< Luka 4 >

1 Kisha, Yesu akiwa amejaa Roho Mtakatifu, alirudi kutoka Mto Jordani, na aliongozwa na Roho jangwani
Then Jesus, being full of the Holy Spirit, returned from the Jordan River, and was led by the Spirit in the wilderness,
2 kwa siku arobaini, na huko alijaribiwa na Ibilisi. Wakati huo hakula chochote, na mwisho wa wakati huo alihisi njaa.
where for forty days he was tempted by the devil. He ate nothing during those days, and at the end of that time he was hungry.
3 Ibilisi akamwambia, “Kama wewe ni Mwana wa Mungu, liamru jiwe hili kuwa mkate.”
The devil said to him, “If you are the Son of God, command this stone to become bread.”
4 Yesu akamjibu, “Imeandikwa; 'mtu hataishi kwa mkate pekee.”
Jesus answered him, “It is written, 'Man does not live on bread alone.'”
5 Kisha Ibilisi alimwongoza juu kwenye kilele cha mlima, na akamwonyesha falme zote za dunia kwa muda mfupi.
Then the devil led Jesus up and showed him all the kingdoms of the world in an instant of time.
6 Ibilisi akamwambia, “Nitakupa mamlaka ya kutawala falme hizi zote pamoja na fahari zake. Naweza kufanya hivyo kwa sababu vyote vimekabidhiwa kwangu nivitawale, na ninaweza kumpa yeyote nitakaye kumpa.
The devil said to him, “I will give to you all this authority and all their splendor, for they have been given to me, and I can give it to anyone I want.
7 Kwahiyo, kama utaniinamia na kuniabudu, vitu hivi vyote vitakuwa vyako.”
So then, if you will bow down and worship me, it will be yours.”
8 Lakini Yesu alijibu na kumwambia, “Imeandikwa, “lazima umwabudu Bwana Mungu wako, na lazima umtumikie Yeye peke yake.”
But Jesus answered and said to him, “It is written, 'You will worship the Lord your God, and you will serve only him.'”
9 Baadaye Ibilisi alimwongoza Yesu hadi Yerusalemu na kumweka sehemu ya juu kabisa ya jengo la hekalu na kumwambia, “Kama wewe ni Mwana wa Mungu, jitupe chini kutoka hapa.
Then the devil led Jesus to Jerusalem and put him on the very highest point of the temple building, and said to him, “If you are the Son of God, throw yourself down from here.
10 Kwa sababu imeandikwa, “Atawaagiza malaika zake wakutunze na kukulinda,
For it is written, 'He will give orders to his angels regarding you, to protect you,'
11 na watakuinua juu mikononi mwao ili kwamba usiumize miguu yako juu ya jiwe.”
and, 'They will lift you up in their hands, so that you will not strike your foot against a stone.'”
12 Yesu akijibu alimwambia, “Imenenwa, “usimjaribu Bwana Mungu wako.”
Answering him, Jesus said, “It is said, 'Do not put the Lord your God to the test.'”
13 Ibilisi alipomaliza kumjaribu Yesu, alienda zake na kumwacha hadi wakati mwingine.
When the devil had finished testing Jesus, he went away and left him until another time.
14 Kisha Yesu alirudi Galilaya kwa nguvu za Roho, na habari kumhusu yeye zikaenea na kusambaa katika mikoa jirani yote.
Then Jesus returned to Galilee in the power of the Spirit, and news about him spread throughout the entire surrounding region.
15 Alifundisha katika masinagogi yao, na kila mmoja alimsifu.
Then he began to teach in their synagogues and he was praised by all.
16 Siku moja alikwenda Nazareti, mji ambao alilelewa na kukulia. Kama ilivyokuwa desturi yake aliingia kwenye sinagogi siku ya sabato, na alisimama kusoma maandiko.
He came into Nazareth, where he had been raised, and as was his custom, he entered the synagogue on the Sabbath day and he stood up to read aloud.
