< Marko 12 >

1 Kisha Yesu alianza kuwafundisha kwa mifano. Akasema, “Mtu alipanda shamba la mizabibu, akalizungushia uzio, na akachimba shimo la kusindika mvinyo. Akajenga mnara na kisha akalipangisha shamba la mizabibu kwa wakulima wa mizabibu. Kisha alisafiri safari ya mbali.
И почна да им говори с притчи: Един човек насади лозе, огради го с плет, изкопа лин, и съгради кула, и даде го под наем на земеделците, и отиде в чужбина.
2 Wakati ulipofika, alimtuma mtumishi kwa wakulima wa mizabibu kupokea kutoka kwao baadhi ya matunda ya shamba la mizabibu.
И във времето на плода изпрати един слуга до земеделците да прибере от земеделците от плода на лозето.
3 Lakini walimkamata, wakampiga, na wakamfukuza bila chochote.
А те го хванаха, биха го, и го отпратиха празен.
4 Akamtuma kwao mtumishi mwingine, wakamjeruhi kichwani na kumtendea mambo ya aibu.
Пак изпрати до тях друг слуга; и нему счупиха главата, и безсрамно го оскърбиха.
5 Bado alimtuma mwingine, na huyu mmoja walimwua. Waliwatendea wengine wengi mambo kama hayo hayo, wakiwapiga na wengine kuwaua.
Изпрати и друг, когото убиха; и мнозина други, от които едни биха, а други убиха.
6 Alikuwa bado na mtu mmoja zaidi wa kumtuma, mwana mpendwa. Naye alikuwa wa mwisho aliyetumwa kwao. Akisema, “Watamheshimu mwanangu”.
Още един имаше той, един възлюбен син; него изпрати последен до тях, като думаше, Ще почетат сина ми.
7 Lakini wapangaji walisemezana wao kwa wao, “Huyu ndiye mrithi. Njoni, hebu na tumwue, na urithi utakuwa wetu.”
А тия земеделци рекоха помежду си: Тоя е наследникът; елате да го убием, и наследството ще бъде наше.
8 Walimvamia, wakamuua na kumtupa nje ya shamba la mizabibu.
И тъй, хванаха го и го убиха, хвърлиха го вън от лозето.
9 Kwa hiyo, Je! Atafanya nini mmiliki wa shamba la mizabibu? Atakuja na kuwaangamiza wakulima wa mizabibu na atalikabidhi shamba la mizabibu kwa wengine.
Какво, прочее, ще стори стопанинът на лозето? Ще дойде и ще погуби тия земеделци, а лозето ще даде на други.
10 Hamjapata kusoma andiko hili? “Jiwe ambalo wajenzi walilikataa, limekuwa jiwe la pembeni.
Не сте ли прочели нито това писание: - "Камъкът, който отхвърлиха зидарите, Той стана глава на ъгъла,
11 Hili lilitoka kwa Bwana, na ni la ajabu machoni petu.”
от Господа е това, и чудно е в нашите очи?"
12 Walitafuta kumkamata Yesu, Lakini waliwaogopa makutano, kwani walijua kuwa alikuwa amenena mfano huo dhidi yao. Hivyo walimwacha na wakaenda zao.
И първенците искаха да Го хванат (но се побояха от народа), понеже разбраха, че за тях изрече тая притча. И оставиха Го и си отидоха.
13 Kisha wakawatuma baadhi ya mafarisayo na maherodia kwake ili kumtega kwa maneno.
Тогава пращат при Него някои от фарисеите и иродианите за да Го впримчат в говоренето Му.
14 Walipofika, wakamwambia, “Mwalimu, tunajua kwamba hujali maoni ya yeyote na huonyeshi upendeleo kati ya watu. Unafundisha njia ya Mungu katika ukweli. Je! Ni haki kulipa kodi kwa Kaisari au la? Je! Twaweza kulipa au la?
И те, като дойдоха, казаха Му: Учителю, знаем, че си искрен и не Те е грижа от никого; защото не гледаш на лицето на човеците, но учиш Божия път според истината. Право ли е да даваме данък на Кесаря, или не?
15 Lakini Yesu alijua unafiki wao na kuwaambia, “Kwa nini mnanijaribu? Nipeni dinari niweze kuitazama.”
Да даваме ли, или да не даваме? А Той, като разбра лицемерието им, рече им: Защо Ме изпитвате? Донесете ми един пеняз да го видя.
