< Luka 8 >

1 Ilitokea muda mfupi baadaye kwamba Yesu alianza kusafiri katika miji na jiji mbalimbali, akihubiri na kutangaza habari njema ya ufalme wa Mungu na wale kumi wawili walikwenda pamoja naye,
And it came to passe afterwarde, that hee himselfe went through euery citie and towne, preaching and publishing the kingdome of God, and the twelue were with him,
2 vilevile wanawake fulani waliokuwa wameponywa kutoka kwa roho wachafu na magonjwa mbalimbali. Walikuwa ni Mariamu aliyeitwa Magdalena ambaye alikuwa ametolewa pepo saba.
And certaine women, which were healed of euill spirites, and infirmities, as Mary which was called Magdalene, out of whom went seuen deuils,
3 Yoana mke wa Kuza na meneja wa Herode, Susana, na wanawake wengine wengi, waliotoa mali vyao kwa ajili yao wenyewe.
And Ioanna the wife of Chuza Herods steward, and Susanna, and many other which ministred vnto him of their substance.
4 Nabaada ya umati wa watu kukusanyika pamoja, wakiwemo na watu waliokuja kwake kutoka miji mbalimbali, akazungumza nao kwa kutumia mifano.
Nowe when much people were gathered together, and were come vnto him out of all cities, he spake by a parable.
5 “mpandaji alienda kupanda mbegu, alipokuwa apanda, baadhi ya mbegu hizo ziliangukia kando ya njia zikakanyagwa chini ya miguu, na ndege wa angani wakazila.
A sower went out to sowe his seede, and as he sowed, some fell by the wayes side, and it was troden vnder feete, and the foules of heauen deuoured it vp.
6 Mbegu zingine zilianguka juu ya udongo wa miamba na zilipoota na kuwa miche zilipooza kwa sababu hakukuwa na unyevunyevu.
And some fell on the stones, and when it was sprong vp, it withered away, because it lacked moystnesse.
7 Mbegu zingine ziliangukia kwenye miti ya miiba, nayo hiyo miti ya miiba ikakua pamoja na zile mbegu na zikasongwa.
And some fell among thornes, and the thornes sprang vp with it, and choked it.
8 Lakini mbegu zingine ziliangukia kwenye udongo unaofaa na zikazaa mazao mara mia zaidi. “Baada ya Yesu kusema mambo haya, alipaza sauti,”Yeyote aliye na masikio ya kusikia na asikie.”
And some fell on good ground, and sprang vp, and bare fruite, an hundreth folde. And as hee sayd these things, he cryed, He that hath eares to heare, let him heare.
9 Tena wanafunzi wake wakamuuliza maana ya mfano huo,
Then his disciples asked him, demaunding what parable that was.
10 Yesu akawaambia, “Mmepewa upendeleo wa kujua siri ya ufalme wa Mungu, lakini watu wengine watafundishwa tu kwa mifano, ili kwamba 'wakiona wasione na wakisikia wasielewe.'
And he sayd, Vnto you it is giuen to know the secrets of ye kingdome of God, but to other in parables, that when they see, they shoulde not see, and when they heare, they should not vnderstand.
11 Na hii ndiyo maana ya mfano huu. Mbegu ni neno la Mungu.
The parable is this, The seede is the worde of God.
12 Mbegu zile zilizoanguka kando kando ya njia ndiyo wale watu wanaolisikia neno, na baadaye mwovu shetani hulichukua mbali kutoka moyoni, ili kwamba wasiamini na kuokolewa.
And they that are beside the way, are they that heare: afterward commeth the deuill, and taketh away the worde out of their hearts, least they should beleeue, and be saued.
13 Kisha na zile zilizoangukia kwenye mwamba ni watu wale wanaosikia neno na kulipokea kwa furaha lakini hawana mizizi yeyote, wanaamini tu kwa muda mfupi, na wakati wa majaribu huanguka.
But they that are on the stones, are they which when they haue heard, receiue ye word with ioy: but they haue no rootes: which for a while beleeue, but in the time of tentation goe away.
14 Na mbegu zile zilizoangukia kwenye miiba ni watu wanaosikia neno, lakini wanapoendelea kukua husongwa na huduma na utajiri na ubora wa maisha haya na hawazai matunda.
And that which fell among thornes, are they which haue heard, and after their departure are choked with cares and with riches, and voluptuous liuing, and bring forth no fruite.
