< Mathayo 18 >

1 Muda huo huo wanafunzi wakaja kwa Yesu na kumwambia, “Ni nani aliye mkubwa katika ufalme wa mbinguni?”
En cette heure-là, les disciples s'approchèrent de Jésus et dirent: « Qui donc est le plus grand dans le Royaume des cieux? »
2 Yesu akamwita mtoto mdogo, akamweka katikati yao,
Jésus appela à lui un petit enfant, le plaça au milieu d'eux
3 na kusema, “Kweli nawaambieni, msipotubu na kuwa kama watoto wadogo hamtaweza kuingia katika ufalme wa Mungu.
et dit: Je vous le dis en vérité, si vous ne vous convertissez et ne devenez comme des petits enfants, vous n'entrerez pas dans le royaume des cieux.
4 Hivyo yeyote ajishushaye kama mtoto mdogo, mtu kama huyo ni mkuu katika ufalme wa mbinguni.
Celui donc qui s'abaisse comme ce petit enfant est le plus grand dans le Royaume des cieux.
5 Na yeyote ampokeaye mtoto mdogo kwa jina langu anipokea mimi.
Quiconque reçoit en mon nom un tel petit enfant me reçoit moi-même,
6 Lakini yeyote asababishaye mmoja kati ya wadogo hawa wanaoniamini kuasi, itakuwa vizuri kwa mtu huyo jiwe kuu la kusagia likafungwa shingoni mwake, na kuzamishwa kilindini mwa bahari.
mais quiconque fait trébucher l'un de ces petits qui croient en moi, il vaudrait mieux pour lui qu'on lui suspende au cou une énorme meule de moulin et qu'on le fasse sombrer dans les profondeurs de la mer.
7 Ole kwa dunia kwa sababu ya wakati wa kukwazwa! kwa kuwa haina budi kwa nyakati hizo kuja, lakini ole kwake kwa mtu yule nyakati hizo zitakuja kwa ajili yake!
« Malheur au monde, à cause des occasions de chute! Car il faut bien que les occasions arrivent, mais malheur à celui par qui l'occasion arrive!
8 kama mkono wako au mguu wako ukikusababishia kukwazika, ukate na uutupe mbali na wewe. Ni vizuri zaidi kwako wewe kuingia kwenye uzima ukiwa bila mkono au kilema, kuliko kutupwa kwenye moto wa milele ukiwa na mikono yote au miguu yote. (aiōnios g166)
Si ta main ou ton pied te font trébucher, coupe-les et jette-les loin de toi. Mieux vaut pour toi entrer dans la vie mutilé ou estropié, plutôt que d'avoir deux mains ou deux pieds pour être jeté dans le feu éternel. (aiōnios g166)
9 Kama jicho lako likikukwaza, uling`oe na ulitupe mbali na wewe. Ni vizuri zaidi kwako wewe uingie kwenye uzima na jicho moja, kuliko kutupwa kwenye moto wa milele ukiwa na macho yote. (Geenna g1067)
Si ton œil te fait trébucher, arrache-le et jette-le loin de toi. Il vaut mieux pour toi entrer dans la vie avec un seul œil, plutôt que d'avoir deux yeux pour être jeté dans la géhenne de feu. (Geenna g1067)
10 Tazameni kwamba msije mkamdharau mmoja wa wadogo hawa. Kwa maana nawambieni kuwa mbinguni kuna malaika wao siku zote wakiutazama uso wa Baba yangu aliye mbinguni.
Veillez à ne pas mépriser l'un de ces petits, car je vous dis que dans les cieux, leurs anges voient toujours le visage de mon Père qui est dans les cieux.
11 (Zingatia: Maneno yanayoonekana kama ya msitari wa 11, “Kwa kuwa Mwana wa Adamu alikuja kuokoa kile kilichokuwa kimepotea” hayakuonekana katika nakala bora za kale).
Car le Fils de l'homme est venu pour sauver ce qui était perdu.
12 Mnafikiri nini? Ikiwa mtu ana kondoo mia moja, na mmoja wao akapotea, je hatawaacha tisini na tisa ya mlimani na kwenda kumtafuta mmoja aliyepotea?
« Que pensez-vous? Si un homme a cent brebis et que l'une d'elles s'égare, ne laisse-t-il pas les quatre-vingt-dix-neuf autres, ne va-t-il pas dans la montagne et ne cherche-t-il pas celle qui s'est égarée?
13 Na akiisha kumpata, kweli nawaambieni, anamfurahia kuliko wale tisini na tisa wasiopotea.
S'il la trouve, je vous le dis en vérité, il s'en réjouit plus que des quatre-vingt-dix-neuf qui ne se sont pas égarées.
14 Vivyo hivyo, siyo mapenzi ya Baba yenu wa mbinguni kuwa mmoja wa wadogo hawa aangamie.
De même, ce n'est pas la volonté de votre Père qui est dans les cieux qu'un seul de ces petits périsse.
15 Kama ndugu yako akikukosea, nenda, kamwonyeshe dosari iliyopo kati yako na yeye akiwa pekee yake. Kama akikusikiliza, utakuwa umemrejesha ndugu yako.
« Si ton frère pèche contre toi, va lui montrer sa faute, entre toi et lui seul. S'il t'écoute, tu as regagné ton frère.
16 Lakini kama hatakusikiliza, mchukue ndugu mmoja au wawili zaidi pamoja nawe, kwa kuwa kwa vinywa vya mashahidi wawili au watatu kila neno linaweza kuthibitishwa.
Mais s'il n'écoute pas, prends-en un ou deux autres avec toi, afin que toute parole soit établie par la bouche de deux ou trois témoins.
17 Na kama akipuuza kuwasikiliza, liambie kanisa jambo hilo, kama akipuuza vilevile kulisikiliza kanisa, basi na awe kama mtu wa mataifa na mtoza ushuru.
