< Mathayo 13 >

1 Katika siku hiyo Yesu aliondoka nyumbani na kukaa kando ya bahari.
On that day Jesus went out of the house and sat beside the sea.
2 Umati mkubwa ulikusanyika kwa kumzunguka, aliingia ndani ya mtumbwi na kukaa ndani yake. Umati wote walisimama kando ya bahari.
A very large crowd gathered around him, so he got into a boat and sat in it, while the whole crowd stood on the beach.
3 Kisha Yesu alisema maneno mengi kwa mifano, Alisema, “Tazama, mpanzi alienda kupanda.
Then Jesus said many things to them in parables. He said, “Behold, a farmer went out to sow seed.
4 Alipokuwa akipanda baadhi ya mbegu zilianguka kando ya njia na ndege walikuja wakazidonoa.
As he sowed, some seeds fell beside the road, and the birds came and devoured them.
5 Mbegu zingine zilianguka juu ya mwamba, ambapo hazikupata udongo wa kutosha. Ghafla zilichipuka kwa sababu udongo haukuwa na kina.
Other seeds fell on rocky ground, where they did not have much soil. Immediately they sprang up, because the soil had no depth.
6 Lakini jua lilipo chomoza zilichomwa kwa sababu hazikuwa na mizizi, na zilikauka.
But when the sun had risen, they were scorched because they had no root, and they withered away.
7 Mbengu zingine zilianguka kati ya miti yenye miiba. Miti yenye miiba ilirefuka juu ikaisonga.
Other seeds fell among the thorn plants. The thorn plants grew up and choked them.
8 Mbegu zingine zilianguka kwenye udongo mzuri na kuzaa mbegu, zingine mara mia moja zaidi, zingine sitini na zingine thelathini
Other seeds fell on good soil and produced a crop, some one hundred times as much, some sixty, and some thirty.
9 Aliye na masikio na asikie.
He who has ears, let him listen.”
10 Wanafunzi walikuja na kumwambia Yesu, “Kwa nini unazungumza na makutano kwa mifano?”
The disciples came and said to Jesus, “Why do you talk to the crowd in parables?”
11 Yesu alijibu kuwaambia, “Mmepewa upendeleo wa kufahamu siri za ufalme wa mbinguni, bali kwao hawajapewa.
Jesus answered and said to them, “You have been given the privilege of understanding mysteries of the kingdom of heaven, but to them it is not given.
12 Lakini yeyote aliyenacho, kwake yeye ataongezewa zaidi, na atapata faida kubwa. Ilasiye nacho hata kile alichonacho atanyang'anywa.
For whoever has will be given more, and he will have an abundance. But whoever does not have, even what he has will be taken away from him.
13 Hivyo naongea nao kwa mifano kwa sababu ingawa wanaona, wasione kweli. Na ingawa wanasikia wasisikie wala kufahamu.
This is why I talk to them in parables: Though they are seeing, they do not see; and though they are hearing, they do not hear, or understand.
14 Unabii wa Isaya umetimia kwao, ule usemao, “Msikiapo msikie, lakini kwa namna yoyote hamtaelewa; wakati mwonapo muweze kuona, lakini kwa namna yeyote ile msijue.
To them the prophecy of Isaiah is fulfilled, that which says, 'While hearing you will hear, but you will in no way understand; while seeing you will see, but you will in no way perceive.
15 Na mioyo ya watu hawa imekuwa giza, ni vigumu kusikia, na wamefumba macho yao, ili wasiweze kuona kwa macho yao, au kusikia kwa masikio yao, au kufahamu kwa mioyo yao, hivyo wangenigeukia tena, na ningewaponya.'
For this people's heart has become dull, and they are hard of hearing, and they have closed their eyes, so they should not see with their eyes, or hear with their ears, or understand with their hearts, so they would turn again, and I would heal them.'
