakamletea mtu aliyepooza amelazwa kwenye godoro. alipooiona imani yao, Yesu akamwambia mtu aliyepooza, “Mwanangu, uwe na furaha, Dhambi zako zimesamehewa”
И, ето, донесоха при Него един паралитик, сложен на постелка; и Исус като видя вярата им, рече на паралитика: Дерзай, синко; прощават ти се греховете.
3 Tazama, Baadhi ya walimu wa sheria wakasemezana wao kwa wao, “Huyu mtu anakufuru”
И, ето, някои от книжниците си казаха: Този богохулствува.
4 Yesu akatambua mawazo yao na kusema, “Kwa nini mnawaza maovu moyoni mwenu?
А Исус, като узна помислите им, рече: Защо мислите зло в сърцата си?
5 Kipi kilicho rahisi kusema, 'Dhambi zako zimesamehewa' au kusema, 'Simama na utembee?'
Защото кое е по-лесно, да река: Прощават ти се греховете, или да река: Стани и ходи?
6 Lakini mtambue ya kwamba Mwana wa Adamu anao uwezo wa kusamehe dhambi...” aliyasema haya kwa yule aliyepooza, “Simama, chukua godoro lako, na uende nyumbani kwako”
Но, за да познаете, че Човешкият Син има власт на земята да прощава греховете (тогава каза на паралитика): Стани, вдигни си постелката и иди у дома си.
7 Ndipo yule mtu akasimama na kuondoka kwenda nyumbani kwake.
И той стана и отиде у дома си.
8 Makutano walipoona hayo, walishangaa na kumsifu Mungu, ambaye amewapa uwezo huo watu.
А множествата, като видяха това, страх ги обзе и прославиха Бога, Който бе дал такава власт на човеците.
9 Na Yesu alipokuwa akipita kutoka hapo, alimwona mtu ambaye aliitwa kwa jina la Mathayo, ambaye alikuwa amekaa sehemu ya watoza ushuru. Naye akamwambia, “Nifuate mimi” Naye akasimama na kumfuata.
И като минаваше оттам, Исус видя един човек, на име Матей, седящ в бирничеството; и рече му: Върви след Мене. И той стана да Го последва.
10 Na Yesu alipoketi ili ale chakula ndani ya nyumba, wakaja watoza ushuru wengi na watu waovu wakashiriki chakula pamoja na Yesu na wanafunzi wake.
И когато бе седнал на трапезата в къщата, ето, мнозина бирници и грешници дойдоха и насядаха с Исуса и с учениците Му.
11 Ndipo Mafarisayo walipoona hayo, wakawaambia wanafunzi “Kwa nini mwalimu wenu anakula chakula pamoja na watoza ushuru na watu waovu?”
И фарисеите, като видяха това, рекоха на учениците Му: Защо яде вашият учител с бирниците и грешниците?
12 Yesu aliposikia hayo, naye alisema “Watu walio na afya nzuri hawahitaji mganga, isipokuwa wale walio wagonjwa.
А Той, като чу това, рече: Здравите нямат нужда от лекар, а болните.
13 Inawapasa muende mkajifunze maana yake, “Ninapenda rehema na siyo dhabihu” Kwa kuwa nilikuja, si kwa wenye haki kutubu, lakini kwa wenye dhambi.
Но идете и научете се що значи тази дума: “Милост искам, а не жертви”, защото не съм дошъл да призова праведните, а грешните [на покаяние].
14 Ndipo wanafunzi wa Yohana wakaja kwake na kusema, “Kwa nini sisi na mafarisayo tunafunga, lakini wanafunzi wako hawafungi?”
Тогава дохождат при Него Йоановите ученици и казват: Защо ние и фарисеите постим много, а Твоите ученици не постят?
15 Yesu akawaambia, Je wasindikizaji wa arusi wanaweza kuwa na huzuni pindi Bwana arusi anapokuwa pamoja nao? Lakini siku zinakuja ambapo Bwana arusi atachukuliwa kutoka kwao, na ndipo watakapofunga.
Исус им каза: Могат ли сватбарите да жалеят, докато е с тях младоженецът? Ще дойде обаче, време, когато младоженецът ще им се отнеме; и тогава ще постят.
16 Hakuna mtu anayeweka kipande cha nguo mpya kwenye nguo ya zamani, kiraka kitatatuliwa kutoka kwenye nguo na mpasuko mkubwa utatokea.
Никой не кърпи вехта дреха с невалян плат; защото това, което трябваше да я запълни, отдира от дрехата, и съдраното става по-лошо.
17 Hakuna watu wanaoweka mvinyo mpya katika chombo cha mvinyo wa zamani, ikiwa watafanya, ngozi itachanika, mvinyo utatoweka na ngozi itaharibika. Badala yake, huweka mvinyo mpya katika ngozi mpya na vyote vitakuwa salama.
Нито наливат ново вино във вехти мехове; инак, меховете се спукват, виното изтича, и меховете се изхабяват. Но наливат ново вино в нови мехове, та и двете се запазват.
18 Wakati Yesu alipokuwa akiwaambia mambo hayo, tazama, afisa akaja akasujudu mbele yake, Naye akasema, “Binti yangu amefariki punde, lakini njoo na uweke mkono wako juu yake na yeye ataishi tena.
