< Luka 5 >

1 Basi ilitokea wakati watu walipomkusanyikia na kumzunguka Yesu na kusikiliza neno la Mungu, ambapo alikuwa amesimama kando ya ziwa Genesareti.
And it came to pass while the multitude was pressing on him to hear the word of God, and he was standing by the lake of Gennesaret,
2 Aliona mashua mbili zimetia nanga pembeni mwa ziwa. Wavuvi walikuwa wametoka na walikuwa wakiosha nyavu zao.
that he saw two ships standing by the lake: but the fishermen had gone out of them, and were washing their nets.
3 Yesu akaingia katika mojawapo ya zile mashua, ambayo ilikuwa ya Simoni na kumwomba aipeleke majini mbali kidogo na nchi kavu. Kisha akakaa na kufundisha kutokea kwenye mashua.
And he entered one of the ships, which was Simon’s, and requested him to push out a little from the land. And he sat down and taught the multitude from the ship.
4 kuongea, akamwambia Simoni, “Ipeleke mashua yako mpaka kwenye kilindi cha maji nakushusha nyavu zako ili kuvua samaki.”
And when he had made an end of speaking, he said to Simon: Push out into the deep water, and let down your nets for a draught.
5 Simon akajibu na kusema, Bwana, tumefanya kazi usiku wote, na hatukukamata chochote, lakini kwa neno lako, nitazishusha nyavu.
And Simon answered and said to him: Master, we have toiled all night and have caught nothing; but at thy command, I will let down the net.
6 Walipofanya hivyo walikusanya kiasi kikubwa cha samaki na nyavu zao zikaanza kukatika.
And when they had done this, they inclosed a great number of fishes, and their net began to break;
7 Hivyo wakawaashiria washirika wao kwenye mashua nyingine ili waja na kuwasaidia. Walikuja wakazijaza mashua zote, kiasi kwamba zikaanza kuzama.
and they beckoned to their partners who were in the other ship, to come and help them. And they came and filled both the ships, so that they began to sink.
8 Lakini Simoni Petro, alipoona hivyo, alianguka magotini pa Yesu akisema,”Ondoka kwangu, kwa sababu mimi ni mtu mwenye dhambi Bwana.”
And when Simon Peter saw it, he fell down at the knees of Jesus, and said: Depart from me, Lord, for I am a sinful man.
9 Kwa sababu alishangazwa, na wote waliokuwa pamoja naye, kwa uvuvi wa samaki waliokuwa wameufanya.
For amazement at the draught of fishes which they had caught had seized upon him and all that were with him;
10 Hili liliwajumuisha Yakobo na Yohana wana wa Zebedayo, ambao walikuwa washirika wa Simoni. Na Yesu akamwambia Simoni, “Usiogope, kwa sababu kuanzia sasa na kuendelea utavua watu.”
and in like manner also upon James and John the sons of Zebedee, who were partners with Simon. And Jesus said to Simon: Fear not; from this time forth you shall catch men.
11 Walipokwishazileta mashua zao nchi kavu, waliacha kila kitu na kumfuata yeye.
And when they had brought their ships to the land, they left all and followed him.
12 Ilitokea kwamba alipokuwa katika mji mmojawapo, mtu aliyekuwa amejaa ukoma alikuwa huko. Wakati alipomuona Yesu, alianguka akiinamisha uso kwake mpaka chini na kumuomba, akisema, “Bwana, ikiwa unataka, waweza kunitakasa.”
And it came to pass, that he was in one of their cities; and behold, a man full of leprosy; and when he saw Jesus, he fell on his face and besought him, saying: Lord, if thou wilt, thou canst make me clean.
13 Kisha Yesu alinyoosha mkono wake na kumgusa, akisema, “Nataka. Takasika.” Na saa ileile ukoma ukamwacha.
And stretching out his hand, he touched him, and said: I will; be clean. And immediately his leprosy departed from him.
14 “Alimwagiza asimwambie mtu yeyote, lakini alimwambia, “Nenda zako, na ukajionyeshe kwa makuhani na utoe sadaka ya utakaso wako, sawasawa na kile Musa alichokiamuru, kwa ushuhuda kwao.”
And he charged him to tell no one; but go, show yourself to the priest, and make offering for your cleansing, as Moses commanded, that it may be a testimony to them.
15 Lakini habari kumuhusu yeye zikaenea mbali zaidi, na umati mkubwa wa watu ukaja pamoja kumsikiliza akifundisha na kuponywa magonjwa yao.
But his fame went abroad the more; and many multitudes came together to hear, and to be cured by him of their infirmities.
16 Lakini mara kwa mara alijitenga faraghani na kuomba.
And he withdrew to the deserts and prayed.
17 Ilitokea siku moja kati ya hizo siku alikuwa akifundisha, na walikuwapo Mafarisayo na waalimu wa sheria wamekaa hapo ambao walikuja wakitokea vijiji vingi tofauti katika mkoa wa Galilaya na Yudea, na pia kutokea katika mji wa Yerusalemu. Nguvu ya Bwana ilikuwa pamoja naye kuponya.
And it came to pass, on a certain day, that he was teaching, and there were Pharisees and teachers of the law sitting by, who had come from every village of Galilee and Judea and Jerusalem; and the power of the Lord was exerted to heal them.
18 watu kadhaa walikuja, wamembeba kwenye mkeka mtu aliyepooza, na wakatafuta njia ya kumwingiza ndani ili kumlaza chini mbele ya Yesu.
And behold, men brought, on a bed, a man who was a paralytic. And they sought how they might bring him in, and lay him before him.
19 Hawakupata njia ya kumwingiza ndani kwa sababu ya umati, hivyo walipanda juu ya paa la nyumba na kumshusha yule mtu chini kupitia kwenye vigae, juu mkeka wake katikati ya watu, mbele kabisa ya Yesu.
