< Marko 13 >

1 Yesu alipokuwa akitembea kutoka hekaluni, mmoja wa wanafunzi wake akamwuliza, “Mwalimu, tazama mawe haya yakushangaza na majengo!”
anantaraM mandirAd bahirgamanakAle tasya ziSyANAmekastaM vyAhRtavAn he guro pazyatu kIdRzAH pASANAH kIdRk ca nicayanaM|
2 Akamwambia, Unaona majengo haya makubwa? Hakuna hata jiwe moja litakalo salia juu ya jingine ambalo halitaangushwa chini”.
tadA yIzustam avadat tvaM kimetad bRhannicayanaM pazyasi? asyaikapASANopi dvitIyapASANopari na sthAsyati sarvve 'dhaHkSepsyante|
3 Naye alipokuwa amekaa juu ya Mlima wa Mizeituni nyuma ya hekalu, Petro, Yakobo, Yohana na Andrea wakamwuliza kwa siri,
atha yasmin kAle jaitungirau mandirasya sammukhe sa samupaviSTastasmin kAle pitaro yAkUb yohan Andriyazcaite taM rahasi papracchuH,
4 “Tuambie, mambo haya yatakuwa lini? Ni nini dalili ya mambo haya kutokea?”
etA ghaTanAH kadA bhaviSyanti? tathaitatsarvvAsAM siddhyupakramasya vA kiM cihnaM? tadasmabhyaM kathayatu bhavAn|
5 Yesu alianza kuwaambia, “Kuweni makini kwamba mtu yoyote asiwapotoshe.
tato yAzustAn vaktumArebhe, kopi yathA yuSmAn na bhrAmayati tathAtra yUyaM sAvadhAnA bhavata|
6 Wengi watakuja kwa jina langu wakisema, 'Mimi ndiye', na watawapotosha wengi.
yataH khrISTohamiti kathayitvA mama nAmnAneke samAgatya lokAnAM bhramaM janayiSyanti;
7 Mtakaposikia vita na tetesi za vita, msiogope; mambo haya hayana budi kutokea, lakini mwisho bado.
kintu yUyaM raNasya vArttAM raNADambaraJca zrutvA mA vyAkulA bhavata, ghaTanA etA avazyammAvinyaH; kintvApAtato na yugAnto bhaviSyati|
8 Taifa litainuka kinyume na taifa jingine, na ufalme kinyume na ufalme. Patakuwa na matetemeko sehemu mbalimbali, na njaa. Huu ni mwanzo wa utungu.
dezasya vipakSatayA dezo rAjyasya vipakSatayA ca rAjyamutthAsyati, tathA sthAne sthAne bhUmikampo durbhikSaM mahAklezAzca samupasthAsyanti, sarvva ete duHkhasyArambhAH|
9 Iweni macho. Watawapeleka hadi mabarazani, na mtapingwa katika masinagogi. Mtasimamishwa mbele ya watawala na wafalme kwa ajili yangu, kama ushuhuda kwao.
kintu yUyam AtmArthe sAvadhAnAstiSThata, yato lokA rAjasabhAyAM yuSmAn samarpayiSyanti, tathA bhajanagRhe prahariSyanti; yUyaM madarthe dezAdhipAn bhUpAMzca prati sAkSyadAnAya teSAM sammukhe upasthApayiSyadhve|
10 Lakini injili lazima kwanza ihubiriwe kwa mataifa yote.
zeSIbhavanAt pUrvvaM sarvvAn dezIyAn prati susaMvAdaH pracArayiSyate|
11 Watakapo wakamata na kuwakabidhi, msiogope kuhusu kile mtakachosema. Ndani ya muda huo, mtapewa nini cha kusema; hamtakuwa ninyi mtakaoongea, bali Roho Mtakatifu.