15 Lakini zile mbegu zilizoangukia kwenye udongo mzuri ni wale watu, ambao ni wanyeyekevu na mioyo mizuri, baada ya kulisikia neno hulishikilia na likawa salama na kuazaa matunda ya uvumilivu.
But that which fell in good ground, are they which with an honest and good heart heare the worde, and keepe it, and bring forth fruite with patience.
16 Sasa, hakuna hata mmoja, anayewasha taa na kuifunika kwa bakuli au kuiweka chini ya kitanda. Badala ya kuiweka kwenye kinara cha taa ili kwamba kila mmoja anayeingia apate kuiona.
No man when he hath lighted a candle, couereth it vnder a vessell, neither putteth it vnder the bed, but setteth it on a candlesticke, that they that enter in, may see the light.
17 Kwa kuwa hakuna kitakachojificha ambacho hakitajulikana, au chochote kilicho sirini ambacho hakitajulikana kikiwa kwenye mwanga.
For nothing is secret, that shall not be euident: neither any thing hid, that shall not be knowen, and come to light.
18 kwa hiyo kuwa makini unapokuwa unasikiliza. Kwa sababu aliye nacho, kwake ataongezewa zaidi, lakini asiye nacho hata kile kidogo alicho nacho kitachukuliwa.”
Take heede therefore how ye heare: for whosoeuer hath, to him shall be giuen: and whosoeuer hath not, from him shalbe taken euen that which it seemeth that he hath.
19 baadaye mama yake Yesu na ndugu zake wakaja kwake hawakaribia kwa sababu ya umati wa watu.
Then came to him his mother and his brethren, and could not come neere to him for the preasse.
20 Na akataarifiwa, “Mama yako na ndugu zako wako pale nje wanahitaji kukuona wewe.
And it was tolde him by certaine which said, Thy mother and thy brethren stand without, and would see thee.
21 Lakini, Yesu akajibu akasema “Mama yangu na ndugu zangu ni wale wanaolisikia neno la Mungu na kulitii.”
But he answered, and sayd vnto them, My mother and my brethren are these which heare the worde of God, and doe it.
22 Ilitokea siku moja kati ya siku zile Yesu na wanafunzi wake alipanda kwenye mtumbwi, na akawaambia, “Na tuvuke ng'ambo ya pili ya ziwa.” Wakaandaa mashua yao.
And it came to passe on a certaine day, that he went into a ship with his disciples, and he sayd vnto them, Let vs goe ouer vnto the other side of the lake. And they lanched forth.
23 Lakini walipoanza kuondoka, Yesu akalala usingizi, na dhoruba kali yenye upepo, na mashua yao ikaanza kujaa maji na walikuwa kwenye katika kubwa sana.
And as they sayled, he fell a sleepe, and there came downe a storme of winde on the lake, and they were filled with water, and were in ieopardie.
24 baadaye wanafunzi wake wakaja kwake na kumwamsha, wakisema, “Bwana mkubwa! Bwana mkubwa! tuko karibu kufa!” Akaamka na akaukemea upepo na mawimbi ya maji vikatulia na kukawa na utulivu.
Then they went to him, and awoke him, saying, Master, Master, we perish. And he arose, and rebuked the winde, and the waues of water: and they ceased, and it was calme.
25 Tena akawaambia, “Imani yenu iko wapi?” Wakaogopa, Walishangaa, wakasemezana kia mmoja na mwenzake,”Huyu ni nani, kiasi kwamba anaamuru hata upepo, na maji na humtii?”
Then he sayde vnto them, Where is your fayth? and they feared, and wondered among them selues, saying, Who is this that commandeth both the windes and water, and they obey him!
26 Wakafika kwenye mji wa Gerasini iliyo upande wa nyuma ya Galilaya.
So they sailed vnto the region of the Gadarenes, which is ouer against Galile.
27 Yesu aliposhuka na kukanya kwenye ardhi, mtu fulani kutoka mjini, akakutana naye, na huyu mtu alikuwa na nguvu za giza. Kwa muda mrefu alikuwa havai nguo, na alikuwa haishi kwenye Nyumba, lakini aliishi kwenye makaburi.
And as he went out to land, there met him a certaine man out of the citie, which had deuils long time, and he ware no garment, neither abode in house, but in the graues.
