< Marko 13 >

1 Yesu alipokuwa akitembea kutoka hekaluni, mmoja wa wanafunzi wake akamwuliza, “Mwalimu, tazama mawe haya yakushangaza na majengo!”
YA anae jumuyong gui templo; ilegña nu güiya uno gui disipuluña: Maestro, liija na jechuran acho, yan guma sija.
2 Akamwambia, Unaona majengo haya makubwa? Hakuna hata jiwe moja litakalo salia juu ya jingine ambalo halitaangushwa chini”.
Ya si Jesus manope ilegña nu sija: Unlie este sija na mandangculon guma? taya usobbla ni un acho gui jilo y otro, na ti umayute papa.
3 Naye alipokuwa amekaa juu ya Mlima wa Mizeituni nyuma ya hekalu, Petro, Yakobo, Yohana na Andrea wakamwuliza kwa siri,
Ya anae matachong gui jilo y finabeca na y naanña Olibo, gui menan y templo, finaesen gui secreto as Pedro, yan Santiago, yan si Juan, yan si Andres,
4 “Tuambie, mambo haya yatakuwa lini? Ni nini dalili ya mambo haya kutokea?”
Ilegñija: Sanganejam, ngaean estesija ufanmato? yan jafa na señat yanguin para todo estesija nae ufanmacumple?
5 Yesu alianza kuwaambia, “Kuweni makini kwamba mtu yoyote asiwapotoshe.
Si Jesus jatutujon ilegña nu sija: Adaje jamyo, ya chamiyo fanmafabababa.
6 Wengi watakuja kwa jina langu wakisema, 'Mimi ndiye', na watawapotosha wengi.
Sa megae ufanmato pot y naanjo, ya ualog: Guajo güiya Jesucristo, ya ufababa megae.
7 Mtakaposikia vita na tetesi za vita, msiogope; mambo haya hayana budi kutokea, lakini mwisho bado.
Yanguin injingog y guera, yan y masangan y guera: chamiyo ninafañachatsaga: sa nesesita estesija jumuyong: lao trabia ti y jinecog.
8 Taifa litainuka kinyume na taifa jingine, na ufalme kinyume na ufalme. Patakuwa na matetemeko sehemu mbalimbali, na njaa. Huu ni mwanzo wa utungu.
Sa y nasion sija ufangajulo contra y nasion, yan y raeno contra raeno: ya uguaja linao gui megae na lugat ya uguaja ñinalang: estesija tutujon y pinite.
9 Iweni macho. Watawapeleka hadi mabarazani, na mtapingwa katika masinagogi. Mtasimamishwa mbele ya watawala na wafalme kwa ajili yangu, kama ushuhuda kwao.
Lao adaje jamyo: sa infanmaentrega gui tribunal sija; ya infanmasaulag gui sinagoga: yan infanojgue gui menan y manmagas sija yan y ray sija, pot causa de guajo para un testimonio contra sija.
10 Lakini injili lazima kwanza ihubiriwe kwa mataifa yote.
Ya y ibangelio nesesita umapredica finenana gui entre todo y nasion.
11 Watakapo wakamata na kuwakabidhi, msiogope kuhusu kile mtakachosema. Ndani ya muda huo, mtapewa nini cha kusema; hamtakuwa ninyi mtakaoongea, bali Roho Mtakatifu.
Lao anae maconejamyo, ya maentregajamyo, chamiyo jumajaso jafa para insangan, ni injasuye jafa: sa jafaja y manaejamyo güije na ora, ayoja insangan: sa ti jamyo infangcuentos, na y Espiritu Santo.
12 Ndugu atamshitaki ndugu kuuawa, baba na mtoto wake. Watoto watasimama kinyume cha baba zao na kuwasababisha kuuawa.
Pago y laje uentrega y cheluña laje, para umapuno; ya y tata y lajiña: ya y famaguon ufangajulo contra y mañaenanñija: ya uuafanmapuno.
13 Mtachukiwa na kila mtu kwa sababu ya jina langu. Lakini atakayevumilia mpaka mwisho, mtu huyo ataokoka.
Ya jamyo infanmachatlie ni todo y taotao sija, pot y naanjo: lao jaye y sumungon asta y uttimo, umasatba.
14 Mtakapoona chukizo la uharibifu limesimama pale lisipotakiwa kusimama (asomaye na afahamu), ndipo walioko ndani ya Yuda wakimbilie milimani,
Lao anae inlie y chinatlie y inginon na yinilang tumotojgue gui anae ti para utojgue, (y mananaetae utungo) ayo sija y mangaegue guiya Judea ufanmalago para y jalomtano:
15 naye aliyeko juu ya nyumba asishuke chini ya nyumba, au kuchukua chochote kilichoko nje,
Ya y gaegue gui jilo guma, chaña tumutunog ni ujalom ya ufañule jafa na güinaja gui jalom gumaña.
16 na aliyeko shambani asirudi kuchukua vazi lake.
Ya y gaegue gui fangualuan, chaña tumatalo tate para uchule y magaguña.
17 Lakini ole wao wanawake wenye mimba na wanyonyeshao katika siku hizo!
Lao mannamaase ayo sija y manmapotgue yan y mannanasusu, güije sija na jaane!
18 Ombeni kwamba isitokee wakati wa baridi.
Fanmanaetae, ya munga y jinanaomiyo gui tiempon y manenggeng.
