< Luka 5 >

1 Basi ilitokea wakati watu walipomkusanyikia na kumzunguka Yesu na kusikiliza neno la Mungu, ambapo alikuwa amesimama kando ya ziwa Genesareti.
Једанпут пак, кад народ належе к Њему да слушају реч Божију Он стајаше код језера генисаретског,
2 Aliona mashua mbili zimetia nanga pembeni mwa ziwa. Wavuvi walikuwa wametoka na walikuwa wakiosha nyavu zao.
И виде две лађе где стоје у крају, а рибари беху изишли из њих и испираху мреже:
3 Yesu akaingia katika mojawapo ya zile mashua, ambayo ilikuwa ya Simoni na kumwomba aipeleke majini mbali kidogo na nchi kavu. Kisha akakaa na kufundisha kutokea kwenye mashua.
И уђе у једну од лађа која беше Симонова, и замоли га да мало одмакне од краја; и седавши учаше народ из лађе.
4 kuongea, akamwambia Simoni, “Ipeleke mashua yako mpaka kwenye kilindi cha maji nakushusha nyavu zako ili kuvua samaki.”
А кад преста говорити, рече Симону: Хајде на дубину, и баците мреже своје те ловите.
5 Simon akajibu na kusema, Bwana, tumefanya kazi usiku wote, na hatukukamata chochote, lakini kwa neno lako, nitazishusha nyavu.
И одговарајући Симон рече Му: Учитељу! Сву ноћ смо се трудили, и ништа не ухватисмо: али по Твојој речи бацићу мрежу.
6 Walipofanya hivyo walikusanya kiasi kikubwa cha samaki na nyavu zao zikaanza kukatika.
И учинивши то ухватише велико мноштво риба, и мреже им се продреше.
7 Hivyo wakawaashiria washirika wao kwenye mashua nyingine ili waja na kuwasaidia. Walikuja wakazijaza mashua zote, kiasi kwamba zikaanza kuzama.
И намагоше на друштво које беше на другој лађи да дођу да им помогну; и дођоше, и напунише обе лађе тако да се готово потопе.
8 Lakini Simoni Petro, alipoona hivyo, alianguka magotini pa Yesu akisema,”Ondoka kwangu, kwa sababu mimi ni mtu mwenye dhambi Bwana.”
А кад виде Симон Петар, припаде ка коленима Исусовим говорећи: Изиђи од мене, Господе! Ја сам човек грешан.
9 Kwa sababu alishangazwa, na wote waliokuwa pamoja naye, kwa uvuvi wa samaki waliokuwa wameufanya.
Јер беше ушао страх у њега и у све који беху с њим од мноштва риба које ухватише;
10 Hili liliwajumuisha Yakobo na Yohana wana wa Zebedayo, ambao walikuwa washirika wa Simoni. Na Yesu akamwambia Simoni, “Usiogope, kwa sababu kuanzia sasa na kuendelea utavua watu.”
А тако и у Јакова и Јована, синове Зеведејеве, који беху другови Симонови. И рече Исус Симону: Не бој се; одселе ћеш људе ловити.
11 Walipokwishazileta mashua zao nchi kavu, waliacha kila kitu na kumfuata yeye.
И извукавши обе лађе на земљу оставише све, и отидоше за Њим.
12 Ilitokea kwamba alipokuwa katika mji mmojawapo, mtu aliyekuwa amejaa ukoma alikuwa huko. Wakati alipomuona Yesu, alianguka akiinamisha uso kwake mpaka chini na kumuomba, akisema, “Bwana, ikiwa unataka, waweza kunitakasa.”
И кад беше Исус у једном граду, и гле, човек сав у губи: и видевши Исуса паде ничице молећи Му се и говорећи: Господе! Ако хоћеш можеш ме очистити.
13 Kisha Yesu alinyoosha mkono wake na kumgusa, akisema, “Nataka. Takasika.” Na saa ileile ukoma ukamwacha.
И пруживши руку дохвати га се. И рече: Хоћу, очисти се. И одмах губа спаде с њега.
