< Luka 5 >

1 Basi ilitokea wakati watu walipomkusanyikia na kumzunguka Yesu na kusikiliza neno la Mungu, ambapo alikuwa amesimama kando ya ziwa Genesareti.
Now while the multitude pressed on him and heard ha D'var Elohim · the Word of God·, he was standing by the lake of Gennesaret.
2 Aliona mashua mbili zimetia nanga pembeni mwa ziwa. Wavuvi walikuwa wametoka na walikuwa wakiosha nyavu zao.
He saw two boats standing by the lake, but the fishermen had gone out of them, and were washing their nets.
3 Yesu akaingia katika mojawapo ya zile mashua, ambayo ilikuwa ya Simoni na kumwomba aipeleke majini mbali kidogo na nchi kavu. Kisha akakaa na kufundisha kutokea kwenye mashua.
He entered into one of the boats, which was Simeon [Hearing]’s, and asked him to put out a little from the land. He sat down and taught the multitudes from the boat.
4 kuongea, akamwambia Simoni, “Ipeleke mashua yako mpaka kwenye kilindi cha maji nakushusha nyavu zako ili kuvua samaki.”
When he had finished speaking, he said to Simeon [Hearing], “Put out into the deep, and let down your nets for a catch.”
5 Simon akajibu na kusema, Bwana, tumefanya kazi usiku wote, na hatukukamata chochote, lakini kwa neno lako, nitazishusha nyavu.
Simeon [Hearing] answered him, “Master, we worked all night, and took nothing; but at your word I will let down the net.”
6 Walipofanya hivyo walikusanya kiasi kikubwa cha samaki na nyavu zao zikaanza kukatika.
When they had done this, they caught a great multitude of fish, and their net was breaking.
7 Hivyo wakawaashiria washirika wao kwenye mashua nyingine ili waja na kuwasaidia. Walikuja wakazijaza mashua zote, kiasi kwamba zikaanza kuzama.
They beckoned to their partners in the other boat, that they should come and help them. They came, and filled both boats, so that they began to sink.
8 Lakini Simoni Petro, alipoona hivyo, alianguka magotini pa Yesu akisema,”Ondoka kwangu, kwa sababu mimi ni mtu mwenye dhambi Bwana.”
But Simeon Peter [Hearing Rock], when he saw it, fell down at Yeshua [Salvation]'s knees, saying, “Depart from me, for I am a sinful man, Lord.”
9 Kwa sababu alishangazwa, na wote waliokuwa pamoja naye, kwa uvuvi wa samaki waliokuwa wameufanya.
For he was amazed, and all who were with him, at the catch of fish which they had caught;
10 Hili liliwajumuisha Yakobo na Yohana wana wa Zebedayo, ambao walikuwa washirika wa Simoni. Na Yesu akamwambia Simoni, “Usiogope, kwa sababu kuanzia sasa na kuendelea utavua watu.”
and so also were James [Surplanter] and John [Yah is gracious], sons of Zebedee [Bestowed by Yah], who were partners with Simeon [Hearing]. Yeshua [Salvation] said to Simeon [Hearing], “Don’t be afraid. From now on you will be catching people alive.”
11 Walipokwishazileta mashua zao nchi kavu, waliacha kila kitu na kumfuata yeye.
When they had brought their boats to land, they left everything, and followed him.
12 Ilitokea kwamba alipokuwa katika mji mmojawapo, mtu aliyekuwa amejaa ukoma alikuwa huko. Wakati alipomuona Yesu, alianguka akiinamisha uso kwake mpaka chini na kumuomba, akisema, “Bwana, ikiwa unataka, waweza kunitakasa.”
While he was in one of the cities, behold, there was a man full of tzara'at ·leprosy·. When he saw Yeshua [Salvation], he fell on his face, and begged him, saying, “Lord, if you want to, you can make me clean.”
13 Kisha Yesu alinyoosha mkono wake na kumgusa, akisema, “Nataka. Takasika.” Na saa ileile ukoma ukamwacha.
He stretched out his hand, and touched him, saying, “I want to. Be made clean.” Immediately the tzara'at ·leprosy· left him.
