< Mathayo 25 >

1 Ndipo ufalme wa mbinguni utafananishwa na wanawali kumi waliochukua taa zao na kuondoka kwenda kumpokea bwana harusi.
Тогава небесното царство ще се уприличи на десет девици, които взеха светилниците си, и излязоха да посрещнат младоженеца.
2 Watano miongoni mwao walikuwa wapumbavu na watano wengine walikuwa werevu.
А от тях пет бяха неразумни и пет разумни.
3 Wanawali wapumbavu walipochukua taa zao, hawakuchukua mafuta yoyote.
Защото неразумните, като взеха светилниците, не взеха масло със себе си.
4 Bali wanawali welevu walichukua vyombo vyenye mafuta pamoja na taa zao.
Но разумните, заедно със светилниците си взеха и масло в съдовете си.
5 Sasa wakati bwana harusi amechelewa kufika, wote walishikwa usingizi na wakalala.
И докато се бавеше младоженецът, додряма се на всичките, и заспаха.
6 Lakini wakati wa usiku wa manane kulikuwa na yowe, 'Tazama, bwana harusi! Tokeni nje mkampokee.'
А по среднощ се нададе вик: Ето младоженецът [иде!] излизайте да го посрещнете!
7 Ndipo hao wanawali waliamka wote na kuwasha taa zao.
Тогава всички ония девици станаха и приготвиха светилниците си.
8 Wale wapumbavu waliwaambia wale welevu, 'Mtupatie sehemu ya mafuta yenu kwa sababu taa zetu zinazimika.'
А неразумните рекоха на разумните: Дайте ни от вашето масло, защото нашите светилници угасват.
9 Lakini wale welevu waliwajibu na kuwaambia, 'Kwa kuwa hayatatutosha sisi na ninyi, badala yake nendeni kwa wanaouza mjinunulie kiasi kwa ajili yenu.'
А разумните в отговор казаха: Да не би да не стигне и за нас и за вас, по-добре идете при продавачите и си купете.
10 Wakati wameenda huko kununua, Bwana harusi alifika, na wote waliokuwa tayari walienda naye kwenye sherehe ya harusi, na mlango ulifungwa.
А когато те отидоха да купят, младоженецът пристигна; и готовите влязоха с него на сватбата, и вратата се затвори.
11 Baadaye wale wanawali wengine pia walifika na kusema, 'Bwana, bwana, tufungulie.'
После дохождат и другите девици и казват: Господи! Господи! Отвори ни.
12 Lakini alijibu na kusema, 'Kweli nawaambia, Mimi siwajui.'
А той в отговор рече: Истина ви казвам: Не ви познавам.
13 Kwa hiyo angalieni, kwa kuwa hamjui siku au saa.
И тъй, бдете; защото не знаете ни деня, ни часа, [в който Човешкият Син ще дойде].
14 Kwa kuwa ni sawa na mtu alipotaka kusafiri kwenda nchi nyingine. Aliwaita watumwa wake na kuwakabidhi utajiri wake.
Защото е както, когато човек при тръгването си за чужбина, свиква своите слуги, и им предаде имота си.
15 Mmoja wao alimpatia talanta tano, mwingine alimpa mbili, na yule mwingine alimpa talanta moja. Kila mmoja alipokea kiasi kulingana na uwezo wake, na yule mtu alisafari kwenda zake.
На един даде пет таланта, на друг два, на трети един, на всеки според способността му; и тръгна.
16 Mapema yule aliyepokea talanta tano alienda kuziwekeza, na kuzalisha talanta zingine tano.
Веднага тоя, който получи петте таланта, отиде и търгува с тях, и спечели още пет таланта.
17 Vilevile yule aliyepokea talanta mbili, alizalisha zingine mbili.
Също и тоя, който получи двата спечели още два.
18 Lakini mtumwa aliyepokea talanta moja, alienda zake, akachimba shimo ardhini, na kuificha fedha ya bwana wake.
А тоя, който получи единия, отиде разкопа в земята, и скри парите на господаря си.