28 Alipomwona Yesu akalia kwa sauti, na akaanguka chini mbele yake. kwa sauti kubwa akisema, Nimefanya nini kwako, Yesu mwana wa Mungu aliye juu? Nakusihi, Usiniadhibu mimi”
And when he sawe Iesus, he cryed out and fell downe before him, and with a loude voyce sayd, What haue I to doe with thee, Iesus the Sonne of God the most High? I beseech thee torment me not.
29 Yesu akaamuru roho chafu imtoke mtu yule, kwa kuwa mara nyingi amepamgaa. hata kama alikuwa amefungwa minyororo na kubanwa na kuwekwa chini ya ulinzi, alivunja vifungo na kuendeshwa na mapepo mpaka jangwani.
For he commanded ye foule spirit to come out of the man: (for oft times he had caught him: therefore he was bound with chaines, and kept in fetters: but he brake the bands, and was caried of the deuill into wildernesses.)
30 Yesu akamwuliza, “Jina lako nani?” akajibu akisema, “Legioni” Kwa maana mapepo mengi yameingia kwake.
Then Iesus asked him, saying, What is thy name? and he sayd, Legion, because many deuils were entred into him.
31 Wakaendelea kumsihi usituamuru twende kwenye shimo. (Abyssos g12)
And they besought him, that he would not commaund them to goe out into the deepe. (Abyssos g12)
32 Kundi la Nguruwe lilikuwa likichunga juu ya kilima, wakamsihi awaruhusu wakaingie kwa hao nguruwe. Na akawaruhusu kufanya hivyo.
And there was there by, an hearde of many swine, feeding on an hill: and the deuils besought him, that he would suffer them to enter into them. So he suffered them.
33 kwa hiyo wale mapepo wakamtoka mtu yule na kuingia kwa wale nguruwe, na lile kundi likakimbia kwenye mwinuko wa mlima mpaka ziwani na wakazama humo.
Then went the deuils out of the man, and entred into the swine: and the hearde was caried with violence from a steepe downe place into the lake, and was choked.
34 wale watu waliokuwa wanachunga wale nguruwe walipoona kilichotokea, wakakimbia na wakatoa taarifa pale mjini na nje katika miji iliyowazunguka.
When the heardmen sawe what was done, they fled: and when they were departed, they tolde it in the citie and in the countrey.
35 Watu waliposikia hayo walienda kuona kilichotokea, na wakaja kwa Yesu na wakamwona mtu ambaye mapepo yalikuwa yamemtoka. alikuwa amevaa vizuri na mwenye akili timamu, amekaa kwenye miguu ya Yesu, na waliogopa.
Then they came out to see what was done, and came to Iesus, and found the man, out of whom the deuils were departed, sitting at the feete of Iesus, clothed, and in his right minde: and they were afrayd.
36 ndipo mmoja wao aliyeona kilichotokea alianza kuwasimlia wengine jinsi huyu mtu aliyekuwa anaongozwa na mapepo alivyoponywa.
They also which saw it, tolde them by what meanes he that was possessed with the deuill, was healed.
37 Watu wote wa mkoa wa Wagerasi na maeneo yaliyozunguka walimwomba Yesu aondoke kwao kwa sababu walikuwa na hofu kuu. Na aliingia kwenye mtumbwi ili arudi.
Then the whole multitude of the countrey about the Gadarenes, besought him that he would depart from them: for they were taken with a great feare: and he went into the ship, and returned.
38 Mtu yule aliyetokwa na pepo alimsihi Yesu kwenda naye, lakini Yesu alimwambia aende na kusema,
Then the man, out of whome the deuils were departed, besought him that hee might be with him: but Iesus sent him away, saying,
39 “Rudi kwenye nyumba yako na uhesabu yale yote ambayo Mungu amekutendea” Huyu mtu aliondoka, akitangaza pote katika mji wote yale yote ambayo Yesu aliyofanya kwa ajili yake.
Returne into thine owne house, and shewe what great things God hath done to thee. So hee went his way, and preached throughout all the citie, what great things Iesus had done vnto him.
40 Na Yesu akarudi, makutano wakamkaribisha, kwa sababu wote walikuwa wanamngoja.
And it came to passe, when Iesus was come againe, that the people receiued him: for they all waited for him.
