< Marko 13 >

1 Yesu alipokuwa akitembea kutoka hekaluni, mmoja wa wanafunzi wake akamwuliza, “Mwalimu, tazama mawe haya yakushangaza na majengo!”
耶稣离开圣殿的时候,有一个门徒对他说:“老师,你看这些大石头,还有这些雄伟的建筑!”
2 Akamwambia, Unaona majengo haya makubwa? Hakuna hata jiwe moja litakalo salia juu ya jingine ambalo halitaangushwa chini”.
耶稣说:“你看这些雄伟的建筑,将来不会哪块石头堆砌在其他石头上,因为一切都会倒塌。”
3 Naye alipokuwa amekaa juu ya Mlima wa Mizeituni nyuma ya hekalu, Petro, Yakobo, Yohana na Andrea wakamwuliza kwa siri,
耶稣坐在橄榄山上,面向圣殿,彼得、雅各、约翰和安得烈私下问他:
4 “Tuambie, mambo haya yatakuwa lini? Ni nini dalili ya mambo haya kutokea?”
“请告诉我们,这一切什么时候会发生?这一切将要发生时,会有什么预兆?”
5 Yesu alianza kuwaambia, “Kuweni makini kwamba mtu yoyote asiwapotoshe.
耶稣告诉他们:“你们要小心,不要被人迷惑。
6 Wengi watakuja kwa jina langu wakisema, 'Mimi ndiye', na watawapotosha wengi.
许多人会跑来假冒我的名,声称‘我就是基督’,迷惑众人。
7 Mtakaposikia vita na tetesi za vita, msiogope; mambo haya hayana budi kutokea, lakini mwisho bado.
如果你们听说附近和远方有战争,不要担心,这些事情必然发生,但不是最终结局。
8 Taifa litainuka kinyume na taifa jingine, na ufalme kinyume na ufalme. Patakuwa na matetemeko sehemu mbalimbali, na njaa. Huu ni mwanzo wa utungu.
一个民族要攻打另一个民族,一个国家要对抗另一个国家,到处有地震和饥荒,但这就是世界诞生所经历痛苦的开始。
9 Iweni macho. Watawapeleka hadi mabarazani, na mtapingwa katika masinagogi. Mtasimamishwa mbele ya watawala na wafalme kwa ajili yangu, kama ushuhuda kwao.
你们要小心!因为人们会把你们交给公议会,你们会在会堂中被鞭打,还因为我的缘故,必须站在总督和君王面前向他们作证。
10 Lakini injili lazima kwanza ihubiriwe kwa mataifa yote.
但必须先将福音传给每个城邦。
11 Watakapo wakamata na kuwakabidhi, msiogope kuhusu kile mtakachosema. Ndani ya muda huo, mtapewa nini cha kusema; hamtakuwa ninyi mtakaoongea, bali Roho Mtakatifu.
当你们被抓并送去审判,无需担心该说什么,到时候你们听到告诉你的话,就说出来,因为说话的不是你们,而是圣灵。
12 Ndugu atamshitaki ndugu kuuawa, baba na mtoto wake. Watoto watasimama kinyume cha baba zao na kuwasababisha kuuawa.
兄弟会彼此背叛丧命,父亲会背叛儿子,儿女会悖逆父母,甚至置他们于死地。
13 Mtachukiwa na kila mtu kwa sababu ya jina langu. Lakini atakayevumilia mpaka mwisho, mtu huyo ataokoka.
因为我的原因,你们会被众人憎恨,但只要坚持忍耐到底,一定会获得救赎。
14 Mtakapoona chukizo la uharibifu limesimama pale lisipotakiwa kusimama (asomaye na afahamu), ndipo walioko ndani ya Yuda wakimbilie milimani,
当你们看见那‘污秽的偶像崇拜’站在但以理先知所说圣地(读至此处应认真思考),这时候,住在犹太的应当逃到山上。
15 naye aliyeko juu ya nyumba asishuke chini ya nyumba, au kuchukua chochote kilichoko nje,
站在屋顶的人,不要跑回屋子里取东西,
16 na aliyeko shambani asirudi kuchukua vazi lake.
如果你在田里,也不要回去取衣服。
17 Lakini ole wao wanawake wenye mimba na wanyonyeshao katika siku hizo!
那样的日子,对于怀孕和哺乳婴儿的女人极为可怕!