14 “Alimwagiza asimwambie mtu yeyote, lakini alimwambia, “Nenda zako, na ukajionyeshe kwa makuhani na utoe sadaka ya utakaso wako, sawasawa na kile Musa alichokiamuru, kwa ushuhuda kwao.”
He commanded him to tell no one. “Instead, as a testimony to the people, go straight to the priest and make an offer for your cleansing, as Moses [Drawn out] commanded.”
15 Lakini habari kumuhusu yeye zikaenea mbali zaidi, na umati mkubwa wa watu ukaja pamoja kumsikiliza akifundisha na kuponywa magonjwa yao.
But the report concerning him spread much more, and great multitudes came together to hear, and to be healed by him of their infirmities.
16 Lakini mara kwa mara alijitenga faraghani na kuomba.
But he withdrew himself into the desert, and prayed.
17 Ilitokea siku moja kati ya hizo siku alikuwa akifundisha, na walikuwapo Mafarisayo na waalimu wa sheria wamekaa hapo ambao walikuja wakitokea vijiji vingi tofauti katika mkoa wa Galilaya na Yudea, na pia kutokea katika mji wa Yerusalemu. Nguvu ya Bwana ilikuwa pamoja naye kuponya.
On one of those days, he was teaching; and there were Pharisees [Separated] and Torah-Teachers sitting by, who had come out of every village of Galilee [District, Circuit], Judea [Praise], and Jerusalem [City of peace]. The power of MarYah [Master Yahweh] was with him to heal them.
18 watu kadhaa walikuja, wamembeba kwenye mkeka mtu aliyepooza, na wakatafuta njia ya kumwingiza ndani ili kumlaza chini mbele ya Yesu.
Behold, men brought a paralyzed man on a cot, and they sought to bring him in to lay before Yeshua [Salvation].
19 Hawakupata njia ya kumwingiza ndani kwa sababu ya umati, hivyo walipanda juu ya paa la nyumba na kumshusha yule mtu chini kupitia kwenye vigae, juu mkeka wake katikati ya watu, mbele kabisa ya Yesu.
Not finding a way to bring him in because of the multitude, they went up to the housetop, and let him down through the tiles with his cot into the middle before Yeshua [Salvation].
20 Akiangalia imani yao, Yesu alisema, “Rafiki, dhambi zako umesamehewa.”
Seeing their trusting faith, he said to him, “Man, your sins are forgiven you.”
21 Waandishi na Mafarisayo waliaanza kuhoji hilo, wakisema, “Huyu ni nani anayeongea makufuru? Ni nani anaweza kusamehe dhambi ila Mungu pekee yake?”
The Torah-Teachers and the Pharisees [Separated] began to reason, saying, “Who is this that speaks blasphemies? Who can forgive sins, but God alone?”
22 Lakini Yesu, akitambua nini walichokuwa wakifikiri, aliwajibu na kuwaambia, “Kwa nini mnaulizana hili mioyoni mwenu?
But Yeshua [Salvation], perceiving their thoughts, answered them, “Why are you reasoning so in your hearts?
23 Kipi ni rahisi kusema, 'Dhambi zako zimesamehewa' au kusema 'Simama utembee?'
Which is easier to say, ‘Your sins are forgiven you;’ or to say, ‘Arise and walk?’
24 Lakini mjue ya kwamba Mwana wa Adamu anayo mamlaka duniani ya kusamehe dhambi, Nakwambia wewe, 'Amka, chukua mkeka wako na uende nyumbani kwako.'”
But that you may know that the Son of Man has authority on earth to forgive sins” (he said to the paralyzed man), “I tell you, arise, and take up your cot, and go to your house.”
25 Wakati huo huo akaamka mbele yao na akachukua mkeka wake aliokuwa ameulalia. Kisha akariudi nyumbani kwake akimtukuza Mungu.
Immediately he rose up before them, and took up that which he was laying on, and departed to his house, glorifying God.