16 Bali macho yenu yamebarikiwa, kwa kuwa yanaona, na masikio yenu kwa kuwa yanasikia.
But blessed are your eyes, for they see; and your ears, for they hear.
17 Hakika nawaambia manabii wengi na watu wenye haki walikuwa na hamu ya kuyaona mambo yale myaonayo, na hawakuweza kuyaona. Walitamani kusikia mambo yale mnayosikia, hawakuyasikia.
Truly I say to you that many prophets and righteous men desired to see the things that you see, and did not see them. They desired to hear the things that you hear, and did not hear them.
18 . Sasa sikilizeni mfano wa mpanzi.
Listen then to the parable of the farmer who sowed his seed.
19 Wakati yeyote asikiapo neno la ufalme na asilifahamu, ndipo mwovu huja na kukinyakua kilichokwisha kupandwa ndani ya moyo wake. Hii ni mbegu ile iliyopandwa kando ya njia.
When anyone hears the word of the kingdom but does not understand it, the evil one comes and snatches away what has been sown in his heart. This is the seed that was sown beside the road.
20 Yeye aliyepandwa katika miamba ni yule asikiaye neno na kulipokea haraka kwa furaha.
What was sown on rocky ground is the person who hears the word and immediately receives it with joy,
21 Bado hana mizizi ndani yake, ila huvumilia kwa kitambo kifupi. Wakati matatizo au mateso yanapotokea kwa sababu ya neno hujikwaa ghafla.
yet he has no root in himself and he endures for a while. When tribulation or persecution arises because of the word, he quickly falls away.
22 Aliyepandwa kati ya miti ya miiba, huyu ni yule alisikiaye neno lakini masumbuko ya ulimwengu na udaganyifu wa utajiri hulisonga lile neno lisije likazaa matunda. (aiōn g165)
What was sown among the thorn plants, this is the person who hears the word, but the cares of the world and the deceitfulness of riches choke the word, and he becomes unfruitful. (aiōn g165)
23 Aliyepandwa kwenye udongo mzuri, huyu ni yule asikiaye neno na kulifahamu. Huyu ni yule azaaye matunda na kuendelea kuzaa moja zaidi ya mara mia, nyingine sitini, nyingine thelathini.''
What was sown on the good soil, this is the person who hears the word and understands it. He bears fruit and makes a crop, some yielding one hundred times as much as was planted, some sixty, and some thirty times as much.”
24 Yesu aliwapa mfano mwingine. Akisema, “Ufalme wa mbinguni unafananishwa na mtu aliye panda mbengu nzuri katika shamba lake
Jesus presented another parable to them. He said, “The kingdom of heaven is like a man who sowed good seed in his field.
25 Lakini watu waliposinzia, adui wake akaja pia akapanda magugu katikati ya ngano kisha akaenda zake.
But while people slept, his enemy came and also sowed weeds among the wheat and then went away.
26 Baadaye ngano ilipoota na kutoa mazao yake, ndipo magugu yalitokea pia.
When the blades sprouted and then produced their crop, then the weeds appeared also.
27 Na watumishi wa mwenye shamba walikuja wakamwambia, 'Bwana, hukupanda mbengu nzuri katika shamba lako? Imekuwaje sasa lina magugu?
The servants of the landowner came and said to him, 'Sir, did you not sow good seed in your field? How does it now have weeds?'
28 Akawaambia, Adui ametenda hili.' Watumishi walimwambia, “Kwa hiyo unataka twende tukayang'oe?”
He said to them, 'An enemy has done this.' The servants said to him, 'So do you want us to go and pull them out?'
29 Mwenye shamba akisema, 'Hapana, wakati mnayang'oa magugu mtang'oa pamoja na ngano.
The landowner said, 'No. Because while you are pulling out the weeds, you might uproot the wheat with them.
30 Yaacheni yakue pamoja mpaka wakati wa mavuno. Wakati wa mavuno nitasema kwa wavunaji, 'Kwanza yang'oeri magugu na yafungeni matita matita na kuyachoma, lakini kusanyeni ngano katika ghala langu.''''
