< Luka 5 >

1 Basi ilitokea wakati watu walipomkusanyikia na kumzunguka Yesu na kusikiliza neno la Mungu, ambapo alikuwa amesimama kando ya ziwa Genesareti.
And it came to pass, that, as the people pressed on him to hear the word of God, he stood by the lake of Gennesaret,
2 Aliona mashua mbili zimetia nanga pembeni mwa ziwa. Wavuvi walikuwa wametoka na walikuwa wakiosha nyavu zao.
And saw two ships standing by the lake: but the fishermen were gone out of them, and were washing their nets.
3 Yesu akaingia katika mojawapo ya zile mashua, ambayo ilikuwa ya Simoni na kumwomba aipeleke majini mbali kidogo na nchi kavu. Kisha akakaa na kufundisha kutokea kwenye mashua.
And he entered into one of the ships, which was Simon’s, and prayed him that he would thrust out a little from the land. And he sat down, and taught the people out of the ship.
4 kuongea, akamwambia Simoni, “Ipeleke mashua yako mpaka kwenye kilindi cha maji nakushusha nyavu zako ili kuvua samaki.”
Now when he had left speaking, he said to Simon, Launch out into the deep, and let down your nets for a draught.
5 Simon akajibu na kusema, Bwana, tumefanya kazi usiku wote, na hatukukamata chochote, lakini kwa neno lako, nitazishusha nyavu.
And Simon answering said to him, Master, we have toiled all the night, and have taken nothing: nevertheless at your word I will let down the net.
6 Walipofanya hivyo walikusanya kiasi kikubwa cha samaki na nyavu zao zikaanza kukatika.
And when they had this done, they enclosed a great multitude of fishes: and their net broke.
7 Hivyo wakawaashiria washirika wao kwenye mashua nyingine ili waja na kuwasaidia. Walikuja wakazijaza mashua zote, kiasi kwamba zikaanza kuzama.
And they beckoned to their partners, which were in the other ship, that they should come and help them. And they came, and filled both the ships, so that they began to sink.
8 Lakini Simoni Petro, alipoona hivyo, alianguka magotini pa Yesu akisema,”Ondoka kwangu, kwa sababu mimi ni mtu mwenye dhambi Bwana.”
When Simon Peter saw it, he fell down at Jesus’ knees, saying, Depart from me; for I am a sinful man, O Lord.
9 Kwa sababu alishangazwa, na wote waliokuwa pamoja naye, kwa uvuvi wa samaki waliokuwa wameufanya.
For he was astonished, and all that were with him, at the draught of the fishes which they had taken:
10 Hili liliwajumuisha Yakobo na Yohana wana wa Zebedayo, ambao walikuwa washirika wa Simoni. Na Yesu akamwambia Simoni, “Usiogope, kwa sababu kuanzia sasa na kuendelea utavua watu.”
And so was also James, and John, the sons of Zebedee, which were partners with Simon. And Jesus said to Simon, Fear not; from now on you shall catch men.
11 Walipokwishazileta mashua zao nchi kavu, waliacha kila kitu na kumfuata yeye.
And when they had brought their ships to land, they forsook all, and followed him.
12 Ilitokea kwamba alipokuwa katika mji mmojawapo, mtu aliyekuwa amejaa ukoma alikuwa huko. Wakati alipomuona Yesu, alianguka akiinamisha uso kwake mpaka chini na kumuomba, akisema, “Bwana, ikiwa unataka, waweza kunitakasa.”
And it came to pass, when he was in a certain city, behold a man full of leprosy: who seeing Jesus fell on his face, and sought him, saying, Lord, if you will, you can make me clean.
13 Kisha Yesu alinyoosha mkono wake na kumgusa, akisema, “Nataka. Takasika.” Na saa ileile ukoma ukamwacha.
And he put forth his hand, and touched him, saying, I will: be you clean. And immediately the leprosy departed from him.
14 “Alimwagiza asimwambie mtu yeyote, lakini alimwambia, “Nenda zako, na ukajionyeshe kwa makuhani na utoe sadaka ya utakaso wako, sawasawa na kile Musa alichokiamuru, kwa ushuhuda kwao.”
And he charged him to tell no man: but go, and show yourself to the priest, and offer for your cleansing, according as Moses commanded, for a testimony to them.
15 Lakini habari kumuhusu yeye zikaenea mbali zaidi, na umati mkubwa wa watu ukaja pamoja kumsikiliza akifundisha na kuponywa magonjwa yao.
But so much the more went there a fame abroad of him: and great multitudes came together to hear, and to be healed by him of their infirmities.
16 Lakini mara kwa mara alijitenga faraghani na kuomba.
And he withdrew himself into the wilderness, and prayed.
17 Ilitokea siku moja kati ya hizo siku alikuwa akifundisha, na walikuwapo Mafarisayo na waalimu wa sheria wamekaa hapo ambao walikuja wakitokea vijiji vingi tofauti katika mkoa wa Galilaya na Yudea, na pia kutokea katika mji wa Yerusalemu. Nguvu ya Bwana ilikuwa pamoja naye kuponya.
And it came to pass on a certain day, as he was teaching, that there were Pharisees and doctors of the law sitting by, which were come out of every town of Galilee, and Judaea, and Jerusalem: and the power of the Lord was present to heal them.
18 watu kadhaa walikuja, wamembeba kwenye mkeka mtu aliyepooza, na wakatafuta njia ya kumwingiza ndani ili kumlaza chini mbele ya Yesu.
And, behold, men brought in a bed a man which was taken with a palsy: and they sought means to bring him in, and to lay him before him.
19 Hawakupata njia ya kumwingiza ndani kwa sababu ya umati, hivyo walipanda juu ya paa la nyumba na kumshusha yule mtu chini kupitia kwenye vigae, juu mkeka wake katikati ya watu, mbele kabisa ya Yesu.
