< Mathayo 26 >

1 Wakati Yesu alipomaliza kusema maneno yote hayo, aliwaambia wanafunzi wake,
Et il arriva, lorsque Jésus eut achevé tous ces discours, qu’il dit à ses disciples:
2 “Mnajua kwamba baada ya siku mbili kutakuwa na sikukuu ya pasaka, na mwana wa Adamu atatolewa ili asulibiwe.”
Vous savez que la Pâque est dans deux jours, et le fils de l’homme est livré pour être crucifié.
3 Baadaye wakuu wa makuhani na wazee wa watu walikutana pamoja katika makao ya Kuhani Mkuu, aliye kuwa anaitwa Kayafa.
Alors les principaux sacrificateurs et les anciens du peuple s’assemblèrent dans le palais du souverain sacrificateur, appelé Caïphe,
4 Kwa pamoja walipanga njama ya kumkamata Yesu kwa siri na kumuua.
et tinrent conseil ensemble pour se saisir de Jésus par ruse et le faire mourir;
5 Kwa kuwa walisema, “Isifanyike wakati wa sikukuu, kusudi isije ikazuka ghasia miongoni mwa watu.”
mais ils disaient: Non pas pendant la fête, afin qu’il n’y ait pas de tumulte parmi le peuple.
6 Wakati Yesu alipokuwa Bethania katika nyumba ya Simoni mkoma,
Et comme Jésus était à Béthanie dans la maison de Simon le lépreux,
7 alipokuwa amejinyoosha mezani, mwanamke mmoja alikuja kwake akiwa amebeba mkebe wa alabasta iliyokuwa na mafuta yenye thamani kubwa, na aliyamimina juu ya kichwa chake.
une femme, ayant un vase d’albâtre [plein] d’un parfum de grand prix, vint à lui et le répandit sur sa tête comme il était à table.
8 Lakini wanafunzi wake walipoona jambo hilo, walichukia na kusema, “Nini sababu ya hasara hii?
Et les disciples, le voyant, en furent indignés, disant: À quoi bon cette perte?
9 Haya yangeweza kuuzwa kwa kiasi kikubwa na kupewa maskini.”
Car ce [parfum] aurait pu être vendu pour une forte somme, et être donné aux pauvres.
10 Lakini Yesu, akiwa anajua hili, aliwaambia, “Kwa nini mnamsumbua mwanamke huyu? Kwa kuwa amefanya kitu kizuri kwangu.
Et Jésus, le sachant, leur dit: Pourquoi donnez-vous du déplaisir à cette femme? car elle a fait une bonne œuvre envers moi;
11 Masikini mnao siku zote, lakini hamtakuwa pamoja nami daima.
car vous avez toujours les pauvres avec vous, mais moi, vous ne m’avez pas toujours;
12 Kwa sababu alipomimina mafuta haya juu ya mwili wangu, alifanya hivyo kwa ajili ya maziko yangu.
car cette femme, en répandant ce parfum sur mon corps, l’a fait pour ma sépulture.
13 Kweli nawaambieni, popote Injili hii itakapohubiriwa katika ulimwengu mzima, kitendo alichofanya huyu mwanamke, pia kitakuwa kinasemwa kwa ajili ya kumkumbuka.”
En vérité, je vous dis: En quelque lieu que cet évangile soit prêché dans le monde entier, on parlera aussi de ce que cette femme a fait, en mémoire d’elle.
14 Ndipo mmoja wa wale Kumi na wawili, aliyeitwa Yuda Iskariote, alienda kwa wakuu wa makuhani
Alors l’un des douze, appelé Judas Iscariote, s’en alla vers les principaux sacrificateurs,
15 na kusema, “Mtanipatia nini nikimsaliti?” Wakampimia Yuda vipande thelathini vya fedha.
et dit: Que voulez-vous me donner, et moi, je vous le livrerai? Et ils lui comptèrent 30 pièces d’argent.
16 Tangu muda huo alitafuta nafasi ya kumsaliti.
Et dès lors, il cherchait une bonne occasion pour le livrer.
17 Hata siku ya kwanza ya mikate isiyotiwa chachu, wanafunzi walimwendea Yesu na kusema, “Wapi unataka tukuandalie ule chakula cha Pasaka?”
Et, le premier jour des pains sans levain, les disciples vinrent à Jésus, disant: Où veux-tu que nous te préparions [ce qu’il faut] pour manger la pâque?
