< Marko 14 >

1 Ilikuwa siku mbili tu baada ya sikukuu ya Pasaka na ya Mikate Isiyotiwa Chachu. Makuhani wakuu na waandishi walikuwa wakitafuta namna ya kumkamata Yesu kwa hila na kumuua.
Or, deux jours après, c’était la Pâque et les Pains sans levain. Et les principaux sacrificateurs et les scribes cherchaient comment ils pourraient se saisir de lui par ruse, et le faire mourir;
2 Kwa kuwa walisema, “Sio wakati huu wa sikukuu, watu wasije wakafanya ghasia.”
car ils disaient: Non pas pendant la fête, de peur qu’il n’y ait du tumulte parmi le peuple.
3 Wakati Yesu alipokuwa Bethania nyumbani kwa Simoni mkoma, na alipokuwa akielekea mezani, mwanamke mmoja alikuja kwake akiwa na chupa ya marashi ya nardo safi yenye gharama kubwa sana, aliivunja chupa na kuimimina juu ya kichwa chake.
Et comme il était à Béthanie dans la maison de Simon le lépreux, et qu’il était à table, une femme vint, ayant un vase d’albâtre [plein] d’un parfum de nard pur et de grand prix; et, ayant brisé le vase, elle le répandit sur sa tête.
4 Lakini kulikuwa na baadhi yao waliokasirika. Waliambiana wao kwa wao wakisema, “Ni nini sababu ya upotevu huu?
Et quelques-uns étaient [là], qui s’indignaient en eux-mêmes et disaient: À quoi bon la perte de ce parfum?
5 Manukato haya yangeweza kuuzwa kwa zaidi ya dinari mia tatu, na wakapewa maskini.” Nao walimkemea.
Car ce parfum aurait pu être vendu plus de 300 deniers, et être donné aux pauvres; et ils la reprenaient vivement.
6 Lakini Yesu alisema, “Mwacheni peke yake. Kwa nini mnamsumbua? Amefanya jambo zuri kwangu.
Mais Jésus dit: Laissez-la; pourquoi lui donnez-vous du déplaisir? Elle a fait une bonne œuvre envers moi;
7 Siku zote maskini mnao, na wakati wowote mnapotamani mnaweza kufanya mazuri kwao, lakini hamtakuwa nami wakati wote.
car vous avez toujours les pauvres avec vous, et quand vous voudrez, vous pourrez leur faire du bien; mais moi, vous ne m’avez pas toujours.
8 Amefanya kile anachoweza: ameupaka mwili wangu mafuta kwa ajili ya maziko.
Ce qui était en son pouvoir, elle l’a fait; elle a anticipé [le moment] d’oindre mon corps pour ma sépulture.
9 Kweli nawaambia, kila mahali injili inapohubiriwa katika ulimwengu wote, kile alichofanya mwanamke huyu kitazungumzwa kwa ukumbusho wake.
Et en vérité, je vous dis: en quelque lieu que cet évangile soit prêché dans le monde entier, on parlera aussi de ce que cette femme a fait, en mémoire d’elle.
10 Kisha Yuda Iskariote, mmoja wa wale kumi na wawili, alikwenda kwa wakuu wa makuhani ili kwamba apate kumkabidhi kwao.
Et Judas Iscariote, l’un des douze, s’en alla vers les principaux sacrificateurs pour le leur livrer;
11 Wakati wakuu wa Makuhani waliposikia hivyo, walifurahi na wakaahidi kumpa fedha. Alianza kutafuta nafasi ya kumkabidhi kwao.
et ceux-ci, l’ayant entendu, s’en réjouirent et promirent de lui donner de l’argent; et il cherchait comment il le livrerait commodément.
12 Katika siku ya kwanza ya mkate usiotiwa chachu, wakati walipotoa mwanakondoo wa pasaka, wanafunzi wake walimwambia, “Unataka twende wapi tukaandae ili upate kula mlo wa Pasaka?”
Et le premier jour des pains sans levain, lorsqu’on sacrifiait la pâque, ses disciples lui disent: Où veux-tu que nous allions préparer [ce qu’il faut], afin que tu manges la pâque?
13 Aliwatuma wanafuzi wake wawili na kuwaambia, “Nendeni mjini, na mwanamume ambaye amebeba mtungi ataonana nanyi. Mfuateni.
