< Marko 13 >

1 Yesu alipokuwa akitembea kutoka hekaluni, mmoja wa wanafunzi wake akamwuliza, “Mwalimu, tazama mawe haya yakushangaza na majengo!”
穌從聖殿裏出來的時候,他的門徒中有一個對他說:「師傅! 看,這是何等的石頭! 何等的建築!」
2 Akamwambia, Unaona majengo haya makubwa? Hakuna hata jiwe moja litakalo salia juu ya jingine ambalo halitaangushwa chini”.
耶穌對他說:「你看見這些偉大的建築嗎﹖將來這裏決沒有一塊石頭留在另一塊石頭上,而不被拆毀的。」
3 Naye alipokuwa amekaa juu ya Mlima wa Mizeituni nyuma ya hekalu, Petro, Yakobo, Yohana na Andrea wakamwuliza kwa siri,
耶穌在橄欖山上,面對聖殿坐著的時候,伯多祿、雅各伯、若望和安德肋私下問他說:「
4 “Tuambie, mambo haya yatakuwa lini? Ni nini dalili ya mambo haya kutokea?”
請告訴我們:什麼時候發生這事﹖一切事要完成時,將有什麼先兆﹖」
5 Yesu alianza kuwaambia, “Kuweni makini kwamba mtu yoyote asiwapotoshe.
耶穌就開始對他們說:「你們要謹慎,免得有人欺騙了你們。
6 Wengi watakuja kwa jina langu wakisema, 'Mimi ndiye', na watawapotosha wengi.
將有許多人假冒我的名字來說:我就是[默西亞] ;並且要欺騙許多人。
7 Mtakaposikia vita na tetesi za vita, msiogope; mambo haya hayana budi kutokea, lakini mwisho bado.
當你們聽到戰爭和戰爭的風聲時,不要驚慌,因為這是必須發生的,但還不是結局。
8 Taifa litainuka kinyume na taifa jingine, na ufalme kinyume na ufalme. Patakuwa na matetemeko sehemu mbalimbali, na njaa. Huu ni mwanzo wa utungu.
因為民族要起來攻擊民族,國家攻擊國家;到處要有地震,要有饑荒;但這只是苦痛的開始。」
9 Iweni macho. Watawapeleka hadi mabarazani, na mtapingwa katika masinagogi. Mtasimamishwa mbele ya watawala na wafalme kwa ajili yangu, kama ushuhuda kwao.
你們自己要謹慎! 人要把你們解送到公議會,你們在會堂裏要受鞭打,並且也要為我的緣故,站在總督和君王面前,對他們作證。
10 Lakini injili lazima kwanza ihubiriwe kwa mataifa yote.
但福音必須先傳於萬國。
11 Watakapo wakamata na kuwakabidhi, msiogope kuhusu kile mtakachosema. Ndani ya muda huo, mtapewa nini cha kusema; hamtakuwa ninyi mtakaoongea, bali Roho Mtakatifu.
人把你們拉去解送到法庭時,你們不要預先思慮該說什麼;在那時刻賜給你們什麼話,你們就說什麼,因為說話的不是你們,而是聖神。
12 Ndugu atamshitaki ndugu kuuawa, baba na mtoto wake. Watoto watasimama kinyume cha baba zao na kuwasababisha kuuawa.
兄弟將把兄弟,父親將把兒子置於死地;兒女將起來反對父母,把他們處死。
13 Mtachukiwa na kila mtu kwa sababu ya jina langu. Lakini atakayevumilia mpaka mwisho, mtu huyo ataokoka.
你們為了我的字,將為眾人所惱恨;但那堅持到底的,必要得救。」
14 Mtakapoona chukizo la uharibifu limesimama pale lisipotakiwa kusimama (asomaye na afahamu), ndipo walioko ndani ya Yuda wakimbilie milimani,
幾時你們看見那『招致荒涼的可憎之物』立在不應在的地方──讀者應明白;那時在猶太的,該逃往山中;
15 naye aliyeko juu ya nyumba asishuke chini ya nyumba, au kuchukua chochote kilichoko nje,
在屋頂上的,不要下來,也不要進去,從屋裏取什麼東西;
16 na aliyeko shambani asirudi kuchukua vazi lake.
在田地裏的,不要回來取自己的外衣。
17 Lakini ole wao wanawake wenye mimba na wanyonyeshao katika siku hizo!
在那些日子裏,懷孕的和哺乳的是有禍的!