Когато им говореше това, ето, един началник дойде и им се кланяше, и казваше: Дъщеря ми току що умря; но дойди и възложи ръката Си на нея и тя ще оживее.
19 Ndipo Yesu akasimama na kumfuata na wanafunzi wake pia.
И, като стана, Исус отиде подир него, тоже и учениците Му.
20 Tazama, mwanamke ambaye alikuwa anatokwa damu kwa muda wa miaka kumi na miwili, akaja karibu na Yesu na akagusa sehemu ya pindo la vazi lake.
И, ето, една жена, която имаше кръвотечение дванадесет години, приближи се изотзад и се допря до полата на дрехата Му;
21 Kwa kuwa alisema, “Endapo nitagusa vazi lake, nami nitapata uponyaji.”
защото си думаше: Ако се допра до дрехата Му, ще оздравея.
22 Yesu akageuka na kumtazama na kumwambia. “Binti, jipe moyo, imani yako imekufanya upone,” Na muda huo huo mwanamke akapata uponyaji muda huo.
А Исус като се обърна и я видя, рече: Дерзай, дъщерьо; твоята вяра те изцели. И от същия час жената оздравя.
23 Na Yesu alipofika kwenye nyumba ya afisa, naye aliwaona wapiga tarumbeta na umati wa watu ulikuwa ukipiga kelele.
И когато дойде Исус в къщата на началника, и видя свирачите и народа разтревожен, рече:
24 Naye akasema, “Tokeni hapa, kwa kuwa binti hajafa, bali amelala. Lakini wao walicheka na kumkebehi.
Идете си, защото момичето не е умряло, но спи. А те Му се присмиваха.
25 Na wale watu walipotolewa nje, naye akaingia chumbani na kumshika mkono na msichana akaamka.
А като изпъдиха народа, Той влезе и я хвана за ръката; и момичето стана.
26 Na habari hizi zikaenea katika mji mzima.
И това са разчу по цялата оная страна.
27 Ndipo Yesu alipokuwa akipita kutoka pale, wanaume wawili vipofu wakamfuata. Waliendelea kupaza sauti wakisema, “Tunaomba uturehemu, Mwana wa Daudi.”
И когато Исус си отиваше оттам, подир Него вървяха двама слепи, които викаха, казвайки: Смили се за нас, Сине Давидов!
28 Pindi Yesu apokuwa amefika kwenye nyumba, wale vipofu wakaja kwake. Yesu akawaambia, “Mnaamini kwamba ninaweza kutenda?” Nao wakamwambia “Ndiyo, Bwana”
И като влезе вкъщи, слепите се приближиха до Него; и Исус им казва: Вярвате ли че мога да сторя това? Казват Му: Вярваме, Господи.
29 Ndipo Yesu akagusa macho yao na kusema “Na ifanyike hivyo kwenu kama imani yenu ilivyo”
Тогава Той се допря до очите им, и рече: Нека ви бъде според вярата ви.
30 Na macho yao yakafumbuka. Ndipo Yesu akasisitiza akawaamuru na kusema “Angalieni mtu yeyote asifahamu kuhusu jambo hili.”
И очите им се отвориха. А Исус им заръча строго, като каза: Внимавайте никой да не знае това.
31 Lakini watu hawa wawili wakaondoka na kutangaza habari hizi sehemu zote za mji.
А те, като излязоха разгласиха славата Му по цялата оная страна.
32 Ndipo wale wanaume wawili walipokuwa wakienda zao, Tazama, mtu mmoja bubu aliyepagawa na pepo akaletwa kwa Yesu.
И когато те излизаха, ето, доведоха при Него един ням човек, хванат от бяс.
33 Na pepo walipomtoka, yule mtu bubu akaanza kuongea. Umati ukashangazwa na kusema “Hii haijawahi kutokea katika Israel.
И след като бе изгонен бесът, немият проговори; и множествата се чудеха и думаха: Никога не се е виждало такова нещо в Израиля.
34 Lakini mafarisayo walikuwa wakisema “Kwa wakuu wa pepo, anawafukuza mapepo”
А фарисеите казваха: Чрез началника на бесовете Той изгонва бесовете.
35 Yesu akaenda kwenye miji yote na vijiji. Naye akaendelea kufundisha katika masinagogi, akihubiri injili ya ufalme, na kuponya magonjwa ya kila aina na udhaifu wa aina zote.
Тогава Исус обикаляше всичките градове и села и поучаваше в синагогите им и проповядваше благовестието на царството; и изцеляваше всякаква болест и всякаква немощ.
36 Wakati alipotazama umati, naye aliwaonea huruma, kwa sababu walisumbuka na kuvunjika moyo. Walikuwa kama kondoo wasio na mchungaji.
А когато видя множествата, смили се за тях, защото бяха отрудени и пръснати като овце, които нямат пастир.
37 Naye akawaambia wanafunzi wake. “Mavuno ni mengi, lakini wafanya kazi ni wachache.
Тогава рече на учениците Си: Жетвата и изобилна, а работниците малко;
38 Hivyo basi upesi mwombeni Bwana wa mavuno, ili kwamba atume wafanya kazi katika mavuno yake.”
затова, молете се на Господаря на жетвата да изпрати работници на жетвата Си.

< Mathayo 9 >