Et il envoie deux de ses disciples et leur dit: Allez à la ville; et un homme portant une cruche d’eau viendra à votre rencontre; suivez-le.
14 Nyumba atakayoingia, mfuateni na mmwambie mwenye nyumba hiyo, 'Mwalimu asema, “Kiko wapi chumba cha wageni mahali nitakapokula Pasaka na wanafunzi wangu?”
Et où qu’il entre, dites au maître de la maison: Le maître dit: Où est mon logis où je mangerai la pâque avec mes disciples?
15 Atawaonesha chumba cha juu kikubwa chenye samani ambacho kiko tayari. Fanyeni maandalizi kwa ajili yetu pale.”
Et lui vous montrera une grande chambre garnie, toute prête; apprêtez-nous là [ce qu’il faut].
16 Wanafunzi waliondoka wakaenda mjini; walikuta kila kitu kama alivyokuwa amewaambia, na wakaandaa mlo wa Pasaka.
Et ses disciples s’en allèrent et entrèrent dans la ville, et trouvèrent [tout] comme il leur avait dit; et ils apprêtèrent la pâque.
17 Wakati ilipokuwa jioni, alikuja na wale Kumi na wawili.
Et le soir étant venu, il vient avec les douze.
18 Na walipokuwa wakiikaribia meza na kula, Yesu alisema, “Kweli nawaambia, mmoja kati yenu anayekula pamoja nami atanisaliti.”
Et comme ils étaient à table et qu’ils mangeaient, Jésus dit: En vérité, je vous dis que l’un d’entre vous qui mange avec moi, me livrera.
19 Wote walisikitika, na mmoja baada ya mwingine walimwambia, “Hakika siyo mimi?”
Et ils commencèrent à s’attrister et à lui dire l’un après l’autre: Est-ce moi? Et un autre: Est-ce moi?
20 Yesu alijibu na kuwaambia, “Ni mmoja wa Kumi na wawili kati yenu, mmoja ambaye sasa anachovya tonge katika bakuli pamoja nami.
Mais répondant, il leur dit: C’est l’un d’entre les douze qui trempe avec moi au plat.
21 Kwa kuwa Mwana wa Adamu atakwenda kama vile maandiko yasemavyo juu yake. Lakini ole wake mtu yule ambaye kupitia yeye Mwana wa Adamu atasalitiwa! Ingekuwa vizuri zaidi kwake kama mtu yule asingezaliwa.”
Le fils de l’homme s’en va, selon qu’il est écrit de lui; mais malheur à cet homme par qui le fils de l’homme est livré! Il aurait été bon pour cet homme-là qu’il ne soit pas né.
22 Na walipokuwa wakila, Yesu alichukua mkate, akaubariki, na kuumega. Aliwapa akisema, “Chukueni. Huu ni mwili wangu.”
Et comme ils mangeaient, Jésus, ayant pris un pain [et] ayant béni, le rompit et le leur donna, et dit: Prenez; ceci est mon corps.
23 Alichukua kikombe, akashukuru, na akawapatia, na wote wakakinywea.
Et ayant pris la coupe [et] ayant rendu grâces, il la leur donna; et ils en burent tous.
24 Aliwaambia, “Hii ni damu yangu ya agano, damu imwagikayo kwa ajili ya wengi.
Et il leur dit: Ceci est mon sang, le [sang] de la nouvelle alliance, qui est versé pour plusieurs.
25 Kweli nawaambia, sitakunywa tena katika zao hili la mzabibu mpaka siku ile nitakapokunywa mpya katika ufalme wa Mungu.”
En vérité, je vous dis que je ne boirai plus du fruit de la vigne, jusqu’à ce jour où je le boirai nouveau dans le royaume de Dieu.
26 Walipokwisha kuimba wimbo, walikwenda nje katika Mlima wa Mizeituni.
Et ayant chanté une hymne, ils sortirent [et s’en allèrent] à la montagne des Oliviers.
27 Yesu aliwaaambia, “Ninyi nyote mtajitenga mbali kwa sababu yangu, kwa kuwa imeandikwa, 'Nitampiga mchungaji na kondoo watatawanyika.'
