< Marko 13 >

1 Yesu alipokuwa akitembea kutoka hekaluni, mmoja wa wanafunzi wake akamwuliza, “Mwalimu, tazama mawe haya yakushangaza na majengo!”
Sina Jesu havali kuyenda kuzwa mwi tempere, zumwi kuva rutwana vakwe cha wamba kwali. “Muruti, lole ha mavwe akokiswa ni muyaho ukomokisa!”
2 Akamwambia, Unaona majengo haya makubwa? Hakuna hata jiwe moja litakalo salia juu ya jingine ambalo halitaangushwa chini”.
Cha mu wambila, “Ubwene iyi mizako mikando?” Kakwina nangati ivwe lyonke lyete nili shale ni lilimbite limwi lyete nili kangwe kuwiswa hansi.”
3 Naye alipokuwa amekaa juu ya Mlima wa Mizeituni nyuma ya hekalu, Petro, Yakobo, Yohana na Andrea wakamwuliza kwa siri,
Sina havali kwikere he Rundu lya Olive kulilolera ni tempere, Pitorosi, Jakovo, Johani ni Anderiasi chivamuvuza kwimbali,
4 “Tuambie, mambo haya yatakuwa lini? Ni nini dalili ya mambo haya kutokea?”
“Tu wambile, izi zintu kazi pangahale lili? Zi supo nzi zitu lukere kuvona heva izi chi zina hafwihi niku pangahala?”
5 Yesu alianza kuwaambia, “Kuweni makini kwamba mtu yoyote asiwapotoshe.
Jesu chatanga kuwamba kuvali, “Mutokomere kuti kakwina zumwiyante ami yembulule.
6 Wengi watakuja kwa jina langu wakisema, 'Mimi ndiye', na watawapotosha wengi.
Vangi kavakeze mwizina lyangu ni kuti, 'Jime iye; mi kava yembulule vaangi.
7 Mtakaposikia vita na tetesi za vita, msiogope; mambo haya hayana budi kutokea, lakini mwisho bado.
Ha mu zuwa ze kondo, ni ma hulyuhulyu e kondo sanzi mu vileli; inzo zintu zi lukere kupangahala, kono mamanimani kaeni kusika.
8 Taifa litainuka kinyume na taifa jingine, na ufalme kinyume na ufalme. Patakuwa na matetemeko sehemu mbalimbali, na njaa. Huu ni mwanzo wa utungu.
Cho kuti i kanda kai lwise i kanda, muvuso ka u lwise mu vuso. Ka kuve ni zikinyeho mu zi vaka zimwi ni nanga. Aa njima ma tangilo a ku sasama kwaku huzumuka (kusumunuka).
9 Iweni macho. Watawapeleka hadi mabarazani, na mtapingwa katika masinagogi. Mtasimamishwa mbele ya watawala na wafalme kwa ajili yangu, kama ushuhuda kwao.
Muve muva mameli venu mu vene. Mu vaka mi twale kuva si tutengo, mi kamu ka kavolwe mwi muma sinangonge. Kamu zimane ha vusi bwa vavusisi ni malena ke vaka lyangu, Sina vupaki kuvali.
10 Lakini injili lazima kwanza ihubiriwe kwa mataifa yote.
Kono pili ivangeli lyi lukere ku ku taziwa mwi kanda zose.
11 Watakapo wakamata na kuwakabidhi, msiogope kuhusu kile mtakachosema. Ndani ya muda huo, mtapewa nini cha kusema; hamtakuwa ninyi mtakaoongea, bali Roho Mtakatifu.
Ha va mi sumina niku mi twala, sezi mu vilelezwa zete muwambe. Ka kuti mweyo ihola zeti muwambe kamu zi hewe; Kese i ve njenwe mu wamba, kono Luhuho lu Njolola.
12 Ndugu atamshitaki ndugu kuuawa, baba na mtoto wake. Watoto watasimama kinyume cha baba zao na kuwasababisha kuuawa.
Mukwakwe mutu ka veteke mukwake kwifuu, mi vesi mwana wa vo. Vaana kava zimane ni kulwisa bashemi va vo, nikuva letera kuvikiwa kwi ifu.
13 Mtachukiwa na kila mtu kwa sababu ya jina langu. Lakini atakayevumilia mpaka mwisho, mtu huyo ataokoka.
Mu mu toiwe kubatu vonse ivaka lye zina lyangu. Kono yense yate a wonderele hesi kuma mani mani, unzo muntu ka hazwe.
14 Mtakapoona chukizo la uharibifu limesimama pale lisipotakiwa kusimama (asomaye na afahamu), ndipo walioko ndani ya Yuda wakimbilie milimani,
Chimwa vona vuvi vu dadola kuti bwina havusa swaneli( yo vala a zuwi sise), mu siye avo vena mwa Judea va tilile ku ma ruundu.
15 naye aliyeko juu ya nyumba asishuke chini ya nyumba, au kuchukua chochote kilichoko nje,
mi wina hakatungandu kezuvo sanzi a voli mwi zuvo kapa kuhinda cimwi mwa teni,
16 na aliyeko shambani asirudi kuchukua vazi lake.
mi mu siye wina mwi waa, sanzi abolyi kuka hinda inguvo.
17 Lakini ole wao wanawake wenye mimba na wanyonyeshao katika siku hizo!
Kono bumai kwavo be minsi mwe yo i nako kapa vanyosa mweyo inako!
18 Ombeni kwamba isitokee wakati wa baridi.
Mulapele kuti kanji nzi pangahali ha maliha.