18 Akawaambia, “Nendeni mjini kwa mtu fulani na mwambieni, Mwalimu anasema, “Muda wangu umekaribia. Nitaitimiza Pasaka pamoja na wanafunzi wangu katika nyumba yako.””
Et il dit: Allez à la ville auprès d’un tel, et dites-lui: Le maître dit: Mon temps est proche; je ferai la pâque chez toi avec mes disciples.
19 Wanafunzi walifanya kama Yesu alivyowaagiza, na waliandaa chakula cha Pasaka.
Et les disciples firent comme Jésus leur avait ordonné, et ils apprêtèrent la pâque.
20 Ilipofika jioni, aliketi kula chakula pamoja na wale wanafunzi Kumi na Wawili.
Et le soir étant venu, il se mit à table avec les douze.
21 Walipokuwa wanakula chakula, alisema, “Kweli nawaambia kwamba mmoja wenu atanisaliti.”
Et comme ils mangeaient, il dit: En vérité, je vous dis que l’un d’entre vous me livrera.
22 Walihuzunika sana, na kila mmoja alianza kumuuliza, “Je, hakika siyo mimi, Bwana?”
Et, en étant fort attristés, ils commencèrent, chacun d’eux, à lui dire: Seigneur, est-ce moi?
23 Akawajibu, “Yule ambaye anachovya mkono wake pamoja nami katika bakuli ndiye atakaye nisaliti.
Et lui, répondant, dit: Celui qui aura trempé la main avec moi dans le plat, celui-là me livrera.
24 Mwana wa Adamu ataondoka, kama alivyoandikiwa. Lakini ole wake mtu ambaye atamsaliti Mwana wa Adamu! Ingekuwa vizuri kwa mtu huyo kama asingezaliwa.”
Le fils de l’homme s’en va, selon qu’il est écrit de lui; mais malheur à cet homme par qui le fils de l’homme est livré! Il aurait été bon pour cet homme-là qu’il ne soit pas né.
25 Yuda, ambaye angemsaliti alisema, “Je!, Ni mimi Rabi?” Yesu akamwambia, “Umesema jambo hilo wewe mwenyewe.”
Et Judas qui le livrait, répondant, dit: Est-ce moi, Rabbi? Il lui dit: Tu l’as dit.
26 Walipokuwa wakila chakula, Yesu aliutwaa mkate, akaubariki, na kuumega. Akawapa wanafunzi wake akisema, “Chukueni, mle. Huu ni mwili wangu.”
Et comme ils mangeaient, Jésus ayant pris le pain et ayant béni, le rompit et le donna aux disciples, et dit: Prenez, mangez; ceci est mon corps.
27 Akatwaa kikombe na kushukuru, akawapa na kusema, “Kunyweni wote katika hiki.
Et, ayant pris la coupe et ayant rendu grâces, il la leur donna, disant: Buvez-en tous.
28 Kwa kuwa hii ni damu ya agano langu, inayomwagwa kwa ajili ya wengi kwa msamaha wa dhambi.
Car ceci est mon sang, le [sang] de la nouvelle alliance, qui est versé pour plusieurs en rémission de péchés.
29 Lakini nawaambieni, sitakunywa tena matunda ya mzabibu huu, hadi siku ile nitakapokunywa mpya pamoja nanyi katika ufalme wa Baba yangu.”
Mais je vous dis que désormais je ne boirai plus de ce fruit de la vigne, jusqu’à ce jour où je le boirai nouveau avec vous dans le royaume de mon Père.
30 Walipokuwa wamemaliza kuimba wimbo, walitoka kwenda Mlima wa Mizeituni.
Et ayant chanté une hymne, ils sortirent [et s’en allèrent] à la montagne des Oliviers.
31 Kisha Yesu aliwaambia, “Usiku huu ninyi nyote mtajikwaa kwa sababu yangu, kwa kuwa imeandikwa, Nitampiga mchungaji na kondoo wa kundi watatawanyika.
Alors Jésus leur dit: Vous serez tous scandalisés en moi cette nuit; car il est écrit: « Je frapperai le berger, et les brebis du troupeau seront dispersées »;
32 Lakini baada ya kufufuka kwangu, nitawatangulia kwenda Galilaya.”
mais, après que j’aurai été ressuscité, j’irai devant vous en Galilée.