17 Alikabidhiwa gombo la nabii Isaya, hivyo, alilifungua gombo na akatafuta sehemu iliyoandikwa,
The scroll of the prophet Isaiah was handed to him. He opened the scroll and found the place where it was written,
18 “Roho wa Bwana yuu juu yangu, kwa sababu alinitia mafuta kuhubiri habari njema kwa maskini. Amenituma kutangaza uhuru kwa wafungwa, na kuwafanya wasioona waweze kuona tena. Kuwaweka huru wale wanaogandamizwa,
“The Spirit of the Lord is upon me, because he anointed me to tell good news to the poor. He has sent me to proclaim freedom to the captives, and recovery of sight to the blind, to set free those who are oppressed,
19 kuutangaza mwaka ambao Bwana ataonesha wema wake.”
to proclaim the year of the Lord's favor.”
20 Kisha akalifunga gombo, akamrudishia kiongozi wa sinagogi, na akaketi chini. Macho ya watu wote waliokuwa katika sinagogi yalimwangalia yeye.
Then he rolled up the scroll, gave it back to the attendant, and sat down. The eyes of all in the synagogue were fixed on him.
21 Alianza kuzungumza nao akisema, “Leo andiko hili limetimizwa masikioni mwenu.”
He began to speak to them, “Today this scripture has been fulfilled in your hearing.”
22 Kila mmoja pale alishuhudia kile alichokisema Yesu, na wengi miongoni mwao walishangazwa na maneno ya hekima yaliyokuwa yakitoka katika kinywa chake. Walikuwa wakisema, “huyu ni kijana tu wa Yusufu, siyo hivyo?”
Everyone there spoke well of him and they were amazed at the gracious words which were coming out of his mouth, and they asked, “Is this not the son of Joseph?”
23 Yesu akawaambia, “hakika mtasema methali hii kwangu, “Tabibu, jiponye mwenyewe. Chochote tulichosikia ukifanya Kapernaumu, kifanye hapa pia kijijini kwako.”
He said to them, “Surely you will say this proverb to me, 'Doctor, heal yourself. Whatever we heard that you did in Capernaum, do the same in your hometown.'”
24 Pia alisema, “hakika nawaambia ninyi, hakuna nabii anayekubalika katika nchi yake.”
But he said, “Truly I say to you, no prophet is received in his own hometown.
25 Lakini nawaambia ninyi kweli kwamba kulikuwa na wajane wengi Israel katika kipindi cha Eliya, wakati mbingu ilipofungwa kusiwe na nvua kwa miaka mitatu na nusu, wakati kulipokuwa na njaa kubwa katika nchi yote.
But in truth I tell you that there were many widows in Israel during the time of Elijah, when the sky was shut up for three years and six months, and a great famine came upon all the land.
26 Lakini Eliya hakutumwa kwa yeyote mmoja wao, lakini kwa mjane mmoja tu aliyeishi Sarepta karibu na mji wa Sidoni.
But Elijah was sent to none of them, but only to Zarephath in Sidon, to a widow living there.
27 Pia, kulikuwa na wakoma wengi Israel katika kipindi cha Elisha nabii, lakini hakuna hatammoja wao aliyeponywa isipokuwa Naamani mtu wa Siria.
There were many lepers in Israel during the time of Elisha the prophet, but none of them were healed except Naaman the Syrian.”
28 Watu wote ndani ya sinagogi walijawa na gadhabu walipoyasikia haya yote.
All the people in the synagogue were filled with rage when they heard these things.
29 Walisimama na kumsukumizia nje ya mji, na kumwongoza mpaka kwenye ukingo wa mlima wa mji ambapo mji wao ulijengwa juu yake, ili waweze kumtupa chini.
They got up, forced him out of the town, and led him to the cliff of the hill on which their town was built, so they might throw him off the cliff.
30 Lakini alipita salama katikati yao na akaenda zake.
But he passed through the middle of them and he went to another place.
31 Kisha alitelemkia Kapernaumu, katika mji wa Galilaya. Sabato moja alikuwa akifundisha watu ndani ya sinagogi.
Then he went down to Capernaum, a city in Galilee, and he began to teach them on the Sabbath.