Et Jésus leur dit: Vous serez tous scandalisés; car il est écrit: « Je frapperai le berger, et les brebis seront dispersées »;
28 Lakini baada ya kufufuka kwangu, nitawatangulia mbele yenu Galilaya.”
mais après que je serai ressuscité, j’irai devant vous en Galilée.
29 Petro alimwambia, “Hata kama wote watakuacha, mimi sitakuacha.”
Et Pierre lui dit: Si même tous étaient scandalisés, je ne le serai pourtant pas, moi.
30 Yesu alimwambia, “Kweli nakuambia, usiku huu, kabla jogoo hajawika mara mbili, utakuwa umenikana mara tatu.”
Et Jésus lui dit: En vérité, je te dis qu’aujourd’hui, cette nuit-ci, avant que le coq ait chanté deux fois, toi, tu me renieras trois fois.
31 Lakini Petro alisema, “Hata itanilazimu kufa pamoja nawe, sitakukana.” Wote walitoa ahadi ile ile.
Mais [Pierre] disait encore plus fortement: Quand il me faudrait mourir avec toi, je ne te renierai point. Et ils dirent tous aussi la même chose.
32 Walikuja kwenye eneo lililoitwa Gethsemane, na Yesu akawaambia wanafunzi wake, “Kaeni hapa wakati nasali.”
Et ils viennent en un lieu dont le nom était Gethsémané. Et il dit à ses disciples: Asseyez-vous ici, jusqu’à ce que j’aie prié.
33 Aliwachukua Petro, Yakobo, na Yohana pamoja naye, akaanza kuhuzunika na kutaabika sana.
Et il prend avec lui Pierre et Jacques et Jean; et il commença à être saisi d’effroi et fort angoissé.
34 Aliwaambia, “Nafsi yangu ina huzuni sana, hata kufa. Bakini hapa na mkeshe.”
Et il leur dit: Mon âme est saisie de tristesse jusqu’à la mort; demeurez ici et veillez.
35 Yesu alienda mbele kidogo, akaanguka chini, akaomba, kama ingewezekana, kwamba saa hii ingemwepuka.
Et s’en allant un peu plus avant, il se jeta contre terre, et il priait que, s’il était possible, l’heure passe loin de lui.
36 Alisema, “Aba, Baba, Mambo yote kwako yanawezekana. Niondolee kikombe hiki. Lakini siyo kwa mapenzi yangu, bali mapenzi yako.”
Et il disait: Abba, Père, toutes choses te sont possibles; fais passer cette coupe loin de moi; toutefois non pas ce que je veux, moi, mais ce que tu veux, toi!
37 Alirudi na kuwakuta wamelala, na akamwambia Petro, “Simoni, je umelala? Hukuweza kukesha hata saa moja?
Et il vient, et les trouve dormant; et il dit à Pierre: Simon, tu dors? Tu n’as pu veiller une heure?
38 Kesheni na muombe kwamba msije mkaingia katika majaribu. Hakika roho i radhi, lakini mwili ni dhaifu.”
Veillez et priez, afin que vous n’entriez pas en tentation; l’esprit est prompt, mais la chair est faible.
39 Alienda tena na kuomba, na alitumia maneno yaleyale.
Et il s’en alla de nouveau, et il pria, disant les mêmes paroles.
40 Alikuja tena akawakuta wamelala, kwa kuwa macho yao yalikuwa mazito na hawakujua nini cha kumwambia.
Et s’en étant retourné, il les trouva de nouveau dormant (car leurs yeux étaient appesantis); et ils ne savaient que lui répondre.
41 Alikuja mara ya tatu na kuwaambia, “Bado mmelala na kupumzika? Yatosha! Saa imefika. Tazama! Mwana wa Adamu atasalitiwa mikononi mwa wenye dhambi.
Et il vient pour la troisième fois et leur dit: Dormez dorénavant et reposez-vous; il suffit, l’heure est venue; voici, le fils de l’homme est livré entre les mains des pécheurs.
42 Amkeni, twendeni. Tazama, yule anayenisaliti yuko karibu.”
Levez-vous, allons; voici, celui qui me livre s’est approché.
43 Mara tu alipokuwa bado anaongea, Yuda, mmoja wa wale kumi na wawili, alifika, na kundi kubwa kutoka kwa wakuu wa makuhani, waandishi na wazee wenye mapanga na marungu.