33 Lakini Petro alimwambia, “Hata kama wote watakukataa kwa sababu ya mambo yatakayokupata, mimi sitakukataa.”
Et Pierre, répondant, lui dit: Si tous étaient scandalisés en toi, moi, je ne serai jamais scandalisé [en toi].
34 Yesu akamjibu, “kweli nakuambia, usiku huu kabla jogoo hajawika, utanikana mara tatu.”
Jésus lui dit: En vérité, je te dis, que cette nuit-ci, avant que le coq ait chanté, tu me renieras trois fois.
35 Petro akamwambia, “hata kama ingenipasa kufa na wewe, sitakukana.” Na wanafunzi wengine wote wakasema vivyo hivyo.
Pierre lui dit: Quand même il me faudrait mourir avec toi, je ne te renierai point. Et tous les disciples dirent la même chose.
36 Baadaye Yesu alienda nao mahali panapoitwa Gethsemane na aliwaambia wanafunzi wake, “Kaeni hapa wakati nikienda huko na kuomba.”
Alors Jésus s’en vient avec eux en un lieu appelé Gethsémané, et dit aux disciples: Asseyez-vous ici, jusqu’à ce que, m’en étant allé, j’aie prié là.
37 Akamchukua Petro na wana wawili wa Zebedayo na akaanza kuhuzunika na kusononeka.
Et ayant pris Pierre et les deux fils de Zébédée, il commença à être attristé et fort angoissé.
38 Kisha aliwaambia, “Roho yangu ina huzuni kubwa sana, hata kiasi cha kufa. Bakini hapa na mkeshe pamoja nami.”
Alors il leur dit: Mon âme est saisie de tristesse jusqu’à la mort; demeurez ici et veillez avec moi.
39 Akenda mbele kidogo, akaanguka kifudifudi, na kuomba. Akasema, “Baba yangu, kama inawezekana, kikombe hiki kiniepuke. Isiwe kama ninavyotaka mimi, bali kama utakavyo wewe.”
Et s’en allant un peu plus avant, il tomba sur sa face, priant et disant: Mon Père, s’il est possible, que cette coupe passe loin de moi; toutefois, non pas comme moi je veux, mais comme toi [tu veux].
40 Akawaendea wanafunzi na akawakuta wamelala usingizi, na akamwambia Petro, “Kwa nini hamkuweza kukesha nami kwa saa moja?
Et il vient vers les disciples, et il les trouve dormant; et il dit à Pierre: Ainsi, vous n’avez pas pu veiller une heure avec moi?
41 Kesheni na kuomba kusudi msiingie majaribuni. Roho i radhi, lakini mwili ni dhaifu.”
Veillez et priez, afin que vous n’entriez pas en tentation; l’esprit est prompt, mais la chair est faible.
42 Akaenda zake mara ya pili na kuomba, akasema, “Baba yangu, kama jambo hili haliwezi kuepukika na ni lazima nikinywee kikombe hiki, mapenzi yako yatimizwe.”
Il s’en alla de nouveau, une seconde fois, et il pria, disant: Mon Père, s’il n’est pas possible que ceci passe loin de moi, sans que je le boive, que ta volonté soit faite.
43 Akarudi tena na kuwakuta wamelala usingizi, kwa kuwa macho yao yalikuwa mazito.
Et étant venu, il les trouva de nouveau dormant; car leurs yeux étaient appesantis.
44 Kisha akawaacha tena akaenda zake. Akaomba mara ya tatu akisema maneno yaleyale.
Et les laissant, il s’en alla de nouveau, et pria une troisième fois, disant les mêmes paroles.
45 Baadaye Yesu aliwaendea wanafunzi wake na kuwaambia, “Bado mmelala tu na kujipumzisha? Tazameni, saa imekaribia, na Mwana wa Adamu anasalitiwa mikononi mwa wenye dhambi.
Alors il vient vers les disciples, et leur dit: Dormez dorénavant et reposez-vous; voici, l’heure s’est approchée, et le fils de l’homme est livré entre les mains des pécheurs.
46 Amkeni, tuondoke. Tazama, yule anaye nisaliti amekaribia.”
Levez-vous, allons; voici, celui qui me livre s’est approché.
47 Wakati alipokuwa bado anaongea, Yuda mmoja wa wale Kumi na Wawili, akafika. Kundi kubwa lilifika pamoja naye likitokea kwa wakuu wa makuhani na wazee wa watu. Walikuja na mapanga na marungu.
