< Mathayo 23 >

1 Baadaye aliongea na umati wa watu na wanafunzi wake. Akasema,
Alors Jésus, parlant à la foule et à ses disciples,
2 “Waandishi na Mafarisayo wanakalia kiti cha Musa.
dit: Les scribes et les pharisiens sont assis sur le siège de Moïse.
3 Kwa hiyo chochote wanacho waamuru kufanya, fanyeni huku mkiwachunguza. Lakini msije mkaiga matendo yao, kwa sababu wao hutamka mambo wasiyoyafanya.
Tout ce qu'ils vous disent d'observer, observez-le et faites-le; mais ne faites pas leurs œuvres, car ils disent et ne font pas.
4 Kweli, wao hufunga mizigo mizito ambayo ni vigumu kuibeba, na kisha huwabebesha watu mabegani mwao. Lakini wao wenyewe hawasogezi hata kidole kuibeba.
Car ils lient des fardeaux lourds et pénibles à porter, et les mettent sur les épaules des hommes; mais eux-mêmes ne lèvent pas le petit doigt pour les aider.
5 Matendo yao yote, huyafanya ili watazamwe na watu. Kwa sababu wao hupanua masanduku yao na huongeza ukubwa wa mapindo ya mavazi yao.
Mais ils font toutes leurs œuvres pour être vus des hommes. Ils élargissent leurs phylactères et agrandissent les franges de leurs vêtements,
6 Wao hupendelea kukaa maeneo ya kifahari katika sherehe na katika viti vya heshima ndani ya masinagogi,
ils aiment les places d'honneur dans les fêtes, les meilleures places dans les synagogues,
7 na kusalimiwa kwa heshima maeneo ya sokoni, na kuitwa “Walimu” na watu.
les salutations sur les places publiques, et être appelés par les hommes « Rabbi, Rabbi".
8 Lakini ninyi hampaswi kuitwa “Walimu,” Kwa kuwa mnaye Mwalimu mmoja, na ninyi wote ni ndugu.
Mais vous ne devez pas être appelés « Rabbi », car un seul est votre maître, le Christ, et vous êtes tous frères.
9 Msimuite mtu yeyote hapa duniani kuwa baba yenu, kwa kuwa mnaye Baba mmoja tu, naye yuko mbinguni.
N'appelez aucun homme sur la terre votre père, car un seul est votre Père, celui qui est dans les cieux.
10 Wala msije kuitwa 'walimu,' kwa kuwa mnaye Mwalimu mmoja tu, yaani Kristo.
Ne vous faites pas appeler maîtres, car un seul est votre maître, le Christ.
11 Bali aliye mkubwa miongoni mwenu atakuwa mtumishi wenu.
Mais celui qui est le plus grand parmi vous sera votre serviteur.
12 Yeyote ajiinuae atashushwa. Na yeyote anaye jishusha atainuliwa.
Quiconque s'élèvera sera abaissé, et quiconque s'abaissera sera élevé.
13 Lakini ole wenu waandishi na Mafarisayo, wanafiki! Mnawafungia watu ufalme wa mbinguni. Nanyi hamwezi kuuingia, na hamwaruhusu wanaoingia kufanya hivyo.
« Malheur à vous, scribes et pharisiens, hypocrites! Car vous dévorez les maisons des veuves, et, pour faire semblant, vous faites de longues prières. C'est pourquoi vous recevrez une plus grande condamnation.
14 (Zingatia: Msitari wa 14 hauonekani katika nakala bora za kale. Baadhi ya nakala huongeza msitari huu baada ya msitari wa 12. Msitari wa 14 “Ole wenu wandishi na Mafarisayo wanafiki! Kwa kuwa mnawameza wajane”).
« Mais malheur à vous, scribes et pharisiens, hypocrites! Car vous fermez le Royaume des cieux aux hommes; vous n'entrez pas vous-mêmes, et vous ne permettez pas à ceux qui entrent d'entrer.