18 Ombeni kwamba isitokee wakati wa baridi.
但你們當祈禱, 不要叫這事逢到冬天。」
19 Kwani patakuwa na mateso makubwa, ambayo hayajawahi kutokea, tangu Mungu alipoumba ulimwengu, mpaka sasa, hapana, wala haitatokea tena.
因為在那些日子裏,必有災難,這是從天主開始,直到如今從未有過的,將來也不會再有。
20 Mpaka Bwana atakapopunguza siku, hakuna mwili utakaookoka, lakini kwa ajili ya wateule, atakaowachagua, atapunguza namba za siku.
若不是上主縮短了那些時日,凡有血肉的人都不會得救; 但為了他所揀選的被選者,他縮短了那些時日。
21 Wakati huo kama mtu yeyote atawaambia, Tazama, Kristo yuko hapa!' au 'Tazama, yuko pale!' msiamini.
那時,若有人對你們說:看,默西亞在這裏! 看,在那裏! 你們不要相信!
22 Kwani Wakristo wa uongo na manabii wa uongo watatokea na watatoa ishara na maajabu, ili kwamba, wawadanganye, yamkini hata wateule.
因為將有假默西亞和假先知興起,行異跡和奇事,如果可能的話,他們連被選者都要欺騙。
23 Iweni macho! Nimekwisha wambia haya yote kabla ya wakati.
所以,你們要謹慎! 看,凡事我都預先告訴了你們!
24 Lakini baada ya mateso ya siku hizo, jua litatiwa giza, mwezi hautatoa mwanga wake,
但是,在那些日子裏,在那災難以後,太陽將要昏暗,月亮不再發光;
25 nyota zitaanguka kutoka angani, na nguvu zilizoko mbinguni zitatikisika.
星辰要從天上墜下,天上的萬象也要動搖。
26 Ndipo watakapomwona Mwana wa Adamu akija mawinguni kwa nguvu kubwa na utukufu.
那時,人要看見人子帶著大威能和光榮乘雲降來。
27 Ndipo atatuma malaika zake na atawakusanya pamoja wateule wake kutoka pande kuu nne za dunia, kutoka mwisho wa dunia mpaka mwisho wa mbingu.
那時,他要派遣天使,由四方,從地極到天邊,聚集他的被選者。」
28 Kwa mtini jifunzeni. Kama tawi liwezavyo kutoa na kuweka haraka majani yake, ndipo mtajua kwamba kiangazi kiko karibu.
你們恁由無花果樹取個比喻:幾時它的枝條已經發嫩,生出葉子,你們就知道夏天近了。
29 Ndivyo ilivyo, mtakapoona mambo haya yakitokea, jueni kwamba yuko karibu, na malango.
同樣,你們幾時看見這些事發生了,就該知道:他已近在門口了。
30 Kweli, nawambieni, hiki kizazi hakitapita mbali kabla mambo haya hayajatokea.
我實在告訴你們:非到這一切發生了,這一世代決不會過去。
31 Mbingu na nchi zitapita, lakini maneno yangu hayatapita kamwe.
天地要過去,但是我的話決不會過去。
32 Lakini kuhusu siku hiyo au saa, hakuna ajuaye, hata malaika wa mbinguni, wala Mwana, ila Baba.
至於那日子和那時刻,除了父以外,誰也不知道,連天上的天使和子都不知道。」
33 Iweni macho, Tazama, kwa sababu hamjui ni muda gani yatatokea. (Zingatia: Mstari huu, “Muwe waangalifu, Tazameni na ombeni kwa sababu...” haumo kwenye nakala za kale).
你們要當心,要醒寤,因為你們不知道那日期什麼時候來到。
34 Ni kama mtu anayeenda safarini: akaacha nyumba yake, na kumweka mtumwa wake kuwa mtawala wa nyumba, kila mmoja na kazi yake. Na kumwamuru mlinzi kukaa macho.
正如一個遠行的人,離開自己的家時,把權柄交給自己的僕人,每人有每人的工作;又囑咐看門的須醒寤。
35 Kwa hiyo iweni macho! Kwani hamjui ni lini bwana wa nyumba atakaporudi nyumbani, yawezekana ni jioni, usiku wa manane, wakati jogoo atakapowika, au asubuhi.
所以,你們要醒寤,因為你們不知道,家主什麼時候回來:或許傍晚,或許夜半,或許雞叫,或許清晨;
36 Kama akija ghafla, asikukute umelala.
免得他忽然來到,遇見你們正在睡覺。
37 Kile nikisemacho kwako nakisema kwa kila mtu: Kesheni”!
我對你們說的,我也對眾人說:你們要醒寤!」

< Marko 13 >