kintu yadA te yuSmAn dhRtvA samarpayiSyanti tadA yUyaM yadyad uttaraM dAsyatha, tadagra tasya vivecanaM mA kuruta tadarthaM kiJcidapi mA cintayata ca, tadAnIM yuSmAkaM manaHsu yadyad vAkyam upasthApayiSyate tadeva vadiSyatha, yato yUyaM na tadvaktAraH kintu pavitra AtmA tasya vaktA|
12 Ndugu atamshitaki ndugu kuuawa, baba na mtoto wake. Watoto watasimama kinyume cha baba zao na kuwasababisha kuuawa.
tadA bhrAtA bhrAtaraM pitA putraM ghAtanArthaM parahasteSu samarpayiSyate, tathA patyAni mAtApitro rvipakSatayA tau ghAtayiSyanti|
13 Mtachukiwa na kila mtu kwa sababu ya jina langu. Lakini atakayevumilia mpaka mwisho, mtu huyo ataokoka.
mama nAmahetoH sarvveSAM savidhe yUyaM jugupsitA bhaviSyatha, kintu yaH kazcit zeSaparyyantaM dhairyyam AlambiSyate saeva paritrAsyate|
14 Mtakapoona chukizo la uharibifu limesimama pale lisipotakiwa kusimama (asomaye na afahamu), ndipo walioko ndani ya Yuda wakimbilie milimani,
dAniyelbhaviSyadvAdinA proktaM sarvvanAzi jugupsitaJca vastu yadA tvayogyasthAne vidyamAnaM drakSatha (yo janaH paThati sa budhyatAM) tadA ye yihUdIyadeze tiSThanti te mahIdhraM prati palAyantAM;
15 naye aliyeko juu ya nyumba asishuke chini ya nyumba, au kuchukua chochote kilichoko nje,
tathA yo naro gRhopari tiSThati sa gRhamadhyaM nAvarohatu, tathA kimapi vastu grahItuM madhyegRhaM na pravizatu;
16 na aliyeko shambani asirudi kuchukua vazi lake.
tathA ca yo naraH kSetre tiSThati sopi svavastraM grahItuM parAvRtya na vrajatu|
17 Lakini ole wao wanawake wenye mimba na wanyonyeshao katika siku hizo!
tadAnIM garbbhavatInAM stanyadAtrINAJca yoSitAM durgati rbhaviSyati|
18 Ombeni kwamba isitokee wakati wa baridi.
yuSmAkaM palAyanaM zItakAle yathA na bhavati tadarthaM prArthayadhvaM|
19 Kwani patakuwa na mateso makubwa, ambayo hayajawahi kutokea, tangu Mungu alipoumba ulimwengu, mpaka sasa, hapana, wala haitatokea tena.
yatastadA yAdRzI durghaTanA ghaTiSyate tAdRzI durghaTanA IzvarasRSTeH prathamamArabhyAdya yAvat kadApi na jAtA na janiSyate ca|
20 Mpaka Bwana atakapopunguza siku, hakuna mwili utakaookoka, lakini kwa ajili ya wateule, atakaowachagua, atapunguza namba za siku.
aparaJca paramezvaro yadi tasya samayasya saMkSepaM na karoti tarhi kasyApi prANabhRto rakSA bhavituM na zakSyati, kintu yAn janAn manonItAn akarot teSAM svamanonItAnAM hetoH sa tadanehasaM saMkSepsyati|
21 Wakati huo kama mtu yeyote atawaambia, Tazama, Kristo yuko hapa!' au 'Tazama, yuko pale!' msiamini.
anyacca pazyata khrISTotra sthAne vA tatra sthAne vidyate, tasminkAle yadi kazcid yuSmAn etAdRzaM vAkyaM vyAharati, tarhi tasmin vAkye bhaiva vizvasita|
22 Kwani Wakristo wa uongo na manabii wa uongo watatokea na watatoa ishara na maajabu, ili kwamba, wawadanganye, yamkini hata wateule.
yatoneke mithyAkhrISTA mithyAbhaviSyadvAdinazca samupasthAya bahUni cihnAnyadbhutAni karmmANi ca darzayiSyanti; tathA yadi sambhavati tarhi manonItalokAnAmapi mithyAmatiM janayiSyanti|
23 Iweni macho! Nimekwisha wambia haya yote kabla ya wakati.
pazyata ghaTanAtaH pUrvvaM sarvvakAryyasya vArttAM yuSmabhyamadAm, yUyaM sAvadhAnAstiSThata|
24 Lakini baada ya mateso ya siku hizo, jua litatiwa giza, mwezi hautatoa mwanga wake,
aparaJca tasya klezakAlasyAvyavahite parakAle bhAskaraH sAndhakAro bhaviSyati tathaiva candrazcandrikAM na dAsyati|
25 nyota zitaanguka kutoka angani, na nguvu zilizoko mbinguni zitatikisika.