15 Ole wenu Waandishi na Mafarisayo, wanafiki! Mnavuka ngambo ya bahari na kufika kumfanya mtu mmoja aamini yale mnayoyafundisha, na anapokuwa kama ninyi, mnamfanya mara mbili mwana wa jehanamu kama ninyi wenyewe mlivyo. (Geenna g1067)
Malheur à vous, scribes et pharisiens hypocrites! Car vous parcourez la mer et la terre pour faire un seul prosélyte; et quand il le devient, vous en faites un fils de la géhenne deux fois plus que vous. (Geenna g1067)
16 Ole wenu viongozi vipofu, ninyi msemao, Yeyote aapaye kwa hekalu, si kitu. Lakini anayeapa kwa dhahabu ya hekalu, amefungwa na kiapo chake.
« Malheur à vous, guides aveugles, qui dites: 'Celui qui jure par le temple n'est rien; mais celui qui jure par l'or du temple s'oblige'.
17 Enyi vipofu wapumbavu, kipi ni kikubwa kuliko kingine, dhahabu au hekalu ambalo limeweka wakfu dhahabu kwa Mungu?
Insensés aveugles! Car lequel est le plus grand, l'or ou le temple qui sanctifie l'or?
18 Na, yeyote aapaye kwa madhabahu, si kitu. Bali anayeapa kwa sadaka iliyo juu yake, amefungwa na kiapo chake.
Et: « Si quelqu'un jure par l'autel, il n'est rien; mais si quelqu'un jure par le don qui est sur l'autel, il est obligé ».
19 Enyi watu vipofu, kipi ni kikubwa kuliko kingine, sadaka au madhabahu ambayo huweka wakfu sadaka zinazotolewa kwa Mungu?
Bande d'aveugles! Car lequel est le plus grand, le don ou l'autel qui sanctifie le don?
20 Kwa hiyo, yeye aapaye kwa madhabahu huapa kwa hiyo na kwa vitu vyote vilivyo juu yake.
Celui donc qui jure par l'autel, jure par lui et par tout ce qui est dessus.
21 Naye aapaye kwa hekalu, huapa kwa hilo na kwa yeye akaaye ndani yake.
Celui qui jure par le temple, jure par lui et par celui qui l'a habité.
22 Na yeye aapaye kwa mbingu, huapa kwa kiti cha enzi cha Mungu na kwa yeye aketie juu yake.
Celui qui jure par le ciel, jure par le trône de Dieu et par celui qui y est assis.
23 Ole wenu, waandishi na Mafarisayo, wanafiki! Kwa kuwa mnalipa zaka kwa bizali, mnaanaa na mchicha, lakini mnaacha mambo mazito ya sheria- haki, rehema, na imani. Lakini haya mnapaswa kuwa mmeyafanya, na siyo kuacha mengine bila kuyatekeleza.
« Malheur à vous, scribes et pharisiens, hypocrites! Car vous payez la dîme de la menthe, de l'aneth et du cumin, et vous avez négligé les choses les plus graves de la loi: la justice, la miséricorde et la foi. Or, vous auriez dû faire ces choses-là, et ne pas laisser les autres en suspens.
24 Enyi viongozi vipofu, ninyi ambao mnachuja mdudu mdogo lakini mnameza ngamia!
Guides aveugles, vous poussez le moucheron et vous avalez le chameau!
25 Ole wenu, waandishi na Mafarisayo, wanafiki! Kwa kuwa mnasafisha nje ya vikombe na nje ya sahani, lakini ndani pamejaa dhuluma na kutokuwa na kiasi.
« Malheur à vous, scribes et pharisiens, hypocrites! Car vous nettoyez le dehors de la coupe et du plat, mais au dedans ils sont pleins de rapines et d'iniquités.
26 Enyi Mafarisayo vipofu, safisheni kwanza ndani ya kikombe na ndani ya sahani, ili upande wa nje nao pia uwe safi.
Pharisien aveugle, nettoie d'abord le dedans de la coupe et du plat, afin que le dehors devienne pur lui aussi.
27 Ole wenu, waandishi na Mafarisayo, wanafiki! Kwa kuwa mnafanana na makaburi yaliyopakwa chokaa, ambayo kwa nje huonekana mazuri, lakini kwa ndani yamejaa mifupa ya wafu na kila kitu kilicho kichafu.