19 Na baada ya muda mrefu, bwana wa watumwa hao alirudi na kutengeneza mahesabu nao.
След дълго време дохожда господарят на тия слуги и прегледа сметката с тях,
20 Yule mtumwa aliyepokea talanta tano alikuja na kuleta talanta zingine tano, akasema, 'Bwana, ulinipa talanta tano. Tazama, nimepata faida ya talanta zingine tano.'
И когато се приближи тоя, който бе получил петте таланта, донесе още пет таланта, и рече: Господарю, ти ми предаде пет таланта; ето, спечелих още пет.
21 Bwana wake alimwambia, 'Hongera, mtumwa mzuri na mwaminifu! Umekuwa mwaminifu kwa vitu vidogo. Nitakupa madaraka juu ya vitu vingi. Ingia katika furaha ya bwana wako.'
Господарят му рече: Хубаво, добри е верни слуго! В малкото си бил верен, над многото ще те поставя; влез в радостта на господаря си.
22 Mtumwa aliyepokea talanta mbili alikuja na kusema, 'Bwana, ulinipa talanta mbili. Tazama, nimepata faida ya talanta zingine mbili,'
Приближи се и тоя, който бе получил двата таланта, и рече: Господарю, ти ми даде два таланта, ето, спечелих още два таланта.
23 Bwana wake alimwambia, 'Hongera, mtumwa mzuri na mwaminifu! Umekuwa mwaminifu kwa vitu vichache. Nitakupa madaraka juu ya vitu vingi. Ingia katika furaha ya bwana wako.'
Господарят му рече: Хубаво, добри и верни слуго! Над малкото си бил верен, над многото ще те поставя; влез в радостта на господаря си.
24 Baadaye mtumwa aliyepokea talanta moja alikuja na kusema, 'Bwana, najua kuwa wewe ni mtu mkali. Unachuma mahali ambapo hukupanda, na unavuna mahali ambapo hukusia.
Тогава се приближи тоя който бе получил един талант, и рече: Господарю, аз те знаех, че си строг човек; жънеш гдето не си сял, и събираш гдето не си пръскал;
25 Mimi niliogopa, nikaenda zangu na kuificha talanta yako katika udongo. Tazama, unayo hapa ile iliyo yako.'
и като се убоях отидох и скрих таланта ти в земята; ето, имаш своето.
26 Lakini bwana wake alijibu na kusema, 'Wewe mtumwa mwovu na mzembe, ulijua kwamba ninachuma mahali ambapo sijapanda na kuvuna mahali ambapo sikusia.
А Господарят му в отговор каза: Зли и лениви слуго! Знаел си, че жъна гдето не съм сял, и събирам гдето не съм пръскал;
27 Kwahiyo ulipaswa kuwapa fedha yangu watu wa benki, na wakati wa kurudi kwangu ningeipokea ile yangu pamoja na faida.
ти, прочее, трябваше да внесеш парите ми на банкерите, и когато си дойдех, щях да взема своето с лихва.
28 Kwa hiyo mnyang'anyeni hiyo talanta na mpeni yule mtumwa aliye na talanta kumi.
Затова, вземете от него таланта и дайте го на този, който има десет таланта.
29 Kila mtu aliye nacho, ataongezewa zaidi-hata kwa kuzidishiwa sana. Lakini kwa yeyote asiye na kitu, hata alicho nacho atanyang'anywa.
Защото на всекиго, който има, ще се даде, и той ще има изобилие; а от този, който няма от него ще се отнеме и това, което има.
30 Mtupeni nje gizani huyo mtumwa asiyefaa, ambako kutakuwa na kilio na kusaga meno.'
А тоя безполезен слуга хвърлете във външната тъмнина; там ще бъде плач и скърцане със зъби.
31 Wakati Mwana wa Adamu atakapokuja katika utukufu wake, na malaika wote pamoja naye, ndipo atakapokaa juu ya kiti chake cha utukufu.
А когато дойде Човешкият Син в славата Си, и всичките [свети] ангели с Него, тогава ще седне на славния Си престол.
32 Mataifa yote yatakusanyika mbele zake, naye atawatenganisha watu, kama vile mchungaji anavyowatenganisha kondoo na mbuzi.