32 Walishangazwa na mafundisho yake, kwasababu alifundisha kwa mamlaka.
They were astonished at his teaching, because he spoke with authority.
33 Sasa siku hiyo ndani ya sinagogi, kulikuwa na mtu aliyekuwa na roho ya pepo mchafu, na alilia kwa sauti ya juu,
Now in the synagogue there was a man who had the spirit of an unclean demon, and he cried out with a loud voice,
34 “Tuna nini nawe, Yesu wa Nazareti? Umekuja kutuangamiza? Ninajua wewe ni nani! Wewe ni mtakatifu wa Mungu!”
“Ah! What do we have to do with you, Jesus of Nazareth? Have you come to destroy us? I know who you are—the Holy One of God!”
35 Yesu alimkemea pepo akisema, “Nyamaza kimya, na umtoke mtu huyu!” Pepo yule alipomtupa mtu yule chini katikati yao, alimtoka yule mtu bila ya kumsababishia maumivu yoyote.
Jesus rebuked the demon, saying, “Do not speak! Come out of him!” When the demon had thrown the man down in the middle of them, he came out of him, and did not harm him in any way.
36 Watu wote walishangaa, na waliendelea kuzungumzia jambo hilo kila mmoja na mwenzake. Wakasema, “Ni maneno ya aina gani haya?” Anawaamuru roho wachafu kwa mamlaka na nguvu na watondoka.”
All the people were very amazed, and they kept talking about it with one another. They said, “What kind of words are these? He commands the unclean spirits with authority and power and they come out.”
37 Hivyo, habari juu ya Yesu zilienea kila sehemu katika maeneo yanayozunguka mkoa huo.
So news about him began to spread into every part of the surrounding region.
38 Kisha Yesu aliondoka katika mji huo na akaingia katika nyumba ya Simoni. Sasa, mama mkwe wake na Simoni alikuwa anaumwa homa kali, na wakamsihi kwa niaba yake.
Then Jesus left the synagogue and entered into the house of Simon. Now Simon's mother-in-law was suffering with a high fever, and they pleaded with him on her behalf.
39 Hivyo, Yesu alimsogelea, akaikemea ile homa na ikamwachia. Ghafla alisimama na akaanza kuwatumikia.
So he stood over her and rebuked the fever, and it left her. Immediately she got up and started serving them.
40 Jua lilipokuwa likizama, watu walimletea Yesu kila mmoja aliyekuwa mgonjwa wa maradhi ya aina mbalimbali. Aliweka mikono yake juu ya kila mgonjwa na akawaponya wote.
When the sun was setting, people brought to Jesus everyone who was sick with various kinds of diseases. He laid his hands on every one of them and healed them.
41 Mapepo pia yaliwatoka wengi wao yakilia kwa sauti na kusema, “Wewe ni mwana wa Mungu!” Yesu aliwakemea mapepo na hakuwaruhusu waongee, kwa sababu walijua kwamba yeye alikuwa ni Kristo.
Demons also came out from many of them, crying out and saying, “You are the Son of God!” Jesus rebuked the demons and would not let them speak, because they knew that he was the Christ.
42 Wakati kulipopambazuka, alienda eneo lisilokuwa na watu. Makutano ya watu walikuwa wakimtafuta na wakaja katika eneo alilokuwapo. Walijaribu kumzuia asiende mbali na wao.
When daybreak came, he went out into a solitary place. Crowds of people were looking for him and came to the place where he was. They tried to keep him from going away from them.
43 Lakini akawaambia, “Lazima pia nihubiri habari njema za ufalme wa Mungu katika miji mingine mingi, kwa kuwa hii ndiyo sababu nilitumwa hapa.”
But he said to them, “I must also preach the good news about the kingdom of God to many other cities, because this is the reason I was sent here.”
44 Kisha aliendelea kuhubiri ndani ya masinagogi katika uyahudi wote.
Then he continued to preach in the synagogues throughout Judea.

< Luka 4 >