< Luka 3 >

1 Sasa, katika mwaka wa kumi na tano wa utawala wa Kaisari Tiberia, wakati Pontio Pilato alikuwa gavana wa Uyahudi, Herode alikuwa mkuu wa mkoa wa Galilaya, na Filipo ndugu yake alikuwa mkuu wa mkoa wa Iturea na Trakoniti, na Lisania alikuwa mkuu wa mkoa wa Abilene,
Now in the fifteenth year of the government of Tiberius Caesar, Pontius Pilate being governor of Judaea, and Herod tetrarch of Galilee, and Philip his brother tetrarch of Ituraea and the region of Trachonitis, and Lysanias tetrarch of Abilene,
2 na wakati wa ukuhani mkuu wa Anasi na Kayafa, Neno la Mungu lilimjia Yohana mwana wa Zakaria, jangwani.
in the high priesthood of Annas and Caiaphas, [the] word of God came upon John, the son of Zacharias, in the wilderness.
3 Alisafiri katika mkoa wote kuzunguka Mto Yordani, akihubiri ubatizo wa toba kwa ajili ya msamaha wa dhambi
And he came into all the district round the Jordan, preaching [the] baptism of repentance for [the] remission of sins,
4 Kama ilivyoandikwa katika kitabu cha maneno ya Isaya nabii, “sauti ya mtu aliaye nyikani, “Itengenezeni tayari njia ya Bwana, yatengenezeni mapito yake yaliyoonyoka.
as it is written in [the] book of [the] words of Esaias the prophet: Voice of one crying in the wilderness: Prepare ye the way of [the] Lord, make straight his paths.
5 Kila bonde litajazwa, kila mlima na kilima vitasawazishwa, barabara zilizopinda zitanyoshwa, na njia zilizoparaza zitalainishwa.
Every gorge shall be filled up, and every mountain and hill shall be brought low, and the crooked [places] shall become a straight [path], and the rough places smooth ways,
6 Watu wote watauona wokovu wa Mungu.”
and all flesh shall see the salvation of God.
7 Hivyo, Yohana akawaambia makutano makubwa ya watu waliomjia wapate kubatizwa na yeye, “Ninyi uzao wa nyoka wenye sumu, nani aliwaonya kuikimbia gadhabu inayokuja?
He said therefore to the crowds which went out to be baptised by him, Offspring of vipers, who has forewarned you to flee from the coming wrath?
8 Zaeni matunda yanayoedana na toba, na msianze kusema ndani yenu, “Tunaye Ibarahimu ambaye ni baba yetu; kwa sababu nawaambia ya kwamba, Mungu anaweza kumwinulia Ibrahimu watoto hata kutokana na mawe haya.
Produce therefore fruits worthy of repentance; and begin not to say in yourselves, We have Abraham for [our] father, for I say unto you that God is able of these stones to raise up children to Abraham.
9 Tayari shoka limeshawekwa kwenye mzizi wa miti. Hivyo, kila mti usiozaa matunda mema, hukatwa na kutupwa motoni.
And already also the axe is applied to the root of the trees; every tree therefore not producing good fruit is cut down and cast into [the] fire.
10 Kisha watu katika makutano walimuuliza wakisema, “Sasa tunatakiwa tufanyeje?”
And the crowds asked him saying, What should we do then?
11 Alijibu na kuwaambia, “kama mtu ana kanzu mbili anatakiwa atoe kanzu moja kwa mwingine ambaye hana kabisa, na ambaye ana chakula na afanye vivyo hivyo.”
And he answering says to them, He that has two body-coats, let him give to him that has none; and he that has food, let him do likewise.
12 Kisha baadhi ya watoza ushuru walikuja pia kubatizwa, na wakamwambia, “Mwalimu, tunatakiwa kufanya nini?
And tax-gatherers came also to be baptised, and they said to him, Teacher, what should we do?
13 Akawaambia, “Msikusanye fedha zaidi kuliko mnachotakiwa kukusanya.”
And he said to them, Take no more [money] than what is appointed to you.
14 Baadhi ya maaskari pia wakamuuliza wakisema, “Na sisi je? Tunatakiwa tufanye nini?” Akawambia, “Msichukue fedha kwa mtu yeyote kwa nguvu, na msimtuhumu mtu yeyote kwa uongo. Ridhikeni na mishahara yenu.”
And persons engaged in military service also asked him saying, And we, what should we do? And he said to them, Oppress no one, nor accuse falsely, and be satisfied with your pay.
15 Sasa, kwa kuwa watu walikuwa na shauku ya kumngojea Kristo atakaye kuja, kila mmoja alikuwa anawaza moyoni mwake kuhusu Yohana kama yeye ndiye Kristo.
But as the people were in expectation, and all were reasoning in their hearts concerning John whether he might be the Christ,
16 Yohana akajibu kwa kuwaambia wote, “Mimi nawabatiza ninyi kwa maji, lakini kuna mmoja ajaye ambaye ana nguvu kuliko mimi, na sisitahili hata kufungua kamba za viatu vyake. Atawabatiza ninyi kwa Roho Mtakatifu na kwa moto.