19 Kwani patakuwa na mateso makubwa, ambayo hayajawahi kutokea, tangu Mungu alipoumba ulimwengu, mpaka sasa, hapana, wala haitatokea tena.
Sa ayo sija na jaane, uguaja pininite, ni y taya nae guaja desde y matutujon y tano, anae jafatinas si Yuus, asta pago; ni uguaja asta jinecog.
20 Mpaka Bwana atakapopunguza siku, hakuna mwili utakaookoka, lakini kwa ajili ya wateule, atakaowachagua, atapunguza namba za siku.
Lao yaguin ti janacadada y Señot ayo sija na jaane, taya catne usatba: lao pot y rason y manmaayigja, ni y inayigña, janacadada ayo sija na jaane.
21 Wakati huo kama mtu yeyote atawaambia, Tazama, Kristo yuko hapa!' au 'Tazama, yuko pale!' msiamini.
Ya yanguin guaja umalog nu jago: Estagüe si Cristo: pat ayogüe guato; chamiyo jumojonggue.
22 Kwani Wakristo wa uongo na manabii wa uongo watatokea na watatoa ishara na maajabu, ili kwamba, wawadanganye, yamkini hata wateule.
Sa ufangajulo sija ti manmagajet na Cristo sija, yan ti manmagajet na profeta sija, ya ufanmamanue sija señat yan mannamanman, para ufanmamababa, yanguin janasiña, asta y manmaayig.
23 Iweni macho! Nimekwisha wambia haya yote kabla ya wakati.
Lao adaje jamyo: Sa estagüeja, na jusangane jamyo todos antes.
24 Lakini baada ya mateso ya siku hizo, jua litatiwa giza, mwezi hautatoa mwanga wake,
Lao ayo sija na jaane an munjayan y pininite sija; ujomjom y atdao, ya y pilan ti ufanina,
25 nyota zitaanguka kutoka angani, na nguvu zilizoko mbinguni zitatikisika.
Ya y pution sija gui langet ufamodong, ya y ninasifia sija gui langet ufanmayengyong.
26 Ndipo watakapomwona Mwana wa Adamu akija mawinguni kwa nguvu kubwa na utukufu.
Ya ayo nae ujalie y Lajin taotao na mamamaela gui sanjalom mapagajes, yan y dangculon ninasiñaña yan y minalagña.
27 Ndipo atatuma malaika zake na atawakusanya pamoja wateule wake kutoka pande kuu nne za dunia, kutoka mwisho wa dunia mpaka mwisho wa mbingu.
Ya ayonae utago y angjetña sija na ujarecoje y inayigña sija, guinen y cuatro na manglo, guinen y uttimon y tano asta y uttimon y langet.
28 Kwa mtini jifunzeni. Kama tawi liwezavyo kutoa na kuweka haraka majani yake, ndipo mtajua kwamba kiangazi kiko karibu.
Tingo y acomparasion y trongcon igos; Anae mamaulegja trabia y ramasña, ya manjajagonja, intingoja na esta jijijot y tiempon maepe.
29 Ndivyo ilivyo, mtakapoona mambo haya yakitokea, jueni kwamba yuko karibu, na malango.
Jamyo locue anae inlie estesija, na manmato, tingoja na güiya esta jijijot, parejoja yan esta gaegue gui petta.
30 Kweli, nawambieni, hiki kizazi hakitapita mbali kabla mambo haya hayajatokea.
Magajet jusangane jamyo: Este na generasion ti ufanmalofan, asta que todo estesija munjayan manmachogüe.
31 Mbingu na nchi zitapita, lakini maneno yangu hayatapita kamwe.
Y langet yan y tano, ufanmalofan, lao y sinanganjo ti ufalofan.
32 Lakini kuhusu siku hiyo au saa, hakuna ajuaye, hata malaika wa mbinguni, wala Mwana, ila Baba.
Lao ayo na jaane pat ayo na ora, taya ni un taotao tumungo; ni y angjet sija ni mangaegue gui langet, ni y Laje; na y Tata güiyaja.
33 Iweni macho, Tazama, kwa sababu hamjui ni muda gani yatatokea. (Zingatia: Mstari huu, “Muwe waangalifu, Tazameni na ombeni kwa sababu...” haumo kwenye nakala za kale).
Adaje jamyo: fanbela, ya infanmanaetae: sa ti intingo ngaean y tiempo.
34 Ni kama mtu anayeenda safarini: akaacha nyumba yake, na kumweka mtumwa wake kuwa mtawala wa nyumba, kila mmoja na kazi yake. Na kumwamuru mlinzi kukaa macho.
Say y Lajin taotao, parejoja yan un taotao ni y jumajanao chago ya jadingo y gumaña; ya janae y tentagoña ninasiñañija yan cada uno y chechoña, ya jatago y pottero na ufanbela.
35 Kwa hiyo iweni macho! Kwani hamjui ni lini bwana wa nyumba atakaporudi nyumbani, yawezekana ni jioni, usiku wa manane, wakati jogoo atakapowika, au asubuhi.
Fanbela, sa ti intingo ngaean nae ufato y magas y guima; cao y pupuenge, pat y tatalopuenge, pat y oogayo, pat y egaan;
36 Kama akija ghafla, asikukute umelala.
Na, noseaja derepente ufato, ya infansineda manmamaego.
37 Kile nikisemacho kwako nakisema kwa kila mtu: Kesheni”!
Ya jafa y jusangane jamyo, jusanganeja todos: Fanbela.

< Marko 13 >