S'il refuse de les écouter, dis-le à l'assemblée. S'il refuse aussi d'écouter l'assemblée, qu'il soit pour vous comme un païen ou un publicain.
18 Kweli nawaambieni, chochote kile mtakachokifunga duniani na mbinguni kitafungwa. na chochote mtakachokifungua duniani na mbinguni kitafunguliwa.
En vérité, je vous le dis, tout ce que vous lierez sur la terre sera lié dans le ciel, et tout ce que vous délierez sur la terre sera délié dans le ciel.
19 Tena nawaambieni kwamba kama watu wawili kati yenu wakikubaliana juu ya jambo lolote duniani waliombalo, hilo Baba yangu wa mbinguni atalifanya.
Je vous le dis encore en vérité, si deux d'entre vous s'accordent sur la terre pour demander quoi que ce soit, cela leur sera accordé par mon Père qui est dans les cieux.
20 Kwa kuwa wawili au watatu wakikusanyika pamoja kwa jina langu, Mimi niko katikati yao.
Car là où deux ou trois sont réunis en mon nom, je suis au milieu d'eux. »
21 Tena Petro akaja na kumwambia Yesu, “Bwana, ni mara ngapi ndugu yangu akinikosea nami nimsamehe? Hata mara saba?”
Alors Pierre s'approcha et lui dit: « Seigneur, combien de fois mon frère péchera-t-il contre moi, et je lui pardonnerai? Jusqu'à sept fois? »
22 Yesu akamwambia, “Sikuambii mara saba, lakini hata sabini mara saba.
Jésus lui répondit: « Je ne te dis pas jusqu'à sept fois, mais jusqu'à soixante-dix fois sept fois.
23 Kwa sababu hiyo ufalme wa mbinguni ni sawa na mfalme fulani aliyetaka kusahihisha hesabu kutoka kwa watumwa wake.
C'est pourquoi le royaume des cieux est semblable à un roi qui voulait régler ses comptes avec ses serviteurs.
24 Alipoanza kusahihisha hesabu, mtumwa moja akaletwa kwake ambaye alikuwa anamdai talanta elfu kumi.
Comme il commençait à régler, on lui en amena un qui lui devait dix mille talents.
25 Kwa kuwa hakuwa na njia ya kulipa, bwana wake aliagiza auzwe, mke wake pamoja na watoto wake na kila kitu alichokuwa nacho, na malipo yafanyike.
Mais comme il ne pouvait pas payer, son maître ordonna qu'il soit vendu, avec sa femme, ses enfants et tout ce qu'il possédait, et que le paiement soit effectué.
26 Hivyo mtumwa alianguka, akapiga magoti mbele yake, akisema, 'Bwana, uwe na uvumilivu pamoja nami, na nitakulipa kila kitu.'
Le serviteur se jeta donc à terre et s'agenouilla devant lui, en disant: « Seigneur, prends patience avec moi, et je te rendrai tout.
27 Hivyo bwana wa yule mtumwa, kwa kuwa alisukumwa sana na huruma, alimwachilia na kumsamehe deni hilo
Le maître de ce serviteur, ému de compassion, le relâcha et lui remit la dette.
28 Lakini mtumwa yule alitoka na kumpata mmoja kati ya watumwa wenzake, aliyekuwa anamdai denari mia. Alimvuta, akamkaba kooni, na kumwambia, 'Nilipe kile ninachokudai.'
« Mais ce serviteur sortit et trouva un de ses compagnons de service qui lui devait cent deniers, il le saisit et le prit à la gorge en disant: « Paie-moi ce que tu dois! ».
29 Lakini yule mtumwa mwenzake alianguka na kumsihi sana, akisema, 'Uwe na uvumilivu nami, na nitakulipa.'
Son compagnon de service se jeta à ses pieds et le supplia en disant: « Prends patience avec moi, et je te rendrai la pareille.
30 Lakini mtumwa yule wa kwanza alikataa. Badala yake, alienda na kumtupa gerezani, mpaka atakapo mlipa kile anachomdai.
Il ne voulut pas, mais il alla le jeter en prison jusqu'à ce qu'il eût remboursé ce qui lui était dû.
31 Na walipoona watumwa wenzake kile kilichotokea. Walisikitishwa sana. Walikuja na kumwambia bwana wao kila kitu kilichotokea.
Lorsque ses compagnons de service virent ce qui s'était passé, ils furent profondément désolés et vinrent raconter à leur maître tout ce qui s'était passé.
32 Ndipo yule bwana wa mtumwa yule alimwita, na kumwambia, 'Ewe mtumwa mwovu, nilikusamehe wewe deni langu lote kwa sababu ulinisihi sana.
Son maître le fit venir et lui dit: « Méchant serviteur! Je t'ai remis toute cette dette parce que tu m'as supplié.
33 Je! Haukutakiwa kuwa na huruma kwa mtumwa mwenzio, kama mimi nilivyokuhurumia wewe?
Ne devais-tu pas avoir pitié de ton compagnon de service, comme j'ai eu pitié de toi?
34 Bwana wake alikasirika na kumkabidhi kwa wale watesaji mpaka atakapolipa kiasi chote alichokuwa anadaiwa.
Son maître se mit en colère et le livra aux bourreaux jusqu'à ce qu'il paie tout ce qui lui était dû.
35 Hivyo ndivyo Baba yangu wa Mbinguni atakavyowafanyia, kama kila mmoja wenu hatamsamehe ndugu yake kutoka moyoni mwenu.”
C'est ainsi que mon Père céleste vous traitera aussi, si vous ne pardonnez pas chacun de votre cœur à votre frère pour ses méfaits. »

< Mathayo 18 >