nabhaHsthAni nakSatrANi patiSyanti, vyomamaNDalasthA grahAzca vicaliSyanti|
26 Ndipo watakapomwona Mwana wa Adamu akija mawinguni kwa nguvu kubwa na utukufu.
tadAnIM mahAparAkrameNa mahaizvaryyeNa ca meghamAruhya samAyAntaM mAnavasutaM mAnavAH samIkSiSyante|
27 Ndipo atatuma malaika zake na atawakusanya pamoja wateule wake kutoka pande kuu nne za dunia, kutoka mwisho wa dunia mpaka mwisho wa mbingu.
anyacca sa nijadUtAn prahitya nabhobhUmyoH sImAM yAvad jagatazcaturdigbhyaH svamanonItalokAn saMgrahISyati|
28 Kwa mtini jifunzeni. Kama tawi liwezavyo kutoa na kuweka haraka majani yake, ndipo mtajua kwamba kiangazi kiko karibu.
uDumbarataro rdRSTAntaM zikSadhvaM yadoDumbarasya taro rnavInAH zAkhA jAyante pallavAdIni ca rnigacchanti, tadA nidAghakAlaH savidho bhavatIti yUyaM jJAtuM zaknutha|
29 Ndivyo ilivyo, mtakapoona mambo haya yakitokea, jueni kwamba yuko karibu, na malango.
tadvad etA ghaTanA dRSTvA sa kAlo dvAryyupasthita iti jAnIta|
30 Kweli, nawambieni, hiki kizazi hakitapita mbali kabla mambo haya hayajatokea.
yuSmAnahaM yathArthaM vadAmi, AdhunikalokAnAM gamanAt pUrvvaM tAni sarvvANi ghaTiSyante|
31 Mbingu na nchi zitapita, lakini maneno yangu hayatapita kamwe.
dyAvApRthivyo rvicalitayoH satyo rmadIyA vANI na vicaliSyati|
32 Lakini kuhusu siku hiyo au saa, hakuna ajuaye, hata malaika wa mbinguni, wala Mwana, ila Baba.
aparaJca svargasthadUtagaNo vA putro vA tAtAdanyaH kopi taM divasaM taM daNDaM vA na jJApayati|
33 Iweni macho, Tazama, kwa sababu hamjui ni muda gani yatatokea. (Zingatia: Mstari huu, “Muwe waangalifu, Tazameni na ombeni kwa sababu...” haumo kwenye nakala za kale).
ataH sa samayaH kadA bhaviSyati, etajjJAnAbhAvAd yUyaM sAvadhAnAstiSThata, satarkAzca bhUtvA prArthayadhvaM;
34 Ni kama mtu anayeenda safarini: akaacha nyumba yake, na kumweka mtumwa wake kuwa mtawala wa nyumba, kila mmoja na kazi yake. Na kumwamuru mlinzi kukaa macho.
yadvat kazcit pumAn svanivezanAd dUradezaM prati yAtrAkaraNakAle dAseSu svakAryyasya bhAramarpayitvA sarvvAn sve sve karmmaNi niyojayati; aparaM dauvArikaM jAgarituM samAdizya yAti, tadvan naraputraH|
35 Kwa hiyo iweni macho! Kwani hamjui ni lini bwana wa nyumba atakaporudi nyumbani, yawezekana ni jioni, usiku wa manane, wakati jogoo atakapowika, au asubuhi.
gRhapatiH sAyaMkAle nizIthe vA tRtIyayAme vA prAtaHkAle vA kadAgamiSyati tad yUyaM na jAnItha;
36 Kama akija ghafla, asikukute umelala.
sa haThAdAgatya yathA yuSmAn nidritAn na pazyati, tadarthaM jAgaritAstiSThata|
37 Kile nikisemacho kwako nakisema kwa kila mtu: Kesheni”!
yuSmAnahaM yad vadAmi tadeva sarvvAn vadAmi, jAgaritAstiSThateti|

< Marko 13 >