Et comme il parlait encore, voici Judas, l’un des douze, vint, et avec lui une grande foule avec des épées et des bâtons, de la part des principaux sacrificateurs et des anciens du peuple.
48 Tena mtu aliyekusudia kumsaliti Yesu alikuwa amewapa ishara, akisema, “Yule nitakayembusu, ndiye yeye. Mkamateni.”
Et celui qui le livrait leur donna un signe, disant: Celui que j’embrasserai, c’est lui; saisissez-le.
49 Mara hiyo alikuja kwa Yesu na kusema, “Salamu, Mwalimu!” Na akambusu.
Et aussitôt, s’approchant de Jésus, il dit: Je te salue, Rabbi; et il l’embrassa avec empressement.
50 Yesu akamwambia, “Rafiki, lifanye lile ambalo limekuleta.” Ndipo wakaja, na kumnyooshea mikono Yesu, na kumkamata.
Et Jésus lui dit: Ami, pourquoi es-tu venu? Alors, s’étant approchés, ils mirent les mains sur Jésus et se saisirent de lui.
51 Tazama, mtu mmoja aliyekuwa pamoja na Yesu, alinyosha mkono wake, akachomoa upanga wake, na akampiga mtumishi wa kuhani mkuu, na kumkata sikio lake.
Et voici, l’un de ceux qui étaient avec Jésus, étendant la main tira son épée, et frappant l’esclave du souverain sacrificateur, lui emporta l’oreille.
52 Ndipo Yesu akamwambia, rudisha upanga wako pale ulipoutoa, kwa kuwa wote watumiao upanga wataangamizwa kwa upanga.
Alors Jésus lui dit: Remets ton épée en son lieu; car tous ceux qui auront pris l’épée périront par l’épée.
53 Mnadhani kuwa siwezi kumwita Baba yangu, naye akanitumia majeshi zaidi ya kumi na mawili ya malaika?
Penses-tu que je ne puisse pas maintenant prier mon Père, et il me fournira plus de douze légions d’anges?
54 Lakini basi jinsi gani maandiko yangeweza kutimizwa, hivi ndivyo inapasa kutokea?”
Comment donc seraient accomplies les écritures, [qui disent] qu’il faut qu’il en arrive ainsi?
55 Wakati huo Yesu akauambia umati, “Je! Mmekuja na mapanga na marungu kunikamata kama mnyang'anyi? Kila siku nilikaa hekaluni nikifundisha, na hamkunishika!
En cette heure-là Jésus dit aux foules: Êtes-vous sortis comme après un brigand, avec des épées et des bâtons, pour me prendre? J’étais tous les jours assis parmi vous, enseignant dans le temple; et vous ne vous êtes pas saisis de moi.
56 Lakini yote haya yametendeka ili Maandiko ya manabii yatimie.” Ndipo wanafunzi wake wakamwacha na kukimbia.
Mais tout ceci est arrivé, afin que les écritures des prophètes soient accomplies. Alors tous les disciples le laissèrent et s’enfuirent.
57 Wale waliomkamata Yesu alimpeleka kwa Kayafa, Kuhani Mkuu, mahali ambapo waandishi na wazee walikuwa wamekusanyika pamoja.
Et ceux qui s’étaient saisis de Jésus l’amenèrent à Caïphe le souverain sacrificateur, où les scribes et les anciens étaient assemblés.
58 Lakini Petro alimfuata nyuma kwa mbali hadi katika ukumbi wa Kuhani Mkuu. Aliingia ndani na kukaa pamoja na walinzi aone kitakachotokea.
Et Pierre le suivait de loin, jusqu’au palais du souverain sacrificateur; et étant entré, il s’assit avec les huissiers pour voir la fin.
59 Basi wakuu wa makuhani na Baraza lote walikuwa wakitafuta ushahidi wa uongo dhidi ya Yesu, kusudi wapate kumuua.
Or les principaux sacrificateurs et les anciens et tout le sanhédrin cherchaient [quelque] faux témoignage contre Jésus, de manière à le faire mourir;
60 Ingawa walijitokeza mashahidi wengi, Lakini hawakupata sababu yoyote. Lakini baadaye mashahidi wawili walijitokeza mbele
et ils n’en trouvèrent point, – bien que plusieurs faux témoins soient venus. Mais, à la fin, deux faux témoins vinrent,
61 na kusema, “Mtu huyu alisema, ''Naweza kulivunja hekalu la Mungu na kulijenga tena kwa siku tatu.”'
et dirent: Celui-ci a dit: Je puis détruire le temple de Dieu, et en trois jours le bâtir.