14 “Alimwagiza asimwambie mtu yeyote, lakini alimwambia, “Nenda zako, na ukajionyeshe kwa makuhani na utoe sadaka ya utakaso wako, sawasawa na kile Musa alichokiamuru, kwa ushuhuda kwao.”
И Он му заповеди да ником не казује: Него иди и покажи се свештенику, и принеси дар за очишћење своје, како је заповедио Мојсије за сведочанство њима.
15 Lakini habari kumuhusu yeye zikaenea mbali zaidi, na umati mkubwa wa watu ukaja pamoja kumsikiliza akifundisha na kuponywa magonjwa yao.
Али се глас о Њему још већма разлажаше, и мноштво народа стецаше се да Га слушају и да их исцељује од њихових болести.
16 Lakini mara kwa mara alijitenga faraghani na kuomba.
А Он одлажаше у пустињу и мољаше се Богу.
17 Ilitokea siku moja kati ya hizo siku alikuwa akifundisha, na walikuwapo Mafarisayo na waalimu wa sheria wamekaa hapo ambao walikuja wakitokea vijiji vingi tofauti katika mkoa wa Galilaya na Yudea, na pia kutokea katika mji wa Yerusalemu. Nguvu ya Bwana ilikuwa pamoja naye kuponya.
И један дан учаше Он, и онде сеђаху фарисеји и законици који беху дошли из свију села галилејских и јудејских и из Јерусалима; и сила Господња исцељиваше их.
18 watu kadhaa walikuja, wamembeba kwenye mkeka mtu aliyepooza, na wakatafuta njia ya kumwingiza ndani ili kumlaza chini mbele ya Yesu.
И гле, људи донесоше на одру човека који беше узет, и тражаху да га унесу и метну преда Њ;
19 Hawakupata njia ya kumwingiza ndani kwa sababu ya umati, hivyo walipanda juu ya paa la nyumba na kumshusha yule mtu chini kupitia kwenye vigae, juu mkeka wake katikati ya watu, mbele kabisa ya Yesu.
И не нашавши куда ће га унети од народа, попеше се на кућу и кроз кров спустише га с одром на среду пред Исуса.
20 Akiangalia imani yao, Yesu alisema, “Rafiki, dhambi zako umesamehewa.”
И видевши веру њихову рече му: Човече! Опраштају ти се греси твоји.
21 Waandishi na Mafarisayo waliaanza kuhoji hilo, wakisema, “Huyu ni nani anayeongea makufuru? Ni nani anaweza kusamehe dhambi ila Mungu pekee yake?”
И почеше помишљати књижевници и фарисеји говорећи: Ко је овај што хули на Бога? Ко може опраштати грехе осим једног Бога?
22 Lakini Yesu, akitambua nini walichokuwa wakifikiri, aliwajibu na kuwaambia, “Kwa nini mnaulizana hili mioyoni mwenu?
А кад разуме Исус помисли њихове, одговарајући рече им: Шта мислите у срцима својим?
23 Kipi ni rahisi kusema, 'Dhambi zako zimesamehewa' au kusema 'Simama utembee?'
Шта је лакше рећи: Опраштају ти се греси твоји? Или рећи: Устани и ходи?
24 Lakini mjue ya kwamba Mwana wa Adamu anayo mamlaka duniani ya kusamehe dhambi, Nakwambia wewe, 'Amka, chukua mkeka wako na uende nyumbani kwako.'”
Него да знате да власт има Син човечији на земљи опраштати грехе, (рече узетоме: ) теби говорим: устани и узми одар свој и иди кући својој.
25 Wakati huo huo akaamka mbele yao na akachukua mkeka wake aliokuwa ameulalia. Kisha akariudi nyumbani kwake akimtukuza Mungu.
И одмах устаде пред њима, и узе на чему лежаше, и отиде кући својој хвалећи Бога.
