< Marko 3 >

1 Na tena aliingia ndani ya sinagogi na mle palikuwa na mtu mwenye mkono uliopooza.
And again, he entered into the synagogue. And there was a man there who had a withered hand.
2 Baadhi ya watu walikuwa wakimfuatilia kwa ukaribu kuona kama atamponya siku ya Sabato ili kwamba wamshitaki.
And they observed him, to see if he would cure on the Sabbaths, so that they might accuse him.
3 Yesu alimwambia mtu mwenye mkono uliopooza, “Inuka na usimame katikati ya umati huu.”
And he said to the man who had the withered hand, “Stand up in the middle.”
4 Kisha akawaambia watu, “Je ni halali kutenda tendo jema siku ya Sabato au kutenda yasiyo haki; kuokoa maisha, au kuua?” Lakini walibaki kimya.
And he said to them: “Is it lawful to do good on the Sabbaths, or to do evil, to give health to a life, or to destroy?” But they remained silent.
5 Akawaangalia kwa hasira, akihuzunika kwa sababu ya ugumu wa mioyo yao, na akamwambia yule mtu, “Nyoosha mkono wako”. Akaunyoosha na Yesu akamponya mkono wake.
And looking around at them with anger, being very saddened over the blindness of their hearts, he said to the man, “Extend your hand.” And he extended it, and his hand was restored to him.
6 Mafarisayo wakaenda nje na mara wakafanya njama pamoja na Maherode dhidi yake ili kumuua.
Then the Pharisees, going out, immediately took counsel with the Herodians against him, as to how they might destroy him.
7 Kisha Yesu, pamoja na wanafunzi wake, walienda baharini, na umati mkubwa wa watu uliwafuata ukitokea Galilaya na Uyahudi
But Jesus withdrew with his disciples to the sea. And a great crowd followed him from Galilee and Judea,
8 na kutoka Yerusalemu na kutoka Idumaya na mbele ya Yorodani na jirani ya Tiro na Sidoni, umati mkubwa, uliposikia kila kitu alichokuwa anakifanya, walikuja kwake.
and from Jerusalem, and from Idumea and across the Jordan. And those around Tyre and Sidon, upon hearing what he was doing, came to him in a great multitude.
9 Na aliwaambia wanafunzi wake kuandaa mtubwi mdongo kwa ajili yake kwa sababu ya umati, ili kwamba wasije wakamsonga.
And he told his disciples that a small boat would be useful to him, because of the crowd, lest they press upon him.
10 Kwa kuwa aliponya wengi, ili kila mtu aliyekuwa na mateso alikuwa na shauku ya kumfikia ili amguse.
For he healed so many, that as many of them as had wounds would rush toward him in order to touch him.
11 Popote roho wachafu walipomwona, walianguka chini mbele yake na kulia, na walisema, “Wewe ni Mwana wa Mungu”.
And the unclean spirits, when they saw him, fell prostrate before him. And they cried out, saying,
12 Aliwaamuru kwa msisitizo wasifanye ajulikane.
“You are the Son of God.” And he strongly admonished them, lest they make him known.
13 Alienda juu ya mlima, na akawaita aliowataka, na wakaenda kwake.
And ascending onto a mountain, he called to himself those whom he willed, and they came to him.
14 Akawachagua kumi na wawili (aliowaita mitume), ili kwamba wawe pamoja naye na aweze kuwatuma kuhubiri,
And he acted so that the twelve would be with him, and so that he might send them out to preach.
15 na kuwa na mamlaka ya kutoa mapepo.
And he gave them authority to cure infirmities, and to cast out demons:
16 Na akawachagua kumi na wawili: Simoni, aliyempa jina la Petro,
and he imposed on Simon the name Peter;
17 Yakobo mwana wa Zebedayo, na Yohana ndugu yake Yakobo, aliyepewa jina la Bonagesi, hao ni, wana wa ngurumo,
and also he imposed on James of Zebedee, and John the brother of James, the name ‘Boanerges,’ that is, ‘Sons of Thunder;’
18 na Andrea, Filipo, Bartholomayo, Mathayo, Tomaso, Yakobo mwana wa Alfayo, Thadayo, Simoni Mkananayo,
and Andrew, and Philip, and Bartholomew, and Matthew, and Thomas, and James of Alphaeus, and Thaddeus, and Simon the Canaanite,
19 na Yuda Iskariote, ambaye atamsaliti.
and Judas Iscariot, who also betrayed him.