И ще се съберат пред Него всичките народи; и ще ги отлъчи един от други, както овчарят отлъчва овцете от козите;
33 Atawaweka kondoo mkono wake wa kuume, bali mbuzi atawaweka mkono wa kushoto.
и ще постави овцете от дясната Си страна, а козите от лявата.
34 Kisha mfalme atawaambia wale walio mkono wake wa kulia, 'Njoni, mliobarikiwa na Baba yangu, urithini ufalme ulioandaliwa kwa ajili yenu tangu kuwekwa msingi wa ulimwengu.
Тогава Царят ще рече на тия, които са от дясната Му страна: Дойдете вие благословени от Отца Ми, наследете царството, приготвено за вас от създанието на света.
35 Kwa kuwa nilikuwa na njaa na mlinipa chakula; Nilikuwa mgeni na mlinikaribisha;
Защото огладнях и Ме нахранихте; ожаднях и Ме напоихте; странник бях, и Ме прибрахте;
36 Nilikuwa uchi, na mlinivika nguo; Nilikuwa mgonjwa na mkanitunza; Nilikuwa kifungoni na mkaniijia.'
гол бях и Ме облякохте; болен бях и Ме посетихте; в тъмница бях и Ме споходихте.
37 Ndipo wenye haki watamjibu na kumwambia, 'Bwana, lini tulikuona ukiwa na njaa, na kukulisha? Au una kiu na tukakupa maji?
Тогава праведните в отговор ще му кажат: Господи, кога Те видяхме гладен, и Те нахранихме; или жаден, и Те напоихме?
38 Na lini tulikuona ukiwa mgeni, na tukakukaribisha? Au ukiwa uchi na tukakuvisha nguo?
И кога Те видяхме странник, и Те прибрахме, или гол и Те облякохме?
39 Na lini tulikuona ukiwa mgonjwa, au katika kifungo, na tukakujia?
И кога Те видяхме болен или в тъмница и Те споходихме?
40 Na mfalme atawajibu na kuwaambia, 'Kweli nawaambia, mlichotenda hapa kwa mmoja wa ndugu zangu wadogo, mlinitendea mimi.'
А Царят в отговор ще им рече: Истина ви казвам: Понеже сте направили това на един от тия най-скромни Мои братя, на Мене сте го направили.
41 Ndipo atawaambia hao walio mkono wake wa kushoto, 'Ondokeni kwangu, mliolaaniwa, nendeni katika moto wa milele ulioandaliwa kwa ajili ya shetani na malaika zake, (aiōnios g166)
Тогава ще рече и на тия, които са от лявата Му страна: Идете си от Мене, вие проклети, във вечния огън, приготвен за дявола и за неговите ангели. (aiōnios g166)
42 kwa sababu nilikuwa na njaa lakini hamkunipa chakula; Nilikuwa na kiu lakini hamkunipa maji;
Защото огладнях и не Ме нахранихте; ожаднях и не Ме напоихте;
43 Nilikuwa mgeni lakini hamkunikaribisha; nikiwa uchi lakini hamkunipa mavazi; nikiwa mgonjwa na nikiwa kifungoni, lakini hamkunitunza.'
странник бях, и не Ме облякохте; болен и в тъмница бях, и не Ме посетихте.
44 Ndipo wao pia watamjibu na kusema, 'Bwana, lini tulikuona ukiwa na njaa, au una kiu, au u mgeni, au ukiwa uchi, au ukiwa mgonjwa, au ukiwa mfungwa, na hatukukuhudumia?
Тогава и те в отговор ще кажат: Господи, кога Те видяхме гладен, или жаден, или странник, или гол, или болен, или в тъмница и не Ти послужихме?
45 Kisha atawajibu na kusema, 'Kweli nawaambia, kile ambacho hamkutenda kwa mmoja wa hawa wadogo, hamkunitendea mimi.'
Тогава в отговор ще им рече: Истина ви казвам: Понеже не сте направили това на ни един от тия най-скромните, нито на Мене сте го направили.
46 Hawa watakwenda katika adhabu ya milele bali wenye haki katika uzima wa milele.” (aiōnios g166)
И тия ще отидат във вечно наказание, а праведните във вечен живот. (aiōnios g166)

< Mathayo 25 >