18 Ombeni kwamba isitokee wakati wa baridi.
要去祈祷,不要让这一切发生在冬季。
19 Kwani patakuwa na mateso makubwa, ambayo hayajawahi kutokea, tangu Mungu alipoumba ulimwengu, mpaka sasa, hapana, wala haitatokea tena.
因为那时必有大灾难,这是从世界的开始到现在未曾有过的,以后也必不会再有。
20 Mpaka Bwana atakapopunguza siku, hakuna mwili utakaookoka, lakini kwa ajili ya wateule, atakaowachagua, atapunguza namba za siku.
如果上帝不想尽快结束那些日子,将无人幸免,但为了上帝所选之人,那些日子必会变短。
21 Wakati huo kama mtu yeyote atawaambia, Tazama, Kristo yuko hapa!' au 'Tazama, yuko pale!' msiamini.
那时如果有人对你们说:‘看,基督在这里!看,基督在那里!’不要信。
22 Kwani Wakristo wa uongo na manabii wa uongo watatokea na watatoa ishara na maajabu, ili kwamba, wawadanganye, yamkini hata wateule.
因为到时必有假弥赛亚和假先知出现,可能会做出神迹和奇事,如果如此,就连天选之子都会迷惑。
23 Iweni macho! Nimekwisha wambia haya yote kabla ya wakati.
所以务必小心!我已经提前把这一切都告诉你们了。
24 Lakini baada ya mateso ya siku hizo, jua litatiwa giza, mwezi hautatoa mwanga wake,
那些灾难过后会发生这样的事情:‘太阳会暗淡,月亮不再发光,
25 nyota zitaanguka kutoka angani, na nguvu zilizoko mbinguni zitatikisika.
众星从天空陨落,天之力量被动摇。’
26 Ndipo watakapomwona Mwana wa Adamu akija mawinguni kwa nguvu kubwa na utukufu.
届时,他们将看到人子携伟大的力量和荣光,驾云降临。
27 Ndipo atatuma malaika zake na atawakusanya pamoja wateule wake kutoka pande kuu nne za dunia, kutoka mwisho wa dunia mpaka mwisho wa mbingu.
他会派出天使,把从极地到天涯的天选之子大批召集而来。
28 Kwa mtini jifunzeni. Kama tawi liwezavyo kutoa na kuweka haraka majani yake, ndipo mtajua kwamba kiangazi kiko karibu.
要学习无花果树,当树枝发出嫩芽并长出叶子,你们便知道夏天已来。
29 Ndivyo ilivyo, mtakapoona mambo haya yakitokea, jueni kwamba yuko karibu, na malango.
同样,当你们看到这些事发生,就知道必须发生的事情已经来到,就在你的门口!
30 Kweli, nawambieni, hiki kizazi hakitapita mbali kabla mambo haya hayajatokea.
告诉你们实话,这一切必将发生,然后这个世界才会过去。
31 Mbingu na nchi zitapita, lakini maneno yangu hayatapita kamwe.
天地都将走向终结,但我的教诲不会消失。
32 Lakini kuhusu siku hiyo au saa, hakuna ajuaye, hata malaika wa mbinguni, wala Mwana, ila Baba.
发生这种事情时,无人再知晓日子或是时间,甚至连天使或人子都不知情,只有天父知道。
33 Iweni macho, Tazama, kwa sababu hamjui ni muda gani yatatokea. (Zingatia: Mstari huu, “Muwe waangalifu, Tazameni na ombeni kwa sababu...” haumo kwenye nakala za kale).
要小心!保持清醒!你们不知道那一天何时来临。
34 Ni kama mtu anayeenda safarini: akaacha nyumba yake, na kumweka mtumwa wake kuwa mtawala wa nyumba, kila mmoja na kazi yake. Na kumwamuru mlinzi kukaa macho.
这就像一个人要出外远行,唤自己的仆人来,把产业交给他们,告诉每个仆人该做什么,然后离开。他还提醒看门人要保持清醒。
35 Kwa hiyo iweni macho! Kwani hamjui ni lini bwana wa nyumba atakaporudi nyumbani, yawezekana ni jioni, usiku wa manane, wakati jogoo atakapowika, au asubuhi.
所以要警醒,因为你们不知道主人何时回来,也许黄昏、也许夜半、也许是黎明、也许清晨。
36 Kama akija ghafla, asikukute umelala.
你肯定不愿意在他忽然回来时,发现你们正在睡觉。
37 Kile nikisemacho kwako nakisema kwa kila mtu: Kesheni”!
我对你们所说的一切,也对众人说过,‘保持警惕!’”

< Marko 13 >