< Marko 13 >

1 Yesu alipokuwa akitembea kutoka hekaluni, mmoja wa wanafunzi wake akamwuliza, “Mwalimu, tazama mawe haya yakushangaza na majengo!”
耶稣从殿里出来的时候,有一个门徒对他说:“夫子,请看,这是何等的石头!何等的殿宇!”
2 Akamwambia, Unaona majengo haya makubwa? Hakuna hata jiwe moja litakalo salia juu ya jingine ambalo halitaangushwa chini”.
耶稣对他说:“你看见这大殿宇吗?将来在这里没有一块石头留在石头上,不被拆毁了。”
3 Naye alipokuwa amekaa juu ya Mlima wa Mizeituni nyuma ya hekalu, Petro, Yakobo, Yohana na Andrea wakamwuliza kwa siri,
耶稣在橄榄山上对圣殿而坐。彼得、雅各、约翰,和安得烈暗暗地问他说:
4 “Tuambie, mambo haya yatakuwa lini? Ni nini dalili ya mambo haya kutokea?”
“请告诉我们,什么时候有这些事呢?这一切事将成的时候有什么预兆呢?”
5 Yesu alianza kuwaambia, “Kuweni makini kwamba mtu yoyote asiwapotoshe.
耶稣说:“你们要谨慎,免得有人迷惑你们。
6 Wengi watakuja kwa jina langu wakisema, 'Mimi ndiye', na watawapotosha wengi.
将来有好些人冒我的名来,说:‘我是基督’,并且要迷惑许多人。
7 Mtakaposikia vita na tetesi za vita, msiogope; mambo haya hayana budi kutokea, lakini mwisho bado.
你们听见打仗和打仗的风声,不要惊慌。这些事是必须有的,只是末期还没有到。
8 Taifa litainuka kinyume na taifa jingine, na ufalme kinyume na ufalme. Patakuwa na matetemeko sehemu mbalimbali, na njaa. Huu ni mwanzo wa utungu.
民要攻打民,国要攻打国;多处必有地震、饥荒。这都是灾难的起头。
9 Iweni macho. Watawapeleka hadi mabarazani, na mtapingwa katika masinagogi. Mtasimamishwa mbele ya watawala na wafalme kwa ajili yangu, kama ushuhuda kwao.
但你们要谨慎;因为人要把你们交给公会,并且你们在会堂里要受鞭打,又为我的缘故站在诸侯与君王面前,对他们作见证。
10 Lakini injili lazima kwanza ihubiriwe kwa mataifa yote.
然而,福音必须先传给万民。
11 Watakapo wakamata na kuwakabidhi, msiogope kuhusu kile mtakachosema. Ndani ya muda huo, mtapewa nini cha kusema; hamtakuwa ninyi mtakaoongea, bali Roho Mtakatifu.
人把你们拉去交官的时候,不要预先思虑说什么;到那时候,赐给你们什么话,你们就说什么;因为说话的不是你们,乃是圣灵。
12 Ndugu atamshitaki ndugu kuuawa, baba na mtoto wake. Watoto watasimama kinyume cha baba zao na kuwasababisha kuuawa.
弟兄要把弟兄,父亲要把儿子,送到死地;儿女要起来与父母为敌,害死他们;
13 Mtachukiwa na kila mtu kwa sababu ya jina langu. Lakini atakayevumilia mpaka mwisho, mtu huyo ataokoka.
并且你们要为我的名被众人恨恶。惟有忍耐到底的,必然得救。”
14 Mtakapoona chukizo la uharibifu limesimama pale lisipotakiwa kusimama (asomaye na afahamu), ndipo walioko ndani ya Yuda wakimbilie milimani,
“你们看见那行毁坏可憎的,站在不当站的地方(读这经的人须要会意)。那时,在犹太的,应当逃到山上;
15 naye aliyeko juu ya nyumba asishuke chini ya nyumba, au kuchukua chochote kilichoko nje,
在房上的,不要下来,也不要进去拿家里的东西;
16 na aliyeko shambani asirudi kuchukua vazi lake.
在田里的,也不要回去取衣裳。
17 Lakini ole wao wanawake wenye mimba na wanyonyeshao katika siku hizo!
当那些日子,怀孕的和奶孩子的有祸了!
18 Ombeni kwamba isitokee wakati wa baridi.
你们应当祈求,叫这些事不在冬天临到。
19 Kwani patakuwa na mateso makubwa, ambayo hayajawahi kutokea, tangu Mungu alipoumba ulimwengu, mpaka sasa, hapana, wala haitatokea tena.