16 Wakaleta moja kwa Yesu, Akawaambia, “Je! ni sura ya nani na maandishi yaliyopo hapa ni ya nani? Wakasema, “Ya Kaisari.”
И те Му донесоха. Тогава им казва: Чий е тоя образ и надпис? А те му рекоха: Кесарев.
17 Yesu akawaambia, “Mpeni Kaisari vitu vya Kaisari na Mungu vitu vya Mungu.” Wakamstaajabia.
Исус им рече: Отдавайте Кесаревото на Кесаря, и Божието на Бога. И те много се зачудиха на Него.
18 Kisha Masadukayo, wasemao hakuna ufufuo, walimwendea. Wakamuwuliza, wakisema,
След това дохождат при Него садукеи, които казват, че няма възкресение; и питат Го, казвайки:
19 “Mwalimu, Musa alituandikia kuwa, 'Ikiwa ndugu ya mtu akifa na kumwacha mke nyuma yake, lakini hakuacha mtoto, mtu atamchukua mke wa ndugu yake, na kujipatia watoto kwa ajili ya ndugu yake.'
Учителю, Мойсей ни написа, че ако някому умре брат и остави жена, а чадо не остави, то брат му да вземе жена му и да въздигне потомък на брата си.
20 Kulikuwa na ndugu saba, wa kwanza alitwaa mke na kisha akafa, hakuacha watoto.
Прочее, имаше седем братя; и първият взе жена; и когато умря не остави потомък.
21 Kisha wa pili alimchukua naye akafa, hakuacha watoto. Na wa tatu hali kadhalika.
Взе я и вторият, умря, и не остави потомък; също и третият.
22 Na wa saba alikufa bila kuacha watoto. Mwishowe na mwanamke pia akafa.
И седмината не оставиха потомство. А подир всички умря и жената.
23 Wakati wa ufufuo, watakapofufuka tena, Je! Atakuwa mke wa nani? Kwani wale ndugu wote saba walikuwa waume wake.”
Във възкресението, на кого от тях ще бъде жена? Защото и седмината я имаха за жена.
24 Yesu aliwaambia, “Je! Hii si sababu kuwa mmepotoshwa, kwa sababu hamjui maandiko wala nguvu za Mungu?”
Исус им рече: Не затова ли се заблуждавате, понеже не знаете писанията, нито Божията сила?
25 Wakati wa kufufuka toka kwa wafu, hawataoa wala kuingia katika ndoa, bali watakuwa kama malaika wa mbinguni.
Защото когато възкръснат от мъртвите, нито се женят, нито се омъжват, но са като ангели на небесата.
26 Lakini, kuhusu wafu ambao wanafufuliwa, Je! Hamkusoma kutoka katika kitabu cha Musa, katika habari za kichaka, jinsi Mungu alivyosema na kumwambia, 'Mimi ni Mungu wa Abrahimu, na Mungu wa Isaka, na Mungu wa Yakobo?'
А за мъртвите, че биват възкресени, не сте ли чели в книгата на Мойсея, на мястото, при къпината, как Бог му говорй, казвайки: "Аз съм Бог Авраамов, Бог Исааков, и Бог Яковов"?
27 Yeye si Mungu wa wafu, bali wa walio hai. Ni dhahiri mmepotoka.”
Той не е Бог на мъртвите, а на живите. Вие много се заблуждавате.
28 Mmoja wa waandishi alikuja na kuyasikia mazungumzo yao; aliona kwamba Yesu aliwajibu vema. Alimwuliza, “Je! ni amri ipi iliyo ya muhimu zaidi katika zote?”
А един от книжниците, който дойде и ги чу, когато се препираха, като видя, че им отговори добре, пита Го: Коя заповед е първа от всички?
29 Yesu alimjibu, “Iliyo ya muhimu ni hii, “Sikia, Israeli, Bwana Mungu wetu, Bwana ni mmoja.
Исус отговори: Първата е: "Слушай, Израилю; Господ нашият Бог е един Господ;
30 Lazima umpende Bwana Mungu wako, kwa moyo wako yote, kwa roho yako yote, kwa akili yako yote, na kwa nguvu zako zote.'
и да възлюбиш Господа твоя Бог от цялото си сърце, с цялата си душа, с всичкия си ум и с всичката си сила".