26 Kila mmoja alishangazwa na wakamtukuza Mungu. Walijawa na hofu, wakisema, “Tumeona mambo yasiyo ya kawaida leo.”
Amazement took hold on all, and they glorified God. They were filled with fear, saying, “We have seen strange things today.”
27 Baada ya mambo haya kutokea, Yesu alitoka huko na akamwona mtoza ushuru aliyeitwa Lawi amekaa eneo la kukusanyia kodi. Akamwambia, “Nifuate.”
After these things he went out, and saw a tax collector named Levi [United with] sitting at the tax office, and said to him, “Follow me!”
28 Hivyo Lawi akanyanyuka na kumfuata, akiacha kila kitu nyuma.
He left everything, and rose up and followed him.
29 Kisha Lawi akaandaa nyumbani kwake karamu kubwa kwa ajili ya Yesu. Walikuwapo watozaushuru wengi kule na watu wengi walioketi mezani wakila pamoja nao.
Levi [United with] made a great feast for him in his house. There was a great crowd of tax collectors and others who were reclining with them.
30 Lakini Mafarisayo na waandishi wao walikuwa wakiwanung'unikia wanafunzi, wakisema, “Kwa nini mnakula na kunywa na watoza ushuru pamoja na watu wengine wenye dhambi?”
Their Torah-Teachers and the Pharisees [Separated] murmured against his disciples, saying, “Why do you eat and drink with the tax collectors and sinners?”
31 Yesu akawajibu, “Watu walio katika afya njema hawahitaji tabibu, ni wale tu wanaoumwa ndiyo watakao mhitaji mmoja.
Yeshua [Salvation] answered them, “Those who are healthy have no need for a physician, but those who are sick do.
32 Sikuja kuwaita watu wenye haki haki wapate kutubu, bali kuwaita wenye dhambi wapate kutubu.”
I have not come to call the upright, but sinners to teshuvah ·complete repentance·.”
33 Wakamwambia, “Wanafunzi wa Yohana mara nyingi hufunga na kuomba, na wanafunzi wa Mafarisayo nao hufanya vivyo hivyo. Lakini wanafunzi wako hula na kunywa.”
They said to him, “Why do John [Yah is gracious]’s disciples often fast and pray, likewise also the disciples of the Pharisees [Separated], but yours eat and drink?”
34 Yesu akawaambia, “Inawezekana mtu yeyote akawafanya waliohudhuria harusi ya Bwana Arusi kufunga wakati Bwana Arusi bado yu pamoja nao?
He said to them, “Can you make the friends of the bridegroom fast, while the bridegroom is with them?
35 Lakini siku zitakuja wakati Bwana Arusi atakapoondolewa kwao, ndipo katika siku hizo watafunga.”
But the days will come when the bridegroom will be taken away from them. Then they will fast in those days.”
36 Kisha Yesu aliongea pia kwao kwa mfano. “Hakuna anayechana kipande cha nguo kutoka kwenye vazi jipya na kukitumia kurekebisha vazi la zamani. Kama akifanya hivyo, ataichana nguo mpya, na kipande cha nguo kutoka vazi jipya kisengefaa kutumika na nguo ya vazi la zamani.
He also told a parable to them. “No one puts a piece from a new garment on an old garment, or else he will tear the new, and also the piece from the new will not match the old.
37 pia, hakuna mtu ambaye huweka divai mpya kwenye viriba vikuukuu. Kama akifanya hivyo, divai mpya ingepasua kile chombo, na divai ingemwagika, na viriba vingeharibika.
No one puts new wine into old wine skins, or else the new wine will burst the skins, and it will be spilled, and the skins will be destroyed.
38 Lakini divai mpya lazima iwekwe kwenye viriba vipya.
But new wine must be put into fresh wine skins, and both are preserved.
39 Na hakuna mtu baada ya kunywa divai ya zamani, hutataka mpya, kwa sababu husema, 'Ya zamani ni bora.”'
No man having drunk old wine immediately desires new, for he says, ‘The old is better.’”

< Luka 5 >