Et aussitôt, comme il parlait encore, Judas, l’un des douze, se trouve là, et avec lui une grande foule avec des épées et des bâtons, de la part des principaux sacrificateurs et des scribes et des anciens.
44 Wakati huo msaliti wake alikuwa amewapa ishara, akisema, Yule nitakayembusu, ndiye. Mkamateni na kumpeleka chini ya ulinzi.”
Et celui qui le livrait leur avait donné un signe, disant: Celui que j’embrasserai, c’est lui; saisissez-le, et emmenez-le sûrement.
45 Wakati Yuda alipofika, moja kwa moja alienda kwa Yesu na kusema, “Mwalimu!” Na akambusu.
Et quand il fut venu, aussitôt s’approchant de lui, il dit: Rabbi, Rabbi! et il l’embrassa avec empressement.
46 Kisha wakumtia chini ya ulinzi na kumkamata.
Et ils mirent les mains sur lui et se saisirent de lui.
47 Lakini mmoja kati yao aliyesimama karibu naye alichomoa upanga wake akampiga mtumishi wa kuhani mkuu na kumkata sikio.
Et l’un de ceux qui étaient là présents, ayant tiré l’épée, frappa l’esclave du souverain sacrificateur, et lui emporta l’oreille.
48 Yesu aliwaambia, “Mmekuja kunikamata kwa mapanga na marungu kama mnyang'anyi?
Et Jésus, répondant, leur dit: Êtes-vous sortis comme après un brigand, avec des épées et des bâtons, pour me prendre?
49 Wakati kila siku nilikuwa nanyi na nikifundisha hekaluni, hamkunikamata. Lakini hili limefanyika ili maandiko yatimie.
J’étais tous les jours avec vous, enseignant dans le temple, et vous ne vous êtes pas saisis de moi; mais c’est afin que les écritures soient accomplies.
50 Na wale wote waliokuwa na Yesu walimwacha na kukimbia.
Et tous le laissèrent et s’enfuirent.
51 Kijana mmoja alimfuata, aliyekuwa amevaa shuka tu aliyokuwa amejifunika kumzunguka; walimkamata lakini
Et un certain jeune homme le suivit, enveloppé d’une toile de fin lin sur le corps nu; et ils le saisissent;
52 aliwaponyoka akaiacha shuka pale akakimbia uchi.
et, abandonnant la toile de fin lin, il leur échappa tout nu.
53 Walimwongoza Yesu kwa kuhani mkuu. Pale walikusanyika pamoja naye makuhani wakuu wote, wazee, na waandishi.
Et ils amenèrent Jésus au souverain sacrificateur; et tous les principaux sacrificateurs et les anciens et les scribes s’assemblent auprès de lui.
54 Petro naye alimfuata Yesu kwa mbali, kuelekea kwenye ua wa kuhani mkuu. Aliketi pamoja na walinzi, waliokuwa karibu na moto wakiota ili kupata joto.
Et Pierre le suivit de loin, jusque dans l’intérieur du palais du souverain sacrificateur, et il s’assit avec les huissiers, et se chauffait près du feu.
55 Wakati huo makuhani wakuu wote na Baraza lote walikuwa wakitafuta ushahidi dhidi ya Yesu ili wapate kumwua. Lakini hawakuupata.
Or les principaux sacrificateurs et tout le sanhédrin cherchaient [quelque] témoignage contre Jésus, pour le faire mourir; et ils n’en trouvaient point.
56 Kwa kuwa watu wengi walileta ushuhuda wa uongo dhidi yake, lakini hata ushahidi wao haukufanana.
Car plusieurs portaient de faux témoignages contre lui; et les témoignages ne s’accordaient pas.
57 Baadhi walisimama na kuleta ushahidi wa uongo dhidi yake; wakisema,
Et quelques-uns s’élevèrent et portèrent un faux témoignage contre lui, disant:
58 “Tulimsikia akisema, 'Nitaliharibu hekalu hili lililotengenezwa kwa mikono, na ndani siku tatu nitajenga lingine lisilotengenezwa kwa mikono.'”
Nous l’avons entendu disant: Moi, je détruirai ce temple qui est fait de main, et en trois jours j’en bâtirai un autre qui ne sera pas fait de main.
59 Lakini hata ushahidi wao haukufanana.
Et ainsi non plus leur témoignage ne s’accordait pas.
