< Mathayo 17 >

1 Siku sita baadaye Yesu aliwachukua pamoja naye Petro, na Yakobo, na Yohana nduguye, na akawachukua mpaka juu ya mlima mrefu wao wenyewe.
Et après six jours, Jésus prend avec lui Pierre, et Jacques, et Jean son frère, et les mène à l’écart sur une haute montagne.
2 Alibadilishwa mbele yao. Uso wake ukang'aa kama jua, na nguo zake zilionekana zenye kung'aa kama nuru.
Et il fut transfiguré devant eux; et son visage resplendit comme le soleil, et ses vêtements devinrent blancs comme la lumière.
3 Tazama, pale walitokea Musa na Eliya wakiongea naye.
Et voici, Moïse et Élie leur apparurent, parlant avec lui.
4 Petro akajibu na kumwambia Yesu, “Bwana, ni vema kwetu sisi kuwepo mahali hapa. Kama ukitamani, nitajenga hapa vibanda vitatu - kimoja chako, na kimoja kwa ajili ya Musa, na kimoja kwa ajili ya Eliya.”
Et Pierre, répondant, dit à Jésus: Seigneur, il est bon que nous soyons ici; si tu le veux, faisons ici trois tentes: une pour toi, et une pour Moïse, et une pour Élie.
5 Wakati anaongea, tazama wingu jeupe likawatia kivuli, na tazama, ikatokea sauti toka kwenye wingu, ikisema, “Huyu ni Mwanangu mpendwa ninayependezwa naye. Msikilizeni yeye.”
Comme il parlait encore, voici, une nuée lumineuse les couvrit; et voici une voix de la nuée, disant: Celui-ci est mon fils bien-aimé, en qui j’ai trouvé mon plaisir; écoutez-le.
6 Wanafunzi waliposikia hayo, wakaanguka kifudifudi na wakaogopa sana.
Ce que les disciples ayant entendu, ils tombèrent le visage contre terre et furent saisis d’une très grande peur.
7 Kisha Yesu akaja akawagusa na kusema, “Inukeni wala msiogope.”
Et Jésus, s’approchant, les toucha et dit: Levez-vous, et n’ayez point de peur.
8 Nao wakainua nyuso zao juu lakini hawakumwona mtu isipokuwa Yesu pekee.
Et eux, levant leurs yeux, ne virent personne que Jésus seul.
9 Na walipokuwa wakishuka mlimani, Yesu akawaagiza, akasema, “Msitoe habari ya maono hayo mpaka Mwana wa Adamu atakapofufuka kutoka katika wafu.”
Et comme ils descendaient de la montagne, Jésus leur enjoignit, disant: Ne dites à personne la vision, jusqu’à ce que le fils de l’homme soit ressuscité d’entre les morts.
10 Wanafunzi wake wakamwuliza, wakisema, “Ni kwanini waandishi wanasema kuwa Eliya atakuja kwanza?
Et ses disciples l’interrogèrent, disant: Pourquoi donc les scribes disent-ils qu’il faut qu’Élie vienne premièrement?
11 Yesu akawajibu na kusema, “Eliya atakuja kweli na atarudisha mambo yote.
Et lui, répondant, leur dit: En effet, Élie vient premièrement, et il rétablira toutes choses;
12 Lakini naawaambieni ninyi, Eliya amekwisha kuja, lakini hawakumtambua. Badala yake, walimfanyia mambo watakayo wao. Na hivyo ndivyo Mwana wa Adamu atakavyoteswa katika mikono yao.”
mais je vous dis qu’Élie est déjà venu, et ils ne l’ont pas reconnu; mais ils lui ont fait tout ce qu’ils ont voulu; ainsi aussi le fils de l’homme va souffrir de leur part.
13 Ndipo wanafunzi wakatambua kuwa alikuwa akiongea habari za Yohana Mbatizaji.
Alors les disciples comprirent qu’il leur parlait de Jean le baptiseur.
14 Walipofika katika umati wa watu, mtu mmoja alimwendea, akapiga magoti mbele zake, na kumwambia,
Et quand ils furent venus auprès de la foule, un homme s’approcha de lui, se jetant à genoux devant lui,
15 “Bwana, umhurumie mwanangu, maana amekuwa na kifafa na kuteseka sana. Kwa kuwa mara nyingi huanguka motoni au kwenye maji.
et disant: Seigneur, aie pitié de mon fils, car il est lunatique et souffre cruellement, car souvent il tombe dans le feu, et souvent dans l’eau;
16 Nilimleta kwa wanafunzi wako, lakini hawakuweza kumponya.
et je l’ai apporté à tes disciples, et ils n’ont pu le guérir.