31 Amri ya pili ni hii, 'Lazima umpende jirani yako kama unavyojipenda mwenyewe.' Hakuna amri nyingine kuu zaidi ya hizi.”
А ето втората [подобна на нея] заповед: "Да възлюбиш ближния си като себе си". Друга заповед по-голяма от тия няма.
32 Mwandishi akasema, “Vema Mwalimu! Umesema kweli kwamba Mungu ni mmoja, na kwamba hakuna mwingine zaidi yake.
И книжникът Му рече: Превъзходно, Учителю! Ти право каза, че Бог е един; и няма друг освен Него;
33 Kumpenda yeye kwa moyo wote, na kwa ufahamu wote na kwa nguvu zote, na kumpenda jirani kama mwenyewe, ni muhimu mno kuliko matoleo na dhabihu za kuteketeza.”
и да Го люби човек от все сърце, с всичкия си разум, и с всичката си сила, и да люби ближния си като себе си, това е много повече от всичките всеизгаряния и жертви.
34 Wakati Yesu alipoona ametoa jibu la busara, alimwambia, “Wewe hauko mbali na ufalme wa Mungu.” Baada ya hapo hakuna hata mmoja aliye thubutu kumwuliza Yesu maswali yoyote.
Исус, като видя, че отговори разумно, рече му: Не си далеч от Божието царство. И никой вече не дръзна да Му задава въпроси.
35 Na Yesu alijibu, wakati alipokuwa akifundisha katika hekalu, akasema, “Je! waandishi husemaje kuwa Kristo ni mwana wa Daudi?
И когато поучаваше в храма, Исус проговори казвайки: Как думат книжниците, че Христос е Давидов Син?
36 Daudi mwenyewe katika Roho Mtakatifu, alisema, 'Bwana alisema kwa Bwana wangu, keti katika mkono wangu wa kuume, mpaka niwafanye maadui wako kuwa chini ya miguu yako.'
Сам Давид каза чрез Святия Дух: - "Рече Господ на Моя Господ; Седи отдясно Ми, Докле положа враговете Ти за Твое подножие".
37 Daudi mwenyewe humwita Kristo, 'Bwana' Je! ni mwana wa Daudi kwa jinsi gani?” Na kusanyiko kuu lilimsikiliza kwa furaha.
Сам Давид го нарича Господ; тогава как да е негов син? И голямото множество Го слушаше с удоволствие.
38 Katika mafundisho yake Yesu alisema, “Jihadharini na waandishi, wanaotamani kutembea na kanzu ndefu na kusalimiwa kwenye masoko
И в поучението Си казваше: Пазете се от книжниците, които обичат да ходят пременени, и да приемат поздравите по пазарите,
39 na kuketi kwenye viti vya wakuu katika masinagogi na katika sikukuu kwa maeneo ya wakuu.
и първите столове по синагогите, и първите места при угощенията;
40 Pia wanakula nyumba za wajane na wanaomba maombi marefu ili watu wawaone. Hawa watu watapokea hukumu iliyo kuu.”
тия, които изпояждат домовете на вдовиците, даже когато за показ принасят дълги молитви. Тия ще приемат по-голямо осъждение.
41 Kisha Yesu aliketi chini karibu na sanduku la sadaka ndani ya eneo la hekalu; alikuwa akitazama watu waliokuwa wakitia pesa zao ndani ya sanduku. Watu wengi matajiri waliweka kiasi kikubwa cha pesa.
И като седна Исус срещу съкровищницата, гледаше как народът пускаше пари в съкровищницата; и мнозина богаташи пускаха много.
42 Kisha mwanamke mjane maskini alikuja na kutia vipande viwili, thamani ya senti.
А една бедна вдовица дойде и пусна две лепти, сиреч, един кодрант.
43 Kisha akawaita wanafunzi wake na kuwaambia, “Amini nawaambia, mwanamke huyu mjane ametia kiasi kikubwa zaidi ya wote ambao wameshatoa katika sanduku la sadaka.
И повика учениците Си и каза им: Истина ви казвам, тая бедна вдовица пусна повече от всичките, които пускат в съкровищницата;
44 Kwani wote wametoa kutokana na wingi wa mapato yao. Lakini mwanamke mjane huyu, kutoka katika umaskini wake, katia pesa yote ambayo alipaswa kuitumia kwa maisha yake.”
защото те всички пускат от излишъка си, а тя от немотията си пусна всичко що имаше, целия си имот.

< Marko 12 >