因为在那些日子必有灾难,自从 神创造万物直到如今,并没有这样的灾难,后来也必没有。
20 Mpaka Bwana atakapopunguza siku, hakuna mwili utakaookoka, lakini kwa ajili ya wateule, atakaowachagua, atapunguza namba za siku.
若不是主减少那日子,凡有血气的,总没有一个得救的;只是为主的选民,他将那日子减少了。
21 Wakati huo kama mtu yeyote atawaambia, Tazama, Kristo yuko hapa!' au 'Tazama, yuko pale!' msiamini.
那时若有人对你们说:‘看哪,基督在这里’,或说:‘基督在那里’,你们不要信!
22 Kwani Wakristo wa uongo na manabii wa uongo watatokea na watatoa ishara na maajabu, ili kwamba, wawadanganye, yamkini hata wateule.
因为假基督、假先知将要起来,显神迹奇事,倘若能行,就把选民迷惑了。
23 Iweni macho! Nimekwisha wambia haya yote kabla ya wakati.
你们要谨慎。看哪,凡事我都预先告诉你们了。”
24 Lakini baada ya mateso ya siku hizo, jua litatiwa giza, mwezi hautatoa mwanga wake,
“在那些日子,那灾难以后, 日头要变黑了, 月亮也不放光,
25 nyota zitaanguka kutoka angani, na nguvu zilizoko mbinguni zitatikisika.
众星要从天上坠落, 天势都要震动。
26 Ndipo watakapomwona Mwana wa Adamu akija mawinguni kwa nguvu kubwa na utukufu.
那时,他们要看见人子有大能力、大荣耀,驾云降临。
27 Ndipo atatuma malaika zake na atawakusanya pamoja wateule wake kutoka pande kuu nne za dunia, kutoka mwisho wa dunia mpaka mwisho wa mbingu.
他要差遣天使,把他的选民,从四方,从地极直到天边,都招聚了来。”
28 Kwa mtini jifunzeni. Kama tawi liwezavyo kutoa na kuweka haraka majani yake, ndipo mtajua kwamba kiangazi kiko karibu.
“你们可以从无花果树学个比方:当树枝发嫩长叶的时候,你们就知道夏天近了。
29 Ndivyo ilivyo, mtakapoona mambo haya yakitokea, jueni kwamba yuko karibu, na malango.
这样,你们几时看见这些事成就,也该知道人子近了,正在门口了。
30 Kweli, nawambieni, hiki kizazi hakitapita mbali kabla mambo haya hayajatokea.
我实在告诉你们,这世代还没有过去,这些事都要成就。
31 Mbingu na nchi zitapita, lakini maneno yangu hayatapita kamwe.
天地要废去,我的话却不能废去。”
32 Lakini kuhusu siku hiyo au saa, hakuna ajuaye, hata malaika wa mbinguni, wala Mwana, ila Baba.
“但那日子,那时辰,没有人知道,连天上的使者也不知道,子也不知道,惟有父知道。
33 Iweni macho, Tazama, kwa sababu hamjui ni muda gani yatatokea. (Zingatia: Mstari huu, “Muwe waangalifu, Tazameni na ombeni kwa sababu...” haumo kwenye nakala za kale).
你们要谨慎,警醒祈祷,因为你们不晓得那日期几时来到。
34 Ni kama mtu anayeenda safarini: akaacha nyumba yake, na kumweka mtumwa wake kuwa mtawala wa nyumba, kila mmoja na kazi yake. Na kumwamuru mlinzi kukaa macho.
这事正如一个人离开本家,寄居外邦,把权柄交给仆人,分派各人当做的工,又吩咐看门的警醒。
35 Kwa hiyo iweni macho! Kwani hamjui ni lini bwana wa nyumba atakaporudi nyumbani, yawezekana ni jioni, usiku wa manane, wakati jogoo atakapowika, au asubuhi.
所以,你们要警醒;因为你们不知道家主什么时候来,或晚上,或半夜,或鸡叫,或早晨;
36 Kama akija ghafla, asikukute umelala.
恐怕他忽然来到,看见你们睡着了。
37 Kile nikisemacho kwako nakisema kwa kila mtu: Kesheni”!
我对你们所说的话,也是对众人说:要警醒!”

< Marko 13 >