Let both grow together until the harvest. At the time of the harvest I will say to the reapers, “First pull out the weeds and tie them in bundles to burn them, but gather the wheat into my barn.”'”
31 Kisha Yesu aliwatolea mfano mwingine. Akasema, “Ufalme wa mbinguni unafanana na mbegu ya haradali ambayo mtu aliichukua na kuipanda katika shamba lake.
Then Jesus presented another parable to them. He said, “The kingdom of heaven is like a mustard seed which a man took and sowed in his field.
32 Mbegu hii kwa hakika ni ndogo kuliko mbegu zingine zote. Lakini imeapo huwa kubwa kuliko mimea yote ya bustani, huwa mti, kiasi kwamba ndege wa angani huja na kujenga viota katika matawi yake.”
This seed is indeed the smallest of all seeds. But when it has grown, it is greater than the garden plants. It becomes a tree, so that the birds of the air come and nest in its branches.”
33 Akawaambia mfano mwingine tena.”Ufalme wa mbinguni ni kama chachu ile iliyo twaliwa na mwanamke na kuichanganya kwa vipimo vitatu kwa unga mpaka viumuke.
Jesus then told them another parable. “The kingdom of heaven is like yeast that a woman took and mixed with three measures of flour until all the dough had risen.”
34 Hayo yote Yesu aliyasema kwenye umati kwa mifano. Na pasipo mifano hakusema chochote kwao.
All these things Jesus said to the crowds in parables; and he said nothing to them without a parable.
35 Hii ilikuwa kwamba kile kilichokwisha semwa kupitia kwa nabii kiweze kutimia, pale aliposema, “Nitafumbua kinywa changu katika mifano. Nitasema mambo yale yaliyokuwa yamefichwa tangu misingi ya ulimwengu”.
This was in order that what had been said through the prophet might come true, when he said, “I will open my mouth in parables. I will say things that were hidden from the foundation of the world.”
36 Kisha Yesu aliwaacha makutano na kwenda nyumbani. Wanafunzi wake walimwendea na kusema, “Tufafanulie mfano wa magugu ya shambani.''
Then Jesus left the crowds and went into the house. His disciples came to him and said, “Explain to us the parable of the weeds of the field.”
37 Yesu alijibu na kusema, “Apandae mbegu nzuri ni Mwana wa Adamu.
Jesus answered and said, “He who sows the good seed is the Son of Man.
38 Shamba ni ulimwengu; na mbegu nzuri, hawa ni wana wa ufalme. Magugu ni wana wa yule mwovu, na adui aliye zipanda ni ibilisi.
The field is the world; and the good seed, these are the sons of the kingdom. The weeds are the sons of the evil one,
39 Na mavuno ni mwisho wa ulimwengu, na wavunaji ni malaika. (aiōn g165)
and the enemy who sowed them is the devil. The harvest is the end of the age, and the reapers are angels. (aiōn g165)
40 Kama vile magugu yanavyo kusanywa na kuchomwa moto, hivyo ndivyo itakavyo kuwa mwisho wa ulimwengu. (aiōn g165)
Therefore, as the weeds are gathered up and burned with fire, so will it be at the end of the age. (aiōn g165)
41 Mwana wa Adamu atatuma malaika wake, na kukusanya kutoka katika ufalme wake mambo yote yaliyosababisha dhambi na wale watendao maasi.
The Son of Man will send out his angels, and they will gather out of his kingdom all the things that cause sin and those who commit iniquity.
42 Watawatupa wote katika tanuru la moto, ambako kutakuwa na kilio na kusaga meno.
They will throw them into the furnace of fire, where there will be weeping and grinding of teeth.