60 Kuhani mkuu alisimama katikati yao na akamwuliza Yesu, “Je, huna jibu? Watu hawa wanashuhudia nini dhidi yako?”
Et le souverain sacrificateur, se levant devant tous, interrogea Jésus, disant: Ne réponds-tu rien? De quoi ceux-ci témoignent-ils contre toi?
61 Lakini alikaa kimya na hakujibu chochote. Mara Kuhani mkuu alimwuliza tena, “Je wewe ni Kristo, mwana wa Mbarikiwa?”
Et il garda le silence, et ne répondit rien. Le souverain sacrificateur l’interrogea encore, et lui dit: Toi, tu es le Christ, le Fils du Béni?
62 Yesu alisema, “Mimi ndiye. Na utamwona Mwana wa Adamu ameketi mkono wa kulia wa nguvu akija na mawingu ya mbinguni.”
Et Jésus dit: Je le suis; et vous verrez le fils de l’homme assis à la droite de la puissance, et venant avec les nuées du ciel.
63 Kuhani mkuu alirarua mavazi yake na kusema, “Je, bado tunahitaji mashahidi?
Et le souverain sacrificateur, ayant déchiré ses vêtements, dit: Qu’avons-nous encore besoin de témoins?
64 Mmesikia kufuru. Uamuzi wenu ni upi?” Na wote walimhukumu kama mmoja aliyestahili kifo.
Vous avez entendu le blasphème: que vous en semble? Et tous le condamnèrent comme méritant la mort.
65 Baadhi wakaanza kumtemea mate na kumfunika uso na kumpiga na kumwambia, “Tabiri!” Maafisa walimchukua na kumpiga.
Et quelques-uns se mirent à cracher contre lui, et à lui couvrir le visage, et à lui donner des soufflets, et à lui dire: Prophétise. Et les huissiers le frappaient de leurs mains.
66 Na Petro alipokuwa bado yuko chini uani, mtumishi mmoja wa wasichana wa kuhani mkuu alikuja kwake.
Et comme Pierre était en bas, dans la cour, une des servantes du souverain sacrificateur vient,
67 Alimwona Petro alipokuwa amesimama akiota moto, na alimtazama kwa kumkaribia. Kisha alisema, “Nawe pia ulikuwa na Mnazareti, Yesu”.
et, apercevant Pierre qui se chauffait, elle le regarda et dit: Et toi, tu étais avec le Nazarénien Jésus.
68 Lakini alikataa, akisema, “Sijui wala sielewi kuhusu kile unachosema!” Kisha alitoka akaenda nje uani. (Zingatia; Mstari huu, “Na jogoo akawika” haumo kwenye nakala za kale).
Et il le nia, disant: Je ne sais ni n’entends ce que tu dis. Et il sortit dehors dans le vestibule; et le coq chanta.
69 Lakini mtumishi wa kike pale, alimwona na alianza kuwaambia tena wale ambao walikuwa wamesimama pale, “Mtu huyu ni mmoja wao!”
Et la servante, l’apercevant encore, se mit à dire à ceux qui étaient là: Celui-ci est de ces gens-là.
70 Lakini alikana tena. Baadaye kidogo wale waliokuwa wamesimama pale walikuwa wakimwambia Petro, “Hakika wewe ni mmoja wao, kwa maana wewe pia ni Mgalilaya.”
Et il le nia de nouveau. Et encore un peu après, ceux qui étaient là présents dirent à Pierre: Certainement tu es de ces gens-là; car aussi tu es Galiléen.
71 Lakini alianza kujiweka mwenyewe chini ya laana na kuapa, “Simjui mtu huyu mnayemsema.”
Et il se mit à faire des imprécations et à jurer: Je ne connais pas cet homme dont vous parlez.
72 Kisha jogoo aliwika mara ya pili. Kisha Petro alikumbuka maneno ambayo Yesu aliyokuwa amemwambia: “Kabla jogoo hajawika mara mbili, utanikana mara tatu.” Na alianguka chini na kulia.
Et le coq chanta pour la seconde fois. Et Pierre se ressouvint de la parole que Jésus lui avait dite: Avant que le coq chante deux fois, tu me renieras trois fois. Et en y pensant, il pleura.

< Marko 14 >