19 Kwani patakuwa na mateso makubwa, ambayo hayajawahi kutokea, tangu Mungu alipoumba ulimwengu, mpaka sasa, hapana, wala haitatokea tena.
Kakuti ka kuve ni manyando makando, aseni kuvonwa kutanga ku matangilo, aho Ireeza ha bumba i kanda, konji hanu, nanta, hape kese ni ku ve vulyo.
20 Mpaka Bwana atakapopunguza siku, hakuna mwili utakaookoka, lakini kwa ajili ya wateule, atakaowachagua, atapunguza namba za siku.
Hesi Simwine cha fwihaza mazuva, kakwina inyama yese ni hazwe, Kono kevaka lyi va ketetwe, avo vava keti ava fwihazi i palo ya mazuva.
21 Wakati huo kama mtu yeyote atawaambia, Tazama, Kristo yuko hapa!' au 'Tazama, yuko pale!' msiamini.
Lyahanu heva zumwi chacho kuti, 'Vone, zunu kiresite!' kapa 'Vone, zuna hana!' sanzi mu zumini.
22 Kwani Wakristo wa uongo na manabii wa uongo watatokea na watatoa ishara na maajabu, ili kwamba, wawadanganye, yamkini hata wateule.
Kakuti va kiresite va mapa ni vapolofita va mapa muva voneke mi kavahe zisupo ni makazo, kuku yembulula, nanga niva ketetwe.
23 Iweni macho! Nimekwisha wambia haya yote kabla ya wakati.
Mu tokomele! China mi wambila izi zintu niku sina i nako.
24 Lakini baada ya mateso ya siku hizo, jua litatiwa giza, mwezi hautatoa mwanga wake,
Kono chi amana manyando ayo mazuva, izuva kalisihiswe, mwezi kese uhe i seli lya teni,
25 nyota zitaanguka kutoka angani, na nguvu zilizoko mbinguni zitatikisika.
i kaani kaziwe kwi wulu, mi ziho zina kwi ulu kazi nyanganiswe.
26 Ndipo watakapomwona Mwana wa Adamu akija mawinguni kwa nguvu kubwa na utukufu.
Lyaho kava vone Mwana Muntu na keza muma kope ni ziho zikando ne kanya.
27 Ndipo atatuma malaika zake na atawakusanya pamoja wateule wake kutoka pande kuu nne za dunia, kutoka mwisho wa dunia mpaka mwisho wa mbingu.
Mi ka tume mañeloyi akwee mi ka kopanye hamwina ba ketetwe, kuzwa muma ihuho zo nee, kuzwa ma mani mani e kanda kuya kumamanizo e wulu.
28 Kwa mtini jifunzeni. Kama tawi liwezavyo kutoa na kuweka haraka majani yake, ndipo mtajua kwamba kiangazi kiko karibu.
Muli tute ituto kwi samu lye Fenga, Haho mutavi hau zuma ni kuwisa makova alyo, mwi ziva kuti imbumbi chiyina hafuhi.
29 Ndivyo ilivyo, mtakapoona mambo haya yakitokea, jueni kwamba yuko karibu, na malango.
Mi hape, hamu vona i zi zintu nizi pangahala mwi zive kuti cho wina hafwihi, ha fuhi ne mulyango.
30 Kweli, nawambieni, hiki kizazi hakitapita mbali kabla mambo haya hayajatokea.
Ka busakusima nimi wambila ulu lu zuvo kese lu fwee inzi zitu nizi seni kupangala.
31 Mbingu na nchi zitapita, lakini maneno yangu hayatapita kamwe.
I wulu ni kanda kazi mane, kono mazwi angu kese ni a mane.
32 Lakini kuhusu siku hiyo au saa, hakuna ajuaye, hata malaika wa mbinguni, wala Mwana, ila Baba.
Kono ku amana nelyo izuva kamba iyo inako, kakwina yo yizi, nangati mañiloyi, kamba Mwana, kono tayo.
33 Iweni macho, Tazama, kwa sababu hamjui ni muda gani yatatokea. (Zingatia: Mstari huu, “Muwe waangalifu, Tazameni na ombeni kwa sababu...” haumo kwenye nakala za kale).
Mu tokomere! Mulole, kakuti ka mwizi kuti inako nzi.
34 Ni kama mtu anayeenda safarini: akaacha nyumba yake, na kumweka mtumwa wake kuwa mtawala wa nyumba, kila mmoja na kazi yake. Na kumwamuru mlinzi kukaa macho.
Ku swana iri mukwame yo yenda mumu musipili, u siya i zuvo yakwe niku vika bahikana vakwe kuku mamele i zuvo, zumwi ne zumwi ne musevezi wakwe, ni ku laela mungateli kuti a tonde.
35 Kwa hiyo iweni macho! Kwani hamjui ni lini bwana wa nyumba atakaporudi nyumbani, yawezekana ni jioni, usiku wa manane, wakati jogoo atakapowika, au asubuhi.
Lyahanu mwikale ni mutonda, kakuti kamwizi aho simwine we zuvo yasaka vole kumuzi; i wola kuva muchitengu, ha kati ka masiku, mukombwe ciwa lila, kapa kakusasani.
36 Kama akija ghafla, asikukute umelala.
Heva nakeza chokuhyera, kanji mumuzuminini kumi wana mulere.
37 Kile nikisemacho kwako nakisema kwa kila mtu: Kesheni”!
Izo zini wamba kwenu ni ziwambira vonse: Mutonde!”

< Marko 13 >