John answered all, saying, I indeed baptise you with water, but the mightier than I is coming, the thong of whose sandals I am not fit to unloose; he shall baptise you with [the] Holy Spirit and fire;
17 Pepeto lake liko mkononi mwake ili kusafisha vizuri uwanda wake wa kupepetea ngano na kuikusanya ngano ghalani mwake. Lakini, atayateketeza makapi kwa moto ambao hauwezi kuzimika.
whose winnowing-fan is in his hand, and he will thoroughly purge his threshing-floor, and will gather the wheat into his garner, but the chaff he will burn with fire unquenchable.
18 Kwa maonyo mengine mengi pia, alihubiri habari njema kwa watu.
Exhorting then many other things also he announced [his] glad tidings to the people.
19 Yohana alimkemea pia Herode mkuu wa mkoa kwa kumuoa Herodia, mke wa ndugu yake na kwa maovu mengine mengi ambayo Herode alikuwa ameyatenda.
But Herod the tetrarch, being reproved by him as to Herodias, the wife of his brother, and as to all the wicked things which Herod had done,
20 Lakini baadaye Herode alifanya uovu mwingine mbaya sana. Alimfunga Yohana gerezani.
added this also to all [the rest], that he shut up John in prison.
21 Kisha ilitokea kwamba, wakati watu wote walipokuwa wakibatizwa na Yohana, naye Yesu alibatizwa pia. Wakati alipokuwa akiomba, mbingu zikafunguka.
And it came to pass, all the people having been baptised, and Jesus having been baptised and praying, that the heaven was opened,
22 Roho Mtakatifu akashuka juu yake kwa mfano wa kiwiliwili kama njiwa, wakati huo huo sauti ikaja kutoka mbinguni ikisema, “Wewe ni Mwanangu mpendwa. Ninapendezwa sana na wewe.”
and the Holy Spirit descended in a bodily form as a dove upon him; and a voice came out of heaven, Thou art my beloved Son, in thee I have found my delight.
23 Sasa Yesu mwenyewe, alipoanza kufundisha, alikuwa na umri upatao miaka thelathini. Alikuwa ni mwana (kama ilivyotadhaniwa) wa Yusufu, mwana wa Eli,
And Jesus himself was beginning to be about thirty years old; being as was supposed son of Joseph; of Eli,
24 mwana wa Mathati, mwana wa Lawi, mwana wa Melki, mwana wa Yana, mwana wa Yusufu,
of Matthat, of Levi, of Melchi, of Janna, of Joseph,
25 mwana wa Matathia, mwana wa Amosi, mwana wa Nahumu, mwana wa Esli, mwana wa Nagai,
of Mattathias, of Amos, of Naoum, of Esli, of Naggai,
26 mwana wa Maati, mwana wa Matathia, mwana wa Semeini, mwana wa Yusufu, mwana wa Yuda,
of Maath, of Mattathias, of Semei, of Joseph, of Juda,
27 mwana wa Yoanani, mwana wa Resa, mwana wa Zerubabeli, mwana wa Shealtieli, mwana wa Neri,
of Joannes, of Resa, of Zorobabel, of Salathiel, of Neri,
28 mwana wa Melki, mwana wa Adi, mwana wa Kosamu, mwana wa Elmadamu, mwana wa Eri,
of Melchi, of Addi, of Cosam, of Elmodam, of Er,
29 mwana wa Yoshua, mwana wa Eliezeri, mwana wa Yorimu, mwana wa Matathi, mwana wa Lawi,
of Joses, of Eliezer, of Joreim, of Matthat, of Levi,
30 mwana wa Simeoni, mwana wa Yuda, mwana wa Yusufu, mwana wa Yonamu, mwana wa Eliyakimu,
of Simeon, of Juda, of Joseph, of Jonan, of Eliakim,
31 mwana wa Melea, mwana wa Mena, mwana wa Matatha, mwana wa Nathani, mwana wa Daudi,
of Meleas, of Menan, of Mattatha, of Nathan, of David,
32 mwana wa Yese, mwana wa Obedi, mwana wa Boazi, mwana wa Salmoni, mwana wa Nashoni,
of Jesse, of Obed, of Booz, of Salmon, of Naasson,
33 mwana wa Abinadabu, mwana wa Aramu, mwana wa Hesroni, mwana wa Peresi, mwana wa Yuda,
of Aminadab, of Aram, of Esrom, of Phares, of Juda,
34 mwana wa Yakobo, mwana wa Isaka, mwana wa Ibrahimu, mwana wa Tera, mwana wa Nahori,
of Jacob, of Isaac, of Abraham, of Terah, of Nachor,
35 mwana wa Seruig, mwana wa Ragau, mwana wa Pelegi, mwana wa Eberi, mwana wa Sala,
of Seruch, of Ragau, of Phalek, of Eber, of Sala,
36 mwana wa Kenani, mwana wa Arfaksadi, mwana wa Shemu, mwana wa Nuhu, mwana wa Lameki,
of Cainan, of Arphaxad, of Sem, of Noe, of Lamech,
37 mwana wa Methusela, mwana wa Henoko, mwana wa Yaredi, mwana Mahalalei, mwana wa Kenani,
of Methusala, of Enoch, of Jared, of Maleleel, of Cainan,
38 mwana wa Enoshi, mwana wa Sethi, mwana wa Adamu, mwana wa Mungu.
of Enos, of Seth, of Adam, of God.

< Luka 3 >