26 Kila mmoja alishangazwa na wakamtukuza Mungu. Walijawa na hofu, wakisema, “Tumeona mambo yasiyo ya kawaida leo.”
И сви се запрепастише, и хваљаху Бога, и напунивши се страха говораху: Чуда се нагледасмо данас!
27 Baada ya mambo haya kutokea, Yesu alitoka huko na akamwona mtoza ushuru aliyeitwa Lawi amekaa eneo la kukusanyia kodi. Akamwambia, “Nifuate.”
И потом изиђе, и виде цариника по имену Левија где седи на царини, и рече му: Хајде за мном.
28 Hivyo Lawi akanyanyuka na kumfuata, akiacha kila kitu nyuma.
И оставивши све, устаде и пође за Њим.
29 Kisha Lawi akaandaa nyumbani kwake karamu kubwa kwa ajili ya Yesu. Walikuwapo watozaushuru wengi kule na watu wengi walioketi mezani wakila pamoja nao.
И зготови Му Левије код куће своје велику част; и беше много цариника и других који сеђаху с Њим за трпезом.
30 Lakini Mafarisayo na waandishi wao walikuwa wakiwanung'unikia wanafunzi, wakisema, “Kwa nini mnakula na kunywa na watoza ushuru pamoja na watu wengine wenye dhambi?”
И викаху на Њега књижевници и фарисеји говорећи ученицима Његовим: Зашто с цариницима и грешницима једете и пијете?
31 Yesu akawajibu, “Watu walio katika afya njema hawahitaji tabibu, ni wale tu wanaoumwa ndiyo watakao mhitaji mmoja.
И одговарајући Исус рече им: Не требају здрави лекара него болесни.
32 Sikuja kuwaita watu wenye haki haki wapate kutubu, bali kuwaita wenye dhambi wapate kutubu.”
Ја нисам дошао да дозовем праведнике него грешнике на покајање.
33 Wakamwambia, “Wanafunzi wa Yohana mara nyingi hufunga na kuomba, na wanafunzi wa Mafarisayo nao hufanya vivyo hivyo. Lakini wanafunzi wako hula na kunywa.”
А они Му рекоше: Зашто ученици Јованови посте често и моле се Богу, тако и фарисејски; а твоји једу и пију?
34 Yesu akawaambia, “Inawezekana mtu yeyote akawafanya waliohudhuria harusi ya Bwana Arusi kufunga wakati Bwana Arusi bado yu pamoja nao?
А Он им рече: Можете ли сватове натерати да посте док је женик с њима?
35 Lakini siku zitakuja wakati Bwana Arusi atakapoondolewa kwao, ndipo katika siku hizo watafunga.”
Него ће доћи дани кад ће се отети од њих женик, и онда ће постити у оне дане.
36 Kisha Yesu aliongea pia kwao kwa mfano. “Hakuna anayechana kipande cha nguo kutoka kwenye vazi jipya na kukitumia kurekebisha vazi la zamani. Kama akifanya hivyo, ataichana nguo mpya, na kipande cha nguo kutoka vazi jipya kisengefaa kutumika na nguo ya vazi la zamani.
Каза им пак и причу: Нико не меће закрпе од нове хаљине на стару хаљину, иначе ће и нову раздрети, и старој не личи шта је од новог.
37 pia, hakuna mtu ambaye huweka divai mpya kwenye viriba vikuukuu. Kama akifanya hivyo, divai mpya ingepasua kile chombo, na divai ingemwagika, na viriba vingeharibika.
И нико не лије вино ново у мехове старе; иначе продре ново вино мехове и оно се пролије, и мехови пропадну;
38 Lakini divai mpya lazima iwekwe kwenye viriba vipya.
Него вино ново у мехове нове треба лити, и обоје ће се сачувати.
39 Na hakuna mtu baada ya kunywa divai ya zamani, hutataka mpya, kwa sababu husema, 'Ya zamani ni bora.”'
И нико пивши старо неће одмах новог; јер вели: Старо је боље.

< Luka 5 >