17 Yesu akajibu akisema, “Enyi Kizazi kisichoamini na kilichoharibika, nitakaa pamoja nanyi mpaka lini? Nitavumiliana nanyi hata lini? Mlete hapa kwangu.”
Et Jésus, répondant, dit: Ô génération incrédule et perverse, jusques à quand serai-je avec vous; jusques à quand vous supporterai-je? Amenez-le-moi ici.
18 Yesu alimkemea, na pepo akamtoka. Kijana aliponywa tangu saa ile.
Et Jésus le tança; et le démon sortit de lui; et le jeune garçon fut guéri dès cette heure-là.
19 Kisha wanafunzi wakamjia Yesu kwa siri na kumwuliza, “Kwanini hatukuweza kumfukuza?”
Alors les disciples, venant à Jésus à l’écart, dirent: Pourquoi n’avons-nous pu le chasser?
20 Yesu akawaambia, “Kwa sababu ya imani yenu ndogo. Kweli nawaambieni, kama mtakuwa na imani hata ndogo kama punje ya mbegu ya haradali, mtaweza kuuambia mlima huu, hama kutoka hapa uende kule, nao utahama na hakutakuwa na kitu chochote cha kushindikana kwenu.
Et Jésus leur dit: À cause de votre incrédulité; car, en vérité, je vous dis: si vous aviez de la foi comme un grain de moutarde, vous diriez à cette montagne: Transporte-toi d’ici là, et elle se transporterait; et rien ne vous serait impossible.
21 (Zingatia: Maneno ya msitari wa 21 “Lakini, aina hii ya pepo haiwezekani kutoka, ila kwa maombi na Kufunga” hayaonekani katika nakala bora za kale).
Mais cette sorte ne sort que par la prière et par le jeûne.
22 Wakati wakiwa bado Galilaya, Yesu akawaambia Wanafunzi wake, “Mwana wa Adamu atatiwa mikononi mwa watu.
Et comme ils séjournaient en Galilée, Jésus leur dit: Le fils de l’homme va être livré entre les mains des hommes;
23 Na watamwua, na siku ya tatu atafufuka.” Wanafunzi walihuzunika sana.
et ils le feront mourir; et le troisième jour il sera ressuscité. Et ils furent fort attristés.
24 Nao walipofika Kapenaumu, watu wakusanyao kodi ya nusu shekeli wakamwendea Petro na kusema, “Je mwalimu wenu hulipa kodi ya nusu shekeli?”
Et lorsqu’ils furent venus à Capernaüm, les receveurs des didrachmes vinrent à Pierre, et dirent: Votre maître ne paie-t-il pas les didrachmes?
25 Akasema, “Ndiyo” Lakini Petro alipoingia ndani ya nyumba, Yesu akaongea na Petro kwanza na kusema, “Unafikiria nini Simon? Wafalme wa dunia, hupokea kodi au ushuru kutoka nani? Kwa wale wanaowatawa kutoka kwa wageni?
Il dit: Oui. Et quand il fut entré dans la maison, Jésus le prévint, disant: Que t’en semble, Simon? Les rois de la terre, de qui reçoivent-ils des tributs ou des impôts, de leurs fils ou des étrangers?
26 Na wakati Petro aliposema, “Kutoka kwa wageni” Yesu akamwambia, hivyo watawaliwa wameondolewa katika ulipaji.
Pierre lui dit: Des étrangers. Jésus lui dit: Les fils en sont donc exempts.
27 Lakini tusije tukawafanya watoza ushuru wakatenda dhambi, nenda baharini, tupa ndoano, na umtwae yule samaki ajaye kwanza. Baada ya kuufungua mdomo wake, utakuta mle shekeli moja. Ichukue na uwape watoza ushuru kwa ajili yangu na wewe.
Mais, afin que nous ne les scandalisions pas, va-t’en à la mer, jette un hameçon, et prends le premier poisson qui montera; et quand tu lui auras ouvert la bouche, tu y trouveras un statère; prends-le, et donne-le-leur pour moi et pour toi.

< Mathayo 17 >