« Malheur à vous, scribes et pharisiens, hypocrites! Car vous êtes semblables à des tombeaux blanchis, qui paraissent beaux au dehors, mais qui, au dedans, sont pleins d'ossements de morts et de toute espèce d'impuretés.
28 Vivyo hivyo, nanyi kwa nje mwaonekana wenye haki mbele ya watu, lakini kwa ndani mmejaa unafiki na udhalimu.
De même, vous aussi, au dehors, vous paraissez justes aux yeux des hommes, mais, au dedans, vous êtes pleins d'hypocrisie et d'iniquité.
29 Ole wenu, waandishi na Mafarisayo, wanafiki! Kwa kuwa mwajenga makaburi ya manabii na kuyapamba makaburi ya wenye haki.
« Malheur à vous, scribes et pharisiens, hypocrites! Car vous bâtissez les tombeaux des prophètes et vous décorez les tombeaux des justes,
30 Ninyi mwasema, kama tungeishi siku za baba zetu, tusingekuwa tumeshiriki pamoja nao kumwaga damu za manabii.
et vous dites: « Si nous avions vécu du temps de nos pères, nous n'aurions pas participé avec eux au sang des prophètes ».
31 Kwa hiyo mwajishuhudia wenyewe kwamba ninyi ni watoto wa hao waliowaua manabii.
Vous vous rendez donc témoignage à vous-mêmes que vous êtes les enfants de ceux qui ont tué les prophètes.
32 Pia ninyi mnakamilisha kujaza sehemu inayostahili dhambi ya baba zenu.
Remplissez donc la mesure de vos pères.
33 Enyi nyoka, wana wa vipiribao, kwa namna gani mtaikwepa hukumu ya jehanamu? (Geenna g1067)
Serpents, rejetons de vipères, comment échapperez-vous au jugement de la géhenne? (Geenna g1067)
34 Kwahiyo, tazama, nawatuma kwenu manabii, watu wenye hekima, na waandishi. Baadhi yao mtawaua na kuwasulibisha. Na baadhi yao mtawachapa ndani ya masinagogi yenu na kuwafukuza kutoka mji mmoja hadi mwingine.
C'est pourquoi voici que je vous envoie des prophètes, des sages et des scribes. Vous tuerez et crucifierez les uns, vous flagellerez les autres dans vos synagogues et vous les persécuterez de ville en ville,
35 Matokeo ni kwamba juu yenu patatokea damu zote za wenye haki zilizomwagwa duniani, kuanzia damu ya Habili mwenye haki hadi kwa damu ya Zakaria mwana wa Barakia, mliye muua kati ya patakatifu na madhabahu.
afin que retombe sur vous tout le sang innocent versé sur la terre, depuis le sang d'Abel le juste jusqu'au sang de Zacharie, fils de Barachie, que vous avez tué entre le sanctuaire et l'autel.
36 Kweli, nawaambieni, mambo haya yote yatakipata kizazi hiki.
En vérité, je vous le dis, toutes ces choses arriveront à cette génération.
37 Yerusalemu, Yerusalemu, wewe unayewaua manabii na kuwapiga mawe wale ambao wanatumwa kwako! mara ngapi nimewakusanya watoto wako pamoja kama vile kuku awakusanyavyo vifaranga wake chini ya mbawa zake, lakini haukukubali!
« Jérusalem, Jérusalem, qui tue les prophètes et lapide ceux qui lui sont envoyés! Combien de fois ai-je voulu rassembler tes enfants, comme une poule rassemble ses poussins sous ses ailes, et tu n'as pas voulu!
38 Tazama, nyumba yako imebaki ukiwa.
Voici, ta maison te sera laissée déserte.
39 Nami nakuambia, Kuanzia sasa na kuendelea hautaniona, hadi utakaposema, 'Amebarikiwa yeye ajaye kwa jina la Bwana.”'
Car, je vous le dis, vous ne me verrez plus désormais, jusqu'à ce que vous disiez: « Béni soit celui qui vient au nom du Seigneur! »".

< Mathayo 23 >