62 Kuhani Mkuu alisimama na kumwuliza, “Hauwezi kujibu? Hawa wanakushuhudia nini dhidi yako?”
Et le souverain sacrificateur, se levant, lui dit: Ne réponds-tu rien? De quoi ceux-ci témoignent-ils contre toi?
63 Lakini Yesu alikaa kimya. Kuhani Mkuu akamwambia, “Kama Mungu aishivyo, nakuamuru utwambie, kama wewe ni Kristo, Mwana wa Mungu.”
Mais Jésus garda le silence. Et le souverain sacrificateur, répondant, lui dit: Je t’adjure, par le Dieu vivant, que tu nous dises si toi, tu es le Christ, le Fils de Dieu.
64 Yesu akamjibu, “Wewe mwenyewe umesema jambo hilo. Lakini nakuambia, toka sasa na kuendelea utamwona Mwana wa Adamu ameketi mkono wa kulia wenye Nguvu, na akija katika mawingu ya mbinguni.”
Jésus lui dit: Tu l’as dit. De plus, je vous dis: dorénavant vous verrez le fils de l’homme assis à la droite de la puissance, et venant sur les nuées du ciel.
65 Ndipo Kuhani Mkuu alirarua mavazi yake na kusema, “Amekufuru! Je, twahitaji tena ushahidi wa nini? Angalia, tayari mmesikia akikufuru.
Alors le souverain sacrificateur déchira ses vêtements, disant: Il a blasphémé; qu’avons-nous encore besoin de témoins? Voici, vous avez entendu maintenant [son] blasphème:
66 Je! Mnawaza nini? Wakajibu na kusema, “Anastahili kifo.”
que vous en semble? Et répondant, ils dirent: Il mérite la mort.
67 Kisha walimtemea mate usoni na kumpiga ngumi, na kumchapa makofi kwa mikono yao,
Alors ils lui crachèrent au visage et lui donnèrent des soufflets; et quelques-uns le frappèrent,
68 na kusema, “Tutabirie, wewe Kristo. Ni nani amekuchapa?”
disant: Prophétise-nous, Christ; qui est celui qui t’a frappé?
69 Wakati huo Petro alikuwa amekaa nje katika ukumbi, na mtumishi wa kike alimwendea na kusema, “Wewe pia ulikuwa pamoja na Yesu wa Galilaya.”
Or Pierre était assis dehors, dans la cour; et une servante vint à lui, disant: Et toi, tu étais avec Jésus le Galiléen.
70 Lakini alikana mbele yao wote, akisema, Sijui kitu unachosema.”
Et il le nia devant tous, disant: Je ne sais ce que tu dis.
71 Alipoenda nje ya lango, mtumishi mwingine wa kike alimwona na kuwaambia waliokuwepo hapo, “Mtu huyu pia alikuwa pamoja na Yesu wa Nazareti.”
Et une autre [servante] le vit, comme il était sorti dans le vestibule; et elle dit à ceux qui étaient là: Celui-ci aussi était avec Jésus le Nazaréen.
72 Akakana tena kwa kiapo, “Mimi simjui mtu huyu.”
Et il le nia de nouveau avec serment: Je ne connais pas cet homme!
73 Muda mfupi baadaye, wale waliokuwa wamesimama karibu, walimwendea na kusema na Petro, “Kwa hakika wewe pia ni mmoja wao, kwa kuwa hata lafudhi yako inaonesha.”
Et un peu après, ceux qui se trouvaient là s’approchèrent et dirent à Pierre: Certainement, toi, tu es aussi de ces gens-là; car aussi ton langage te fait reconnaître.
74 Ndipo alianza kulaani na kuapa, “Mimi simfahamu mtu huyu,” na mara hiyo jogoo akawika.
Alors il se mit à faire des imprécations et à jurer: Je ne connais pas cet homme! Et aussitôt le coq chanta.
75 Petro alikumbuka maneno aliyoambiwa na Yesu, “Kabla jogoo hajawika utanikana mara tatu.”
Et Pierre se souvint de la parole de Jésus, qui lui avait dit: Avant que le coq chante, tu me renieras trois fois. Et étant sorti dehors, il pleura amèrement.

< Mathayo 26 >