And finding no way by which they could bring him in, because of the multitude, they went up on the top of the house, and, through the tiling, let him down, with his bed, into the midst before Jesus.
20 Akiangalia imani yao, Yesu alisema, “Rafiki, dhambi zako umesamehewa.”
And when he saw their faith, he said to him: Man, your sins are forgiven you.
21 Waandishi na Mafarisayo waliaanza kuhoji hilo, wakisema, “Huyu ni nani anayeongea makufuru? Ni nani anaweza kusamehe dhambi ila Mungu pekee yake?”
And the scribes and Pharisees began to reason, saying: Who is this that utters impious words? Who can forgive sins but God alone?
22 Lakini Yesu, akitambua nini walichokuwa wakifikiri, aliwajibu na kuwaambia, “Kwa nini mnaulizana hili mioyoni mwenu?
But Jesus perceived their reasonings, and answered and said to them: Why are you reasoning in your hearts?
23 Kipi ni rahisi kusema, 'Dhambi zako zimesamehewa' au kusema 'Simama utembee?'
Which is easier, to say., Your sins are forgiven you; or to say, Arise and walk?
24 Lakini mjue ya kwamba Mwana wa Adamu anayo mamlaka duniani ya kusamehe dhambi, Nakwambia wewe, 'Amka, chukua mkeka wako na uende nyumbani kwako.'”
But that you may know that the Son of man on the earth has power to forgive sins, (he said to the paralytic, ) I say to you, Arise, and take up your bed, and go to your house.
25 Wakati huo huo akaamka mbele yao na akachukua mkeka wake aliokuwa ameulalia. Kisha akariudi nyumbani kwake akimtukuza Mungu.
And he immediately arose before them, took up that on which he had been lying, and went away to his own house, glorifying God.
26 Kila mmoja alishangazwa na wakamtukuza Mungu. Walijawa na hofu, wakisema, “Tumeona mambo yasiyo ya kawaida leo.”
And astonishment seized upon all, and they glorified God, and were filled with fear, saying: We have seen strange things to-day.
27 Baada ya mambo haya kutokea, Yesu alitoka huko na akamwona mtoza ushuru aliyeitwa Lawi amekaa eneo la kukusanyia kodi. Akamwambia, “Nifuate.”
And after these tilings, he went out and saw a publican named Levi, sitting at the custom-house; and he said to him: Follow me.
28 Hivyo Lawi akanyanyuka na kumfuata, akiacha kila kitu nyuma.
And leaving all, he arose and followed him.
29 Kisha Lawi akaandaa nyumbani kwake karamu kubwa kwa ajili ya Yesu. Walikuwapo watozaushuru wengi kule na watu wengi walioketi mezani wakila pamoja nao.
And Levi made him a great feast at his own house; and there was a great multitude of publicans and others, who reclined at table with them.
30 Lakini Mafarisayo na waandishi wao walikuwa wakiwanung'unikia wanafunzi, wakisema, “Kwa nini mnakula na kunywa na watoza ushuru pamoja na watu wengine wenye dhambi?”
And their scribes and the Pharisees murmured against his disciples, saying: Why do you eat and drink with publicans and sinners?
31 Yesu akawajibu, “Watu walio katika afya njema hawahitaji tabibu, ni wale tu wanaoumwa ndiyo watakao mhitaji mmoja.
And Jesus answered arid said to them: They that are well have no need of a physician, but they that are sick.
32 Sikuja kuwaita watu wenye haki haki wapate kutubu, bali kuwaita wenye dhambi wapate kutubu.”
I have not come to call righteous men, but sinners, to repentance.
33 Wakamwambia, “Wanafunzi wa Yohana mara nyingi hufunga na kuomba, na wanafunzi wa Mafarisayo nao hufanya vivyo hivyo. Lakini wanafunzi wako hula na kunywa.”
And they said to him: Why do the disciples of John fast often, and make prayers, and likewise the disciples of the Pharisees, but yours eat and drink?
34 Yesu akawaambia, “Inawezekana mtu yeyote akawafanya waliohudhuria harusi ya Bwana Arusi kufunga wakati Bwana Arusi bado yu pamoja nao?
And he said to them: Can you make the sons of the bride-chamber fast, while the bridegroom is with them?
35 Lakini siku zitakuja wakati Bwana Arusi atakapoondolewa kwao, ndipo katika siku hizo watafunga.”
But the days will come when the bridegroom shall be taken from them; then shall they fast in those days.
36 Kisha Yesu aliongea pia kwao kwa mfano. “Hakuna anayechana kipande cha nguo kutoka kwenye vazi jipya na kukitumia kurekebisha vazi la zamani. Kama akifanya hivyo, ataichana nguo mpya, na kipande cha nguo kutoka vazi jipya kisengefaa kutumika na nguo ya vazi la zamani.
And he spoke also a parable to them: No one patches an old garment with a piece taken from a new garment. If so, the new tears it, and the patch from the new suits not the old.
37 pia, hakuna mtu ambaye huweka divai mpya kwenye viriba vikuukuu. Kama akifanya hivyo, divai mpya ingepasua kile chombo, na divai ingemwagika, na viriba vingeharibika.
And no one puts new wine into old bottles; if so, the new wine will burst the bottles, and it will be spilled, and the bottles will be destroyed.
38 Lakini divai mpya lazima iwekwe kwenye viriba vipya.
But new wine must be put into new bottles, and both will be preserved.
39 Na hakuna mtu baada ya kunywa divai ya zamani, hutataka mpya, kwa sababu husema, 'Ya zamani ni bora.”'
And no one, after drinking old wine, immediately desires new; for he says: The old is better.

< Luka 5 >