41 Tazama akaja mtu mmoja anaitwa Yairo ni mmoja kati ya viongozi katika sinagogi. Yairo akaanguka miguuni pa Yesu na kumsihi aende nyumbani kwake,
And beholde, there came a man named Iairus, and he was the ruler of the Synagogue, who fell downe at Iesus feete, and besought him that he would come into his house.
42 kwa sababu alikuwa na mtoto msichana mmoja tu, mwenye umri wa miaka kumi na wibili, na alikuwa katika hali ya kufa. Na alipokuwa akienda, makutano walikuwa wakisongama dhidi yake.
For he had but a daughter onely, about twelue yeeres of age, and she lay a dying (and as he went, the people thronged him.
43 Mwanamke mwenye kutokwa damu kwa miaka kumi na miwili alikuwa pale na alitumia pesa zote kwa waganga, lakini hakuna aliyemponya hata mmoja,
And a woman hauing an yssue of blood, twelue yeeres long, which had spent all her substance vpon physicians, and could not be healed of any:
44 alikuja nyuma ya yesu na kugusa pindo la vazi lake, na ghafla kutokwa damu kukakoma.
When she came behind him, she touched the hemme of his garment, and immediatly her yssue of blood stanched.
45 Yesu akasema, “Nani ambaye kanigusa?” Walipokataa wote, Petro akasema, Bwana Mkubwa, umati wa watu wanakusukuma na wanakusonga.”
Then Iesus sayd, Who is it that hath touched me? When euery man denied, Peter sayd and they that were with him, Master, the multitude thrust thee, and tread on thee, and sayest thou, Who hath touched me?
46 Lakini Yesu akasema, “Mtu mmoja alinigusa, maana nilijua nguvu zimetoka kwangu.”
And Iesus sayde, Some one hath touched me: for I perceiue that vertue is gone out of me.
47 Mwanamke alipoona ya kuwa hawezi kuficha alichokifanya, akaanza kutetemeka, akaanguka chini mbele za Yesu alitangaza mbele ya watu wote sababu zilizofanya amguse na vile alivyoponywa gafla.
When the woman sawe that she was not hid, she came trembling, and fell downe before him, and tolde him before all the people, for what cause she had touched him, and how she was healed immediatly.
48 Kisha akasema kwake, “Binti, imani yako imekufanya uwe mzima. Enenda kwa Amani.”
And he said vnto her, Daughter, be of good comfort: thy faith hath saued thee: go in peace.)
49 Alipokuwa akiendelea kusema, mtu mmoja akaja kutoka kwenye nyumba ya kiongozi wa sinagogi, akisema, “Binti yako amefariki. Usimsumbue mwalimu.”
While he yet spake, there came one from the ruler of the Synagogues house, which sayde to him, Thy daughter is dead: disease not the Master.
50 Lakini Yesu aliposikia hivyo, alimjibu, “Usiogope. Amini tu, na ataokolewa.”
When Iesus heard it, he answered him, saying, Feare not: beleeue onely, and she shall be saued.
51 Kisha alipoingia kwenye hiyo nyumba, hakuruhusu mtu yeyote kuingia pamoja naye, isipokuwa Petro, Yohana na Yakobo, baba yake binti, na mama yake.
And when he went into the house, he suffered no man to goe in with him, saue Peter, and Iames, and Iohn, and the father and mother of the maide.
52 Sasa watu wote walikuwa wanaomboleza na kutoa sauti kwa ajili yake, lakini akasema, “Msipige kelele, hajafa, lakini amelala tu.”
And all wept, and sorowed for her: but he sayd, Weepe not: for she is not dead, but sleepeth.
53 Lakini wakamcheka kwa dharau, wakijua kuwa amekufa.
And they laught him to scorne, knowing that she was dead.
54 Lakini Yeye, akimshika binti mkono, akaita kwa sauti, akisema, “Mtoto, inuka”
So he thrust them all out, and tooke her by the hand, and cryed, saying, Maide, arise.
55 roho yake ikamrudia, na akainuka wakati huohuo. Akaamrisha kwamba, apewe kitu furani kwa ili ale.
And her spirite came againe, and she rose straightway: and he comanded to giue her meate.
56 Wazazi wake wakashangaa, lakini aliwaamuru wasimwambie mtu kilichokuwa kimetokea.
Then her parents were astonied: but hee commanded them that they should tell no man what was done.

< Luka 8 >