43 Ndipo watu wenye haki watakapong'aa kama jua katika Ufalme wa Baba yao. Yeye aliye na masikio na sikie.
Then will the righteous people shine like the sun in the kingdom of their Father. He who has ears, let him listen.
44 Ufalme wa mbinguni ni kama hazina iliyofichwa shambani. Mtu akaiona na kuificha. Katika furaha yake akaenda kuuza vyote alivyokuwa navyo, na kulinunua shamba.
The kingdom of heaven is like a treasure hidden in a field. A man found it and hid it. In his joy he goes, sells everything he possesses, and buys that field.
45 Tena, ufalme wa mbinguni ni kama mtu anayefanya biashara atafutaye lulu yenye thamani.
Again, the kingdom of heaven is like a man who is a merchant looking for valuable pearls.
46 Wakati alipoiona ile yenye thamani, alienda akauza kila kitu alichokuwa nacho na akainunua.
When he found one pearl of very great value, he went and sold everything that he possessed and bought it.
47 Ufalme wa mbinguni ni kama nyavu iliyo ndani ya bahari, na kwamba hukusanya viumbe vya kila aina.
Again, the kingdom of heaven is like a net that was cast into the sea, and that gathered creatures of every kind.
48 Ulipojaa wavuvi waliuvuta ufukweni. Kisha wakakaa chini wakakusanya vitu vyema ndani ya vyombo, lakini visivyo na thamani vilitupwa mbali.
When it was filled, the fishermen drew it up on the beach. Then they sat down and gathered the good things into containers, but the worthless things they threw away.
49 Itakuwa namna hii katika mwisho wa dunia. Malaika watakuja na kuwatenga watu waovu kutoka miongoni mwa wenye haki. (aiōn g165)
It will be this way at the end of the age. The angels will come and separate the wicked from among the righteous. (aiōn g165)
50 Na kuwatupa ndani ya tanuru ya moto, ambako kutakuwa na maombolezo na kusaga meno.
They will throw them into the furnace of fire, where there will be weeping and grinding of teeth.
51 Mmefahamu mambo yote haya? Wanafunzi walimjibu, ''Ndiyo.''
Have you understood all these things?” The disciples said to him, “Yes.”
52 Kisha Yesu akawambia, ''Kila mwandishi ambaye amekuwa mwanafunzi wa ufalme anafanana na mwenye nyumba atoaye katika hazina yake vitu vipya na vya kale.''
Then Jesus said to them, “Therefore every scribe who has become a disciple to the kingdom of heaven is like a man who is the owner of a house, who draws out old and new things from his treasure.”
53 IkawaYesu alipomaliza mifano yote hiyo, akaondoka katika sehemu hiyo.
Then it came about that when Jesus had finished these parables, he departed from that place.
54 Kisha Yesu akafika katika mkoa wake na akawafundisha watu katika sinagogi. Matokeo yake ni kuwa walishangaa na kusema, “Ni wapi mtu huyu alipopata hekima hii na miujiza hii?
Then Jesus entered his own region and taught the people in their synagogue. The result was that they were astonished and said, “Where does this man get his wisdom and these miracles from?
55 Mtu huyu siyo mwana wa seremala? Mariamu siyo mamaye? Na ndugu zake siyo Yakobo, Yusuph, Simoni na Yuda?
Is not this man the carpenter's son? Is not his mother called Mary? Are not his brothers James, Joseph, Simon, and Judas?
56 Na dada zake tunao hapa petu? Basi mtu huyu ameyapata wapi haya yote?”.
Are not all his sisters with us? Where did he get all these things?”
57 Aliwachukiza. Lakini Yesu aliwambia, “Nabii hakosi kuwa na heshima isipokuwa kwao na katika nchi yao.
They were offended by him. But Jesus said to them, “A prophet is not without honor except in his own country and in his own family.”
58 Na hakuweza kufanya miujiza mingi kwa sababu hawakuwa na imani naye.
He did not do many miracles there because of their unbelief.

< Mathayo 13 >