20 Kisha alienda nyumbani, na umati wa watu wakaja pamoja tena, hata wasiweze kula hata mkate.
And they went to a house, and the crowd gathered together again, so much so that they were not even able to eat bread.
21 Familia yake waliposikia habari hiyo, walienda kumkamata, kwani walisema, “Amerukwa na akili”.
And when his own had heard of it, they went out to take hold of him. For they said: “Because he has gone mad.”
22 Waandishi waliokuja kutoka Yerusalemu walisema, “Amepagawa na Beelzebuli,” na, “Kwa mtawala wa mapepo anatoa mapepo”.
And the scribes who had descended from Jerusalem said, “Because he has Beelzebub, and because by the prince of demons does he cast out demons.”
23 Yesu aliwaita kwake na kusema nao kwa mifano, “Jinsi gani Shetani aweza kumtoa Shetani?
And having called them together, he spoke to them in parables: “How can Satan cast out Satan?
24 Kama ufalme ukigawanyika wenyewe, ufalme huo hauwezi kusimama.
For if a kingdom is divided against itself, that kingdom is not able to stand.
25 Kama nyumba ikigawanyika yenyewe, nyumba hiyo haiwezi kusimama.
And if a house is divided against itself, that house is not able to stand.
26 Kama Shetani atainuka kinyume chake mwenyewe na kugawanyika, hawezi kusimama, na atakuwa amefika mwisho wake.
And if Satan has risen up against himself, he would be divided, and he would not be able to stand; instead he reaches the end.
27 Lakini hakuna hata mmoja awezaye kuingia ndani ya nyumba ya mtu mwenye nguvu na kuiba vitu vyake bila kumfunga mwenye nguvu kwanza, na kisha kukusanya kilichomo nyumbani.
No one is able to plunder the goods of a strong man, having entered into the house, unless he first binds the strong man, and then he shall plunder his house.
28 Kweli nawambieni, dhambi zote za wana wa watu zitasamehewa, pamoja na kufuru ambazo wanatamka,
Amen I say to you, that all sins will be forgiven the sons of men, and the blasphemies by which they will have blasphemed.
29 lakini yeyote atakaye mkufuru Roho Mtakatifu hatasamehewa kamwe, bali ana hatia ya dhambi ya milele”. (aiōn g165, aiōnios g166)
But he who will have blasphemed against the Holy Spirit shall not have forgiveness in eternity; instead he shall be guilty of an eternal offense.” (aiōn g165, aiōnios g166)
30 Yesu alilisema hili kwa sababu walikuwa wakisema, “Ana roho chafu”.
For they said: “He has an unclean spirit.”
31 Kisha mama yake na ndugu zake walikuja na kusimama nje. Wakamtuma mtu, kumwita.
And his mother and brothers arrived. And standing outside, they sent to him, calling him.
32 Na umati wa watu uliokuwa umekaa karibu naye wakamwambia, “mama yako na ndugu zako wako nje, na wanakutafuta wewe”.
And the crowd was sitting around him. And they said to him, “Behold, your mother and your brothers are outside, seeking you.”
33 Aliwajibu, “Ni nani mama yangu na ndugu zangu?”
And responding to them, he said, “Who is my mother and my brothers?”
34 Aliwaangalia waliokuwa wamekaa wamemzunguka, na akasema, “Tazama, hawa ni mama zangu na ndugu zangu!
And looking around at those who were sitting all around him, he said: “Behold, my mother and my brothers.
35 Yeyote afanyaye mapenzi ya Mungu, mtu huyo ni ndugu yangu, na dada yangu, na mama yangu”.
For whoever has done the will of God, the same is my brother, and my sister and mother.”

< Marko 3 >