And when they could not find by what way they might bring him in because of the multitude, they went on the housetop, and let him down through the tiling with his couch into the middle before Jesus.
20 Akiangalia imani yao, Yesu alisema, “Rafiki, dhambi zako umesamehewa.”
And when he saw their faith, he said to him, Man, your sins are forgiven you.
21 Waandishi na Mafarisayo waliaanza kuhoji hilo, wakisema, “Huyu ni nani anayeongea makufuru? Ni nani anaweza kusamehe dhambi ila Mungu pekee yake?”
And the scribes and the Pharisees began to reason, saying, Who is this which speaks blasphemies? Who can forgive sins, but God alone?
22 Lakini Yesu, akitambua nini walichokuwa wakifikiri, aliwajibu na kuwaambia, “Kwa nini mnaulizana hili mioyoni mwenu?
But when Jesus perceived their thoughts, he answering said to them, What reason you in your hearts?
23 Kipi ni rahisi kusema, 'Dhambi zako zimesamehewa' au kusema 'Simama utembee?'
Whether is easier, to say, Your sins be forgiven you; or to say, Rise up and walk?
24 Lakini mjue ya kwamba Mwana wa Adamu anayo mamlaka duniani ya kusamehe dhambi, Nakwambia wewe, 'Amka, chukua mkeka wako na uende nyumbani kwako.'”
But that you may know that the Son of man has power on earth to forgive sins, (he said to the sick of the palsy, ) I say to you, Arise, and take up your couch, and go into your house.
25 Wakati huo huo akaamka mbele yao na akachukua mkeka wake aliokuwa ameulalia. Kisha akariudi nyumbani kwake akimtukuza Mungu.
And immediately he rose up before them, and took up that where on he lay, and departed to his own house, glorifying God.
26 Kila mmoja alishangazwa na wakamtukuza Mungu. Walijawa na hofu, wakisema, “Tumeona mambo yasiyo ya kawaida leo.”
And they were all amazed, and they glorified God, and were filled with fear, saying, We have seen strange things to day.
27 Baada ya mambo haya kutokea, Yesu alitoka huko na akamwona mtoza ushuru aliyeitwa Lawi amekaa eneo la kukusanyia kodi. Akamwambia, “Nifuate.”
And after these things he went forth, and saw a publican, named Levi, sitting at the receipt of custom: and he said to him, Follow me.
28 Hivyo Lawi akanyanyuka na kumfuata, akiacha kila kitu nyuma.
And he left all, rose up, and followed him.
29 Kisha Lawi akaandaa nyumbani kwake karamu kubwa kwa ajili ya Yesu. Walikuwapo watozaushuru wengi kule na watu wengi walioketi mezani wakila pamoja nao.
And Levi made him a great feast in his own house: and there was a great company of publicans and of others that sat down with them.
30 Lakini Mafarisayo na waandishi wao walikuwa wakiwanung'unikia wanafunzi, wakisema, “Kwa nini mnakula na kunywa na watoza ushuru pamoja na watu wengine wenye dhambi?”
But their scribes and Pharisees murmured against his disciples, saying, Why do you eat and drink with publicans and sinners?
31 Yesu akawajibu, “Watu walio katika afya njema hawahitaji tabibu, ni wale tu wanaoumwa ndiyo watakao mhitaji mmoja.
And Jesus answering said to them, They that are whole need not a physician; but they that are sick.
32 Sikuja kuwaita watu wenye haki haki wapate kutubu, bali kuwaita wenye dhambi wapate kutubu.”
I came not to call the righteous, but sinners to repentance.
33 Wakamwambia, “Wanafunzi wa Yohana mara nyingi hufunga na kuomba, na wanafunzi wa Mafarisayo nao hufanya vivyo hivyo. Lakini wanafunzi wako hula na kunywa.”
And they said to him, Why do the disciples of John fast often, and make prayers, and likewise the disciples of the Pharisees; but your eat and drink?
34 Yesu akawaambia, “Inawezekana mtu yeyote akawafanya waliohudhuria harusi ya Bwana Arusi kufunga wakati Bwana Arusi bado yu pamoja nao?
And he said to them, Can you make the children of the bridal chamber fast, while the bridegroom is with them?
35 Lakini siku zitakuja wakati Bwana Arusi atakapoondolewa kwao, ndipo katika siku hizo watafunga.”
But the days will come, when the bridegroom shall be taken away from them, and then shall they fast in those days.
36 Kisha Yesu aliongea pia kwao kwa mfano. “Hakuna anayechana kipande cha nguo kutoka kwenye vazi jipya na kukitumia kurekebisha vazi la zamani. Kama akifanya hivyo, ataichana nguo mpya, na kipande cha nguo kutoka vazi jipya kisengefaa kutumika na nguo ya vazi la zamani.
And he spoke also a parable to them; No man puts a piece of a new garment on an old; if otherwise, then both the new makes a rent, and the piece that was taken out of the new agrees not with the old.
37 pia, hakuna mtu ambaye huweka divai mpya kwenye viriba vikuukuu. Kama akifanya hivyo, divai mpya ingepasua kile chombo, na divai ingemwagika, na viriba vingeharibika.
And no man puts new wine into old bottles; else the new wine will burst the bottles, and be spilled, and the bottles shall perish.
38 Lakini divai mpya lazima iwekwe kwenye viriba vipya.
But new wine must be put into new bottles; and both are preserved.
39 Na hakuna mtu baada ya kunywa divai ya zamani, hutataka mpya, kwa sababu husema, 'Ya zamani ni bora.”'
No man also having drunk old wine straightway desires new: for he says, The old is better.

< Luka 5 >